VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Kwa ngazi zote za Urais, Ubunge na Udiwani. Kama chama tawala kinachoomba ridhaa ya miaka mitano mingine, tukeshe tukiomba kuwa hawa wafuatao wasiende kupiga kura Oktoba 28 mwaka huu. Wakienda na wakipiga kura, CCM hatutakuwa na chetu. Watapiga kura za uchungu na kuukataa uchungu zaidi. Zitakuwa kura za kuponya mioyo yao kwakuwa watakuwa wametoa maumivu yao kupitia kukataa.
Hawa wakienda kupiga kura, CCM lazima ije na mbinu mbadala kuliko daladala. Wataikataa CCM na wagombea wake mchana peupe. Wataikataa CCM na wagombea wake kwa kutumia kadi zao za kupigia kura, kwenda kwao kupiga kura. CCM itakataliwa kwa maumivu yaliyotokana na matendo na maneno ya Serikali iliyoundwa nao. Nawataja wa uchache watu hao ambao kama CCM tunapaswa kukesha tukiomba wasiende kupiga kura.
Waliobomolewa nyumba na biashara zao bila kulipwa fidia pamoja na ndugu, jamaa na marafiki zao; waliofukuzwa kazi kwa sakata la vyeti bila kupewa hata sumni pamoja na kufanya kazi kwa miongo kadhaa pamoja na ndugu, jamaa na marafiki zao; waliopatwa na majanga ya asili bila kupata msaada wa kiserikali pamoja na ndugu, jamaa na marafiki zao; waliofungiwa biashara na shughuli zao za kiuchumi kwa njia za kibabe pamoja na wategemezi wao.
Na wote ambao wameoisoma namba kwa namna moja au nyingine!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kagera, Tanzania)
Hawa wakienda kupiga kura, CCM lazima ije na mbinu mbadala kuliko daladala. Wataikataa CCM na wagombea wake mchana peupe. Wataikataa CCM na wagombea wake kwa kutumia kadi zao za kupigia kura, kwenda kwao kupiga kura. CCM itakataliwa kwa maumivu yaliyotokana na matendo na maneno ya Serikali iliyoundwa nao. Nawataja wa uchache watu hao ambao kama CCM tunapaswa kukesha tukiomba wasiende kupiga kura.
Waliobomolewa nyumba na biashara zao bila kulipwa fidia pamoja na ndugu, jamaa na marafiki zao; waliofukuzwa kazi kwa sakata la vyeti bila kupewa hata sumni pamoja na kufanya kazi kwa miongo kadhaa pamoja na ndugu, jamaa na marafiki zao; waliopatwa na majanga ya asili bila kupata msaada wa kiserikali pamoja na ndugu, jamaa na marafiki zao; waliofungiwa biashara na shughuli zao za kiuchumi kwa njia za kibabe pamoja na wategemezi wao.
Na wote ambao wameoisoma namba kwa namna moja au nyingine!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kagera, Tanzania)