Hawa watu ndio wameniacha hoi.

proton pump

JF-Expert Member
Apr 30, 2017
5,352
6,896
ffd8d648f4cadff704e900fdbe428114.jpg
Mimi ni mgeni katika mkoa mmojawapo hapa kanda ya ziwa sijachunguza vizuri jinsi hawa watu walivyo si unajua macho hayana pazia,nikaona demu mkalii yaan yupo vizuri chocolate mrefu mnene.si nikaanza kushuka verse demu akaingia kingi akaniahidi atakuja geto siku baada ya kesho kumbe NILIKUA NAOA KWA LAZIMA BILA KUJUA.demu ile siku ya verse alienda kusema na kuandaa jeshi la kunifumania ikafika siku ya game nikaanza kupinch kama kawaida baada ya dakika kadhaa nikasikia mlango unavunjwa huku yowe zikipigwa na kundi kubwa la watu yaan stimu ilikata ghafla kabla ya mlango kuvunjika nikaamriwa kufungua mlango mwenyewe ikanibidi nifungue. baada ya mlango kufunguka nikakalishwa chini ya ulinzi na demu akaletwa karibu yangu huku kajifunga taulo langu tu wazee wa kimila nao walihudhuria pale pamoja na wazazi wa yule demu walichokisema waliniambia kwamba kama hupendi kufungwa tunataka ng'ombe 17 na huyo ni mke wako kuanzia leo,sikuachiwa kwanza walianza kuingia ndani kusachi wakabahatisha stuff id huku wakitishia wataenda kusema kwa mwaajiri du nilisarenda. nikaanza kusumbua ndg na jamaa ili nisipoteze kazi nilikusanya kiasi cha sh 2000000 nikanunua ng'ombe 15 nikawapa hapo ndio ikawa ponea yangu sa ivi naishi na mke wangu na mpigisha kazi za mashambani balaa hadi arudishe hela yangu bila yeye kujua na unajua hili kabila wanavyojitahidi kwenye kazi..HII NI ONYO NA KWA WENGINE .
7957bc30b7cfdfe1f87a793a0176c0e2.jpg
 
Back
Top Bottom