Hatunywi maji ndiyo maana tunauguwa

Fadhili Paulo

JF-Expert Member
Sep 1, 2011
3,211
987
kwa kawaida ukilima bustani unaimwagilia asubuhi kabla jua halijawa kali, na hata ukitembea umbali mrefu na gari na maji yakiisha katika injini hushuki tu na kuongeza maji mengine papo hapo! itakubidi usubiri injini ipowe ndipo uongeze maji!!!!....lakini sisi binadamu tunakunywa maji baada ya kusikia kiu, tena ya baridi!!, mwili wa binadamu unapopungukiwa maji hutoa ishara (indicators), tumeziita ishara hizo kuwa ni magonjwa. hauumwi, una kiu. kunywa maji kwa staili ifuatayo na ujitibu na ugonjwa wowote.


MAMBO YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZA TIBA YA MAJI:

Kanuni ya kimakisio kwa mahitaji ya maji ni; kunywa nusu ya uzito wako katika aunsi (ounces) ugawe mara mfululizo utakaoufuata kwa siku nzima. Kiasi kidogo chini au juu ya hiki, kinakubalika. Aunsi 1=miligramu 31.25.

Kanuni ya kimakisio kwa mahitaji ya chumvi ni, Robo tatu gramu za chumvi kwa kila nusu lita ya maji, nusu kijiko cha chakula kwa kila nusu galoni ya maji au kijiko kimoja cha chakula kwa kila galoni moja la maji.

Pengine umeshageuza kichwa na kujisemea, “Wewe ni kichaa.....hicho ni kiasi kingi sana cha maji”. Ukweli ni kuwa, ni rahisi kunywa hivyo hasa tukitumia sentensi, glasi 8 za maji zikigawanywa mara nane kwa siku (glasi 1 = ml 250 au robo lita).

Mfano, kwa mtu mwenye uzito wa kilogramu 75:

  • Badili kilogramu kwenda aunsi kwa kuzidisha mara 2.2. Hivyo, 75x2.2=aunsi 165.

  • Tafuta nusu ya aunsi kwa kugawa aunsi na 2. Hivyo, aunsi 165/2=aunsi 82.5.

  • Gawanya mara mfululizo utakaoamua kuufuata kwa siku nzima, mfano mara 8 kwa siku. Kwa hiyo aunsi 82.5/8=aunsi 10.3.

  • Badili aunsi kuwa miligramu za maji. Aunsi 1=miligramu 31.25. Kwa hiyo aunsi 10.3x31.25=miligramu 322.

Kwa hiyo itampasa mtu huyo mwenye uzito kilo 75, kunywa ml 322 za maji mara nane kwa siku.

Kila mmoja wetu sasa anaweza kutumia uzito wake kwa kutumia fomula hii na kujua ni kiasi gani cha maji anahitaji kwa siku.

Kumbuka, Kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi ni kiasi cha chini kabisa, lakini mahala pazuri pa kuanzia, ikiwa ni mtu unayejishughurisha zaidi na mazoezi au unaishi katika mazingira ya joto zaidi, utahitaji zaidi ya hapo.

Sasa, hutakubali kuwa kunywa maji kwa protokolo hii ni kazi rahisi?.

Ikiwa haunywi kiasi hiki cha maji kwa sasa, unapaswa kuanza kuongeza kiasi cha ziada kwa taratibu sana. Hii itaupa nafasi mwili kujirekebisha kuendana na kiasi ulichoanza kukiongeza, na ikiwa hautaupa mwili muda wa kujirekebisha, basi maji yatakuwa kama dawa ya kukojosha (diuretic), yakisukuma madini na vitamini za mhimu nje ya mwili, pengine na kukusababishia madhara zaidi kuliko faida.

Watu wazee na watoto wadogo wanatakiwa kuanza kuongeza maji kufikia mahitaji yao kwa taratibu zaidi.

Kwa kutumia mfano wa uzito hapo juu, itakupasa kuanza na glasi 3 siku ya kwanza huku ukiongeza glasi moja zaidi kila siku inayofuata mpaka ufikie glasi zote 8.

Kumbuka kuwa, kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi na kula chumvi robo tatu gramu kwa kila nusu lita ya maji, ni kanuni ya kimakisio tu. Baadhi ya wengine watahitaji maji zaidi wakati wengine watahitaji chumvi zaidi. Baada ya muda, mahitaji ya mwili kwa maji na chumvi yanaweza kuongezeka kidogo zaidi sababu ya mazingira ya joto, mazingira ya baridi au mazoezi ya viungo.

Kila mmoja lazima apate kujua kiasi cha mahitaji ya mwili wake kwa maji kuanzia sasa.


  • Kamwe usinywe zaidi ya aunsi 33.8 (lita moja) za maji kwa wakati mmoja ukiwa umekaa au umesimama.


  • Watoto wadogo kuanzia miaka 2 mpaka 12, hasa wale wepesi kujishughulisha na mazoezi wanahitaji asilimia 75 mpaka 100 za aunsi za maji katika uzito wao kwa sababu miili yao inakua muda wote na kila seli katika miili yao inayokua inayahitaji maji haya ya ziada (mytosis).


  • Tiba hii ya maji haitumiki kwa watoto chini ya miaka 2.


  • Chumvi ya kawaida ya mezani iliyoongezwa madini ya iodini, itakusaidia kidogo, chumvi ya mawe ya baharini ambayo haijasafishwa (unrefined sea salt) ndiyo nzuri zaidi sababu ya madini mengine mengi ya ziada zaidi ya 80 yaliyomo ndani yake. Chumvi ya baharini pia huwa na radha nzuri, nyeupe na umajimaji kidogo.


Namna bora za kula chumvi:



  • Njia ya kwanza ni kuiweka chumvi katika sehemu ya mbele ya ulimi, hakikisha unaihisi radha yake, na kisha kunywa maji juu yake yakiisafisha kuelekea chini.


  • Unaweza pia kuongeza chumvi ya ziada kwenye chakula chako.Tatizo la njia hii ni kuwa, chakula kinahisika kuwa na chumvi zaidi ya radha zingine.


  • Ukiona viwiko, vidole, miguu, mikono au kope za macho zinavimba (kuvimba kusikotokana na ajali au jeraha), au unaharisha zaidi, usitumie chumvi kwa siku 2 mpaka 3, kunywa maji halisi pekee na kisha siku ya tatu, endelea kuchukuwa chumvi tena, lakini ichukuliwe taratibu. Kamwe usitumie chumvi zaidi ya robo tatu gramu kwa kila nusu lita ya maji.

Kumbuka chumvi ikizidi hupelekea kuharisha.

Dr.Batmanghelidj anasema, kunywa maji matupu kunaweza pelekea mwili kupoteza baadhi ya madini na vitamini zake mhimu nje ya mwili na hivyo kutozipa seli muda wa kutosha kuyatumia maji. Inashauriwa kutumia vidonge vyenye vitamini nyingi kwa pamoja (multivitamins) katika kila mlo wako ili kurudishia kile kitakachokuwa kimepotea (hasa ikiwa haufanyi mazoezi na kula kiasi kingi cha mboga za majani).

Uvimbe utakapokuwa umepotea au umeacha kuharisha, unaweza kuendelea na mpango wako wa kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi ingawa mara hii utayachukua kwa kiasi kidogo.

Kwa siku nzima, anza kuongeza kiasi cha unywaji wako wa maji mpaka ufikie tena nusu ya uzito wako katika aunsi, anza pia kuchukua chumvi pamoja na maji. Unatakiwa kuhakikisha kuwa unapata gramu 150 za madini ya iodine kwenye “multivitamins” zako kila siku mpaka gramu 450 kwa siku.

Kisha kunywa maji, maji yanapaswa kubaki ndani ya mwili masaa 2 mpaka 2 na nusu ili kuupa mwili muda wa kutosha kuyatumia maji hayo vizuri.

Ikiwa inakulazimu kukojoa (peeing) chini ya muda wa masaa 2 tangu unywe maji, utalazimika kuacha kunywa maji matupu, jaribu kunywa juisi (uliyotengeneza mwenyewe) ya chungwa, ya limau au ya zabibu au juisi nyingine yeyote isipokuwa kwa watu wanaosumbuliwa na pumu (asthma) ambao hawatakiwi kunywa juisi ya chungwa.

Wakati huo huo mhimu kukumbuka kuongeza robo tatu gramu za chumvi katika kila nusu lita ya juisi yako.

Ikiwa kunywa juisi hakutasaidia kupunguza kwenda bafuni kila mara, jaribu kunywa maji huku ukila mkate. Unaweza kuongeza krimu ya siagi au jamu kwenye mkate wako (the magic bagel).

Kisha kutumia mkate siku moja au mbili unaweza kupunguza sasa kiasi cha mkate mpaka nusu yake, robo yake na mwisho juisi pekee pamoja na mlo wako.

Utapaswa kurudi taratibu tena kutoka kunywa maji juisi mpaka kunywa maji matupu tena, baada ya siku kadhaa itakupasa kujaribu aunsi 2 za maji matupu nusu saa kabla ya chakula, kesho yake aunsi 4, siku inayofuata itakuwa aunsi 6 kisha 8 na kuendelea mpaka ufikie kiasi chako unachotakiwa.

Ikiwa kunywa maji pamoja na kula mkate au katika juisi hakukusaidii kupunguza kwenda bafuni, Glasi ya maji (ml 250) matupu ikiongezwa na kijiko (kijiko cha chakula) kimoja cha asali au sukari halisi au walau sukari nyeupe kutakutatulia tatizo hili ukiongeza na chumvi 1/8 ya kijiko cha chai , tikisa na kisha kunywa mchanganyiko huo.

Bilashaka umewahi kusikia msemo, “Kwa sehemu kubwa tumetokana na maji”, hii ndiyo sababu zaidi ya asilimia 94 ya damu yetu ni maji, zaidi ya asilimia 85 ya ubongo wetu ni maji, huku zaidi ya asilimia 75 ya sisi ni maji.

Muda gani unywe maji:

  • Kitu cha kwanza kufanya mara uamkapo tu, ni kunywa glasi 2 za maji (ml 500) kwakuwa umetumia glasi 2 za maji kwa kulala mpaka asubuhi.
  • Kunywa glasi 1 robo saa au glasi 2 nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni, kisha hesabu masaa 2 au 2 na nusu kila baada ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni bila kunywa wala kula chochote, ndipo unywe glasi 1 ya maji.
  • Kunywa glasi 1 ya maji kila uendapo kulala.
  • Muda wowote uamkapo usiku kwenda bafuni, kunywa nusu glasi ya maji na kipande cha chumvi kisha rudi kulala.
  • Muda wowote unapopatwa na kiu kunywa maji.

Kwanini unywe maji robo lita, robo saa kabla ya kula, au nusu lita, nusu saa kabla ya kula?:

Wanyama wote hunywa maji halisi (plain water). Ikiwa
utawachunguza paka na mbwa, mara zote hunywa maji na kusubiri wastani wa nusu saa kabla ya kula. Ratiba inabadilika wanapokuwa wanatibiwa, hapa hunywa na kisha hula papo hapo ama baadaye.

Mfululizo huu ni mhimu ili kubaki na afya bora.

Unapokunywa maji na kusubiri nusu saa kabla ya kula, maji yanaenda tumboni na kuziamsha tezi kutoa kemikali (homoni) kuzifunika kuta za tumbo ili kuzirinda dhidi ya haidrokloriki asidi ambayo huzarishwa wakati chakula kinawekwa mdomoni.

Maji na kemikali hizo kisha huenda kwenye utumbo mdogo ambako kemikali hizi hukaa kusubiri chakula kitakachokuwa kinakuja baadaye. Maji hayo huru, yanauacha utumbo mdogo na kwenda
katika seli zote za mwili na kuzijaza (kuzinyweshea) maji
kama vile unavyonywesha bustani. Baada ya seli kuwa
zimenyeshewa, maji yanayobaki kisha yanasukumwa tena kwenda tumboni ili kunyeshea chakula kilichofika.


Nguvu zetu hazitokani na vyakula tunavyokula, bali zinatoka katika MAJI ambayo yanaiweka atomu ya haidrojeni katika chakula.

Tunatembea katika haidrojeni.

Vyakula tulavyo hutupatia vitamini na madini tunayoyahitaji ili kubaki katika afya.

Ikiwa haunywi maji halisi (glasi 1 au 2) kabla ya kula
chakula na kusubiri (robo saa au nusu saa), basi mwili lazima ujikope maji wenyewe.


Kama mwili utakopa maji toka katika damu, basi ateri lazima zipunguze vipenyo vyake na moyo lazima utumie nguvu nyingi ili kusukuma damu ambayo ni nene (nyingi), kitendo hiki tunakiita 'shinikizo la damu'(BP).

Ikiwa mwili utajikopa maji toka katika ubongo, utapatwa na 'kichwa kizito' au kichwa kuuma ambacho
kinaweza pelekea maumivu ya kichwa.


Ikiwa unakunywa alikoholi (pombe) na inavuta maji toka kwenye ubongo, utapatwa na kutokujisikia vizuri au uchovu (hangover).

Watu wanaoishi katika nchi za baridi huweka alikoholi kwenye tenki zao za gesi ili kuvuta maji ndani ya gesi na hivyo kuifanya gesi isigande.

Kokote katika ogani au tishu mwili utakakokopa maji, lazima ogani au tishu hiyo iachiwe madhara na hivyo kusababisha maumivu ama ufanyaji kazi wa ogani au tishu hiyo usio wa kawaida kama vile kufunga choo (constipation).

kufunga choo au kupata choo kigumu sana kunatokea wakati mwili umekopa maji toka katika utumbo mdogo na sehemu ya chini ya utumbo mpana kunakopelekea taka za mwili kusimama kwenye kuta za utumbo mdogo na sehemu ya chini ya utumbo mpana (colon). Wakati mambo yako yanapokuwa na umajimaji, huteleza yenyewe chini bila kutumia nguvu yoyote.

Kila tunapopumuwa hewa nje (exhale) tunapoteza maji.

Ikiwa utahema juu ya kioo, utauona ukungu (maji). Tunapoteza glasi 4 za maji kwa kupumuwa tu kila baada ya masaa 24!!.

kama mwili utakopa maji toka mapafuni, utapatwa na pumzi fupi itakayopelekea upatwe na pumu (asthima) na matatizo mengine yanayohusiana na mfumo wa upumuwaji.

Mapafu na Moyo vinauhusiano wa karibu, kwa hiyo kama mwili utakopa baadhi ya maji toka katika mishipa ya moyo, utapatwa na maumivu ya moyo ambayo yanaweza kurahisisha kutokea kwa shambulio la moyo (heart attack).

Mishipa inahitaji damu na maji wakati unafanya mazoezi, kwa hiyo kama unatakiwa kula chakula na kisha kutembea au kupandisha ngazi (za ghorofa) na una upungufu wa
maji (dehydrated), unaweza ukapatwa na pumzi fupi, shambulio la pumu, utapatwa na maumivu ya moyo (angina) au kukakamaa kwa mishipa (cramps).


Ndiyo maana wanasema; kamwe usiende kuogelea
mara tu baada ya kumaliza kula kwa sababu mishipa
itakakamaa.


Mwili unapokuwa katika kazi yake ya umeng'enyaji
chakula, huielekeza (diverts) damu toka katika mikono na miguu kwenda katika utumbo mdogo ili kusaidia umeng'enyaji wa chakula.

Baadhi ya vyakula ni rahisi kumeng'enywa na vinawezeshwa na maji pekee, kama vile matunda na mboga za majani.

Vinywaji vingine (liquid beverages) kama vile
kahawa, chai, soda na juisi, siyo maji kwa mwili. Hivi ni
vyakula pia kwa sababu ulimi unaipata radha ya
viongezi (additives) na siyo radha ya maji halisi, na hivyo
tumbo litaitowa haidrokloriki asidi. Mwili utakishughurikia
kinywaji hicho kama chakula.


Utafaidika na baadhi ya maji kama vile katika matunda na mboga za majani kwa masharti ya kinywaji hicho kutokuwa na kafeina (caffeine).

Kafeina ni kikojoshi (diuretic), huyalazimisha maji kutoka nje ya mwili.

Magonjwa mengine yanayoweza kuepukika kwa kunywa maji kabla ya kula ni pamoja na vidonda vya tumbo, tumbo kunyonga, kiungulia, mafuta yaliyozidi, kansa ya utumbo mdogo, kukinaishwa na chakula, na ernia.

Kunywa maji masaa 2 au 2 na nusu baada ya chakula kunasaidia kumalizia umeng'enyaji wa chakula na kuunywesha mwili maji baada ya kukaukiwa kulikosababishwa na kazi ya umeng'enyaji wa chakula.

kunywa maji ya kawaida katika joto la kawaida.

Magonjwa mengine yanayotibika au kukingika kwa kutumia tiba ya maji ni; Kansa, kisukari, kifua kikuu (TB), shinikizo la damu(BP), mfadhaiko (stress), matatizo ya moyo na kuzimia, magonjwa ya tumbo, magonjwa ya ngozi, magonjwa ya Ini, pumu (Asthima), mzio (Allergy), chunusi, homa, kupunguwa nguvu na kinga ya mwili, matatizo ya kina mama, magonjwa mengine ni pamoja na homa ya uti wa mgongo, kansa ya kizazi, kikohozi, kuharisha, kikundu, nyongo, matatizo ya tumbo, kupungua uzito, upungufu wa damu (anaemia), vichomi, vidonda vya tumbo, utipwatipwa, kuzeeka mapema, na magonjwa mengine mengi.

Tiba hii ni nzuri kwa wote, wagonjwa watapona na wazima watabaki na afya bora na kujirinda dhidi ya maradhi kwa maisha yao yote.

''Kuna maajabu zaidi ya milioni katika glasi moja ya maji kuliko katika dawa yeyote utakayoandikiwa na muuguzi wako – dr.Batmanghelidj''.


ANGALIZO:



  • Ikiwa hauendi chooni walau mara tatu kwa siku,unapaswa kumwona daktari kabla ya kuanza tiba hii.

  • Figo zako lazima ziwe zinafanya kazi vizuri, hii inamaanisha, kiasi cha maji unachokunywa lazima kiwe karibu sawa na unachotoa.

  • Wakati huo huo, kwenda chooni mara nyingi kwa siku kunaweza kukusababishia kupoteza vitamini mhimu, madini na elektrolaiti na kukufanya vibaya zaidi ya vizuri.

  • Unatakiwa kuwa makini sana unapoanza kuongeza uchukuaji wa maji mwilini, anza pole pole kwa kuongeza glasi 1 kila siku mpaka utakapofikia nusu ya uzito wako katika aunsi. lazima uupe mwili muda wa kujirekebisha baada ya kuzoea vinywaji kama kahawa, chai na soda, kwa kuwa vinywaji hivi huufanya mwili kujiendesha kwa namna nyingine.

  • Unaweza kuumwa na kichwa au unaweza usijisikie vizuri tu siku tatu mpaka wiki moja za kuanza tiba, usiache kunywa maji kwakuwa hayo si madhara bali ni dalili kuwa taka za sumu zimeanza kuondoka mwilini, baada ya muda utarudi katika hali yako ya kawaida.

  • Tunashauri watu wenye matatizo ya figo, Ini na moyo, kutofuata tiba hii mpaka watakapopata ruhusa ya daktari na muongozo sahihi.

  • Usinywe maji zaidi ya lita 3.78 kwa siku.

  • Usinywe maji kuanzia lita moja kwa pamoja au ukiwa umekaa katika mkao mmoja iwe kusimama au kukaa.
Home | maajabuyamaji2.artisteer.net


Kumbuka pia kuwa hii ni elimu tu na siyo kumuondoa daktari wako au chaguo lako la kutumia dawa, ni programu iliyopendekezwa kwa manufaa yako.
 
ndefu

binafsi maji nakunywa kama nameza dawa vile...sijui ntatatuaje hili tatizo...
 
HIi ndefu sana,nilipo maliza kusoma nimekunywa glass moja ya maji,je ni sahihi?

umenichekesha, hii siyo ndefu. glasi moja lazima imaanishe ml 250 au robo lita (chini kidogo ya ujazo wa soda). kwahiyo kwa sababu tunaipa miili yetu maji ya mgawo(tunapokunywa baada ya kusikia kiu), mwili lazima utuambie kuwa napungukiwa maji (dehydrated) kwa kuzarisha ishara ambazo sisi tumeziita 'magonjwa'. Tatizo ni kuwa maji ni suluhu kwa magonjwa yote isipokuwa tu hatutatumia ghalama yeyote!!!!!!!!!!!!!!!!!. angalia uhusiano uliopo baina ya BP na upungufu wa maji mwilini: maajabuyamaji2.artisteer.net/shinikizo. kumbuka kuwaelimisha wengine
 
unatakiwa kunywa walau glasi 8 kwa siku mara nane tofauti. asubuhi baada ya kuamka, nusu kabla ya chakula cha asubuhi, masaa 2 baada ya chakula cha asubuhi, nusu saa kabla ya chakula cha mchana, masaa 2 baada ya chakula cha mchana, nusu saa kabla ya chakula cha jioni, masaa 2 baada ya chakula cha jioni, na kabla ya kwenda kulala. soma vizuri taratibu post hii kwa kuwa ina masharti yote unayopaswa kuyafuata. tembelea pia maajabuyamaji2.artisteer.net. wajurishe uwapendao kuhusu maajabu ya maji ambayo ni suluhu kwa ugonjwa wowote. goodluck!!
 
aisee nitaanza kujilazimisha kunywa maji, hakuna anishandae kwa uvivu wa kunywa maji, ata ya kumezea dawa lazima yawe kiduchu tu. asante nitajitaidi
 
Ahsante mkuu. Nimepata maarifa zaidi kuhusu matumizi sahihi ya maji, make elimu ni bahari.
 
vizuri mkuu, kwanza hongera kwa kunywa maji mengi kiasi hicho!!!, bali hutakiwi uzidishe lita 3 na nusu kwa siku. kumbuka pombe ni kikojoshi (diuretic) huyalazimisha maji kukimbia nje ya mwili kwa haraka, yaani unapokunywa pombe kikombe kimoja, utaenda kukojowa vikombe viwili, kwahiyo unapungukiwa maji mara 2. utaona mwenyewe ukinywa tu maji, haukawii kwenda kukojowa. kitendo hiki cha kukojowa muda mfupi tu baada ya kunywa kimiminika hupelekea madini na vitamini za mhimu kutoka nje ya mwili na kuandaa ngazi ya ugonjwa fulani huko mbeleni. kumbuka; usizidishe lita tatu na nusu kwa siku na pombe ni kikojoshi(diuretic). tembelea: maajabuyamaji2.artisteer.net
 
Magonjwa mengi yanasababishwa na mtu kutokunywa maji ya kutoksha. Kama halimashauri za miji, wilaya na manispaa zingefanya hili jambo la dharura kuokoa maisha ya watu. Hatuna technolojia ya kutosha kutibu watu lakini vitu vingine kama maji hatuhitaji muwekezaji kuokoa maisha ya watu. Ni sera, ulafi na umimi ndo unaowafanya viongozi wetu washindwa kuwa na uzalendo.
 
Magonjwa mengi yanasababishwa na mtu kutokunywa maji ya kutoksha. Kama halimashauri za miji, wilaya na manispaa zingefanya hili jambo la dharura kuokoa maisha ya watu. Hatuna technolojia ya kutosha kutibu watu lakini vitu vingine kama maji hatuhitaji muwekezaji kuokoa maisha ya watu. Ni sera, ulafi na umimi ndo unaowafanya viongozi wetu washindwa kuwa na uzalendo.

kwa sasa viongozi wetu wengi hawajuwi hili. kwanini hawajuwi kwamba maji ndiyo kila kitu? kwa sababu kama magonjwa mengi yatatibika kwa maji tu tena bila gharama yeyote ina maana tutalazimika kutii kauli mbiu ya ubinadamu kwanza. siku hizi kwa sehemu kubwa 'hela kwanza'. thanks 4 ur contribution, visit: maajabuyamaji2.artisteer.net
 
Ahsante sana Dr FP.! Me nimeanza kutumia tiba hii ya maji kwa takribani miaezi mitatu sasa.! Lakini huwa natokewa na shida hizi zifuatazo ndani ya tumbo langu:-
1. Kuhc kutapika na kichefuchefu wakati nakunywa maji asubuh baada ya kutoka kuamka kitandani.
2. Tumbo linajaa gesi na linanguruma sana.
3. Huwa najamba jamba sana na harufu yake siwezi hata kuisema ni kunuka mnoo.!
4. Kupata haja huwa ni shida sana (huwa x1 kwa cku) na kinyesi changu ni kigumu sana tena nacho huwa na rangi rangi (ya kahawia, njano, nyekundu, nyeusi nk) na huwa kinatoa harufu kali sana.
Je nifanyeje kuweza kutatua hili tatizo langu la muda mrefu.
 
HIi ndefu sana,nilipo maliza kusoma nimekunywa glass moja ya maji,je ni sahihi?

hahahahaaa wee hujatulia kbs
nimeshindwa soma yote maana ina hesabu nyingi na sie wengine NO kbs na nambaz
nachojua nakunywa maji atleast kwa siku/24 hrs one litre namaliza

mtoa mada kutusaidia ungeweka vitu vya msingi tu,sii kiivi aseee!!
 
Ahsante sana Dr FP.! Me nimeanza kutumia tiba hii ya maji kwa takribani miaezi mitatu sasa.! Lakini huwa natokewa na shida hizi zifuatazo ndani ya tumbo langu:-
1. Kuhc kutapika na kichefuchefu wakati nakunywa maji asubuh baada ya kutoka kuamka kitandani.
2. Tumbo linajaa gesi na linanguruma sana.
3. Huwa najamba jamba sana na harufu yake siwezi hata kuisema ni kunuka mnoo.!
4. Kupata haja huwa ni shida sana (huwa x1 kwa cku) na kinyesi changu ni kigumu sana tena nacho huwa na rangi rangi (ya kahawia, njano, nyekundu, nyeusi nk) na huwa kinatoa harufu kali sana.
Je nifanyeje kuweza kutatua hili tatizo langu la muda mrefu.

mkuu vizuri, mimi ilinichukuwa miaka kadhaa kuifahamu tiba hii, wengi wakiambiwa maji wanakimbilia tu kunywa. ni rahisi lakini inahitaji darasa kidogo. cha mhimu ni kuwa kisha kunywa maji, maji yanapaswa kubaki ndani ya mwili kwa muda usiopunguwa masaa mawili mpaka mawili na nusu, ikiwa unalazimika kukojowa kabla ya masaa 2 tangu unywe maji basi uwezekano ni kuwa unaishiwa maji mara mbili zaidi. cha kufanya kwanza soma vizuri na taratibu maelezo yote ya post yangu mwanzo mwisho. kwahiyo suala siyo kunywa tu, bali ni jinsi unayabakisha maji mwilini kwa masaa 2 au 2 na nusu. jaribu hivi, acha kabisa vinywaji vyenye kaffeina kama vile soda, juisi karibu zote za dukani, kahawa, chai ya rangi na pombe aina yeyote kwani vyote hivi ni vikojoshi (diuretics) huyalazimisha maji kutoka nje ya mwili kwa haraka. maji yanapotoka nje ya mwili haraka yatakupelekea kwanza kukaukiwa na maji zaidi, pili madini na vitamini mhimu ndani ya mwili mwako vitatoka nje na kukusababishia madhara zaidi. kwahiyo utagunduwa kuwa hii siyo suala la kuamka tu na kuanza kuyatumia maji kama tiba. ni sayansi. sasa tembelea; maajabuyamaji2.artisteer.net ujifunze zaidi. unaweza kunipigia pia hasa usiku kuanzia saa mbili hivi 0769779533. kumbuka hii ni elimu tu.
 
tatizo letu kubwa siku zote ni muda. hatuna muda kabisa. kama unakutana na sentensi inasema; ''mwili wa binadamu unapopungukiwa maji hutoa ishara (indicators), tumeziita ishara hizo kuwa ni magonjwa''. hata kama kuna hesabu nyingi ndani yake, kwa mimi ninayeogopa kuuguwa na gharama za hospitali zilivyo siku hizi, lazima nitajitahidi kila niwezavyo nizielewe hesabu hizo. unapaswa kunywa walau lita 2 na nusu kila siku na usizidishe lita 3 na nusu. hizo lita 2 na nusu gawa mara 8, usizinywe zote kwa pamoja!. rahisi tu; ukiamka, nusu saa kila kabla ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni, halafu kila masaa 2 baada ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni, na kisha kabla ya kulala. glasi 8 (ml 250) mara 8 TU. GOODLUCKY!!.
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom