Hatuwezi kuendelea kuilaumu Kenya na Mabeberu kwa matatizo binafsi ya Tanzania: 'We are paying the price of our own Wrongdoings!'

Its all about perspective...maendeleo ya nchi ni relative..kujilinganisha na nchi zingine tutajidanganya na ndio maana tunafeli...ni km mtoto asiejitambua yuko wapi ametoka wapi na anataka kwenda wapi...kila kiongozi akija anafanya lake...

Mwingine perspective yake ni ujamaa wote ni kitu kimoja tufanye kazi kwa bidii kwa manufaa yetu wote

Mwingine kila mtu na akili yake kichwani..survival of the fittest/private sector watu waje wawekeze,hatuwezi wote tukawa sawa, km unauwezo wakupiga piga, ila mradi kuonekane kumechangamka..pesa ina zunguka transaction zinaonekana hata km hazi reflect uhalisia..twende kazi

Mwingine hapana hii si sawa Tanzania ni yetu wote, rasilimali zote ni zetu zitatumika kutunufaisha wote, tumefanywa shamba la bibi, watu wanaiba wanajinufaisha wakati mwananchi wa kawaida hapati haki za msingi...

sasa katika kila stage hapo juu lazima victim atalalamika...kwahio kusema tusilaumu mabeberu ni relative pia...

Mimi mtazamo wangu ni tukae chini tujitambue...strength na weakness zetu..halafu tusimamie strength tusonge mbele...

Kwa mfano tuna ardhi yenye rutba ya kutosha Mungu wetu tusamehe juzi kwenye radio kuna sehemu sijui uko sumbawanga kama sikosei wanasema miwa inakubali hatari hawajui waipeleke wapi inaoza shambani huku tunalia hatuna sukari tuna import...kinachotushinda nini kuwezesha kufungua kiwanda cha sukari kule..mimi naona labda kuna laana inatutafuna...tunaviongozi kila kona ya nchi..sijui RAS sijui katibu tawala..sijui mtendaji wanini wote hawa km hawako ujasiriamali minded kwa ajili ya rural development..

Kwa kifupi nobody can fix us but ourselves, sasa viongozi km hawalitambui hilo kazi ni kupigana vijembe huyu yuko hv, yule mshamba, huyu diplomat, huyu CCM B, huyu sukuma Gang..basi ili mradi tafrani..

Kenya hv, Kenya vile wale Urafiki yao tokea enzi za Nyerere inaendelea bado..maviwanda tokea enzi hizo bado zipo operational zinachapa kazi..sie sijui tunaviwanda vingapi vyakujilinganisha..tutauza mali ghafi tuambulie chenji tu..wakati wao wanazalisha wanapata manoti

Sasa tunawatafutia soko la products zao wakati sisi hatuna products za kucompete nao..mwisho wa siku tunauwa viwanda vilivyoanza kujikongoja...km vile tunaenda mbele kumbe tunarudi nyuma sababu hatujielewi..tutabaki kutoa mapovu tu huku kwenye mitandao
Unapozungumzia uchumi na kukuza uchumi hautakaa ukwepe namna fulani ya kukuza uchumi. Ndo mana kwenye theories za development, unaona mifano mingi inatoka Asian Tigers, na hata kuna nchi za sasa huwa wana borrow strategies zilizofanywa na Asian Tigers.

So nikukosoe kwanza, kwenye uchumi ni lazima uangalie mwenzako anafanya nini na wewe unafanya nini, na wewe amefanikiwa vip.. Ndo maana kuna kitu tunaita economic intelligence. Huwez ukasema eti hatutakiwi kufananisha.. utakuwa unakosea sana.. unless wewe utakuwa haufahamu haswa kuhusu masuala ya kiuchumi.
 
Sababu yako namba 3. Hizo ni hisia zako na si uhalisia.
Hivi unajua ni kwa nini watu hutoka nchini mwao na kwenda nchi nyingine?? Kwa taarifa yako, kwa ukanda huu wa A. Mashariki Somalia na Ethiopia ndiyo nchi zinazoongoza kuwa na watu wengi sana nje ya mipaka ya mipaka yao. Ukizunguka ulaya utawaona wengi mno wakifanya kazi za kawaida mpaka kuwa walimu wa vyuo vikuu. wengine wanaendesha subways na wengine askari. Kwa hiyo unataka kuniambia elimu ya somalia na ethiopia ni bora sana ndiyo imefanya watu wavuke mipaka?
Kwa taarifa yako, kama raia wa nchi fulani hawapendi kukaa nchini kwao, bali wanapenda kutoka nje. Hiyo siyo credit, hilo ni tatizo. ndiyo maana huwezi kuta waigereza, japan, ujerumani, nchi za skandinavia wanakimbia nchi zao na kwenda kwingine. Factor kubwa ni social and political unrest. kama unakumbuka kwenye historia, wangoni waliondoka A. Kusini kwa sababu ya mazingira magumu. ni kama osmosis movement from high concentration to low. Kwa hiyo watu wanaondoka kenya kwa sababu ya ugumu wa maisha. ndiyo maana kuna wengine mayaya walitelekezwa kule sana nchini yemen.
Ume mention Ethiopia na Somalia kwamba wengi wanaishi nje ya nchi, lakini umesahau kueleza ni kwanini wengi wapo nje ya nchi zao..

Kuna issue ya political instability kwa Somalia na hata Ethiopia, halafu kuna issue za baa la njaa, kwa hiyo hata ukichunguza wengi wa wa ethiopia na wa somalia walio nje ya nchi zao, hawa walikuwa granted hati ya ukimbizi.

Kwahiyo mpaka hapa, hakuna relevance ya unachotaka kukicommunicate.

Halafu naona una downplay role ya remittances flow.. itakuwa huelewi vema umuhimu wa remittances. Na kama huelewi hautakiwi uendelee kubishana kwa kitu ambacho hukifahamu. Nenda kakisome ndo uje tueleweshane vema
 
Wasalauumu wakuu!!

Uzi huu nilianza kuuandaa wakati Mama Samia anaenda Kenya, lakini sikuweza kuumaliza kwa wakati, nimeamua niuweke kwa sasa, japo muktadha wa sasa haupo kuijadili Kenya, ila itabidi niuweke kwasababu kuna mambo ambayo yapo relevant sana.

Imekuwa ni kawaida sana hapa jamvini kuona nyuzi ama comment za ‘wakuu’ kuishambulia sana nchi ya Kenya na wamekuwa wakitumia neno ‘Manyang’au’ kwa kunasabisha chuki zao dhidi ya Kenya ambazo pia zimekuwa zikichagizwa na hatua stahiki za viongozi wetu waandamizi dhidi ya Kenya. Mwelekeo wa maoni ya wadau na fikra za viongozi wengi wa ngazi za juu za Tanzania ni kwamba ‘Kenya imekuwa ikiihujumu Tanzania’ hivo ni jirani ambaye lazima atiliwe shaka.

Binafsi ntakuwa mmoja wa watu wachache wasiokuwa na ubaya wowote na Kenya, na ntakuwa wa mwisho duniani kuamini kwamba ni Kenya ndio imekuwa ikiihujumu Tanzania mpaka nchi yetu ipo hapa leo ilipo na Kenya ipo pale walipo. Nimefurahi pia sana kwa Mama Samia kuchukua hatua ya kuhuisha mahusiano yetu na Kenya. Kiongozi yeyote mwenye akili lazima angefanya kama Mama Samia. Ni kwasababu gani kwanza uwachukie Kenya?

Kama kichwa kinavosema, uzi huu ni mahsusi kuwapasha wale wote wenye mtizamo hasi juu ya Kenya. Na ujumbe ni kwamba ‘Kenya haiwezi kamwe kulaumiwa kwa matatizo yetu sisi watanzania, Tanzania inafaa kujilaumu yenyewe’

Ukifuatilia kwa makini, utofauti wa kiuchumi unaoonekana leo, kati ya nchi ya Tanzania na Kenya, umeanza kuonekana haswa miaka takribani 15 iliyopita – maana yake ni kwamba mwaka 2005 kurudi nyuma uchumi wa Kenya na Tanzania ulikuwa kwenye levels ambazo ni sawa kwa kuangalia urari wa pato la taifa kwa nchi hizi mbili.

View attachment 1805845

View attachment 1805846

So mpaka hapa, hoja ya msingi ni: Je? Wakenya wamefanya nini cha tofauti ambacho Watanzania hatukutilia maanani kuanzia mwaka 2005 mpaka sasa, kiasi cha uchumi wao kutuzidi kwa karibu USD 32 Billion (TZS 74 Trillioni) wakati mwaka 2005 tulikuwa nao sawa?

Kwa mtizamo wangu wa jicho la kiuchumi, niliweza kung’amua masuala yafuatayo. (Na tathmini yangu inaanzia mwaka 2005 kuja mbele) ambayo waKenya wameyafanya na ambayo waTanzania tuliyazembea.

1. Kuongozwa na viongozi wenye uelewa wa namna uchumi unavofanya kazi (Kuongozwa na vichwa wa kiuchumi)

‘Never underrate knowledge and what it can do to development’

Nimekuwa na mahaba makubwa na Marais wa Kenya kuanzia kwa Mwai Kibaki na hata kwa Uhuru Kenyatta, nakumbuka mwaka 2002 wakati Mwai Kibaki anamuangusha Daniel Arap Moi na chama chake cha KANU, nilikuwa darasa la sita kwa wakati huo, ila nakumbuka nilikuwa nikifuatilia utangazwaji wa matokeo ya urais kwenye redio na sikuweza kubanduka, nilimfurahia sana Mwai Kibaki bila sababu yoyote.

Ila ni wakati huu wa ukubwani, ndo nakuja kutambua haswa Mwai Kibaki alikuwa mtu wa namna gani, naweza sema ndo ambaye ameweka foundation yah ii rapid economic growth ya wakenya ndani ya hii miongo miwili. Na ndio umuhimu wa kuwa na viongozi wanaoelewa vema namna ya kukuza uchumi.

Mwai Kibaki -----> CV“ …. Kibaki instead attended Makerere University in Kampala, Uganda, where he studied Economics, History and Political Science, and graduated best in his class in 1955 with a First Class Honours Degree (BA) in Economics.[4] After his graduation, Kibaki took up an appointment as Assistant Sales Manager Shell Company of East Africa, Uganda Division. During the same year, he earned a scholarship entitling him to postgraduate studies in any British University. He consequently enrolled at the prestigious London School of Economics for a BSc in public finance, graduating with a distinction. He went back to Makerere in 1958 where he taught as an Assistant Lecturer in the economics department until 1961…..”

Baada ya Mwai Kibaki 2013, akamufuata Uhuru Kenyatta – exposed person, economist, bepari, mzalendo wa ukweli, opportunist. Huyu mwamba amefanya makubwa sana kwa Kenya.

Uhuru Kenyatta ---> CV “….After attending St. Mary's school, Uhuru went on to study economics, political science and government at Amherst College in the United States.[8][9][2] Upon his graduation, Uhuru returned to Kenya, and started a company Wilham Kenya Limited, through which he sourced and exported agricultural produce…..”

Kwa Tanzania, kutoka kwa Mkapa mpaka kwa Kikwete, tulikuwa at least heading in the right path, kwa sababu ni viongozi ambao walikuwa wanajua ni namna gani ya kukuza uchumi, na sera zao za uchumi wa soko ndio haswa zilisababisha booming ya private sector in Tanzania.

Laiti kama aliyempokea kijiti Kikwete angekuwa ni mtu dizaini ya Uhuru Kenyatta, Tanzania ingekuwa ya tofauti sana, hicho ndo nnachoamini. Ndo mana daima ntaamini kwamba, ujio wa Rais Magufuli ambaye hakuelewa vema the role of private sector to economic growth, itabaki kuwa janga la kihistoria kwa nchi ya Tanzania, as a result of Magufuli regime, kuna dynamics nyingi sana za kiuchumi zimebadilika ambazo zilisababisha huu uchumi uchechemee kwa at least 5 years, while in the same time, uchumi wa Kenya ulikuwa unapaa, chini ya MasterMind Uhuru Kenyatta.


2. Cost of doing business (mazingira ya ufanyaji wa biashara na uwekezaji)

Ni biashara na uwekezaji ndo unakuza uchumi wa taifa, nchi ya kenya imekuwa iki improve sana kwenye mazingira ya ufanyaji wa biashara na uwekezaji kwa miaka ya hivi karibuni kulinganisha na nchi ya Tanzania. Hii imepelekea mazingira rahisi ya kibiashara na uwekezaji kwa wakenya wenyewe na wawekezaji wa nje.

View attachment 1805847
View attachment 1805848

Ukiangalia hizi takwimu za ease of doing business kwa nchi ya Tanzania na Kenya, unaweza kuona kabisa kwamba kwa miaka mitano iliyopita, nchi ya Kenya imeweza ku improve in cost of doing business kwa points 15.21 wakati kwa Tanzania improvement ya mazingira ya kufanya biashara na uwekezaji yaliongezeka kwa points 4.77. (Ni kama kwenye era nzima ya Magufuli, ambayo unahesabu kuanzia mwaka 2017 kwa sababu hizi takwimu zinatolewa mwaka mmoja kabla, ni kwamba hakukuwa na improvement yoyote katika mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji)

Kwenye hizi takwimu za mazingira ya ufanyaji biashara, huwa wanaangalia viashiria vifuatavyo

  • Paying Taxes – mazingira ya ulipaji kodi
  • Getting credits – kupata mikopo, riba za mikopo etc
  • Starting a business – leseni ya biashara, vibali etc
  • Construction permit – vibali vya ujenzi
  • Getting electricity
  • Registering properties
  • Protecting minority investors
  • Trading across borders
  • Enforcing contracts.
  • Resolving insolvency
Bila kuingia kwa ndani kabisa, kwenye hivo vigezo hapo juu, ila tuelewe tu kwamba Kenya walifanya improvements kubwa sana kwenye kuboresha mazingira kama ya upatikanaji wa mikopo (mfano bunge la Kenye lilileta sheria ya ku cap interest rate at 13% ambayo kwa kiasi fulani ilisaidia sana wakenya ku access mikopo) bila kusahau uraisi wa kufungua kampuni Kenya ambapo nadhani sheria yao, inaruhusu mtu kuanzisha kampuni bila kuwa na capital. Wameweza pia kuwa na uboreshaji mkubwa wa sheria za kodi.

Kwa Tanzania sote tunajua mambo yaliyotokea miaka ya hivi karibuni, na unaweza kuona ni namna gani mazingira yetu ya kufanya biashara yamakuwa ni mabovu mno na hii imekuwa na matokeo yake kwenye shuhuli za kiuchumi.


3. Elimu yenye tija kwa watu wake na lugha ya kiingereza.

Mfumo wa elimu wa Kenya umeimarika sana, sijui ni kwasababu ya mchango wa lugha ya ‘Kiingereza’ ila Wakenya wengi waliosoma tena shule na vyuo vyao vya ndani, wamekuwa ni watu wakujiamini sana, hii imepelekea miaka ya hivi karibuni wakenya wengi waende kufanya kazi nje ya nchi yao, as a result wengi wamepata exposure kulinganisha na watanzania ambao wengi ni waoga kutoka nje ya nchi yao kwa sababu ya kutokujiamini partly inawezekana ni kwasababu wengi wa watanzania Kiingereza imekuwa ni tatizo, kwahiyo wanaogopa kuvuka boda.

Mwisho wa siku impact inaonekana kwenye uchumi, ukiangalia kwenye takwimu za remittances flow, utakubaliana na huu ukweli ambao mimi nauhusianisha na ‘elimu na lugha ya kiingereza’ – whether ukubali au ukatae, ndo ukweli huo.

View attachment 1805850

So basically, Tanzania is paying the heavy price kwa vitu ambavyo tunakuwa tunavipuuzia na ambavyo wakenya wanavipa kipaumbele. Tumekuwa nyuma sana Tanzania na wanasiasa wetu bado hawajatambua namna ya kubadilisha.


4. Katiba, sheria, na miongozo

Kipindi cha Mwai Kibaki, Kenya walibahatika kupata katiba bora sana ambayo imeweza kutoa mazingira bora ya kufanya shughuli za kiuchumi kwa wakenya. Imefanya wakenya ku embrace ubepari ambao ndo mfumo unaofanya kazi katika kukuza uchumi, while Tanzania bado tunagandana na ujamaa usiofanya kazi.

As a result, katiba ya wakenya ambayo ime grant freedom of thinking imekuwa chachu ya kufungua akili za wakenya, no matter hata ukiona trend ya remittances flow, inakuambia kitu fulani.

Huku kwingine Tanzania, na vyombo vya kutuga sheria wamekuwa wapo busy kuzidi kukandamiza watanzania kwa kutunga sheria ambazo zinaminya uhuru wa fikra ambayo ni chachu ya kukuza uchumi na kufanya innovation.

Ni kama vile wanasiasa na watunga sheria wa Tanzania wamekuwa wapo busy kuonesha wao ni miamba na miungu watu, utaangalia type ya viongozi kama Magufuli, Ole Sabaya, Paul Makonda, Job Ndugai and the likes.. yaani ni kama walikuwa na uadui na watanzania wakati wangetakiwa kuwa busy kufikiri ni namna gani wataboresha mazingira wao walikuwa busy kuwakomesha watu – Take it or leave.. ndo ukweli ambao wengi tunaochambua haya mambo tutabaki kuushika.


Hitimisho
So all in all, sioni ni kwanini tuwe tunaendelea kulaumu Wakenya au Mabeberu kwa matatizo ambayo watanzania wenyewe tunayalea na tumeyatengeneza wenyewe.
  • Wakenya au mabeberu hawakutuambia tuwe na mazingira magumu ya kufanya biashara na kuwekeza – tulichagua wenyewe kuwa sheria kandamizi za uwekezaji.
  • Sio wakenya au mabeberu waliotuambia tuendelee kuwa na elimu ambayo haiwapi watu kujiamini kuvuka border na ku explore the world – tulichagua wenyewe
  • Sio wakenya au mabeberu walituambia tuendelee kuwa na mfumo wa kijamaa usiofanya kazi – tulichagua wenyewe
  • Sio wakenya au mabeberu walituambia tuwe na viongozi wanaokanyaga sheria – tulichagua wenyewe
  • Sio wakenya au mabeberu walituambia tununue ndege cash wakati kuna vipaumbele vingine ambavyo tungeweza kuwekeza na kutoa return nzuri kwa jamii – ni sisi wenyewe tulilipa pesa cash hawakutushika mkono
  • Sio wakenya au mabeberu walituambia tununue ndege halafu tuandike ‘Hapa kazi tu’ badala ya kuandika ‘Karibu Tanzania nchi ya Mlima Kilimanjaro’ – ni sisi wenyewe
So, watanzania wenzangu, tuache hii tabia ya kupenda kuwatwisha mizigo Kenya na nchi nyingine hata Mabeberu, kwa matatizo ambayo ni sisi wenyewe tunayasababisha, tunayakumbatia, na tulichagua kuwa nayo.

