Hatutakubali serikali yetu kuaibishwa na wanasheria wasiojua sheria kama hawa

Sokoro waito

JF-Expert Member
Nov 21, 2014
2,201
2,587
Wale walio wanasheria au wajuzi wa sheria popote mlipo mnatambua kabisa kuwa kabla ya kupeleka hati za mashitaka au maombi ama kiapo mahakamani ili kufungua kesi au maombi yoyote, ni lazima kwanza uyapitie tena ili kuyahakiki na kuona kama kuna kitu au jambo limesahaulika.

Kwa mfano: Tarehe na sehemu ulipoapia kwenye kiapo na mengineyo yaliyo muhimu. Lakini hali imekuwa tofauti kwa wanasheria hawa waliopeleka maombi ya pingamizi la dhamana kuzuia tundu lisu asipewe dhamana.

Haiwezekani washindwe kirahisi kiasi hicho kujaza tarehe na sehemu walipoapia kiapo chao, ukizingatia kuwa hii ilikuwa ni kesi kubwa iliyohitaji umakini mkubwa, na hatahivyo walikuwa wanasheria zaidi ya mmoja, iweje sasa washindwe wote kukipitia kiapo hicho kabla ya kukipeleka mahakamani.

Badala yake wameiaibisha serikali kwa kushindwa katika hatua ya awali kabisa. Haliwezekani kufikirika jambo hili, wanasheria hawa wakamatwe wahojiwe kwanini washindwe kirahisi hivyo na waseme ukweli maana huenda hawa wanasheria wako pamoja na tundu lisu japokuwa walijifanya kumpinga mahakamani. Hatutaki wanasheria dhaifu
 
Huwa kuna story, kuwa Mbwa akimuona au kuhisi harufu ya chatu,hujipeleka mwenyewe mdomoni.Ndivyo mlivyo wanasheria wengi wa Tanzania kwa Tundu Lisu.Uwezo wenu Mdogo kwa huyu nguli wa sheria.
Si ajabu hata wewe unayewasema wenzio,ukawa huna Uwezo kupambana na Lisu.
 
Wale walio wanasheria au wajuzi wa sheria popote mlipo mnatambua kabisa kuwa kabla ya kupeleka hati za mashitaka au maombi ama kiapo mahakamani ili kufungua kesi au maombi yoyote, ni lazima kwanza uyapitie tena ili kuyahakiki na kuona kama kuna kitu au jambo limesahaulika. Kwa mfano: Tarehe na sehemu ulipoapia kwenye KIAPO na mengineyo yaliyo muhimu. LAKINI HALI IMEKUWA TOFAUTI KWA WANASHERIA HAWA WALIOPELEKA MAOMBI YA PINGAMIZI LA DHAMANA KUZUIA TUNDU LISU ASIPEWE DHAMANA. Haiwezekani washindwe kirahisi kiasi hicho kujaza tarehe na sehemu walipoapia kiapo chao, ukizingatia kuwa hii ilikuwa ni KESI KUBWA iliyohitaji umakini mkubwa, na hatahivyo walikuwa wanasheria zaidi ya mmoja, iweje sasa washindwe wote kukipitia kiapo hicho kabla ya kukipeleka mahakamani. BADALA YAKE WAMEIAIBISHA SERIKALI KWA KUSHINDWA KATIKA HATUA YA AWALI KABISA. Haliwezekani kufikirika jambo hili, Wanasheria hawa wakamatwe wahojiwe kwanini washindwe kirahisi hivyo na waseme ukweli maana huenda hawa wanasheria wako pamoja na TUNDU LISU JAPOKUWA WALIJIFANYA KUMPINGA MAHAKAMANI. HATUTAKI WANASHERIA ******.
Kesi kubwa kivipi?? Ameua au amefanya uhaini? Jipange urudi tena!Tena hao jamaa hawana uhusiano wowote na Lissu wamefanya hivyo kwa makusudi manake hawaoni mantiki ya kisheria ya hiyo kesi,na wanajua atashinda na serikali itabidi kumlipa fidia ya usumbufu!Viva Lissu
 
Wale walio wanasheria au wajuzi wa sheria popote mlipo mnatambua kabisa kuwa kabla ya kupeleka hati za mashitaka au maombi ama kiapo mahakamani ili kufungua kesi au maombi yoyote, ni lazima kwanza uyapitie tena ili kuyahakiki na kuona kama kuna kitu au jambo limesahaulika. Kwa mfano: Tarehe na sehemu ulipoapia kwenye KIAPO na mengineyo yaliyo muhimu. LAKINI HALI IMEKUWA TOFAUTI KWA WANASHERIA HAWA WALIOPELEKA MAOMBI YA PINGAMIZI LA DHAMANA KUZUIA TUNDU LISU ASIPEWE DHAMANA. Haiwezekani washindwe kirahisi kiasi hicho kujaza tarehe na sehemu walipoapia kiapo chao, ukizingatia kuwa hii ilikuwa ni KESI KUBWA iliyohitaji umakini mkubwa, na hatahivyo walikuwa wanasheria zaidi ya mmoja, iweje sasa washindwe wote kukipitia kiapo hicho kabla ya kukipeleka mahakamani. BADALA YAKE WAMEIAIBISHA SERIKALI KWA KUSHINDWA KATIKA HATUA YA AWALI KABISA. Haliwezekani kufikirika jambo hili, Wanasheria hawa wakamatwe wahojiwe kwanini washindwe kirahisi hivyo na waseme ukweli maana huenda hawa wanasheria wako pamoja na TUNDU LISU JAPOKUWA WALIJIFANYA KUMPINGA MAHAKAMANI. HATUTAKI WANASHERIA ******.
Acha hasira sheria ni technical kosa dogo linakutoa knockout.

By the way umewahi kusikia kitu kinaitwa mikataba mibovu hawa ndiyo waliotufikisha huko
 
Wee sikia, nikupe just hints..!!

1: Wanasheria wengi vi.laza sana, tokea A-level wanachukua masomo ya Arts, HGL, HKL, ni vil.aza sana, kama huamini hili, wakumbuke ur friends wa A-level au hata O-level waliochukua masomo hayo ya Arts, ni vi.laza mno... So vikija soma laws kidogo na u.kilaza wao wanajiona wako ON TOP OF THE WORLD.... kumbe chicke.n head kabisa...!!

2: Never ever expect umakini kwa wanasheria as i mentioned most their background ni vi.laza mno... wengine hata kujenga hoja tu hawawezi kazi yao UBISHI, na wakidhania UBISHI ndio hoja... most 95% even legal argument hawawezi, they can't stick ktk issue unao argue nao legally, wanaongea very general...

So, wakikutana uso kwa uso na mtu kama Tundu Lissu anaye practice Law kila siku, kwa miaka, anawatoa Knock out...!!

Nimalizie tu, don't expect umakini kwa watu wenye background ya Arts subjects, hasa kwa Africa, hilo sahau...!!
 
Tatizo sio wanasheria,tatizo ni yule anaewamrisha wanasheria kufanya jambo ambalo haliwezekani. Lisu ajavunja sheria na mahakama haiwezi kumhukumu.
Na kamishna wa viapo na yeye akataka kuonyesha jinsi gani hii ni serikali ya mwendokasi akaamua kutoandika anuani na tarehe.
 
Wee sikia, nikupe just hints..!!

1: Wanasheria wengi vi.laza sana, tokea A-level wanachukua masomo ya Arts, HGL, HKL, ni vil.aza sana, kama huamini hili, wakumbuke ur friends wa A-level au hata O-level waliochukua masomo hayo ya Arts, ni vi.laza mno... So vikija soma laws kidogo na u.****** wao wanajiona wako ON TOP OF THE WORLD.... kumbe chicke.n head kabisa...!!

2: Never ever expect umakini kwa wanasheria as i mentioned most their background ni vi.laza mno... wengine hata kujenga hoja tu hawawezi kazi yao UBISHI, na wakidhania UBISHI ndio hoja... most 95% even legal argument hawawezi, they can't stick ktk issue unao argue nao legally, wanaongea very general...

So, wakikutana uso kwa uso na mtu kama Tundu Lissu anaye practice Law kila siku, kwa miaka, anawatoa Knock out...!!

Nimalizie tu, don't expect umakini kwa watu wenye background ya Arts subjects, hasa kwa Africa, hilo sahau...!!

Hivi kuna kigezo cha mtu aliesoma sayansi Advance aweze kusomea sheria?
Najua sheria ni kwa watu wa Arts tu
 
Thank God mtu kama wewe huna cheo chochote serikalini, maana ukipewa uongozi utakua kama wengi waliopo sasa hivi, mnaendeshwa na moyo sio akili.

Wameshindwa kesi kwa hiyo wakamatwe kuhojiwa! Hehehe watu wengine sijui bongo zenu zina nini ndani. Walikua hawana stand yoyote kushinda ile kesi, hata ungeleta lawyer kutoka Harvard pale angechemka tu. Tafadhali kabla hujaanzisha mada em tafuta mtu wako wa karibu mwambie akague ulichoandika, mnajaza tu server na ujinga, watoto wasijeiga, tunajitahidi kukuza watoto ambao hawatokua kama watu wa generation hii miaka ijayo.
 
Hivi kuna kigezo cha mtu aliesoma sayansi Advance aweze kusomea sheria?
Najua sheria ni kwa watu wa Arts tu

Think usiandike andike tu..!!

In general, lazima usome Arts subjects ili uwe lawyer baadae...!! Iko hivyo...!!

But, nimekwambia hapo juu, kama una memory nzuri, just kumbuka few of ur friends tokea O-level, A-level waliosomea Arts subjects, ni vi.la.za sana sana, of which wengi ni wanasheria leo...!! Take few mins, wakumbuke...!!

So, kutegemea umakini, kwa watu hao ni ngumu, wengi walikuwa maa.ndazi kweli..!!
Ni wachache sana walikuwa brilliant ktk masomo ya arts... mm hata siwakumbuki..!!
 
Hata state attorneys wakati fulani huwa hawafurahii baadhi ya kesi bali hulazimizwa tu na wakubwa wao kisiasa, hivyo wanafanya kwa shingo upande tu kuwafurahisha wakubwa. Usikute hiyo ni hujuma ya hao wawakili wa nchi.
 
Wale walio wanasheria au wajuzi wa sheria popote mlipo mnatambua kabisa kuwa kabla ya kupeleka hati za mashitaka au maombi ama kiapo mahakamani ili kufungua kesi au maombi yoyote, ni lazima kwanza uyapitie tena ili kuyahakiki na kuona kama kuna kitu au jambo limesahaulika. Kwa mfano: Tarehe na sehemu ulipoapia kwenye KIAPO na mengineyo yaliyo muhimu. LAKINI HALI IMEKUWA TOFAUTI KWA WANASHERIA HAWA WALIOPELEKA MAOMBI YA PINGAMIZI LA DHAMANA KUZUIA TUNDU LISU ASIPEWE DHAMANA. Haiwezekani washindwe kirahisi kiasi hicho kujaza tarehe na sehemu walipoapia kiapo chao, ukizingatia kuwa hii ilikuwa ni KESI KUBWA iliyohitaji umakini mkubwa, na hatahivyo walikuwa wanasheria zaidi ya mmoja, iweje sasa washindwe wote kukipitia kiapo hicho kabla ya kukipeleka mahakamani. BADALA YAKE WAMEIAIBISHA SERIKALI KWA KUSHINDWA KATIKA HATUA YA AWALI KABISA. Haliwezekani kufikirika jambo hili, Wanasheria hawa wakamatwe wahojiwe kwanini washindwe kirahisi hivyo na waseme ukweli maana huenda hawa wanasheria wako pamoja na TUNDU LISU JAPOKUWA WALIJIFANYA KUMPINGA MAHAKAMANI. HATUTAKI WANASHERIA ******.
Nadhani huwajui vizuri wale wanasheria wa serikali kwenye Ile kesi. Wale jamaa ni vichwa na hata mawakili wote wanawafahamu. Kama unabisha fuatilia kesi moja ya Ling Ling ya mahakama ya rufaa na wale jamaa ndo waliiwakilisha serikali na kushinda. wale jamaa ndo waliargue na kushinda. Uwe unauliza kabla hata hujakurupuka kupost huku.
 
Kesi kubwa kivipi?? Ameua au amefanya uhaini? Jipange urudi tena!Tena hao jamaa hawana uhusiano wowote na Lissu wamefanya hivyo kwa makusudi manake hawaoni mantiki ya kisheria ya hiyo kesi,na wanajua atashinda na serikali itabidi kumlipa fidia ya usumbufu!Viva Lissu
Hawajafanya kwa makusudi ndugu "uwezo wao ni mdogo tuu" so kusema wamefanya makusudi unawapendelea ndugu!!
 
Back
Top Bottom