BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Jeetu Patel, Manji wawatikisa wabunge
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
16/Jan/2010
VITA ya kibiashara kati wafanyabiashara maarufu nchini, Yusuph Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kama Jeetu Patel, inayotokana na zabuni ya kuingiza matrekta ya mpango wa Kilimo ya Kwanza, jana iliitikisa kamati ya Bunge ya Kilimo, Chakula na Mifugo.
Zabuni hiyo ya kuingiza matrekta 1,000 yenye thamani ya zaidi ya Sh50 bilioni iliibua mjadala mzito katika kikao hicho na kumlazimisha mwenyekiti wa kamati hiyo kutumia mamlaka yake kuuzima.
Tayari kumeibuka hisia nyingi kuhusu zabuni hiyo iliyoingiza wafanyabiashara hao wenye asili ya Kiasia katika mgogoro mkubwa, huku ikielezwa kuwa Ikulu imeingilia kati baada ya Rais Jakaya Kikwete, kusitushwa na taarifa hizo.
Jana wabunge wa kamati hiyo waliibua upya sataka hilo baada ya kumbana Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, David Mathayo atoe kauli kuhusu mgogoro huo.
Mbunge wa Chambani (CUF), Hemed Salim Hamis alikuwa wa kwanza kuibua sakata hilo baada ya kumtaka Mathayo aeleze mgogoro kati ya wafanyabiashara hao wakubwa.
Hamisi hakuwataja kwa majina wafanyabiashara hao. Alihoji: "Swali la nyongeza liko katika matrekta 1,000 yanayopaswa kuingizwa na sekta binafsi. Kuna taarifa za mgogoro wa zabuni kati ya wafanyabiashara wawili wakubwa, mfanyabiashara Y na X sitaki kutaja majina yao wanajulikana, je unaweza kueleza kamati ukweli ni upi?"
Baada ya swali hilo Waziri Mathayo alionekana kushusha pumzi na kusema: "Eheee!...Huo mgogoro unashughulikiwa kati ya Wizara na SUMA JKT ambao ndiyo walihusika moja kwa moja na zabuni."
Hata hivyo, Hamis alimwuliza tena naibu waziri huyo akisema: "Ina maana, wizara ya Kilimo haihusiki?"
Mathayo alifafanua kwa kukiri nafasi ya wizara yake katika mchakato huo, lakini akasisitiza kwamba mambo ya zabuni hiyo kwa kuwa yanahusu fedha nyingi zaidi, yanashughulikiwa na hazina na SUMA JKT.
Naibu waziri huyo, ambaye aliongozana na wataalamu mbalimbali wa wizara alisema, wazo la SUMA JKT kutaka kuwa sehemu ya uingizaji huo matrekta hayo kwa kutumia Mfuko wa Pembejeo, lilikuwa zuri.
"Wenzetu SUMA JKT walikuja na wazo zuri kutaka wasaidiane na taasisi nyingine kuingiza matrekta kupitia mfuko wetu wa pembejeo. Tulikubali kwa kuwa ni wazo zuri na kwamba yangekuwa yakiunganishwa Nyumbu," alitetea Suma JKT.
Hata hivyo, mbunge wa Ubungo ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Kilimo katika serikali ya awamu ya tatu, Charles Keenja alizidi kupigilia msumari baada ya kuhoji "kwanini fedha hizi zichukuliwe na kuingizwa tu katika jeshi.
"Huku ni kuishi kwa matumaini tu, kuamini Nyumbu wanaweza kuunganisha matrekta yote 1,000 wakati ukiangalia uwezo wao wa vitendeakazi si mkubwa. Kwanini msipeleke TAMCO (Kibaha) ambao wana uwezo mkubwa?"
Lakini, Mathayo alijaribu kutetea akisema si tu kwamba serikali imechukua fedha hizo na kuziiingiza jeshini kwa kuwa SUMA JKT pia imekuwa ikishiriki hata katika mradi wa kuingiza mbegu bora.
Bado baada ya majibu hayo, Keenja alinyoosha tena mkono na kutaka kuendelea kumbana Mathayo, ndipo mwenyekiti wa kamati hiyo, Gideon Cheyo, alipozima mjadala akisema utajadiliwa zaidi mbele.
"Inatosha, nafikiri tutajadili zaidi mbele ya safari. Hili ni suala ambalo ni pana tutalijadili tu waheshimiwa, kwa sasa tuendelee na mengine," alifafanua Cheyo.
Awali, Hamis alitaka kujua idadi ya matrekta ambayo yataingizwa nchini kuanzia ngazi zote ikiwemo katika halmashauri mbalimbali za wilaya kwa ajili ya Kilimo Kwanza.
Waziri Mathayo, ambaye alikuwa akiwasilisha Taarifa ya Mpango na Utekelezaji wa Bajeti kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2009, alisema jumla ya matrekta madogo (power tillers) yanayotarajiwa kuingizwa katika halmashauri ni 1,628, makubwa 28, wakati kati ya hayo 1,000 ndiyo hayo yatakayoingizwa na sekta binafsi, 400 mkopo kutoka Benki ya Exim India.
Kuhusu upotevu wa vipuri kwa baadhi ya matrekta, alisema hilo linafanyiwa kazi na kuongeza kwamba, wiki moja ijayo kutakuwa na mkutano mkuu wa wadau ambao jambo hilo litazungumzwa kwa kina.
Mgogoro wa Manji na Jeetu umekuwa ukichukua sura mpya kila kukicha. Tayari Manji aliwahi kunukuliwa akisema anajiandaa kuweka wazi jinsi Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004, ilivyokiukwa wakati wa mchakato wa utoaji zabuni hiyo.
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
16/Jan/2010
VITA ya kibiashara kati wafanyabiashara maarufu nchini, Yusuph Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kama Jeetu Patel, inayotokana na zabuni ya kuingiza matrekta ya mpango wa Kilimo ya Kwanza, jana iliitikisa kamati ya Bunge ya Kilimo, Chakula na Mifugo.
Zabuni hiyo ya kuingiza matrekta 1,000 yenye thamani ya zaidi ya Sh50 bilioni iliibua mjadala mzito katika kikao hicho na kumlazimisha mwenyekiti wa kamati hiyo kutumia mamlaka yake kuuzima.
Tayari kumeibuka hisia nyingi kuhusu zabuni hiyo iliyoingiza wafanyabiashara hao wenye asili ya Kiasia katika mgogoro mkubwa, huku ikielezwa kuwa Ikulu imeingilia kati baada ya Rais Jakaya Kikwete, kusitushwa na taarifa hizo.
Jana wabunge wa kamati hiyo waliibua upya sataka hilo baada ya kumbana Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, David Mathayo atoe kauli kuhusu mgogoro huo.
Mbunge wa Chambani (CUF), Hemed Salim Hamis alikuwa wa kwanza kuibua sakata hilo baada ya kumtaka Mathayo aeleze mgogoro kati ya wafanyabiashara hao wakubwa.
Hamisi hakuwataja kwa majina wafanyabiashara hao. Alihoji: "Swali la nyongeza liko katika matrekta 1,000 yanayopaswa kuingizwa na sekta binafsi. Kuna taarifa za mgogoro wa zabuni kati ya wafanyabiashara wawili wakubwa, mfanyabiashara Y na X sitaki kutaja majina yao wanajulikana, je unaweza kueleza kamati ukweli ni upi?"
Baada ya swali hilo Waziri Mathayo alionekana kushusha pumzi na kusema: "Eheee!...Huo mgogoro unashughulikiwa kati ya Wizara na SUMA JKT ambao ndiyo walihusika moja kwa moja na zabuni."
Hata hivyo, Hamis alimwuliza tena naibu waziri huyo akisema: "Ina maana, wizara ya Kilimo haihusiki?"
Mathayo alifafanua kwa kukiri nafasi ya wizara yake katika mchakato huo, lakini akasisitiza kwamba mambo ya zabuni hiyo kwa kuwa yanahusu fedha nyingi zaidi, yanashughulikiwa na hazina na SUMA JKT.
Naibu waziri huyo, ambaye aliongozana na wataalamu mbalimbali wa wizara alisema, wazo la SUMA JKT kutaka kuwa sehemu ya uingizaji huo matrekta hayo kwa kutumia Mfuko wa Pembejeo, lilikuwa zuri.
"Wenzetu SUMA JKT walikuja na wazo zuri kutaka wasaidiane na taasisi nyingine kuingiza matrekta kupitia mfuko wetu wa pembejeo. Tulikubali kwa kuwa ni wazo zuri na kwamba yangekuwa yakiunganishwa Nyumbu," alitetea Suma JKT.
Hata hivyo, mbunge wa Ubungo ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Kilimo katika serikali ya awamu ya tatu, Charles Keenja alizidi kupigilia msumari baada ya kuhoji "kwanini fedha hizi zichukuliwe na kuingizwa tu katika jeshi.
"Huku ni kuishi kwa matumaini tu, kuamini Nyumbu wanaweza kuunganisha matrekta yote 1,000 wakati ukiangalia uwezo wao wa vitendeakazi si mkubwa. Kwanini msipeleke TAMCO (Kibaha) ambao wana uwezo mkubwa?"
Lakini, Mathayo alijaribu kutetea akisema si tu kwamba serikali imechukua fedha hizo na kuziiingiza jeshini kwa kuwa SUMA JKT pia imekuwa ikishiriki hata katika mradi wa kuingiza mbegu bora.
Bado baada ya majibu hayo, Keenja alinyoosha tena mkono na kutaka kuendelea kumbana Mathayo, ndipo mwenyekiti wa kamati hiyo, Gideon Cheyo, alipozima mjadala akisema utajadiliwa zaidi mbele.
"Inatosha, nafikiri tutajadili zaidi mbele ya safari. Hili ni suala ambalo ni pana tutalijadili tu waheshimiwa, kwa sasa tuendelee na mengine," alifafanua Cheyo.
Awali, Hamis alitaka kujua idadi ya matrekta ambayo yataingizwa nchini kuanzia ngazi zote ikiwemo katika halmashauri mbalimbali za wilaya kwa ajili ya Kilimo Kwanza.
Waziri Mathayo, ambaye alikuwa akiwasilisha Taarifa ya Mpango na Utekelezaji wa Bajeti kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2009, alisema jumla ya matrekta madogo (power tillers) yanayotarajiwa kuingizwa katika halmashauri ni 1,628, makubwa 28, wakati kati ya hayo 1,000 ndiyo hayo yatakayoingizwa na sekta binafsi, 400 mkopo kutoka Benki ya Exim India.
Kuhusu upotevu wa vipuri kwa baadhi ya matrekta, alisema hilo linafanyiwa kazi na kuongeza kwamba, wiki moja ijayo kutakuwa na mkutano mkuu wa wadau ambao jambo hilo litazungumzwa kwa kina.
Mgogoro wa Manji na Jeetu umekuwa ukichukua sura mpya kila kukicha. Tayari Manji aliwahi kunukuliwa akisema anajiandaa kuweka wazi jinsi Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004, ilivyokiukwa wakati wa mchakato wa utoaji zabuni hiyo.