Maisha yamenifundisha kwamba, ‘you will always pay the price of your mistakes’ iwe kwenye mahusiano, iwe kwenye kitu chochote, utalipia makosa yako. So watanzania wenzangu wenye akili, adui wentu hawezi kuwa Kenya, adui wetu hawezi kuwa Mabeberu, adui wetu ni hawa ambao mpaka sasa hatuna katiba ya kueleweka, demokrasia ya kueleweka, sheria kandamizi, na wapo wanadunda kila siku tunawaona. Ni hawa hawa ndio wanakesha wakituaminisha kwamba Wakenya ni wabaya, mabeberu ni wabaya, wakati wao ndo wabaya.

Wako katiba ujenzi wa Taifa
N.Mushi
Umeandika sana sana na umeonesha namna Kenya imefanya tena kwa kiwango na mifano na hapa tuna safari ndefu sana kwetu,

Kizazi cha Mkapa Na JK kilipaswa kuandaliwa kama wenzetu Kenya wana vizazi vinavotaka Urais vyenye maono ya Kiuchumi wa sasa duniani.
 
Kwanini Aliko Dangote alishindwa kuwekeza kenya?

Kwanini Rostam Aziz alishindwa kuwekeza kenya upande wa gesi?

Bakhresa aliomba awekeze kenya na hawakumpa nafasi

CRDB waliomba kuwekeza na walinyimwa fursa

Sasa wakenya kwenye maendeleo yao wanavuna $ ngapi kwa makampuni 500 yaliyopo Tanzania?

Kenya wanajua hili wakiweka mazingingira rafiki kwa Tanzania kuingia kuwekeza kenya, nchi yetu itavuna $ za kutosha

Ni kweli wapo juu kiuchumi kwanini hakuna double standard kwenye uwekezaji ingali ni nchi majirani?

Inaumiza Sana Rudi kaangalie YouTube ya Rostam Aziz alivyoongea kwa niaba ya wafanyabiashra kutoka Tanzania

Bado wanaitaka gesi yetu iende kwao kenya ili nao waruhusu mahindi ya Tanzanian yauzwe kenya

Faida watakayoipata kenya wakiuza gesi iliyotoka Tanzania utakuja kutuambia kenya wako vizuri kuliko Tanzania kiuchumi
 
Kwanini Aliko Dangote alishindwa kuwekeza kenya?

Kwanini Rostam Aziz alishindwa kuwekeza kenya upande wa gesi?

Bakhresa aliomba awekeze kenya na hawakumpa nafasi

CRDB waliomba kuwekeza na walinyimwa fursa

Sasa wakenya kwenye maendeleo yao wanavuna $ ngapi kwa makampuni 500 yaliyopo Tanzania?

Kenya wanajua hili wakiweka mazingingira rafiki kwa Tanzania kuingia kuwekeza kenya, nchi yetu itavuna $ za kutosha

Ni kweli wapo juu kiuchumi kwanini hakuna double standard kwenye uwekezaji ingali ni nchi majirani?

Inaumiza Sana Rudi kaangalie YouTube ya Rostam Aziz alivyoongea kwa niaba ya wafanyabiashra kutoka Tanzania

Bado wanaitaka gesi yetu iende kwao kenya ili nao waruhusu mahindi ya Tanzanian yauzwe kenya

Faida watakayoipata kenya wakiuza gesi iliyotoka Tanzania utakuja kutuambia kenya wako vizuri kuliko Tanzania kiuchumi

..Rostam amechuma hapa Tanzania halafu anataka kwenda kuwekeza Kenya.

..Mimi nimefurahi Rostam alivyonyimwa kuwekeza Kenya.

..badala ya kutengeneza ajira hapa Tanzania, Rostam anataka kwenda kutengeza ajira Kenya?!

..Hayo mabilioni angeyawekeza hapahapa Tanzania ambapo ndipo palipompa utajiri.

..Rostam Aziz anapaswa kuwa mza-RENDO.
 
Nadhani miaka ya 1999 mpaka 2005 ambayo ni kipindi cha Mkapa, ni kipindi ambacho Mkapa ali introduce taasisi za kuregulate uchumi huku akiendelea kufungulia na kulea sekta binafsi. Hiyo ndiyo ilikuwa key kwa upande wangu.

Point ya kuwa na dira ya taifa pia naikubali, na utaona tangu kipindi cha mkapa, JK, na Magufuli nchi haijaweza kusimama na sera moja ambayo ilitakiwa ili kufanya mapinduzi ya kiuchumi, ni kama vile uchumi wetu umekuwa kama kuku aliyekatwa kichwa.. no direction

..kuna waraka unaitwa " tanzania vision 2025 " ambao uliandaliwa wakati wa Mzee Mkapa.

..sina uhakika kwa kiasi gani Kikwete na Magufuli walisimamia utekelezaji wa waraka huo.
 
Unapozungumzia uchumi na kukuza uchumi hautakaa ukwepe namna fulani ya kukuza uchumi. Ndo mana kwenye theories za development, unaona mifano mingi inatoka Asian Tigers, na hata kuna nchi za sasa huwa wana borrow strategies zilizofanywa na Asian Tigers.

So nikukosoe kwanza, kwenye uchumi ni lazima uangalie mwenzako anafanya nini na wewe unafanya nini, na wewe amefanikiwa vip.. Ndo maana kuna kitu tunaita economic intelligence. Huwez ukasema eti hatutakiwi kufananisha.. utakuwa unakosea sana.. unless wewe utakuwa haufahamu haswa kuhusu masuala ya kiuchumi.
Kukuza uchumi wa nchi hakuhitaji rocket science aisee...nikuongeza production period...sasa Tanzania tuna produce nini yarabi..ni hayo mahindi tunayoombea soko Kenya..

Tunatafuta watu nje waje kuwekeza which is fine...terms za mikataba ni siri...watanzania wapole sana hatuna shida tunaimani na viongozi wetu...ninaamini hakuna mfanyabiashara anaetaka kuwekeza asietaka apate faida zaidi...akija kiongozi akituambia jamani tunaibiwa mikataba mibovu..km uwekezaji hauna tija kwa nchi yangu sepeni mnasema ditekta anafukuza wawekezaji...mikataba mibovu maana yake nini muwekezaji anazalisha anachukua noti sisi tunabaki na coin..na unakuja kuambiwa hizo coin asilimia kubwa inaishia kwa wachache...

Haya sasa tunafungua nchi watu waje kuwekeza kwa terms zipi...na tunavyoomba kwa kupiga magoti nina shaka km tutaweza kuchallenge terms zao...msione watu wanalalamika, viongozi wenyewe ndio wanatuchanganya...Upinzani ajenda yao kubwa bungeni ilikuwa mikataba mibovu...sasa hv kiko wapi...

Tumlaumu nani
 

Mkuu,this is a thread of the year!!! Nimesoma hoja zako zote pamoja na jinsi unavyojibu kina "walee" nikagundua,WEWE NI NGULI na unautashi wa kutosha kwenye uandishi,uwasilishaji na ujenzi wa hoja. KONGOLE YAKHE.

Pili,labda nitupie wazo langu hapa. Binafsi nadhani elimu mbovu ndio imetufikisha hapa. Hadi Karne hii yupo mbunge bungeni ambaye ni darasa la Saba! SAMAHANI,darasa la nne!!! Cha kushangaza,kamati ya chama eti iliwapitisha kisa ni hodari wa kubwabwaja matusi na upyoro wa lugha chafu pindi wanapojibu hoja za wapinzani😂😂😂😂

Papa,we can never compete with a country whose lawmakers in the assembly a chosen by the people on the ground of credibility, intelligence and academics. For instance,for anybody to become a senator in Kenya,must have at least masters from a recognized public institution and not those fetched from the streets of Delhi, India!!! While a member of parliament should at least be a degree holder...!!! Tunaanzaje sasa ushindani???

Tatu,tunaanzaje ushindani na watu ambao si waoga kudai haki yao? Mkuu,kumbuka nchi ile kiongozi wa upinzani anazunguka na rais kuzindua miradi ilhali huku mpinzani anatakiwa atolewe kafara ili viuongo vyake na damu vitumike kuisokota hirizi ya Muungano ili isipoteze uhalali???

Tunaanzaje kushindana na taifa ambazo ili uchaguliwe kuwa CEO,CHIEF JUSTICE,POLICE COMMISSIONER etc lazima ufanyiwe public vetting tofauti na huku kwetu ambapo kamishna wa polisi sharti awe mbabe mwenye alama nyingi usoni zinazoashiria makovu yaliyomkuta katika medani ya mapambano au uwe na sura ngumu inayoweza kutisha maandamano ya wapinzani!!!

Tunaanzaje ushindani na nchi amabayo inaamini katika ushindani wa kielimu ilhali sisi tumewekeza katika kushawishi waganga wa jadi kwamba tuko pamoja nao na tunaendelea kutetea haki zao!!! Kenya mabango ya kuonyesha taasisi zinazotoa elimu ya juu ni mengi sawa na yale yanayoonyesha wasafisha nyota,warefusha uume,warudisha wapenzi,wauza Pete za bahati Tanzania!!! Dadeki!!!

Tunaanzaje ushindani na nchi ambayo ili uwe askari angalau uwe na elimu ya form four ilhali huku kwetu Bongo kigezo ni uwe mwana green brigade au la,wazazi wako wawe wastaafu wa jeshi au walau wanafahamiana na washika dau.!!! Tunaanzaje Mushi huu ushindani kakaangu?

Tunaanzaje ushindani na wakenya ambao ili uonekane smart ni kichwani uwe vizuri ilhali huku kwetu kijana smart ni anae miliki I.S.T au Kama ni mwanamke,awe na makalio makubwa ambayo akipita karibu na wewe unaitika "naam"hususan Kama unaitwa Paul maana yanapiga kelele "poo,poo,poo"apitapo. Kenya mdada anahangaika na mafaili ya vyetu ilhali huku kwetu wadada ni kubusti maziwa na kuhangaika kuyarudisha kwenye brezia kila Mara gari linapogonga bampsi!!!

Viongozi wakenya huwa wanajadili masuala ya kitaifa hususan wawapo bungeni,sisi wakwetu huwa wanajadili vyama kila Leo na kutaka wananchi wamseme na kumsoma kwenye magazeti. Uhuru Kenyatta anasifika kila kina ilhali Magufuli anasifika kwenye zilizokiki za Milad Ayo!!! What a stoke!!!

Wakenya wamewekeza sana kwenye ujasusi wa kiuchumi,kisera na hata kisisasa. Maraisi wao huwandalia mapema sana kiasi kwamba unaweza kupredict huku kwetu raisi anadeveop political pressure kwa kupitishwa kuiongoza nchi bila kutegemea au kuota! Afu anasema hadharani,"Mimi SI mwanasiasa" ila bado Wana wa ujamaa wanamshangilia na kumpamba kwa nyodo na mikogo afu tuanze kushindana na wakenya!!!

Kaka Nina mengi ila tayari hasira zimenipanda naomba nisiendelee. Nikichokozwa na "wale" nitarejea......ila tukitaka kubadili upepo na kuwa kimbiza wakenya,TUWEKEZE KWENYE ELIMU YENYE TIJA. SI HII YA "WANYONGE"
 
Ume mention Ethiopia na Somalia kwamba wengi wanaishi nje ya nchi, lakini umesahau kueleza ni kwanini wengi wapo nje ya nchi zao..

Kuna issue ya political instability kwa Somalia na hata Ethiopia, halafu kuna issue za baa la njaa, kwa hiyo hata ukichunguza wengi wa wa ethiopia na wa somalia walio nje ya nchi zao, hawa walikuwa granted hati ya ukimbizi.

Kwahiyo mpaka hapa, hakuna relevance ya unachotaka kukicommunicate.

Halafu naona una downplay role ya remittances flow.. itakuwa huelewi vema umuhimu wa remittances. Na kama huelewi hautakiwi uendelee kubishana kwa kitu ambacho hukifahamu. Nenda kakisome ndo uje tueleweshane vema

Pitia post yangu tena, ili uelewe ni kwa nini nilikubishia kwamba sababu ya wakenya kwa kiasi fulani kutoka nje ni nini!!? Wewe ulikazia sana kiingereza (🤣🤣🤣)
 
Leo tarehe 03/06/2021 wametua matajiri wakubwa wawili kutoka Marekani kuja kuwekeza TZ .
Wamepokelewa na viongozi wetu!

Inaonesha mama yupo serious na falsafa yake ya uwekezaji...?
Source: clouds media
 
Leo tarehe 03/06/2021 wametua matajiri wakubwa wawili kutoka Marekani kuja kuwekeza TZ .
Wamepokelewa na viongozi wetu!

Inaonesha mama yupo serious na falsafa yake ya uwekezaji...?
Source: clouds media
Ndo tunataka mambo kama haya sasa
 

Mkuu,this is a thread of the year!!! Nimesoma hoja zako zote pamoja na jinsi unavyojibu kina "walee" nikagundua,WEWE NI NGULI na unautashi wa kutosha kwenye uandishi,uwasilishaji na ujenzi wa hoja. KONGOLE YAKHE.

Pili,labda nitupie wazo langu hapa. Binafsi nadhani elimu mbovu ndio imetufikisha hapa. Hadi Karne hii yupo mbunge bungeni ambaye ni darasa la Saba! SAMAHANI,darasa la nne!!! Cha kushangaza,kamati ya chama eti iliwapitisha kisa ni hodari wa kubwabwaja matusi na upyoro wa lugha chafu pindi wanapojibu hoja za wapinzani😂😂😂😂

Papa,we can never compete with a country whose lawmakers in the assembly a chosen by the people on the ground of credibility, intelligence and academics. For instance,for anybody to become a senator in Kenya,must have at least masters from a recognized public institution and not those fetched from the streets of Delhi, India!!! While a member of parliament should at least be a degree holder...!!! Tunaanzaje sasa ushindani???

Tatu,tunaanzaje ushindani na watu ambao si waoga kudai haki yao? Mkuu,kumbuka nchi ile kiongozi wa upinzani anazunguka na rais kuzindua miradi ilhali huku mpinzani anatakiwa atolewe kafara ili viuongo vyake na damu vitumike kuisokota hirizi ya Muungano ili isipoteze uhalali???

Tunaanzaje kushindana na taifa ambazo ili uchaguliwe kuwa CEO,CHIEF JUSTICE,POLICE COMMISSIONER etc lazima ufanyiwe public vetting tofauti na huku kwetu ambapo kamishna wa polisi sharti awe mbabe mwenye alama nyingi usoni zinazoashiria makovu yaliyomkuta katika medani ya mapambano au uwe na sura ngumu inayoweza kutisha maandamano ya wapinzani!!!

Tunaanzaje ushindani na nchi amabayo inaamini katika ushindani wa kielimu ilhali sisi tumewekeza katika kushawishi waganga wa jadi kwamba tuko pamoja nao na tunaendelea kutetea haki zao!!! Kenya mabango ya kuonyesha taasisi zinazotoa elimu ya juu ni mengi sawa na yale yanayoonyesha wasafisha nyota,warefusha uume,warudisha wapenzi,wauza Pete za bahati Tanzania!!! Dadeki!!!

Tunaanzaje ushindani na nchi ambayo ili uwe askari angalau uwe na elimu ya form four ilhali huku kwetu Bongo kigezo ni uwe mwana green brigade au la,wazazi wako wawe wastaafu wa jeshi au walau wanafahamiana na washika dau.!!! Tunaanzaje Mushi huu ushindani kakaangu?

Tunaanzaje ushindani na wakenya ambao ili uonekane smart ni kichwani uwe vizuri ilhali huku kwetu kijana smart ni anae miliki I.S.T au Kama ni mwanamke,awe na makalio makubwa ambayo akipita karibu na wewe unaitika "naam"hususan Kama unaitwa Paul maana yanapiga kelele "poo,poo,poo"apitapo. Kenya mdada anahangaika na mafaili ya vyetu ilhali huku kwetu wadada ni kubusti maziwa na kuhangaika kuyarudisha kwenye brezia kila Mara gari linapogonga bampsi!!!

Viongozi wakenya huwa wanajadili masuala ya kitaifa hususan wawapo bungeni,sisi wakwetu huwa wanajadili vyama kila Leo na kutaka wananchi wamseme na kumsoma kwenye magazeti. Uhuru Kenyatta anasifika kila kina ilhali Magufuli anasifika kwenye zilizokiki za Milad Ayo!!! What a stoke!!!

Wakenya wamewekeza sana kwenye ujasusi wa kiuchumi,kisera na hata kisisasa. Maraisi wao huwandalia mapema sana kiasi kwamba unaweza kupredict huku kwetu raisi anadeveop political pressure kwa kupitishwa kuiongoza nchi bila kutegemea au kuota! Afu anasema hadharani,"Mimi SI mwanasiasa" ila bado Wana wa ujamaa wanamshangilia na kumpamba kwa nyodo na mikogo afu tuanze kushindana na wakenya!!!

Kaka Nina mengi ila tayari hasira zimenipanda naomba nisiendelee. Nikichokozwa na "wale" nitarejea......ila tukitaka kubadili upepo na kuwa kimbiza wakenya,TUWEKEZE KWENYE ELIMU YENYE TIJA. SI HII YA "WANYONGE"
Pamoja sana mkuu... umemwaga point nzito na wewe ngoja nizipitie taratibu
 
..kuna waraka unaitwa " tanzania vision 2025 " ambao uliandaliwa wakati wa Mzee Mkapa.

..sina uhakika kwa kiasi gani Kikwete na Magufuli walisimamia utekelezaji wa waraka huo.
Shida ni kwamba Tanzania hakuna dira ambayo ipo constant kila Rais anakuja na dira yake na mipango yake, ndo makosa huanzia hapo.. but kikubwa zaidi mi nnachoona hizi sheria zetu ndo zinatuponza
 

Mkuu,this is a thread of the year!!! Nimesoma hoja zako zote pamoja na jinsi unavyojibu kina "walee" nikagundua,WEWE NI NGULI na unautashi wa kutosha kwenye uandishi,uwasilishaji na ujenzi wa hoja. KONGOLE YAKHE.

Pili,labda nitupie wazo langu hapa. Binafsi nadhani elimu mbovu ndio imetufikisha hapa. Hadi Karne hii yupo mbunge bungeni ambaye ni darasa la Saba! SAMAHANI,darasa la nne!!! Cha kushangaza,kamati ya chama eti iliwapitisha kisa ni hodari wa kubwabwaja matusi na upyoro wa lugha chafu pindi wanapojibu hoja za wapinzani😂😂😂😂

Papa,we can never compete with a country whose lawmakers in the assembly a chosen by the people on the ground of credibility, intelligence and academics. For instance,for anybody to become a senator in Kenya,must have at least masters from a recognized public institution and not those fetched from the streets of Delhi, India!!! While a member of parliament should at least be a degree holder...!!! Tunaanzaje sasa ushindani???

Tatu,tunaanzaje ushindani na watu ambao si waoga kudai haki yao? Mkuu,kumbuka nchi ile kiongozi wa upinzani anazunguka na rais kuzindua miradi ilhali huku mpinzani anatakiwa atolewe kafara ili viuongo vyake na damu vitumike kuisokota hirizi ya Muungano ili isipoteze uhalali???

Tunaanzaje kushindana na taifa ambazo ili uchaguliwe kuwa CEO,CHIEF JUSTICE,POLICE COMMISSIONER etc lazima ufanyiwe public vetting tofauti na huku kwetu ambapo kamishna wa polisi sharti awe mbabe mwenye alama nyingi usoni zinazoashiria makovu yaliyomkuta katika medani ya mapambano au uwe na sura ngumu inayoweza kutisha maandamano ya wapinzani!!!

Tunaanzaje ushindani na nchi amabayo inaamini katika ushindani wa kielimu ilhali sisi tumewekeza katika kushawishi waganga wa jadi kwamba tuko pamoja nao na tunaendelea kutetea haki zao!!! Kenya mabango ya kuonyesha taasisi zinazotoa elimu ya juu ni mengi sawa na yale yanayoonyesha wasafisha nyota,warefusha uume,warudisha wapenzi,wauza Pete za bahati Tanzania!!! Dadeki!!!

Tunaanzaje ushindani na nchi ambayo ili uwe askari angalau uwe na elimu ya form four ilhali huku kwetu Bongo kigezo ni uwe mwana green brigade au la,wazazi wako wawe wastaafu wa jeshi au walau wanafahamiana na washika dau.!!! Tunaanzaje Mushi huu ushindani kakaangu?

Tunaanzaje ushindani na wakenya ambao ili uonekane smart ni kichwani uwe vizuri ilhali huku kwetu kijana smart ni anae miliki I.S.T au Kama ni mwanamke,awe na makalio makubwa ambayo akipita karibu na wewe unaitika "naam"hususan Kama unaitwa Paul maana yanapiga kelele "poo,poo,poo"apitapo. Kenya mdada anahangaika na mafaili ya vyetu ilhali huku kwetu wadada ni kubusti maziwa na kuhangaika kuyarudisha kwenye brezia kila Mara gari linapogonga bampsi!!!

Viongozi wakenya huwa wanajadili masuala ya kitaifa hususan wawapo bungeni,sisi wakwetu huwa wanajadili vyama kila Leo na kutaka wananchi wamseme na kumsoma kwenye magazeti. Uhuru Kenyatta anasifika kila kina ilhali Magufuli anasifika kwenye zilizokiki za Milad Ayo!!! What a stoke!!!

Wakenya wamewekeza sana kwenye ujasusi wa kiuchumi,kisera na hata kisisasa. Maraisi wao huwandalia mapema sana kiasi kwamba unaweza kupredict huku kwetu raisi anadeveop political pressure kwa kupitishwa kuiongoza nchi bila kutegemea au kuota! Afu anasema hadharani,"Mimi SI mwanasiasa" ila bado Wana wa ujamaa wanamshangilia na kumpamba kwa nyodo na mikogo afu tuanze kushindana na wakenya!!!

Kaka Nina mengi ila tayari hasira zimenipanda naomba nisiendelee. Nikichokozwa na "wale" nitarejea......ila tukitaka kubadili upepo na kuwa kimbiza wakenya,TUWEKEZE KWENYE ELIMU YENYE TIJA. SI HII YA "WANYONGE"

Andiko lefu sana, lkn vingi hapo ni hisia tu. Kwa hiyo ili uwe askari bongo, lazima utokee chipkiz ya sisiem (mbavu zangu 🤣 🤣 🤣 ). Lkn niongee kwa kifupi tu. wengi wanaochangia uzi huu ni wale exposure yao imefikia,labda sana sana nairobi. lkn kwa mtu ambaye ameenda nchi nyingine za Afrika. Hususan ni za kusini kama Botswana, Namibia na sasa Angola. ukiwahi fika nchi hizi na kujua siasa zake, hutakuja tena kuongea kuhusu nchi ya kenya. a bandit society, unaipa sifa lukuki wakati kuna uozo uliopitiliza. Nchi haina udhibiti, kuna sehemu watu wanajilinda wenyewe na smg. Halafu unakuja na maneno meengi ya kusifia vitu usivyovijua. Kenya is like a jungle, everyone is striving hard to make a living, otherwise you will be eatenby your fellow people. Ndiyo maana kule pokot wana mifugo mingi, na wako katika hatari ya kuvamiwa na kuuawa huku wakiporwa mifugo yao, lkn serikali haifanyi kitu. matokeo yake wananchi wa kule wamejinunulia smg kutoka wanakokujua wao wenyewe, ili wajilinde. serikali ya kenya wala haina habari na hilo. Yaani ni shida. lkn cha kushangaz unasifia mpaka unatia huruma. kwa kifupi, nenda nchi hizo nilizo kutajia halafu ulinganishe na kesha, nadhani utakuwa na mtazamo uliobadirika na bora zaidi.
 
Andiko lefu sana, lkn vingi hapo ni hisia tu. Kwa hiyo ili uwe askari bongo, lazima utokee chipkiz ya sisiem (mbavu zangu 🤣 🤣 🤣 ). Lkn niongee kwa kifupi tu. wengi wanaochangia uzi huu ni wale exposure yao imefikia,labda sana sana nairobi. lkn kwa mtu ambaye ameenda nchi nyingine za Afrika. Hususan ni za kusini kama Botswana, Namibia na sasa Angola. ukiwahi fika nchi hizi na kujua siasa zake, hutakuja tena kuongea kuhusu nchi ya kenya. a bandit society, unaipa sifa lukuki wakati kuna uozo uliopitiliza. Nchi haina udhibiti, kuna sehemu watu wanajilinda wenyewe na smg. Halafu unakuja na maneno meengi ya kusifia vitu usivyovijua. Kenya is like a jungle, everyone is striving hard to make a living, otherwise you will be eatenby your fellow people. Ndiyo maana kule pokot wana mifugo mingi, na wako katika hatari ya kuvamiwa na kuuawa huku wakiporwa mifugo yao, lkn serikali haifanyi kitu. matokeo yake wananchi wa kule wamejinunulia smg kutoka wanakokujua wao wenyewe, ili wajilinde. serikali ya kenya wala haina habari na hilo. Yaani ni shida. lkn cha kushangaz unasifia mpaka unatia huruma. kwa kifupi, nenda nchi hizo nilizo kutajia halafu ulinganishe na kesha, nadhani utakuwa na mtazamo uliobadirika na bora zaidi.
wacha Wivu Mingi WWE😆
 
Andiko lefu sana, lkn vingi hapo ni hisia tu. Kwa hiyo ili uwe askari bongo, lazima utokee chipkiz ya sisiem (mbavu zangu 🤣 🤣 🤣 ). Lkn niongee kwa kifupi tu. wengi wanaochangia uzi huu ni wale exposure yao imefikia,labda sana sana nairobi. lkn kwa mtu ambaye ameenda nchi nyingine za Afrika. Hususan ni za kusini kama Botswana, Namibia na sasa Angola. ukiwahi fika nchi hizi na kujua siasa zake, hutakuja tena kuongea kuhusu nchi ya kenya. a bandit society, unaipa sifa lukuki wakati kuna uozo uliopitiliza. Nchi haina udhibiti, kuna sehemu watu wanajilinda wenyewe na smg. Halafu unakuja na maneno meengi ya kusifia vitu usivyovijua. Kenya is like a jungle, everyone is striving hard to make a living, otherwise you will be eatenby your fellow people. Ndiyo maana kule pokot wana mifugo mingi, na wako katika hatari ya kuvamiwa na kuuawa huku wakiporwa mifugo yao, lkn serikali haifanyi kitu. matokeo yake wananchi wa kule wamejinunulia smg kutoka wanakokujua wao wenyewe, ili wajilinde. serikali ya kenya wala haina habari na hilo. Yaani ni shida. lkn cha kushangaz unasifia mpaka unatia huruma. kwa kifupi, nenda nchi hizo nilizo kutajia halafu ulinganishe na kesha, nadhani utakuwa na mtazamo uliobadirika na bora zaidi.
Ata Nigeria na Liberia Kuna Usalama hatari,heri Kenya Usalama uko shwari😏Na usisahau wame border Nchi amabazo zimejaa Terrorists Lakini Bado Kenya iko Imara bana🔥🇰🇪🔥Wacha kudanganya watu wwe
 
Andiko lefu sana, lkn vingi hapo ni hisia tu. Kwa hiyo ili uwe askari bongo, lazima utokee chipkiz ya sisiem (mbavu zangu 🤣 🤣 🤣 ). Lkn niongee kwa kifupi tu. wengi wanaochangia uzi huu ni wale exposure yao imefikia,labda sana sana nairobi. lkn kwa mtu ambaye ameenda nchi nyingine za Afrika. Hususan ni za kusini kama Botswana, Namibia na sasa Angola. ukiwahi fika nchi hizi na kujua siasa zake, hutakuja tena kuongea kuhusu nchi ya kenya. a bandit society, unaipa sifa lukuki wakati kuna uozo uliopitiliza. Nchi haina udhibiti, kuna sehemu watu wanajilinda wenyewe na smg. Halafu unakuja na maneno meengi ya kusifia vitu usivyovijua. Kenya is like a jungle, everyone is striving hard to make a living, otherwise you will be eatenby your fellow people. Ndiyo maana kule pokot wana mifugo mingi, na wako katika hatari ya kuvamiwa na kuuawa huku wakiporwa mifugo yao, lkn serikali haifanyi kitu. matokeo yake wananchi wa kule wamejinunulia smg kutoka wanakokujua wao wenyewe, ili wajilinde. serikali ya kenya wala haina habari na hilo. Yaani ni shida. lkn cha kushangaz unasifia mpaka unatia huruma. kwa kifupi, nenda nchi hizo nilizo kutajia halafu ulinganishe na kesha, nadhani utakuwa na mtazamo uliobadirika na bora zaidi.
Being a son of a gun doesn't mean you've lost life direction buddy. Pili,laiti ungejua naandika nikiwa wapi,usingetoa mifano ya hizo nchi za ajabu ajabu! Pole sana kaka
 
Being a son of a gun doesn't mean you've lost life direction buddy. Pili,laiti ungejua naandika nikiwa wapi,usingetoa mifano ya hizo nchi za ajabu ajabu! Pole sana kaka

Bado hizo ni hisia tu, jibu hoja. Hatuongelei wapi kila mmoja wetu anakoandikia. Maana hilo halitusaidii.

Kwa taarifa yako nchi unazoziita za ajabu ajabu, ndiyo nchi ambazo zinapigiwa mfano Afrika.
 
Ata Nigeria na Liberia Kuna Usalama hatari,heri Kenya Usalama uko shwari😏Na usisahau wame border Nchi amabazo zimejaa Terrorists Lakini Bado Kenya iko Imara bana🔥🇰🇪🔥Wacha kudanganya watu wwe

Jibuni hoja jamani. Naelezea what is the mood on ground in Kenya. Nyie mnaongea mambo yasiyo eleweka.
Mengi tutaelewana kipindi cha uchaguzi 2022.
 
Back
Top Bottom