saliel
Member
- Apr 11, 2011
- 84
- 18
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kitasimamia na kuhakikisha kuwa hakuna kura yake inayoibiwa katijka uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Igunga, mkoani Tabora hakitaliachia Jimbo la Igunga, mkoani Tabora kufanyika Oktoba 2, mwaka huuu.
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini (Chadema), Godbles Lema, alitoa kauli hiyo mjini Singida juzi jioni alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya kituo cha zamani cha mabasi.
Lema ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, alifafanua kuwa licha ya CCM kutamba kwamba jimbo hilo hawatalipoteza, lakini hawana jipya la kuwaeleza wananchi wa Igunga kutokana na ukali wa maisha unaowakabili watanzania hivi sasa.
Hata hivyo, Lema aliyefuatana na wabunge wa Viti Maalum wa Chadema, Chiku Abwao Mkoa wa Iringa na Regia Mtema (Morogoro) wakitokea Igunga, aliweka bayana kwamba ni ukweli usiopingika kwamba jimbo hilo ni lazima liende Chadema.
Alidai kuwa pamoja na mbinu chafu zinazotarajiwa kufanywa na chama tawala, lakini alisema chama chake kina uhakika wa kulichukua Jimbo la Igunga lililoachwa wazi na Rostam Azizi aliyejiuzulu kwa maelezo kuwa amechoshwa na siasa uchwara ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Ndugu zangu wana Singida wabunge wote wa Chadema mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Bunge la bajeti, tutakwenda majimboni kwanza kusalimia na kisha baadaye wote tutaelekeza nguvu zetu kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga na hakuna kura itakayoibiwa safari hii mpaka tutatangazwa kulinyakua jimbo hilo, alisisitiza Lema huku akishangiliwa na wananchi waliokuwa wakimsikiliza.
Abwao alisema mara baada ya kuingia mkoani Singida wakitokea Igunga alisikitishwa sana baada ya kuwakuta wanawake wa mjini Singida wakiteseka kutafuta maji ambayo ni kazi ya siku nzima.
Hivi ni kweli wanasingida mmeridhika muishi maisha haya mnayoishi? alihoji Abwao na kuongeza: Wenzenu wa Iringa maji tunamwaga mpaka vyooni maji ni ya kumwaga kwa sababu Iringa tumeamka hatutaki kudanganywa.
Kwa upande wake, Mtema alitumia fursa hiyo kuwataka Watanzania kutodanganyika kutoa kura zao kwa kupewa kanga, fulana, kofia, fedha taslimu na hata vyakula.
CHANZO: NIPASHE
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini (Chadema), Godbles Lema, alitoa kauli hiyo mjini Singida juzi jioni alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya kituo cha zamani cha mabasi.
Lema ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, alifafanua kuwa licha ya CCM kutamba kwamba jimbo hilo hawatalipoteza, lakini hawana jipya la kuwaeleza wananchi wa Igunga kutokana na ukali wa maisha unaowakabili watanzania hivi sasa.
Hata hivyo, Lema aliyefuatana na wabunge wa Viti Maalum wa Chadema, Chiku Abwao Mkoa wa Iringa na Regia Mtema (Morogoro) wakitokea Igunga, aliweka bayana kwamba ni ukweli usiopingika kwamba jimbo hilo ni lazima liende Chadema.
Alidai kuwa pamoja na mbinu chafu zinazotarajiwa kufanywa na chama tawala, lakini alisema chama chake kina uhakika wa kulichukua Jimbo la Igunga lililoachwa wazi na Rostam Azizi aliyejiuzulu kwa maelezo kuwa amechoshwa na siasa uchwara ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Ndugu zangu wana Singida wabunge wote wa Chadema mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Bunge la bajeti, tutakwenda majimboni kwanza kusalimia na kisha baadaye wote tutaelekeza nguvu zetu kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga na hakuna kura itakayoibiwa safari hii mpaka tutatangazwa kulinyakua jimbo hilo, alisisitiza Lema huku akishangiliwa na wananchi waliokuwa wakimsikiliza.
Abwao alisema mara baada ya kuingia mkoani Singida wakitokea Igunga alisikitishwa sana baada ya kuwakuta wanawake wa mjini Singida wakiteseka kutafuta maji ambayo ni kazi ya siku nzima.
Hivi ni kweli wanasingida mmeridhika muishi maisha haya mnayoishi? alihoji Abwao na kuongeza: Wenzenu wa Iringa maji tunamwaga mpaka vyooni maji ni ya kumwaga kwa sababu Iringa tumeamka hatutaki kudanganywa.
Kwa upande wake, Mtema alitumia fursa hiyo kuwataka Watanzania kutodanganyika kutoa kura zao kwa kupewa kanga, fulana, kofia, fedha taslimu na hata vyakula.
CHANZO: NIPASHE