Hatuwezi kurudisha utaratibu wa Mwl Nyerere na Karume?

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,216
3,585
Hivi hatuwezi kurejesha utaratibu wa Mwl Nyerere na Abeid Karume kuhusu mfumo wa muungano ambapo Rais wa Znz ndiyo lazima anakuwa Makamu wa Rais wa JMT?

Rais wa JMT akitoka Znz basi Makamu wake ndiyo atafutwe kutoka Bara. Mfumo wa Makamu wawili (wa Kwanza na wa Pili ungerejeshwa). Hivi sasa Rais akitoka Bara Makamu wake hawi Rais wa Znz bali anateuliwa toka miongoni mwa Wazanzibari.

Nadhani utaratibu huu wa waasisi wa Muungano ungeimarisha umoja wa kitaifa unaochagizwa na wapinzani na kuifanya agenda kuu; kwa sababu hata kama mpizani ndiye angeshinda kiti cha urais Znz lazima yeye ndiyo angekuwa Makamu wa Rais wa JMT hata kama nafasi ya rais wa JMT ingechukuliwa na chama tawala. Ya kale ni dhahabu!

Kwahiyo katika mazingira ya leo Makamu wa Pili wa Rais wa JMT angekuwa ni Rais wa SMZ Dr. Mwinyi.
 
Fihavango, G.M. (2017) katika kitabu chake “Tumpate wapi mtu kama huyu? Uongozi, Uadilifu, Uwajibikaji. Dai la uadilifu na uongozi wa karne ya 21” anasema yafuatayo:-

1. Mtu anayefaa kuwa kiongozi ni yule aliye tayari kuishi bila kuwa kiongozi na aliye tayari kuachia uongozi.

2. MUNGU atusamehe kwa kusema tulipotakiwa kunyamaza na kunyamaza tulipotakiwa kusema.

Mwandishi Askofu. Mch. Dkt. Fihavango anachambua uongozi wa Ki-kanisa, uchambuzi ambao kwa namna moja au nyingine unaakisi uongozi wa dola kutokana na mahusiano yao ya kitaasisi ya Kanisa na Dola.
 
Muungano ila kila nchi na rais yake.. . .kweli tumeungana kisungura na siyo kidogdog
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom