Hawa watoto wameweza kuishi kwenye Msitu wa Amazon kwa siku 40 bila chakula wala malazi

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Wanasema mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.

Hawa watoto wa wameweza kunusurika na mazingira hatarishi ya msitu mkubwa wa Amazon kwa siku 40 bila chakula wala malazi yoyote hadi walipopatikana leo kutoka kwenye kikosi cha waokoaji.

Watoto hao 4 walipotea mwanzoni mwa mwezi wa 5 baada ya ndege waliyokua wakisafiria kupata hitilafu ya injini na kuanguka kwenye msitu wa Amazon na kuua watu 3, rubani 2 na mama yao na hao watoto.

Baada ya jeshi la uokozi kufika eneo la tukio la ajali ya ndege wakakuta miili 3 lakini hakuna watoto, mtoto mkubwa ambae ni binti ana miaka 13 na mdogo kabisa ana mwaka 1.

Watoto hao ni jamii ya watu wa asili ya msitu wa Amazon. Hii ndio sababu inayosemekana kuchangia watoto hao kuweza kuishi siku 40 msituni kutokana na kujua mbinu za asili ya kuishi, survival skills toka wakiwa wadogo.

Watoto hao wamepatikana wakiwa wazima ila wenye afya iliyodhoofu hasa mkubwa wa miaka 13 ambae inadaiwa alikua akiwapa wadogo zake chakula chote wanachokipata wale kwanza kisha yeye anakula kitakachobaki.

Tukumbuke. Amazon imejaa nyoka wakubwa na wakali kama Anaconda, Chui wakali wanaoitwa Jaguar na mamba wakali pamoja na wale samaki wanaopiga shoti za umeme ukiingia kwenye himaya yao.

Je ikitokea ukajikuta kwenye mazingira magumu kama hayo can you survive?
 
Kutokuwa na hofu ndiyo sababu.

Ukishajaza tu nafsi yako hofu, hata ambayo hayakupasa kukupata yatakupata.

Ninatamani sana. Mwaka 2030 nikijaliwa Uhai, nitakuwa nastaafu kwa hiyari. Niende kwenye msitu wa Amazon. Niishi walau mwezi mmoja.
Kama unataka mafao yako wagombanie bila wewe kujulikana umetafunwa na mnyama gani nenda. Yapo mambo ya kuyapima,lakini si kila Jambo hata unaloliona wazi hatari yake. Kwa nini usitembelee tu Serengeti,mikumi,Ruaha au Amboni. Zote zipo kwa ajili yako.
 
Naam.

Nataka niwe mpya..niondoe uchafu wote niliouvaa katika dunia hii. Kuna makabila mawili natamani sana kuyafikia. Kuna kabila la Sentinelese na Awa.

Hawataki watu wa nje. Wanaua. Ila hata nikifia huko nitakufa kwa amani.

Napatamani mno.
Sentinelese Hawa usijaribu, wapo kisiwa nadhani ni India huko, Dunia ilishaweka makubaliano wawaache kama walivyo maana mki interact nao wanaweza kupata magonjwa na wakawa hawana Kinga wakafa, Hawa hawajawahi kujichanganya na Dunia tokea iumbwe, Kuna mzungu alikua anawashobokea sana Hawa watu akalazimisha kwenda wakamtia mshale wa shingo akafa!!! Dunia ilishaamua Hawa watu waachwe tu wenyewe
 
Sentinelese Hawa usijaribu, wapo kisiwa nadhani ni India huko, Dunia ilishaweka makubaliano wawaache kama walivyo maana mki interact nao wanaweza kupata magonjwa na wakawa hawana Kinga wakafa, Hawa hawajawahi kujichanganya na Dunia tokea iumbwe, Kuna mzungu alikua anawashobokea sana Hawa watu akalazimisha kwenda wakamtia mshale wa shingo akafa!!! Dunia ilishaamua Hawa watu waachwe tu wenyewe
Shukrani mkuu. Na uzee wangu ndo nafahamu leo. Imenibidi nigoogle. Sema mbona naona wazungu wanapiga nao picha?
 
Sentinelese Hawa usijaribu, wapo kisiwa nadhani ni India huko, Dunia ilishaweka makubaliano wawaache kama walivyo maana mki interact nao wanaweza kupata magonjwa na wakawa hawana Kinga wakafa, Hawa hawajawahi kujichanganya na Dunia tokea iumbwe, Kuna mzungu alikua anawashobokea sana Hawa watu akalazimisha kwenda wakamtia mshale wa shingo akafa!!! Dunia ilishaamua Hawa watu waachwe tu wenyewe
Uncontacted tribe kuna mzungu ameajiriwa na serikali kasi yake ni kupita na ndege kila baada ya muda kuwacheki tu lakini hairuhusiwi kuwasogelea jamaa anawacheki na binocular angani basi "seen is believing" Na haijulikani wanaishi vp lifestyle na serikali ikaona ni bora ibaki hivyohivyo kuliko kuwaingilia hiyo tribe ipo katikati ya msitu wa amazon na first footage ya camera ilishootiwa na bbc documentary inaitwa human planet episode ya forest
 
Uncontacted tribe kuna mzungu ameajiriwa na serikali kasi yake ni kupita na ndege kila baada ya muda kuwacheki tu lakini hairuhusiwi kuwasogelea jamaa anawacheki na binocular angani basi "seen is believing" Na haijulikani wanaishi vp lifestyle na serikali ikaona ni bora ibaki hivyohivyo kuliko kuwaingilia hiyo tribe ipo katikati ya msitu wa amazon na first footage ya camera ilishootiwa na bbc documentary inaitwa human planet episode ya forest
Jamaa vipi, Hawa wapo kisiwa Cha India mambo ya Amazon yametoka wapi tena?
 
Jamaa vipi, Hawa wapo kisiwa Cha India mambo ya Amazon yametoka wapi tena?
Me nawazungumzia "AWA TRIBE"
Screenshot_2023-06-11-08-27-14-544_com.chrome.beta.jpg
 
Back
Top Bottom