Hawara aliyempiga kibuti aukwaa u-Jaji... Kidume ajipanga upya!

LD labda anaangalia masilahi ya mtoto/watoto wapate malezi ya baba pia kwa hiyo yeye anajitoa kafara kwa hilo.............

Baba hajitambulishi majukumu pekee ndio humtambulisha.. Teamo Ti
 
Last edited by a moderator:
wanaume niwepesi wa kupenda na ni wepesi wa kusahau penzi.wanawakw ni wagumu sana ktk kupemnda lakini na akisha kupenda ni ngumu sana kukutoa moyoni

engmtolera hapo ndipo kazi ilipo....................
 
Last edited by a moderator:
BADILI TABIA Bi jaji alivyokufa kwa kidume unafikiri ugali atamnyima kama siyo kumkabidhi waote aupangie matumizi aonavyo ili mradi kidume amkubali tu?

Kama jaji anamuhitaji jamaa na kamdondokea kwelikweli, sioni sababu ya kwa nini jamaa anasita kurudisha majeshi.
 
Last edited by a moderator:
Baba hajitambulishi majukumu pekee ndio humtambulisha.. Teamo Ti

[MENTION]LD[/MENTION] hivi kurudi kundini siyo kajitambulisha kimajukumu hapo? Mnataka afanye nini zaidi kama makosa amesamehewa na mla kuku kakumbuka utamu wa jogoo lake atakwa limuikie usiku kucha.........iko mbaya gani hapo?
 
Kama jaji anamuhitaji jamaa na kamdondokea kwelikweli, sioni sababu ya kwa nini jamaa anasita kurudisha majeshi.

Katavi kidume hasiti lakini anatafuta ushauri wangu na mimi naelekea kumshauri vivyo hivyo.................arudi tu wakaanzane upya upya,,,,,,,,,,,,,,,,,kwani kipya ni kinyemi ingawaje kidonda..........
 
Last edited by a moderator:
LD hivi kurudi kundini siyo kajitambulisha kimajukumu hapo? Mnataka afanye nini zaidi kama makosa amesamehewa na mla kuku kakumbuka utamu wa jogoo lake atakwa limuikie usiku kucha.........iko mbaya gani hapo?

Kwa kuwa tunatofautiana, kwa kuwa tuna mioyo tofauti. Kwa kuwa huyo mdada kaona hapo ndio mwisho wa mambo yote. Aende kwa amani. Ila mimi@Rutashubanyuma hata urudi na Ghorofa, miaka mitano? Yani hata mmoja nitajiuliza mara 70. Mmmh mwanaume au mwingine, hapana...Nooooooo.

Hapana kabisa labda kama sikukupenda Mwanzo. Yani nikupende nikupe moyo wangu, na damu yako nibebe, na mtoto wako nimlee miaka mitano. Afu uone nimefanikiwa ujilete lete......ha ha ha lazima utakuwa house boy wangu kama nitaamua kukurudisha walahi. Khaa yani miaka mitano?

Aku.....ulizaliwa peke yako au? Kwanza miaka mitano yote hiyo wengine hawajaniona? He he he anatafuta kazi ya house boy huyo. Halafu na huyo dada anajitafutia matatizo tu. WE KIBABA ka hicho unakileta ndani cha nini? SI kitakutesa balaa? Manake atatafuta kusikika hata mahali ambapo hatakiwi kusikika. Ohoooo unanidharau eeh zitakuwa nyingi umo ndani mpaka basi. Mwanaume wa kiafrika au mwingine? Tena usiombe awe mchagga au Mhaya.
 
Sawa tu, ikiwa mungu anasamehe kwanini sisi tusisameheane. Zimwi likujualo halikuli likakwisha, huyo itakuwa pia watoto wa mjini walishamuweza akaona bora arudie old is gold. Mimi sioni shida endapo wenyewe wameridhiana!

nakubali na nimekuheshimu,madame!i believe in second chance....na vinginevyo sisi wengine tusingekuwa tulivyo leo wala na tulio nao aisee!
 
Kipenda Roho hula Nyama Mbichi.... TRUE LOVE NEVER DIE unless Lovers DIE
 
Simply elewa kuwa being a parent means that you are a leader of a very sensitive pilar of any state. or nation and if you don't have a family or people that depend on you and trust you having faith in that you will protect guide and lead them then you don not have the qualities of leadership..being a leader means that we have entrusted our faith and dreams in you believing that you will show us the right way in achieving them...
Mwanzo wala sikuwa na nia ya kuchangia hapa, lakini kipengele hiki kimenigusa.

Kuongoza familia ya mpaka watu 10 na zaidi (kadirio la familia zetu) si sawa na kuongoza watu zaidi ya milioni 40; na wanaokusaidia kuongoza wengi wao hata si wajomba zako, kwa wingi watakuwa wapambe wako tu, ambapo zaidi ya asilimia 75 kati yao wapo kwa maslahi. Tunao mifano hai nchini petu - angalia kuanzia uhuru mpaka sasa, ikiwa kuwa na familia ni kigezo cha uongozi bora wa taifa, Tanzania tumesibiwa na nini?.

Uongozi ni karama, ni kuwa na msimamo, ni kutokuwa dhaifu - lol. Wapo viongozi wa nchi, taasisi na asasi ambao wamemudu kuziongoza vyema hizo lakini wameshindwa kuongoza familia zao, na kinyume chake. Bado tunang'ang'ania dhana ya kuwa na familia ndio kigezo cha mwanzo cha kupewa uongozi wa nchi?
 
Kimaslahi zaidi. Nimeipenda hii....siku akipigwa chini ujaji na ndoa itakuwa imemshinda maana atakuwa na ugali kidogo unaomfaa kula peke yake
 
Huu si ustaarabu hata kidogo! Anafuata pesa ya ujaji Na wala si MAPENZI, akija mwingine mwenye fedha zaidi atamwacha Na kufuata pesa mingi. Dunia hii kweli hadaa.
 
hehehehehe dar majamboz hayo bhana haya aangalie asije akahukumiwa kifungo cha maisha kwa kutelekeza mtoto....
 
Kwa upande wa ndoa,, ni jambo la heshima na hilo lipo sio kwa waafrika tu.. wanaosema kinyume ni wale tu ambao hawako ktk ndoa ama waliolazimisha wakakiona cha moto sasa wako nje.. (in other word WANAJIFARIJI jambo ambalo ni kawaida na ni sahihi kwa binadamu yeyote.. usipojifariji unajitakia magojwa ya moyo n.k.

Kwa huyu mamito anayeruana na jamaa kwa sababu mshiko umepaa mh!! kuna walakini hapo.. Huyo baba asijekuwa anafata pesa.. ila undani wa issue nina uhakika wanaijua wao!
 
hao zamani walikua wameoana aua ndio sasa bibi Mkubwa anataka harusi? yawezekana walikua wanaishi kinyumba sasa mwanamke ndio anataka harusi kama. ruta chezea pingu ya maisha wewe? kilichounganishwa na Mungu mwanadamu hawezi kukitenganisha. nahisi hao kabla walikua wanakaa kinyumba
 
Last edited by a moderator:
Kuna njemba m'moja wa karibu kanitonya leo hii asubuhi ya kuwa anajipanga upya kurejesha majeshi..........kwa mzazi mwenzie ambaye ana karibu miaka 5 tangia ampige kibuti..................utetezi wake ni kuwa hawakuachana kwa ubaya na yakuwa mwenzie sasa huo ugali wa ujaji ni mkubwa sana haipendezi akiula pekee yake......................

Jiingine adai ni sababu za kiubinadamu nazo zimemkalia kooni kwa kipindi hivi ya kuwa mwenzie amekuwa akimlilia kwenye simu kila siku ya kuwa aache kumnyanyasa kwa kumpiga kibuti kwa hiyo kumrudia atakuwa kaitika wito na......kumtendea ubinadamu aache kuwa na masimango ambayo kidume anahisi yanamletea tafurani hata yeye.........

lingine anadai haifai jaji aonekane ni kapera wakati mzazi mwenzie yupo ila ni harakati za pimbi tu ndizo zilimtia majaribuni........................

hii ni sahihi kweli???????????...............kurudia matapishi yako mwenyewe eti mkate umewiva na tumbo lina wakawaka kwa njaa....................sina uhakika kwenye hilo............Nisaidieni namna ya kumshauri kidume mwenye macheche nguli.......

Mkuu ndo maana mimi mtizamo wangu huwa ni huu: sema usemavyo lakini ukweli ni kwamba si rahisi kutenganisha mapenzi na pesa, iwe kwa mwanamke au mwanaume. Katika mahusiano pesa itabaki kuwa kivutio cha kwanza au cha pili, hayo mengine ni added advantage
 
Back
Top Bottom