Hawa ndio binadamu, kuwaweza huwawezi

Freed Freed

JF-Expert Member
Jun 27, 2017
6,224
6,468
Binadamu tuna mengi ya kutosha, tena sana.
1. Ukiwa mkimya watakuita zoba, mshamba.

2. Ukiwa huna hela watakutenga, ukiwa tajiri watakuchukia na kukuzushia mengi juu ya utajiri wako.

3. Ukiwa mcheshi utawakera na kukuita mjuaji.

4. Ukiwa na mume/mke watafuatilia maisha yenu ya ndani. Ukiwa na mahusiano yoyote watafuatilia wajue yanayoendelea hata kumnyakua mtu wako kama vipi. Ukiolewa/kuoa au usipooa au kuolewa uuuuuuuiiiiii kwao ni maneno tu

5. Ukijibana au ukijiachia sana ktk bajeti yako wao ni maneno tu hawakosi cha kusema.

6. Ukivaa vizuri, ukiwa simple duuuuuuihhh, hao wataongea.

7. Uwe mkali au mkarimu. Hao watababwabwaja tu.

Nanyi bila shaka mna mengi yetu binadamu ...
 
Back
Top Bottom