Hawa ndio wakuu wa nchi na wala nchi

Lucchese DeCavalcante

JF-Expert Member
Jan 10, 2009
5,471
733
DSC_1991.JPG
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefungua Bunge la Kumi leo kwa kuelezea vipaumbele kumi na tatu vya kipindi cha pili cha serikali yake ya awamu ya nne kama ifuatavyo;


Vipaumbele 13



Mheshimiwa Spika,


Kwa ajili ya hiyo basi, Serikali nitakayoiunda siku chache zijazo itakuwa na vipaumbele 13 vifuatavyo:


1. Kuhakikisha kwamba nchi yetu inaendelea kuwa yenye umoja, amani na usalama, na Muungano wetu unaendelea kudumu na kuimarika;
2. Kuendeleza juhudi za kukuza uchumi na kupunguza umaskini nchini kwa kuchukua hatua thabiti za kuharakisha mapinduzi ya kilimo, ufugaji, uvuvi na viwanda. Aidha, tuboreshe mazingira ya uwekezaji na biashara nchini ili tuvutie wawekezaji wengi wa ndani na nje kuwekeza katika sekta mbalimbali;


3. Kuongeza jitihada za kuwawezesha kiuchumi wananchi wa makundi yote ili waweze kushiriki na kunufaika na uchumi wetu unaokua. Tuboreshe mipango iliyopo ya kusaidia wajasiriamali wadogo na wote wanaotaka kujiajiri. Aidha, tuweke mipango thabiti ya kuwatambua na kuwawezesha wajasiriamali wa tabaka la kati ili wastawi na waweze kushiriki katika uwekezaji mkubwa ndani na hata nje ya nchi yetu;


4. Kuendelea kujenga na kuimarisha sekta binafsi nchini na kutengeneza mazingira mazuri zaidi ya ushirikiano na sekta ya umma. Aidha, tuimarishe uwezo wa Serikali kupanga mipango ya maendeleo na kusimamia utekelezaji wake bila kuingilia isivyostahili shughuli za sekta binafsi;


5. Kutumia fursa ya kijiografia ya nchi yetu na kuifanya Tanzania kuwa lango kuu la biashara na usafirishaji kwa nchi za Afrika ya Mashariki na Kati. Kwa ajili hiyo hatuna budi kuboresha miundombinu ya barabara, reli, bandari, viwanja vya ndege na teknohama. Aidha, tuongeze ufanisi katika utendaji na utoaji wa huduma wa miundombinu hiyo;


6. Kuongeza jitihada za kuhakikisha Taifa letu linanufaika zaidi na maliasili zake zilizopo juu na chini ya ardhi. Tutahakikisha kuwa tunazo sera na sheria za uvunaji na matumizi ya rasilimali hizo zinazonufaisha taifa letu sawia;
7. Kuboresha zaidi ukusanyaji wa mapato ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa pamoja na kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za umma;


8. Kuendeleza juhudi za kupanua fursa za elimu kwa vijana wetu tangu elimu ya awali, msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu. Aidha, tutoe msukumo na kipaumbele maalum kwa masomo ya sayansi katika ngazi zote. Pia, tuweke mkazo maalum wa kuboresha elimu ya msingi na sekondari ambazo kwa sasa zinakabiliwa na changamoto nyingi;

9. Kuongeza jitihada za kupanua na kuboresha huduma muhimu za kiuchumi na kijamii hususan afya, maji, umeme, barabara, reli, bandari, anga, simu, teknohama na huduma za fedha;


10. Kuimarisha utawala bora, demokrasia, utawala wa sheria, haki za binadamu na kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya rushwa, dawa za kulevya, matumizi mabaya ya madaraka na ubadhirifu wa mali ya umma. Kwa ajili hiyo tutaendelea kuvijenga na kuviwezesha kirasilimali, kimuundo na kisheria vyombo vinavyoongoza mapambano hayo na vile vya kutoa na kusimamia haki nchini;


11. Kuendelea kuimarisha uhusiano mzuri uliyopo baina ya nchi yetu na majirani zetu pamoja na mataifa mengine duniani na mashirika ya kimataifa. Aidha, tutaendelea kutafuta marafiki wapya na kuboresha diplomasia ya uchumi kwa manufaa ya nchi yetu;


12. Kuongeza maradufu juhudi za kuhifadhi mazingira hasa wakati huu ambapo makali ya athari za mabadiliko ya tabia nchi yanazidi kutuumiza sote; na


13. Kulinda mafanikio tuliyoyapata katika kipindi cha miaka mitano iliyopita pamoja na yale ya tangu uhuru mpaka sasa. Aidha, tukamilishe yale tuliyoyaahidi mwaka 2005 ambayo hatukuweza kuyakamilisha.


 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefungua Bunge la Kumi leo kwa kuelezea vipaumbele kumi na tatu vya kipindi cha pili cha serikali yake ya awamu ya nne kama ifuatavyo;


Vipaumbele 13



Mheshimiwa Spika,


Kwa ajili ya hiyo basi, Serikali nitakayoiunda siku chache zijazo itakuwa na vipaumbele 13 vifuatavyo:


1. Kuhakikisha kwamba nchi yetu inaendelea kuwa yenye umoja, amani na usalama, na Muungano wetu unaendelea kudumu na kuimarika;
2. Kuendeleza juhudi za kukuza uchumi na kupunguza umaskini nchini kwa kuchukua hatua thabiti za kuharakisha mapinduzi ya kilimo, ufugaji, uvuvi na viwanda. Aidha, tuboreshe mazingira ya uwekezaji na biashara nchini ili tuvutie wawekezaji wengi wa ndani na nje kuwekeza katika sekta mbalimbali;


3. Kuongeza jitihada za kuwawezesha kiuchumi wananchi wa makundi yote ili waweze kushiriki na kunufaika na uchumi wetu unaokua. Tuboreshe mipango iliyopo ya kusaidia wajasiriamali wadogo na wote wanaotaka kujiajiri. Aidha, tuweke mipango thabiti ya kuwatambua na kuwawezesha wajasiriamali wa tabaka la kati ili wastawi na waweze kushiriki katika uwekezaji mkubwa ndani na hata nje ya nchi yetu;


4. Kuendelea kujenga na kuimarisha sekta binafsi nchini na kutengeneza mazingira mazuri zaidi ya ushirikiano na sekta ya umma. Aidha, tuimarishe uwezo wa Serikali kupanga mipango ya maendeleo na kusimamia utekelezaji wake bila kuingilia isivyostahili shughuli za sekta binafsi;


5. Kutumia fursa ya kijiografia ya nchi yetu na kuifanya Tanzania kuwa lango kuu la biashara na usafirishaji kwa nchi za Afrika ya Mashariki na Kati. Kwa ajili hiyo hatuna budi kuboresha miundombinu ya barabara, reli, bandari, viwanja vya ndege na teknohama. Aidha, tuongeze ufanisi katika utendaji na utoaji wa huduma wa miundombinu hiyo;


6. Kuongeza jitihada za kuhakikisha Taifa letu linanufaika zaidi na maliasili zake zilizopo juu na chini ya ardhi. Tutahakikisha kuwa tunazo sera na sheria za uvunaji na matumizi ya rasilimali hizo zinazonufaisha taifa letu sawia;
7. Kuboresha zaidi ukusanyaji wa mapato ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa pamoja na kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za umma;


8. Kuendeleza juhudi za kupanua fursa za elimu kwa vijana wetu tangu elimu ya awali, msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu. Aidha, tutoe msukumo na kipaumbele maalum kwa masomo ya sayansi katika ngazi zote. Pia, tuweke mkazo maalum wa kuboresha elimu ya msingi na sekondari ambazo kwa sasa zinakabiliwa na changamoto nyingi;

9. Kuongeza jitihada za kupanua na kuboresha huduma muhimu za kiuchumi na kijamii hususan afya, maji, umeme, barabara, reli, bandari, anga, simu, teknohama na huduma za fedha;


10. Kuimarisha utawala bora, demokrasia, utawala wa sheria, haki za binadamu na kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya rushwa, dawa za kulevya, matumizi mabaya ya madaraka na ubadhirifu wa mali ya umma. Kwa ajili hiyo tutaendelea kuvijenga na kuviwezesha kirasilimali, kimuundo na kisheria vyombo vinavyoongoza mapambano hayo na vile vya kutoa na kusimamia haki nchini;


11. Kuendelea kuimarisha uhusiano mzuri uliyopo baina ya nchi yetu na majirani zetu pamoja na mataifa mengine duniani na mashirika ya kimataifa. Aidha, tutaendelea kutafuta marafiki wapya na kuboresha diplomasia ya uchumi kwa manufaa ya nchi yetu;


12. Kuongeza maradufu juhudi za kuhifadhi mazingira hasa wakati huu ambapo makali ya athari za mabadiliko ya tabia nchi yanazidi kutuumiza sote; na


13. Kulinda mafanikio tuliyoyapata katika kipindi cha miaka mitano iliyopita pamoja na yale ya tangu uhuru mpaka sasa. Aidha, tukamilishe yale tuliyoyaahidi mwaka 2005 ambayo hatukuweza kuyakamilisha.

Kusomea watanzania tu, hilo anaweza. Hata ungemweka rostam azizi angeweza kutusomea. Kwangu JK hana jipya zaidi ya Olds is cold.
 
99
Udini uko wazi 5 kati ya viongozi 6 wakuu wa serikali ni waislamu

Serikali ni Bunge ( Mkuu wake ni Anna- Mkristo . Tena hapa naibu mkristo, katibu wa bunge Thomas MKRISTO), Mahakama ( Mkuu wake ni Agustino- Mkristo) na Executive ( Jakaya- Muislamu). Hivyo udini uko wapi hapa? acheni hizooooooo!
 
Tanzania Hamna udini lakini hapo 83.3% ya viiongozi wa juu ni wa ki-i...m. Ni mtazamo wangu tu!

Jaribu kuangalia picha ya Hayati Mwalimu Nyerere pale juu ya Maalim na Bilal, mimi naona kama picha hile inaonesha kupigwa na butwaa vile kwa hao jamaa kuwa viongozi wa nchi hii.

DSC_1991.JPG
 
Hawa wenzetu waislamu ni washari sana, ingekuwa hapo ni 5 kristo, 1 muislamu, nakuambia misikiti yote ingepiga makelele, kwa hiyo tunamwomba huyo muheshimiwa sana kwa jina la Kikwete hakae kimwa kama maji ya mtungi linapokuja kwenye suala la udini, kwani aliprove failure tokea anaanza awamu yake ya kwanza ya uraisi. Yeye ashukuru Mungu kwamba wakristo wa nchi hii wanahofu na Mungu na wanamuombea yeye na serikali yake pamoja na kwamba wanajua ya kuwa CCM ni mabwingwa wa kuchakachua na kudhulumu. Hakika hukumu ya CCM inakuja, na anguko lao litakuwa anguko kuu, natamani sana niwe shuhuda wa hilo anguko.
 
Udini uko wazi 5 kati ya viongozi 6 wakuu wa serikali ni waislamu

Usihesabu kwa kuchanganya nyanya na ndimu au hesabu mgogoro????????
Zanzibar ni nchi yenye waislam kwa 97% na wasiowaislam ni wahamiaji wachache ambao hawakubaliki kisiasa sasa unategemea miujiza gani ya kuwepo kwenye serikali. by the way hawa wamechaguliwa na hawajaajiriwa. Mada ya udini hamjaielewa wengi wenu kama wewe kazi mnayo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
haya sasa kazi kwako seif sharif oh nataka kuongoza umepewa sasa uongozi ongoza tuone...
 
jaribu kuangalia picha ya hayati mwalimu nyerere pale juu ya maalim na bilal, mimi naona kama picha hile inaonesha kupigwa na butwaa vile kwa hao jamaa kuwa viongozi wa nchi hii.

dsc_1991.jpg

kweli kabisa halafu na wao wamekaa tu kama hawaioni vile?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom