hawa ndiyo tuliowakabadhi kutuamulii hatima yetu

cencer09

JF-Expert Member
Oct 19, 2012
3,622
1,751
Unakumbuka wakati Tibaigana akiwa kamanda wa polisi wa mkoa wa Dae es salaam,wa mkuu wa mkoa akiwa Mzee Makamba?
Wakiwa wakuu wa kamati ya ulizni ya mkoa wa Dar es salaam kwangu mimi bado naita kituko pale walipopiga marufuku magari ya abiria yanayotoa huduma ya usafiri mkoani kusimamisha abiria.Yaani mjidcm ule watu wakae tu kwenye viti kama vile wanaenda Lushoto

Na ule mjibasi wa semitrailer uliosemekana ni wa mdau Mwaibula ambao ulikuwa ukipita kituoni habaki abiria nao wakaupiga marufuku usisimamishe abiria.madai yao nisheria,hivi nimji wapi hata huko walikoendelea ambako wasafiri wa mjini hawashiki bomba kwa maana ya kusimama kwenye usafiri?

Unakumbuka jinsi wananchi walivyopata shida ya usafiri wakati wao wakitembealea Landcruiser?na baadae akaja kuwa katibu wa chamakinachotawala Tanzania ungetegemea nini hapo.

Waziri mkuu alikuwa Sumaye ambaye bado anataka uongoze na wakati ule alikaa kimya wakati watanzania tukiteseka na uongozi mbovu usiozingatia maslahi wa wananchi.

Unakumbuka wakati Sumaye akiwa waziri mkuu alipolazimisha vizibiti mwendo kwenye mabasi?hata mabasi ya daladala na akalazimisha hata kuyazuia yasitoe huduma licha ya kuweko na shutuma za rushwa kwa kampuni moja kupewa tenda ya kuzisambaza nchini.kwa foleni hii ya Dar kizibiti mwendo cha nini?wizi mtupu.

Je unakumbuka kamanda mmoja wa uslama barabarani wakati akijitahidi kuelezea kwa nini wanayazuia mabasiyanayotumia chasis za malori yasitoe huduma? Mara engine zake zinakuwa zina nguvusana kwa sababu zimetengenezwa kwa ajili ya kubeba mizigo mikubwa, mara yanakimbia sana, mara position ya dereva inamfanya asiweze kulimudu, nikiwa mdogo kule moshi mabasi yaliyotengenezwa kwa namna hiyo yalikuwa yanaitwa kichwa ya ng'ombe na yamefanya kazi kwaufanisi mkubwa.

Nilimsikia Juha mwingine akisema eti gharama zinakuwa chini sana kupata,sasa badala ya kuaplaud viongozi wanakasirika wanatoa sababu za kijinga. BUSY POLITICAL ENGINEERS.

kumbe janja yao leo hii tetesi zinasema karibu viongozi wengi wakubwa wamejiingiza kwenye biashara ya mabasi kwa hiyo walikuwa wnasafisha uwanja kwa kutumia hata polisi wa usalama barabarani ambao kama kawaida bila kutumia akili wao hujitosa kichwa kichwa.

Viongozi hawa tena wengine bado wanaona watanzania ni mabwegenazi wanataka kurudi kwenye uongozi kuna walichosahahau? Angalia walivyoingiza watoto wao kwarushwa kwenye chaguzi za jumuia za chama chao ili waje wawarithishe.

swali nawauliza watanzania umeshapita oysterbay Masaki,Mbezi beach na kwingineko wanakokaa wala nchi ukakuta mashina ya wakereketwa wa ccm?au umeishamsikia mathalaniridh Kikwete,nanihii Lowassa au ..Pinda,...Ndugai wanashinda au wana matawi ya wakereketwa wanapokaa?

Jibu ni hapana yako uswahilini kwa wenye shida ambao wanahongwa senti ambazo baba zao wametuibia muwachague waingie madarakani waendeleze wizi wa wazazi wao,Wao wanaokula hawakereketwi wewe mwenye shidaunayehongwa msimu wa uchaguzi hadi msimu wa uchaguziunakereketwa na nini?

Wewe usiokula unajuaje utamu wake hadi ukereketwe?MENTAL CASE FOR GODSAKE
HAWA WATOTO WA MAFISADI WALIOJIPENYEZA KWENYE UONGOZI WANAJUA KABISA KWAMBA HAWA NI WAJINGA AMBAO WAZAZI WAO WAMEWATUMIAILI KUWA JUU,NA WAO WANAWATUMIA NA HAWAKEREKERWI KWA SABABU WAJUA NI ZUGA TU YA KUPATA NAFASI YA ULAJI.

Wewemjinga wa uswahili AMKA ujitambue,wakati wa ukombozi ni huu jitayarishe 2015
 
Kwel nakubali sasa watu wanazid kuona mbali, unajua hata adui yako wakat anakupa sumu anakuw anacheka saana na ww akijifana mwena,subiria akuone unakata roho...
Ni kwel ulio sema ndugu na niwakat wa wa tz kujisahihisha pale tulipo kosea,anza kujitazama ww kwanz hali yako ya maisha na ya mwenzio, tena wakat mwngine hana hata elimu na uwezo kama wako lakin ana magari zaidi ya mia 350 na filling stations za ajabu!
NISIPATE UKICHAA NGOJA NI LALE..
 
Back
Top Bottom