Hawa Ghasia asema wengi wanasema hana uwezo kuongoza TAMISEMI

Ndiyo maana katiba mpya inamapendekezo yatakayotutoa hapa tulipo, mapendekezo ambayo binafsi nayaunga mkono na kuamini kwamba yakifuatwa 90% ya mawaziri watakuwa ni wale walio mahiri katika kazi.

Mawaziri wataomba kazi hizo au watapendekezwa na watu wa kawaida kwa rais.
Rais atawateua Bunge litawahoji umahiri wao ili kuamua uteuzi uhalalishwe au aletwe mtu mwingine kuwania kazi hiyo.

Rais akiteua mtu hufanya hivyo kwa sababu sheria inaruhusu kuteua na ukweli kwamba aliyembali haangukiwi na mti.
Rais halazimishwi kuchagua watu mahiri na wenye uwezo. Elimu ni kigezo lakini si kigezo pekee muhimu. Namna mtu anavyoitumia elimu yake katika kutatua matatizo yake binafsi na jamii ni muhimu hata kuliko ile sifa kwamba amesoma.

Rais mara nyingi huteua timu ya watu wanao mjenga kisiasa, japokuwa anajua fika kwamba timu yake ya mawziri ni lazima iwe na watu wenye uwezo wa kuijenga nchi. Akiwa na timu ya watu wanaomjenga kisiasa ana uhakika wa kuendelea kuwepo msimu unaofuatia, pia anauhakika wa kuendelea kuwa na influensi fulani siku akikaa Benchi.
Mawaziri wenye uwezo wa kuijenga nchi si lazima wawe ndiyo wenye uwezo wa kumjenga MH Rais kisiasa na kumhakikishia KURA na KULA.
Viongozi muhimu kama mawaziri wanatakiwa kuwa wasomi wenye historia ya utendaji wa kazi katika maeneo yao ya utaalamu. Muhimu zaidi ya usomi, wanatakiwa kuwa watu wenye uwezo wa kuona mbele,nia na hamu ya kutatua matatizo mengi ya kiutendaji yaliyolundikana kila wizara.

Elimu ni zana au ni kama NYENGO ya kule kwetu Lilinga(Iringa). Nyengo inaweza kuwa na makali yote lakini mtumiaji akawa si mtaalamu wa kuitumia ipasavyo kwenye Rili Werldi. Kwa mfano Namna anavyoshika mpini wake, Angle anayoiprojecti kwenye tageti, pia Fosi anayo iaplai wakati wa kukata Wihala(Vichaka) nk.

Naamini mama huyu akikubali kuwa mwanafunzi tena anaweza kugeuza mambo katika wizara.

Mimi natambua kwamba,Mtu yeyote mwenye PhD ni mwanafunzi wa kudumu.

Nisahihishwe.
 
Amalizie tu muda wake.

Kwanini asitoke mapema angalau tuambulie mazuri ya wanaostahili hiyo nafasi kuliko kukosa kama sasa.... miaka miwili mingi mkuu.... Wakurugenzi wanatafuna kila kitu.... na hakuna wa kuwaadhibu.... haya maneno siyaamini kabisa kuwa Wabunge wakiulizwa kuhusu wakurugenzi wabunge hujibu kuwa ni Wazuri tu yeye hawezi kuwaadhibu... wakati Mkaguzi mkuu huwapa report mabaya.... Naamini nafasi aliyonayo haimfai...

Majuzi kati nilisikia Mbunge akilalamika kuwa ameenda kwenye ukaguzi anakuta matumizi ya ununuzi wa zaidi ya million na miradi ya mabillion yote yametumika lakini hayana risiti... na ndio imetoka hiyo.... naye akalalamika kuwa matumizi ya serikali hayana nidhamu ndio imetoka hiyo... sasa kama waziri husika hachukui hatua yeyote ndio tutafika????????????????????????? au ndio amalize muda wake ?????? Sawa hiyo.....! aaaa hhh ta
 
Amesoma masomo gani huyu? Hivi huyu pia ni ndg au rafiki wa JK? Ina maana Report za CAG za kila mwaka hajui kuzisoma au anataka tumletee kitandani mwake?
 
Back
Top Bottom