Bi. Senti 50
JF-Expert Member
- Apr 17, 2007
- 290
- 12
Leo baada ya Lowassa kutoka kwenye Ukumbi na hasa baada ya maneno ya Dr. Mwakyembe ni wazi kuwa hawa ndugu zetu hawaaminiani tena. Chama chetu ambacho kimetulea na kutufikisha hapa; chama ambacho kilisikifika kwa umoja na mshikamano, leo hii kimejaa shuku na kebehi. Kuna wabunge hawakai sehemu moja na juzi kuna mahali tulikuwa na mbunge fulani wa kaskazini alipokuja mwenzie wa kusini kama kusabahi yule mwingine akatuaga haraka haraka kabla hajapokea mkono wa mbunge mwenzie.
Ndugu zangu hali ni mbaya ndani ya CCM. Hata maneno ya Chitalilo juzi hii kuhusu "kuvunja ndoa ya mtu" alikuwa anawalenga watu fulani fulani. Sijui CCM itakwenda wapi. Naomba wana CCM wenzangu tuwatake viongozi wetu kukaa chini pamoja na kumaliza tofauti zao ndani ya chama. Vinginevyo lile "lililotabiriwa" litatokea. Tusiwape wapinzani wetu nafasi ya kufurahi na wabaya wetu kushangilia.
Wale mnaofanya kazi maeneo ya Bungeni na wakeretwa tuwasiliane tuone jinsi gani tunaweza kuwasaidia wabunge wetu na kukiimarisha chama chetu. Tusiache wapinzani wavune wasichopanda. Kuna watu ambao wanapata sifa za bure tu kutokana na mapungufu ya chama chetu. Tusimame na sisi.
Asanteni.
Ndugu zangu hali ni mbaya ndani ya CCM. Hata maneno ya Chitalilo juzi hii kuhusu "kuvunja ndoa ya mtu" alikuwa anawalenga watu fulani fulani. Sijui CCM itakwenda wapi. Naomba wana CCM wenzangu tuwatake viongozi wetu kukaa chini pamoja na kumaliza tofauti zao ndani ya chama. Vinginevyo lile "lililotabiriwa" litatokea. Tusiwape wapinzani wetu nafasi ya kufurahi na wabaya wetu kushangilia.
Wale mnaofanya kazi maeneo ya Bungeni na wakeretwa tuwasiliane tuone jinsi gani tunaweza kuwasaidia wabunge wetu na kukiimarisha chama chetu. Tusiache wapinzani wavune wasichopanda. Kuna watu ambao wanapata sifa za bure tu kutokana na mapungufu ya chama chetu. Tusimame na sisi.
Asanteni.