Hawa wanafunzi wa chuo kikuu wanafanya nini majumbani?

fenestra rotunda

JF-Expert Member
Jun 18, 2015
608
614
Nimekutana na baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma wa mwaka wa tatu kozi ya uuguzi na ukunga mtaani kwetu hali iliyonifanya kuuliza kulikoni wapo majumbani ilhali chuo chao kilishafunguliwa.

Wanadai hata hao hawaelewi kwani waliambiwa wataripoti mbeya kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo na sio Dodoma kwa kuwa hospitali ya Dodoma kuna msongamani wa wanafunzi hivyo wanashindwa kusoma kwa umakini.

Siku ja Jumatatu waliambiwa wanatakiwa kuripoti Mbeya siku ya Jumamosi ya tarehe 12 lakini mpaka sasa hawajaambiwa watafikia wapi, makazi yao, ratiba ya mafunzo kwa vitendo (clinical practice), usajili, kusaini boom N.k na siku yenyewe imekaribia.

Hata hivyo wamelalamika kuwa taarifa hiyo ilichelewa kuwafikia kwani ilikuja siku ya alhamis ya tarehe 3 huku baadhi wakiwa wameshatangulia Dodoma kwa ajili ya kuwa hi usajili ambao ulikuwa unaanza tarehe 5.
 
We are not hanging ourselves neither drinking poison.. Ccm front to front... Leave them read the numerous ennhhh.. Ccm front to front
Nimecheka sana kwa sababu ya hii tafsiri yako ya wimbo wa Kepteni Komba kwa kizungu!
 
Halafu wakiulizia lini wataendelea na mafunzo yao watapelekwa magereza kwa tuhuma za uchochezi, poleni sana sasa hapo ni muendelezo wa mafunzo figisu kibao wakimaliza hizo ajira si ndio takuwa shughuli pevu?!
 
Nimekutana na baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha dodoma wa mwaka wa tatu kozi ya uuguzi na ukunga mtaani kwetu hali iliyonifanya kuuliza kulikoni wapo majumbani ilhali chuo chao kilishafunguliwa..wanadai hata hao hawaelewi kwani waliambiwa wataripoti mbeya kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo na sio dodoma kwa kuwa hospitali ya dodoma kuna msongamani wa wanafunzi hivyo wanashindwa kusoma kwa umakini.siku ja jumatatu waliambiwa wanatakiwa kuripoti mbeya siku ya jumamosi ya tarehe 12 lakini mpaka sasa hawajaambiwa watafikia wapi,makazi yao,ratiba ya mafunzo kwa vitendo(clinical practice),usajili,kusain boom N.k na siku yenyewe imekaribia.
Hata hivyo wamelalamika kuwa taarifa hiyo ilichelewa kuwafikia kwani ilikuja siku ya alhamis ya tarehe 3 huku baadhi wakiwa wameshatangulia dodoma kwa ajili ya kuwa hi usajili ambao ulikuwa unaanza tarehe 5.
Msomi hukutakiwa kuwa.kunguru kiasi hiki.

Je ungesema haya kwamba uummoja wa waathirika wa jambo hili ungekufa?
 
Back
Top Bottom