Hatuutaki mfumo dume tunautaka mfumo gani?

mnyikungu

JF-Expert Member
Jul 26, 2009
1,960
2,464
Mi nashangaa sana eti mjadala wa sasa ni 'haki sawa kwa wote' eti wakiwa na maana kuwa mwanamme na mwanamke wote wawe sawa kwenye kila nyanja, wana hoja yao eti wanawake wamekandamizwa mda mrefu hinyo wanataka kujikomboa kwa hilo.
kelele zao kubwa eti ni kuuzika mfumo dume! hivi walishawahi kujiuliza ule msemo wa babu zetu wa mafahari wawili hawakai zizi moja ulikuwa unamaanisha nini? haki sawa ni kitu ambacho hakiwezekani, toka enzi mifumo ilikuwa miwili tu yaani au wa wanawake kutawala kama baadhi ya makabila ya tanga au wanaume kuwa juu, mifumo hii miwili kamwe haiwezi kufanya kazi poamoja.
eti wanataka uchaguzi ujao bunge liwe na usawa! yaani tuchague kwa jinsia au kwa ubora wa kiongozi?hata tusemaje kuna tofauti kubwa mno kati ya mwanamke na mwanaume, wanaume ni watu wa kufanya wanawake ni watu wa kufanjiwa, hata wao huthibitisha hili.
siku hizi ndoa zinavurugika eti kisa wanawake wanataka haki, hivi ni nchi gani wanawake na wanaume wana haki sawa? hata hao wanaowapa vijihela NGO kuja kutuvuruga kwa hili kwao hamna kitu usawa, mke wa crinton mwenyewe sababu moja wapo ya kushidwa ilikuwa ni jinsia yake,yaani wazungu wasivyoipenda langi nyeusi kwa mwanamke kuwa raisi wao waliona bora hiyo rangi nyeusi.kama kweli mnaweza ukataeni upendeleo twende bega kwa bega tuone mtafika wapi? maana hata hizi harakati zao wanasaidiwa na wanamme.
Tusikubali kuyumbishwa na wazungu kwa hili tushikirie utamaduni wetu ili tuishi kwa misingi bora
 
Simba dume ndiyo humiliki kaya yake, jogoo ndiyo humiliki majike yote, hata ng'ombe utaona dume ndilo humiliki kundi zima, beberu ndiyo mfalme kwa majike yote, hata wadudu, dume ndilo lenye mamlaka nk. nk. nk......... orodha ni ndefu. Huu ni mpango wa Mungu alipoumba viumbe wake, lazima awepo kiongozi na akamweka mwanaume/dume kuongoza kaya. Wanaopingana na mfumo huu wanajaribu kumsahihisha Mungu na hivyo adhabu yao ni MOTO WA MILELE. Kwa mwanadamu Mungu alimuumba Adam kwanza halafu Hawa akatolewa katika ubavu wake, hata baada ya dhambi kuingia, Mungu alitamka wazi kwa mwanamke kwamba atatawaliwa na mumewe (Mwanzo 3:15).

Hizi kampeni ni za yule Ibilisi mkuu wa giza ambaye alimdanganya mwanamke na sasa kaibuka tena anawadanganya kwa mbinu hii ya USAWA. Hili haliwezekani. Na ninyi wanawake, kuweni makini na haya madai yenu, laa sivyo mnatafuta tena laana nyingine. Na ninyi wanaume, kumbukeni Hawa alipompelekea tunda Adamu naye akala wote waliingia katika dhambi, hivyo, wanawake wamekuja na mbinu ile ile ya kuwapeni tunda ili mkubaliane nao kumpinga Mungu. Mtakiona cha moto. SHAURI YENU, ILA MIMI SIMO KABISA. Mwenye masikio na asikie. Mzee Kibiongo kanena.
 
Simba dume ndiyo humiliki kaya yake, jogoo ndiyo humiliki majike yote, hata ng'ombe utaona dume ndilo humiliki kundi zima, beberu ndiyo mfalme kwa majike yote, hata wadudu, dume ndilo lenye mamlaka nk. nk. nk......... orodha ni ndefu. Huu ni mpango wa Mungu alipoumba viumbe wake, lazima awepo kiongozi na akamweka mwanaume/dume kuongoza kaya. Wanaopingana na mfumo huu wanajaribu kumsahihisha Mungu na hivyo adhabu yao ni MOTO WA MILELE. Kwa mwanadamu Mungu alimuumba Adam kwanza halafu Hawa akatolewa katika ubavu wake, hata baada ya dhambi kuingia, Mungu alitamka wazi kwa mwanamke kwamba atatawaliwa na mumewe (Mwanzo 3:15).

Hizi kampeni ni za yule Ibilisi mkuu wa giza ambaye alimdanganya mwanamke na sasa kaibuka tena anawadanganya kwa mbinu hii ya USAWA. Hili haliwezekani. Na ninyi wanawake, kuweni makini na haya madai yenu, laa sivyo mnatafuta tena laana nyingine. Na ninyi wanaume, kumbukeni Hawa alipompelekea tunda Adamu naye akala wote waliingia katika dhambi, hivyo, wanawake wamekuja na mbinu ile ile ya kuwapeni tunda ili mkubaliane nao kumpinga Mungu. Mtakiona cha moto. SHAURI YENU, ILA MIMI SIMO KABISA. Mwenye masikio na asikie. Mzee Kibiongo kanena.
kweli huyu ni shetani
 
...As it was in the beginning JAH created everything, he gave MEN dominion over all things, but now its too late, you see MEN has lost all .......(hata Bob Marley ali quote from the bible) Kweli kwenye Bibble hiyo ipo na MUNGU alituagiza hivyo lkn sisi wanadamu always against GOD. Repent ye!!!!!! people of the world, hath wrath of GOD will destroy thy WORLD!!
 
Kuna vitu vingi sana vya kuangalia tunapojaribu kuwapa kipaumbele hawa mama zetu. Kwanza lazima tofauti kati ya SEX, GENDER, Gender equity, gender equality na mengineyo ieleweke. When looking at the subject as it is, unaweza kusema kumepotoka sana ila kiukweli ni kuteleza tu ambako bado hata hatujaanguka. We are preaching of profficiency, efficiency and effectiveness at work and yet we are talking of giving some posts to individuals/persons on the ground of balanced gender. Are we in a free market or we trying to pull back into the communism states? To me giving them equal and fair respect on what they are capable of isn't a problem, the problems comes pale kila kitu cha mwanamke kinapoonekana kuwa bora zaidi ya mwanaume hata kama kimezidiwa kinapendelewa. For instance katika education wasichana wanapewa upendeleo dhidi ya wavulana and yet all pupils seat in the same class na wanafundishwa na mwalimu huyo huyo. Sa ndugu zangu hapa tunaongelea usawa wa aina gani? if messing up wanamess ile mbaya. Nionavyo mimi ni bora na heri tuache nature ichukue nafasi yake na sisi wanaume tusiwagandamize simply because they are women. Pitia maneno hayo hapo juu, Sex, Gender (all its associated terminologies) hapo ndio tutaweza kujadili hili vizuri. Vitabu vitakatifu vinasehemu yake ila sijavipuuza (ignore) coz kila mtu anaimani yake, ila kinachonisumbua mimi ni pale baadhi ya wanaume wanopkuwa mbele mbele kuwasupport wanawake kwa interest zao binafisi pasipo hao wanawake kujua kuwa wanatumiwa kama ngazi ya kuwawezesha hao mabwana kuarchieve objectives zao.
 
Ananilea Nkya akiwasikia,anawamaliza ninyi,hamjui kuwa jana ndo katunukiwa tuzo ya harakati za jinsia?

Hayo hapo juu, tuachane nayo,jambo ambalo huwa najiuliza ni mwanamke wa aina gani ambaye harakati hizi zinalenga kumkomboa.Agenda imekuwa ni kwa mwanamke kunyanyaswa na mumewe.Lakini ukichunguza kwa undani asilimia karibu 99% ya wanaharakati wanawake,wote hawako kwenye ndoa.Wengi wameachika na wengine hawajaolewa kabisa.
 
Tatizo nikuwa watu wanaume na wanawake pia wamechukulia vibaya hii dhana ya haki sawa kwa wote. Haitakuja itokee mwanaume akawa sawa na mwanamke kwa sababu za kimaumbile,mazingira na hata kidini.
Ni ukweli kwamba wanaume wengi wanachukulia advantage yao waliyopewa na Mungu kumtawala mwanamke kwa kumkandamiza na kumuonea.Wanaume wengi wanamawazo hayo ya ukandamizaji japo siku hizi kwa ajili ya elimu watu wanabadilika.Ilifika kipindi mwanamke haruhusiwi kusoma eti kwa vile yeye ni wa kuolewa.sasa mambo kama haya ndio hayafai
kumtawala mtu haina maana umuonee.Kila mtu aelewe wajibu wake na mambo yataenda sawa.
Na sasa inavyokuja haya mambo ya haki sawa ,wanawake nao wanakuwa hawaelewi kwa kutaka kuwa watawala kitu ambacho si sahihi.
Cha msingi ni kuelewa wajibu ,kupendana na kuheshimiana.
 
Kuna vitu vingi sana vya kuangalia tunapojaribu kuwapa kipaumbele hawa mama zetu. Kwanza lazima tofauti kati ya SEX, GENDER, Gender equity, gender equality na mengineyo ieleweke. When looking at the subject as it is, unaweza kusema kumepotoka sana ila kiukweli ni kuteleza tu ambako bado hata hatujaanguka. We are preaching of profficiency, efficiency and effectiveness at work and yet we are talking of giving some posts to individuals/persons on the ground of balanced gender. Are we in a free market or we trying to pull back into the communism states? To me giving them equal and fair respect on what they are capable of isn't a problem, the problems comes pale kila kitu cha mwanamke kinapoonekana kuwa bora zaidi ya mwanaume hata kama kimezidiwa kinapendelewa. For instance katika education wasichana wanapewa upendeleo dhidi ya wavulana and yet all pupils seat in the same class na wanafundishwa na mwalimu huyo huyo. Sa ndugu zangu hapa tunaongelea usawa wa aina gani? if messing up wanamess ile mbaya. Nionavyo mimi ni bora na heri tuache nature ichukue nafasi yake na sisi wanaume tusiwagandamize simply because they are women. Pitia maneno hayo hapo juu, Sex, Gender (all its associated terminologies) hapo ndio tutaweza kujadili hili vizuri. Vitabu vitakatifu vinasehemu yake ila sijavipuuza (ignore) coz kila mtu anaimani yake, ila kinachonisumbua mimi ni pale baadhi ya wanaume wanopkuwa mbele mbele kuwasupport wanawake kwa interest zao binafisi pasipo hao wanawake kujua kuwa wanatumiwa kama ngazi ya kuwawezesha hao mabwana kuarchieve objectives zao.
japo nimesoma kwa shida post yako(badilisha rangi na font size bana) nakubaliana na wewe 87%
the rest is controversal.
 
.Ilifika kipindi mwanamke haruhusiwi kusoma eti kwa vile yeye ni wa kuolewa.sasa mambo kama haya ndio hayafai

unamaana gani? kumbuka kuna makabila ambayo kwa mila zao, shule is not important, kwa mfano, wamasai, mvulana is expected to herd cattle na msichana kuolewa. lakini kwa sababu za kimazingira zaidi, ilifika wakati watoto wa kiume wakawa wanenda shule WHY, because they were not yet moranis to be able to chunga mifugo, so as a way of passing time...sisi tulikuwa tunasema tumeenda shule kukua, walipelekwa shule ili muda ufike. lakini mtoto wa kike alitakiwa kukaa na mama ili ajifunze responsibilities kama mama as she was expected to be married off at a much younger age than the boys would marry. hatuwezi hata siku moja kuita tamaduni hizi ni za kishenzi...nakataa.walikuwa na maana kwa kabila lao.

kumtawala mtu haina maana umuonee.Kila mtu aelewe wajibu wake na mambo yataenda sawa.
Na sasa inavyokuja haya mambo ya haki sawa ,wanawake nao wanakuwa hawaelewi kwa kutaka kuwa watawala kitu ambacho si sahihi.
Cha msingi ni kuelewa wajibu ,kupendana na kuheshimiana.

hapo kwenye red unataka kutuambia kuwa tamaduni zilizokuwa zinapendelea mambo mabali mbali na kutokuwa na usawa walikuwa hawapendani? yani ndani ya nyumba? the problem is, we are forgeting that we Africans live a communal life, sisi sio baba na mama na watoto basi.......hapo ndo wanaharakati wanapojisahau.....USAWA is being advocated to families and not the the community.
Kwa mfano, kuna makabila ambayo, mnyama lazima achinjwe na wanaume, wanawake hawachinji mbuzi au ng'ombe, lakini pia, wanakula nyama zaidi ya wanawake. women never complained about that, they were getting their share. same to milk, women would handle milk and get the lions share out of it, men never complained.
Kuna makabila amabyo kuku akichinjwa, mapaja ni ya baba, full stop. no body complained then. LAKINI sasa hilo linaonekana ni uonevu, kila mtu anahaki ya kula paja, bab anatakiwa aache watoto wale kwanza. the same person ambaye alikulia kwenye mazingira ya baba kwanza leo hii anajifanya kwamba hilo sio jambo jema. Watoto walipendwa na watu wote, na walijisikia kupendwa. watoto walikuwa wanacheza na kula kwa majirani zao bila tatizo lolote. sasa hivi watu wanajisikia wamekuwa westernized sana, kama vile wapo londan. aaggreeeee
 
Watu tunajdanganya, mwanamke kutawalwa na mwanaume ni katiba ambayo mungu mwenyewe alitunga na akaptisha mwenyewe,na kama mwanadamu ametokana na mkono wa mungu basi utakua ukifata katiba hiyo,kama siyo kwa hiyari bas ni kwa lazima.mana kuna mazingira mwanamke mwenyewe anajitoa na kumpisha mwanamme atekereze majukumu yake.hii inaeleweka,watanzania tusiwe wajinga kwani kinacho fanyika sasa hivi ni kama vile tupo safarini, lakini wanaume tumeambie tumsubilie mwenzetu yuko nyuma,jaman hivyo vipaumbele vigawiwe sawa tusonge mbele kimaendeleo
 
,jambo ambalo huwa najiuliza ni mwanamke wa aina gani ambaye harakati hizi zinalenga kumkomboa.Agenda imekuwa ni kwa mwanamke kunyanyaswa na mumewe.Lakini ukichunguza kwa undani asilimia karibu 99% ya wanaharakati wanawake,wote hawako kwenye ndoa.Wengi wameachika na wengine hawajaolewa kabisa.

Mkuu umenena kitu cha maana sana....especially nilipo bold. My rough/informal research inaonyesha karibu 92% ya wanaojifanya wanataka haki sawa kati ya mwanaume na mwanamke wako fustrated na ndoa zao zimewashinda. Mfano kuna mama mmoja yuko between the age of 35-42 hivi, ni maarufu sana hapa Tanzania kwa kupiga mayowe ya huu upuuzi, lakini kila siku anabadilisha wanaume.....(naamini wanaume wanamkimbia) hata foundation yake ina migogoro tele!!

Huwa nashangaa wanaposema....oohhh wanawake wananyanyasika kwenye ndoa...lakini hawaonyeshi kujali wale wanaume ambao nao wananyanyasika kwenye ndoa zao, hawajali suala la mila na utamaduni wa kiafrika.

Ndo maana miaka hii mijini kumkuta mwanamke anampikia chakula mumewe ni nadra sana.......utamkuta house girl anapika..yeye yuko salon ana retouch nywele!!

Mi nimeshamwambia my wife wangu.....the moment she fails to do things an african woman is supposed to be doing to his man.....right away....I'm marrying another woman! Period
 
Mi nashangaa sana eti mjadala wa sasa ni 'haki sawa kwa wote' eti wakiwa na maana kuwa mwanamme na mwanamke wote wawe sawa kwenye kila nyanja, wana hoja yao eti wanawake wamekandamizwa mda mrefu hinyo wanataka kujikomboa kwa hilo.

Kwani kuna ubaya wowote binaadamu (watanzania) wote wakiwa na fursa sawa?


kelele zao kubwa eti ni kuuzika mfumo dume! hivi walishawahi kujiuliza ule msemo wa babu zetu wa mafahari wawili hawakai zizi moja ulikuwa unamaanisha nini? haki sawa ni kitu ambacho hakiwezekani, toka enzi mifumo ilikuwa miwili tu yaani au wa wanawake kutawala kama baadhi ya makabila ya tanga au wanaume kuwa juu, mifumo hii miwili kamwe haiwezi kufanya kazi poamoja.

Kwa hiyo unataka kusema ni lazima upande mmoja ukandamizwe ndo mambo yanaenda? Mimi naamini inawezekana kama tunaweza kubadilika kifikra. Najua itachukuwa muda lakini inawezekana. Ni lazima kuwepo na mahali pa kuanzia ndio maana unaona huo upendeleo kwenye nafasi za bunge na kwengineko.


eti wanataka uchaguzi ujao bunge liwe na usawa! yaani tuchague kwa jinsia au kwa ubora wa kiongozi?hata tusemaje kuna tofauti kubwa mno kati ya mwanamke na mwanaume, wanaume ni watu wa kufanya wanawake ni watu wa kufanjiwa, hata wao huthibitisha hili.

Ni vema kuzingatia ubora wa viongozi. Lakini sote mimi na wewe tunajua jinsi chaguzi hizi zinavyoendeshwa na aina ya viongozi tunaowapata. Ni lazima kuwe na namna nyingine ya intervention. Kutokana na sababu za kihistoria na kifikra bado sio rahisi kuwashindanisha wanaume na wanawake (ingawa kuna mafanikio kwa baadhi ya maeneo).

siku hizi ndoa zinavurugika eti kisa wanawake wanataka haki, hivi ni nchi gani wanawake na wanaume wana haki sawa? hata hao wanaowapa vijihela NGO kuja kutuvuruga kwa hili kwao hamna kitu usawa, mke wa crinton mwenyewe sababu moja wapo ya kushidwa ilikuwa ni jinsia yake,yaani wazungu wasivyoipenda langi nyeusi kwa mwanamke kuwa raisi wao waliona bora hiyo rangi nyeusi.kama kweli mnaweza ukataeni upendeleo twende bega kwa bega tuone mtafika wapi? maana hata hizi harakati zao wanasaidiwa na wanamme.

Nadhani kuna tatizo la uelewa wa mambo haya ya usawa wa kijinsia hata kwa baadhi ya wanaharakati wanawake. Kwanza ni vema kujua mabadiliko ya mfumo yanachukua muda mrefu na pia yanaguza vitu vingi. Si rahisi kuwabadilisha watu fikra overnight hivyo hata majumbani mwetu ni vema wanawake wakawa na subra na kuelewa kuwa mabadiliko yanakwenda polepole. Na kwa kweli mabadiliko yapo mengi tu kwenye familia zetu kuelekea kwenye usawa tunaouzungumzia.

Tusikubali kuyumbishwa na wazungu kwa hili tushikirie utamaduni wetu ili tuishi kwa misingi bora

Utamaduni wetu ni upi? nijuavyo mimi, utamaduni unabadilika. Tunacopy mambo mengi tu kutoka nje na hivyo hatuwezi kubakia palepale. Maendeleo ya kielimu na kikuchumi pia yanaleta mabadiliko mengi tu. Kwa mfano mwanamke msomi na anayejimudu kiuchumi hawezi kukubali kirahisi kuporwa haki zake na mwanaume na yeye akae kimya.
 
Hivi ni halali mimi kukaa home na watoto na jamaa kwenda kubeba zege au kibarua kwenye kiwanda cha chuma na kupata 2,800 per day, then arudi home nimwambie aogeshe watoto wakati mm napika?

Tuwe wakweli, hata kama kuna kufua na kupikia watoto - tuangalie uswazi, sio masaki. chumba kimoja utasema nafanya usafi nachoka sana? kwa kipato hicho nitakuwa nafua minguo mingi? itatoka wapi kwanza.
 
Hivi ni halali mimi kukaa home na watoto na jamaa kwenda kubeba zege au kibarua kwenye kiwanda cha chuma na kupata 2,800 per day, then arudi home nimwambie aogeshe watoto wakati mm napika?

Kugawana majukumu sio tatizo. Nadhani tatizo mnagawanaje hayo majukumu. Hapo umezungumzia kama baba ndo ameajiriwa, vipi kama wote wameajiriwa au mwanamke ndio ameajiriwa? Wanagawana vipi majukumu. Kama tukibadilika kifikra sidhani kama kuna haja ya mama kukwambia umuogesha mtoto wenu bali ni wewe mwenyewe utaona hiyo haja ya kutoa msaada. Kwani mwanaume akiogesha mtoto wake wa kumzaa kuna tatizo gani?
 
Mkuu umenena kitu cha maana sana....especially nilipo bold. My rough/informal research inaonyesha karibu 92% ya wanaojifanya wanataka haki sawa kati ya mwanaume na mwanamke wako fustrated na ndoa zao zimewashinda. Mfano kuna mama mmoja yuko between the age of 35-42 hivi, ni maarufu sana hapa Tanzania kwa kupiga mayowe ya huu upuuzi, lakini kila siku anabadilisha wanaume.....(naamini wanaume wanamkimbia) hata foundation yake ina migogoro tele!!

Huwa nashangaa wanaposema....oohhh wanawake wananyanyasika kwenye ndoa...lakini hawaonyeshi kujali wale wanaume ambao nao wananyanyasika kwenye ndoa zao, hawajali suala la mila na utamaduni wa kiafrika.

Ndo maana miaka hii mijini kumkuta mwanamke anampikia chakula mumewe ni nadra sana.......utamkuta house girl anapika..yeye yuko salon ana retouch nywele!!

Mi nimeshamwambia my wife wangu.....the moment she fails to do things an african woman is supposed to be doing to his man.....right away....I'm marrying another woman! Period

Haya yote uliyosema ndiyo 'mfumo dume' wenyewe!
 
Wanawake watabakia wanawake na wanaume watabakia wanaume milele milele amina. Usawa mathalan kwenye umilki wa mali ni nadharia tu na chimbuko lake ni past history ya wanawake wenyewe. Wakipewa kinakuwa chake binafsi . Cha wanaume ni cha wote.

Kwa hesabu hiyo baada ya muda mfupi kwa mfano zaidi ya nusu ya ardhi yote itakuwa mali ya wanawake ambao ndio wengi na hawataridhisha mwingine hata akifa, maana ndio asili yao. Then inakuwa hamna continuity tena. Dead end.
 
Kuna vitu vingi sana vya kuangalia tunapojaribu kuwapa kipaumbele hawa mama zetu. Kwanza lazima tofauti kati ya SEX, GENDER, Gender equity, gender equality na mengineyo ieleweke. When looking at the subject as it is, unaweza kusema kumepotoka sana ila kiukweli ni kuteleza tu ambako bado hata hatujaanguka. We are preaching of profficiency, efficiency and effectiveness at work and yet we are talking of giving some posts to individuals/persons on the ground of balanced gender. Are we in a free market or we trying to pull back into the communism states? To me giving them equal and fair respect on what they are capable of isn't a problem, the problems comes pale kila kitu cha mwanamke kinapoonekana kuwa bora zaidi ya mwanaume hata kama kimezidiwa kinapendelewa. For instance katika education wasichana wanapewa upendeleo dhidi ya wavulana and yet all pupils seat in the same class na wanafundishwa na mwalimu huyo huyo. Sa ndugu zangu hapa tunaongelea usawa wa aina gani? if messing up wanamess ile mbaya. Nionavyo mimi ni bora na heri tuache nature ichukue nafasi yake na sisi wanaume tusiwagandamize simply because they are women. Pitia maneno hayo hapo juu, Sex, Gender (all its associated terminologies) hapo ndio tutaweza kujadili hili vizuri. Vitabu vitakatifu vinasehemu yake ila sijavipuuza (ignore) coz kila mtu anaimani yake, ila kinachonisumbua mimi ni pale baadhi ya wanaume wanopkuwa mbele mbele kuwasupport wanawake kwa interest zao binafisi pasipo hao wanawake kujua kuwa wanatumiwa kama ngazi ya kuwawezesha hao mabwana kuarchieve objectives zao.
ni kweli tunatakiwa kuangalia namna ya kuwacare yaani kuwaheshimu ila kusema usawa hilo ni gumu kuna mambo ya kuyafanya mwanamke na kuna mambo ya kuyafanya mwanaume, wanawake tumewazidi sana kiakili na kimaamuzi sasa hatuwezi kulazimisha moja ikae mbili kama tunavyofanya hivi sasa, kwanza tumetafsiri vibaya yaani badala ya kuwaezesha sisi tunawapendelea.
 
Wanawake watabakia wanawake na wanaume watabakia wanaume milele milele amina. Usawa mathalan kwenye umilki wa mali ni nadharia tu na chimbuko lake ni past history ya wanawake wenyewe. Wakipewa kinakuwa chake binafsi . Cha wanaume ni cha wote.

Kwa hesabu hiyo baada ya muda mfupi kwa mfano zaidi ya nusu ya ardhi yote itakuwa mali ya wanawake ambao ndio wengi na hawataridhisha mwingine hata akifa, maana ndio asili yao. Then inakuwa hamna continuity tena. Dead end.
kwa mtindo huu nahisi baada ya miaka kadhaa wanaume nao watadai haki zao
 
ni kweli tunatakiwa kuangalia namna ya kuwacare yaani kuwaheshimu ila kusema usawa hilo ni gumu kuna mambo ya kuyafanya mwanamke na kuna mambo ya kuyafanya mwanaume

Ugumu unatokana na fikra/imani tulizonazo dhidi ya wanawake. Tukiweza kuondoka huko, suala la usawa sio gumu kihivyo. Nchi za scandinavia wamefanikiwa sana katika hili (ingawa bado sio 100%) na hiyo inaonesha kwamba ni suala linalowezekana.

wanawake tumewazidi sana kiakili na kimaamuzi sasa hatuwezi kulazimisha moja ikae mbili kama tunavyofanya hivi sasa, kwanza tumetafsiri vibaya yaani badala ya kuwaezesha sisi tunawapendelea.

'Kuwapendelea' hiyo ni intervention tu baada ya muda wataweza kusimama wenyewe sawa sawa na wanaume. Kwenye hilo la kuwazidi akili, sina cha kusema kwa sasa...ila ni debatable!
 
Back
Top Bottom