Sangarara
JF-Expert Member
- Sep 29, 2011
- 13,100
- 5,649
Toka mheshimiwa rais apokee report ya pili ya mchanga wa dhahabu ni zaidi ya wiki imepita.
Baada ya kupokea report hiyo mheshimiwa Rais hakumung'unya maneno , alisema anakubaliana na mapendekezo yote ya Kamati na akaelekeza mamraka zote za serikali kila moja katika nafasi yake zishiriki katika kuyafanyia kazi mapendekezo hayo.
Hakuishia hapo, akaelekeza vyombo vya dola viwahoji wote waliotajwa katika report hiyo.
Ikumbukwe,wakati akipokea report ya kwanza katika hotuba yake alitoa maelezo ambayo yalimaanisha waziri wa nishat na madini hastahiri kuendelea kushikiria nafasi hiyo na masaa machache baadae Siku hiyo hiyo alimfuta kazi.
Waliotajwa katika report ile wanajulikana kwa majina na mmoja wao (karamagi) amekaririwa na vyombo vya habari akisema yuko tayari kutoa ushirikiano.
Sasa sielewi ni kwa nini hawajaanza kuhojiwa , na cha ajabu Ikulu,waziri wa sheria na katiba na waziri wa mambo ya ndani ghafla wamejikita kwenye hoja za watu ambao tunajua hawatahojiwa achilia mbali kwamba hawakutajwa kwenye report.
Hivi hata kumuita mmoja wao tu na kumwambia mnafikiria kumuhoji imekuwa shida?
Baada ya kupokea report hiyo mheshimiwa Rais hakumung'unya maneno , alisema anakubaliana na mapendekezo yote ya Kamati na akaelekeza mamraka zote za serikali kila moja katika nafasi yake zishiriki katika kuyafanyia kazi mapendekezo hayo.
Hakuishia hapo, akaelekeza vyombo vya dola viwahoji wote waliotajwa katika report hiyo.
Ikumbukwe,wakati akipokea report ya kwanza katika hotuba yake alitoa maelezo ambayo yalimaanisha waziri wa nishat na madini hastahiri kuendelea kushikiria nafasi hiyo na masaa machache baadae Siku hiyo hiyo alimfuta kazi.
Waliotajwa katika report ile wanajulikana kwa majina na mmoja wao (karamagi) amekaririwa na vyombo vya habari akisema yuko tayari kutoa ushirikiano.
Sasa sielewi ni kwa nini hawajaanza kuhojiwa , na cha ajabu Ikulu,waziri wa sheria na katiba na waziri wa mambo ya ndani ghafla wamejikita kwenye hoja za watu ambao tunajua hawatahojiwa achilia mbali kwamba hawakutajwa kwenye report.
Hivi hata kumuita mmoja wao tu na kumwambia mnafikiria kumuhoji imekuwa shida?