Hatutapata katiba mpya kwakuwa tumeingiza katika siasa

Abel 2015

Senior Member
Sep 5, 2015
112
55
Juzi tati Uingereza swala la E.U Lilikua halina itikadi za kisiasa.David Cameroon alipishana na wanachama wenzao kuhusu swala hili, mfano alipishana na Boris Johnson na Thereza may wote wa concervative.

Baadhi ya wabunge na wanachama wa labour waliungana na wa chama cha concervative mfano kiongoz wa upinzan Jeremy Corbyn akawa kitu kimoja na Cameroon.Hapa kwetu Tz swala la katiba mpya limeingiliwa na msimamo isiyo na tija, CCM wanataka wanachama wao wawe na msimamo mmoja same to vyama vya upinzani.

Swala la katiba ni la kitaifa hakuna ulazima kuingiza misimamo ya kiitikadi kwani kwa mwendo huo kupata katiba ni ndoto, tujaribu kuwaiga wakoloni wetu kama baba wa demokrasia ambapo tumetoa mambo mengi ya kiutawala.

Abel Elijah Sere
 
Back
Top Bottom