Hawa ndio wanaopaswa kufunga mipaka ya nchi?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Mpaka wa namanga ulifungwa kwa tangazo la mtumishi kutoka wizara ya afya

Holili akafunga RC Kilimanjaro na Kuacha Rongai na Tarakea wazi.

Horohoro Tanga kafunga Rc Tanga

Sirari Mara bado hatujajua atafunga Nani.

Hii mipaka yote ni Kati ya Tanzania na Kenya, waliofunga kila mtu alitoa maelezo amefunga Nini na Nini kinaruhusiwa.

Wafungaji wa mipaka wote kinadharia au kwa ufahamu wao au kwa namna walivyotoa matangazo ni kana kwamba mipaka hii siyo ya nchi Bali Ni mipaka ya mkoa, mfano RC Tanga anaeleza katika taarifa yake kwamba asilimia 90 ya wakenya wanategemea bidhaa kutoka Tanzania.

Kwa aliyefika horohoro ataelewa RC alimaanisha mzunguko wa biashara mpakani unawategemea zaidi wakenya kuja kununua kwa 90% hivyo mchango wa manunuzi ya Watanzania mpakani hapo ni 10%. Means tumewaambia wafanyabiashara wa Tanzania wajiandae kufanya biashara na 10% ya wateja wao huku tukiwaambia 90% ya wateja watafute bidhaa kutoka nchini mwao.

Katika mkutadha huu, Ni ipi nafasi ya wizara na Mawaziri kwenye mipaka yetu? Mamlaka ya kufunga mpaka wa nchi kisheria ipo kwa Nani?

Wakulima waliovuna watauza wapi mazao yao Kama tumewadhibiti wanunuzi kwa 90%

Hatuoni kwamba tunawaambia wakenya kisaikolojia kutoitegemea Tanzania na kutafuta soko jipya?
 
Nafikiri jambo baya lililokuwa likifanyika tangia hapo awali ilikuwa ni kutaja nchi wanazotoka watu wanaopimwa na kukutwa na corona, hili lilikuwa jambo baya sana, kwasababu pamoja na juhudi ambazo serikali ya nchi husika inayotajwa itakazozichukua katika kunusuru watu wake bado itaendelea kuchafuliwa na nchi nyingine.

Wewe unapambana kudhibiti ndani na kuhakikisha hakuna panic, mwenzako wa nchi jirani kutwa anakurusha hewani, wagonjwa 20 kutoka Tanzania, wagonjwa 17 kutoka Tanzania, wagonjwa 5 kutoka Tanzania. Kwani ungesema raia 20 ni wa kigeni, ungepungukiwa na nini? Ni mwendo wa kutunishiana misuli sasa.
 
Waziri wa afya anatangaza kufunga mpaka wa nchi lakini haruhusiwi kutangaza idadi ya waliambukizwa corona!
 
Wana watangazia vile Viongozi wetu hawataki kutanganza
Nafikiri jambo baya lililokuwa likifanyika tangia hapo awali ilikuwa ni kutaja nchi wanazotoka watu wanaopimwa na kukutwa na corona, hili lilikuwa jambo baya sana, kwasababu pamoja na juhudi ambazo serikali ya nchi husika inayotajwa itakazozichukua katika kunusuru watu wake bado itaendelea kuchafuliwa na nchi nyingine.

Wewe unapambana kudhibiti ndani na kuhakikisha hakuna panic, mwenzako wa nchi jirani kutwa anakurusha hewani, wagonjwa 20 kutoka Tanzania, wagonjwa 17 kutoka Tanzania, wagonjwa 5 kutoka Tanzania. Kwani ungesema raia 20 ni wa kigeni, ungepungukiwa na nini? Ni mwendo wa kutunishiana misuli sasa.

Dark Side
 
Waziri wa afya anatangaza kufunga mpaka wa nchi lakini haruhusiwi kutangaza idadi ya waliambukizwa corona!
Hakuna sehemu waziri wa Afya alitangaza kufunga mipaka, Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ndiye aliyetoa tamko la kufunga mpaka sasa baadhiyenu kwa mihemko mka mfananisha na wazir wa Afya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wa Africa bado Sanaa. Nilipomsikiliza kenyata nilijua kuwa wa Africa bado tuko hovyo. Alionyesha kabisa Tanzania na Somalia ndo nchi zenye korona Sanaa kati ya majirani wake wote. Kwahiyo tusubiri mchezo huu tuone mwisho wake.
 
Corona imepiga kambi kwa muda mrefu
La muhimu ni kuishi kwa amani tu maana huyu mdudu sio wa kufa leo wala kesho
Tutamzoea tu na hakuna ujanja
Mfunge msifunge yupo tu


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom