Hatutaruhusu kura yetu kuibiwa Igunga - CHADEMA

saliel

Member
Apr 11, 2011
84
18
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kitasimamia na kuhakikisha kuwa hakuna kura yake inayoibiwa katijka uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Igunga, mkoani Tabora hakitaliachia Jimbo la Igunga, mkoani Tabora kufanyika Oktoba 2, mwaka huuu.
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini (Chadema), Godbles Lema, alitoa kauli hiyo mjini Singida juzi jioni alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya kituo cha zamani cha mabasi.
Lema ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, alifafanua kuwa licha ya CCM kutamba kwamba jimbo hilo hawatalipoteza, lakini hawana jipya la kuwaeleza wananchi wa Igunga kutokana na ukali wa maisha unaowakabili watanzania hivi sasa.
Hata hivyo, Lema aliyefuatana na wabunge wa Viti Maalum wa Chadema, Chiku Abwao Mkoa wa Iringa na Regia Mtema (Morogoro) wakitokea Igunga, aliweka bayana kwamba ni ukweli usiopingika kwamba jimbo hilo ni lazima liende Chadema.
Alidai kuwa pamoja na mbinu chafu zinazotarajiwa kufanywa na chama tawala, lakini alisema chama chake kina uhakika wa kulichukua Jimbo la Igunga lililoachwa wazi na Rostam Azizi aliyejiuzulu kwa maelezo kuwa amechoshwa na siasa uchwara ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Ndugu zangu wana Singida wabunge wote wa Chadema mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Bunge la bajeti, tutakwenda majimboni kwanza kusalimia na kisha baadaye wote tutaelekeza nguvu zetu kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga na hakuna kura itakayoibiwa safari hii mpaka tutatangazwa kulinyakua jimbo hilo,” alisisitiza Lema huku akishangiliwa na wananchi waliokuwa wakimsikiliza.
Abwao alisema mara baada ya kuingia mkoani Singida wakitokea Igunga alisikitishwa sana baada ya kuwakuta wanawake wa mjini Singida wakiteseka kutafuta maji ambayo ni kazi ya siku nzima.
“Hivi ni kweli wanasingida mmeridhika muishi maisha haya mnayoishi?” alihoji Abwao na kuongeza: “Wenzenu wa Iringa maji tunamwaga mpaka vyooni maji ni ya kumwaga…kwa sababu Iringa tumeamka hatutaki kudanganywa.”
Kwa upande wake, Mtema alitumia fursa hiyo kuwataka Watanzania kutodanganyika kutoa kura zao kwa kupewa kanga, fulana, kofia, fedha taslimu na hata vyakula.
CHANZO: NIPASHE
 
strategies za kuhakikisha hawaibiwi ni zipi? maana si kuishia kuzungumza tu majukwaani. au huo ni mkakati wa ndani hautajwi tajwi hovyo! anyway all in all kazi kubwa lazima ifanyike kukabiliana na DED mteule wa rais na manyang'au wengine mawakala wa uchakachuaji
 
  • Thanks
Reactions: FJM
strategies za kuhakikisha hawaibiwi ni zipi? maana si kuishia kuzungumza tu majukwaani. au huo ni mkakati wa ndani hautajwi tajwi hovyo! anyway all in all kazi kubwa lazima ifanyike kukabiliana na DED mteule wa rais na manyang'au wengine mawakala wa uchakachuaji
<br />
<br />
mbinu zitakazotumika zitakuwa kama zile zilizotumika Tarime kwenye uchaguzi mdogo, kila kituo cha kupigia kura kunakuwa na mawakala watatu, hakuna anayemjua mwenzake. Hata hivyo kazi itakuwa rahisi kwa chadema, kwani wasimamizi watakuwa waalimu, ambao hawatapenda kumchakachua mwalimu mwenzao
 
CCM wizi upo kwenye dam. Wataiba tu, na mi nashauri tujipange sasa kuchukua nchi kanzia Igunga.
 
Wananchi wa Igunga ndio hao siku Rostam alipobwaga manyanga walilia na kusaga meno na kuzirai. Nina imani watachagua magamba tena
 
Nasikia wale walioangua kilio walikuwa wamelipwa.
Are u serious mkuu? Mtu alipwe kwaajili ya kulia na kuzirai?? Basi ina maana kwenye misiba mingi siku hizi ukiona waliaji ni wengi kumbe wengine wamelipwa!!! Ha!
 
kikubwa cha kuangalia ni uhesabuji na ukaguzi wa program zinazotumika na NEC. ninavyohisi kama programmer what greencard does is; if x =greenbalots, and y=cdmbalots, then greenbalots= x + 0.6cdm balots and
cdm balots=0.4 y. Ndugu zanguni sasa hivi codes ndizo zinazotuua kwa sababu you see what you input but results from the system are different from the manual ones
 
strategies za kuhakikisha hawaibiwi ni zipi? maana si kuishia kuzungumza tu majukwaani. au huo ni mkakati wa ndani hautajwi tajwi hovyo! anyway all in all kazi kubwa lazima ifanyike kukabiliana na DED mteule wa rais na manyang'au wengine mawakala wa uchakachuaji
si kila kitu kinapaswa kuanikwa lakini njia moja wapo ya kusimamia ni kuwafanya wana Igunga wajue umhimu wa kura zao, kuwa na wakala kila kituo, kuto kula chochote hovyo ili kupunguza kwenda chooni..
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
mbinu zitakazotumika zitakuwa kama zile zilizotumika Tarime kwenye uchaguzi mdogo, kila kituo cha kupigia kura kunakuwa na mawakala watatu, hakuna anayemjua mwenzake. Hata hivyo kazi itakuwa rahisi kwa chadema, kwani wasimamizi watakuwa waalimu, ambao hawatapenda kumchakachua mwalimu mwenzao
pesa kitu kingine kaka cha msingi kila mmoja awe mlizi wa mwenzake...
 
kikubwa cha kuangalia ni uhesabuji na ukaguzi wa program zinazotumika na NEC. ninavyohisi kama programmer what greencard does is; if x =greenbalots, and y=cdmbalots, then greenbalots= x + 0.6cdm balots and<br />
cdm balots=0.4 y. Ndugu zanguni sasa hivi codes ndizo zinazotuua kwa sababu you see what you input but results from the system are different from the manual ones
kwa kura za jimbo moja kushi kuzilinda ni upumbavu hata kama watakuwa na program ya aina yoyote...
 
Lema ametoa uhakika kuwa hakuna kura itakayo ibwa,Ina maana CCM wakishinda mtakubali matokeo? Kama mnasema watu wa igunga walilipwa kulia na kuzirai sasa kutakuwa na ugumu gani kuwalipa wachague CCM? Naona nyie CHADEMA kila siku zinavyo kwenda mnazidi kuwa matahira.
 
Are u serious mkuu? Mtu alipwe kwaajili ya kulia na kuzirai?? Basi ina maana kwenye misiba mingi siku hizi ukiona waliaji ni wengi kumbe wengine wamelipwa!!! Ha!
<br />
<br />Wewe hujui kwamba kuna vikundi vya kulia na kugalagala misibani? Umechelewa. Kimoja kipo hapo mburahati. Hata waombolezaji wa kawaida wafikapo karibu na msiba ndo hujipanga na kuambizana 'tuanze' hapo ndo kilio cha kusaga meno huanza.
Unadhani kama hawakukodia mafuso yaliyoletwa na bashe kutola Nzege yakiwa na wafuati kibao yalikuwa ya nini?
 
mbona mmeanza kulia lia mapema kabla hata mtanange wa igunga haujaanza mnatafuta huruma ya wapiga kura wa igunga, kuweni kama cuf ngangari, cdm acheni kulalama!
 
hivi vyama vimeshakagua daftari la majina ya wapiga kura...........mimi nilipata kuliona hivi karibuni mchezo mchafu umetendeka mule yani majina hayaendani na namba ya shahada za watu na mengine hayapo nadhani chadema,ccm na cuf lazima mmoja atakuwa anahujumu wenzake
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom