Hatutaki Mbowe aachiwe huru, tunataka Serikali iliyomshitaki kwa ugaidi iithibitishie dunia ugaidi wake

My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,283
Kuna nyuzi nyingi mno humu hasa za mataga zikimshauri Rais Samia asimwachie huru Mbowe.

Kosa yote usikose akili, mataga hayajui kuwa Rais haruhusiwi kisheria kuingilia Mahakama, shauri la Mbowe lipo Mahakamani kwa hiyo Rais hahusiki.

Sisi wanachama wa Chadema hatutaki mwenyekiti wetu Mbowe aachiwe huru, tunataka Serikali iliyomshtaki kwa ugaidi iidhibitishie Dunia ugaidi wa Mbowe na siyo kumwachia huru.

Tunazo taarifa za kina na uhakika jinsi Serikali inavyowatuma wanafamilia ili wamsihi Mbowe akubali yaishe.

Kwa sababu kesi ipo Mahakamani siwezi kusema yote yanayoendelea.

Kifupi ni kwamba, Mbowe alijua kuwa atakamatwa, kwa hiyo hana cha kupoteza kabisa na yupo tayari hata kufa.

Wana CCM, mtake msitake, Mbowe ni Mandela wa Tanzania. Mkisikia hivyo it makes you go nuts, kesi mlianzisha wenyewe bila kutathimini madhara ya kutunga uongo, sasa hivi mnataka kuitema ndoana wakati imeshanasa uulimi

Pambaneni na hii kesi hadi mwisho, iweje mnataka suluhu na Gaidi?
 
Kesi ya mchongo

Majaji wa mchongo

Polis wa mchongo

Mashahidi wa jamuhuri wa mchongo.

Jaji pamoja na kukiri certificate seizure of seizure imeunganishwa na kuongezewa kurasa jaji huyu wa mchongo amepokea jinsi ilivyo kama kielelezo
Wakina chavula/kidando wa mchongo.

Inachekesha Sana

Jaji tiganga: mahakama haiwezi kuwa Dillema kama mshitakiwa aliteswa hatoni haja ya kupimwa hospitali kwa kuwa nawaona washtakiwa wote wana afya njema

Jaji: Naomba tuendelee na shauri
 
Kosa yote usikose akili, mataga hayajui kuwa Rais haruhusiwi kisheria kuingilia Mahakama,shauri la Mbowe lipo Mahakamani,kwa hiyo Rais hahusiki.

Sisi wanachama wa Chadema hatutaki mwenyekiti wetu Mbowe aachiwe huru, tunataka Serikali iliyomshtaki kwa ugaidi iidhibitishie Dunia ugaidi wa Mbowe na siyo kumwachia huru.
 
Kesi ya mchongo
Majaji wa mchongo
Polis wa mchongo....
Nimekuja gundua siasa za Tanzania n ujinga na uchafu mtupu, wenye akili wanawaendesha wasio na akili , siku zote nilijua watu tunapambana Mbowe aachiwe kumbe i was wrong, completely wrong, viongozi wangu wao kwao politics milage, political agenda n bora zaid kuliko Mbowe kuachiwa

Mahakama haipo huru, Mbowe atafungwa na chakufanya hatuna, tunaongozwa na vipofu wasiojia kisoma alama za nyakati, kimsingi ilipopatikana nafasi ya Mbowe kuachiwa alafu viongozi waakaanza vimba nilijua ni kias gani tulivyo na watu selfish , wako tayari mtu aozee jela kwa sababu ya ego za kijinga , busara n Muhim, n Muhim sana kutumika , tofaut na hapo anafungwa maisha na chakufanya hakuna
 
Kosa yote usikose akili, mataga hayajui kuwa Rais haruhusiwi kisheria kuingilia Mahakama,shauri la Mbowe lipo Mahakamani,kwa hiyo Rais hahusiki.
Sisi wanachama wa Chadema hatutaki mwenyekiti wetu Mbowe aachiwe huru, tunataka Serikali iliyomshtaki kwa ugaidi iidhibitishie Dunia ugaidi wa Mbowe na siyo kumwachia huru.
Rais wa wapi haruhusiwi? Raisi anaingilia kupitia DPP , acheni kua na akili finyu hivi
 
Kosa yote usikose akili, mataga hayajui kuwa Rais haruhusiwi kisheria kuingilia Mahakama,shauri la Mbowe lipo Mahakamani,kwa hiyo Rais hahusiki.
Sisi wanachama wa Chadema hatutaki mwenyekiti wetu Mbowe aachiwe huru, tunataka Serikali iliyomshtaki kwa ugaidi iidhibitishie Dunia ugaidi wa Mbowe na siyo kumwachia huru.
Burasa ni muhimu sana , tunaivimbia serikal na chakuifanya hatuna , Mbowe atafungwa maisha na chakufanya hatuna

Narudia tena, busara n Muhim mno mno mno mno
 
Mandela hakuachiwa huru hivihivi. Sababu za yeye kuachiwa huru si kwa sababu alikua na msimamo sana hivyo Kaburu akaona amuachie, jibu ni hapana. Aliachiwa huru sababu watu waliokua nje yaani Wana ANC na mkewe Winnie walikua wanakiwasha sana mitaa haitamaniki wala kutawalikika na sababu ya pili ulimwengu ulikua ushabadilika kutoka old school colonialism to neo colonialism hivyo Makaburu wakakosa support ya mabeberu wengine.

Sasa CDM katika hivyo hapo hawana hata kimoja support ya Wananchi hawana na si kwa bahati mbaya Chama wamekifanya kama mali yao pekee, maoni yao ndio ya maana mwengine ukiongea unaonekana ni msaliti ama unatumika (kiufupi ukiwa na mawazo tofauti wewe ni CCM). Mikutano ya ndani hawafanyi kujenga spirit ya wanachama kuona umuhimu wa Uhuru wa M/Kiti wanashinda space kujadili yale yale.

Na jambo lengine ni Western Countries don't give a damn kuhusu demokrasia za nchi za Africa wanachojali ni maslahi yao tu. Usipogusa maslahi yao you're safe na sidhani kama Tanzania ishaanza chezea Sharubu za Mabeberu katika maslahi yao.

And last but not list kua ndani kwa M/Kiti ndio asylum tickets ya watu wengine zinakua extended katika nchi za watu. So it's better for some yeye kuendelea kuwepo ndani kuliko kurudi uraiani.​
 
Back
Top Bottom