Hatuna maji, Umeme, CT scanner, tunakimbilia kujenga Kigamboni kwa Matrilioni!!!

mzozaji

JF-Expert Member
Jul 28, 2010
255
13
Wakuu nashangazwa sana na kasi ya hii serikali kushikilia kujenga mradi wa majumba ya kifahari Kigamboni kana kwamba ndio suruhisho la umaskini wetu. Nchi yetu haina maji safi sehemu nyingi na umeme wa mashaka kila siku lakini tunaona Mabilioni yakawekezwe kwenye majumba ambayo hatujui nani atapanga huku tukiwatimua watu toka makazi yao.Mimi kwa haraka naona kuna kitu kimejificha kwenye huu mradi mpaka unapelekwa puta hivi. Waziri wa ardhi katangaza bajeti ya mwaka huu kwenye huu mradi tena ni 10% ambayo ni Mabilioni na akasema hizo 90% zilizobaki 'watajua namna ya kuzipata'!! Hapa lazima kuna jambo.. Utaanzishaje mradi wakati hata fedha hujui utatoa wapi? Wenye kujua kidogo kuhusu huu mradi watujuze labda wengine tunashindwa kuelewa kwa akili ya kawaida.
 
Nusu ya Bajeti ya Ardhi kujenga Kigamboni mpya
Wednesday, 11 July 2012 20:36
Florence Majani, Dodoma
Mwananchi

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imetenga zaidi ya nusu ya bajeti yake kwa mwaka wa fedha, 2012/2013 kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni, Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam.Fedha zilizotengwa kwa ajili ya kuendeleza mji huo ni Sh60 bilioni ambazo ni sawa na asilimia 59 ya makadirio ya matumizi ya wizara hiyo, ambayo ni Sh101.731 bilioni.

Hata hivyo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alisema Bungeni jana kuwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi huo ni sawa na asilimia 10 tu ya mahitaji ya kiasi cha Sh605.
"Kwa hiyo tutatumia mbinu za kisasa (kupitisha bakuli letu la omba omba)kutafuta pesa nyingine Sh605 bilioni nje ya Bajeti kutekeleza mradi huu bila kuchelewa zaidi. Mradi huu unahitaji kiasi hicho cha fedha kwa miaka mitatu ya kwanza," alisema Profesa Tibaijuka alipokuwa akiwasilisha makadirio ya matumizi ya wizara yake jana na kuongeza:

"Nitasimamia mradi huu kwa kasi, ari na nguvu mpya. Ingawa pia sitakuwa nimetenda haki iwapo sitawashukuru wananchi wa Kigamboni kwa uvumilivu na ushirikiano wanaotuonyesha."

Katika Bajeti ya wizara hiyo ya Sh101.7 bilioni, matumizi ya kawaida ni Sh30.7 bilioni na Sh71 bilioni ni za maendeleo. Katika fedha hizo za maendeleo, Sh61 bilioni ni fedha za ndani na Sh10 bilioni ni fedha za nje.

Kuhusu wananchi wanaoishi katika eneo hilo, Profesa Tibaijuka alisema hakuna mkazi yeyote wa Kigamboni atakayehamishwa kwani idadi ya wananchi waliopo ni ndogo ikilinganishwa na idadi ya makazi mapya yanayotakiwa kujengwa katika eneo hilo.
Alisema ni ushauri wake kwamba wakazi wote wa Kigamboni wachague kubaki katika mji huo kwani wawekezaji wa ndani na nje watapewa maeneo kwa ajili ya kujenga makazi ambayo yatatumika kuwahamishia wananchi watakaoamua kubaki.

"Tunashauri wote wabaki kwa kuwa sasa hivi kuna wananchi takribani 82,000 wakati tunajenga mji mpya wenye uwezo wa wakazi 400,000. Hakuna sababu ya wananchi kuhama eneo hili ila makazi yao yatapangwa upya na kuboreshwa," alisema.

Gharama za mradi
Profesa Tibaijuka alisema ujenzi wa Mji wa Kigamboni utafanywa kwa awamu tatu, ambazo zitatekelezwa kati ya mwaka huu na 2032 na gharama zinazotarajiwa kutumika hadi utakapokamilika ni Sh11.6 trilioni.

Alisema awamu ya kwanza itakuwa kati ya mwaka 2012 na 2022, awamu ya pili kati ya 2022 na 2027 na awamu ya tatu ni kati ya 2027 na 2032.
Profesa Tibaijuka alisema miongoni mwa kazi zitakazofanywa katika mwaka huu wa fedha ni kuundwa kwa wakala mpya wa kusimamia mradi huo anayejulikana kama Kigamboni Development Agency (KDA).

Kazi nyingine ni kuidhinisha mpango na kuanza utekelezaji, kufanya uthamini wa mali zilizomo katika maeneo ya miundombinu, huduma za maji na eneo mbadala na kulipa fidia kwa mali zilizomo katika maeneo yaliyofanyiwa uthamini.
Kuhusu fidia, Waziri Tibaijuka alisema wananchi ambao hawajakiuka maagizo ya mradi kwa kufanya maendelezo haramu, wasiwe na wasiwasi kuhusu fidia kwa sababu mradi utazingatia haki na ni endelevu... "Fidia itatolewa kwa mujibu wa sheria kwa tathmini ya kiujumla ambayo itakokotolewa kutokana na viwango vya soko na kuhusishwa ili iwe sahihi."

Alisema atafanya ziara ya mafunzo kwa wawakilishi kutoka Kigamboni kutembelea mji mpya ili uwepo uelewa wa pamoja juu ya jinsi mji huo utakavyokuwa.

Hazina ya Ardhi
Katika hatua nyingine, Profesa Tibaijuka alisema wizara yake inakamilisha uanzishaji wa Hazina ya Ardhi pamoja na Mfuko wa Fidia ya Ardhi.
Alisema vyombo hivyo vitasimamia utoaji wa ardhi kwa wawekezaji wa ndani na nje kwa misingi ya kuingia ubia wa kumiliki pamoja hisa zitakazotolewa kwa uwiano kati ya wananchi na wawekezaji husika.

Kuhusu kuweka na kutunza alama za mipaka ya Tanzania na nchi jirani, Profesa Tibaijuka alisema majadiliano ya kupima maeneo hayo yalishakamilika.
Alisema majadiliano yalishafanyika baina ya Tanzania na nchi za Comoro na Msumbiji na mkataba wa kwanza kati ya Tanzania, Msumbiji na Comoro kwenye alama za utatu baharini inayotenganisha nchi hizo ulikamilika na kutiwa saini Desemba 5, mwaka jana.

"Mkataba wa pili kati ya Tanzania, Shelisheli na Comoro ulitiwa saini Februari 17, mwaka huu. Hivyo basi, Tanzania imekamilisha upimaji wa mipaka katika Bahari ya Hindi na itatangaza eneo lake la ukanda wa kiuchumi baharini bila kipingamizi kwa nchi jirani," alisema.

Alisema wizara yake imewasilisha andiko la kudai nyongeza ya eneo ya ukanda wa kiuchumi baharini Januari, mwaka huu na Tume ya Mipaka ya Baharini ya Umoja wa Mataifa, inapitia andiko hilo.

Profesa Tibaijuka alisema kupatikana kwa eneo hilo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 61,000 kutaiwezesha Tanzania kuvuna rasilimali za chini ya bahari kwa manufaa ya sasa na kwa vizazi vijavyo.

Kurasini kulipwa fidia
Kuhusu mradi wa uendelezaji wa eneo la Kurasini ulioanza 2006 kwa ajili ya upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Profesa Tibaijuka alisema wizara imetenga fedha chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara kulipa fidia kwa wananchi watakaopisha mradi huo katika eneo la Kurasini na Shimo la Udongo.

"Wizara itaendelea na malipo hayo kwani hata mwaka jana tulilipa kiasi cha Sh550 milioni kwa wakazi wa Mtaa wa Kurasini waliopo jirani na Mabwawa ya Majitaka," alisema.

Alisema wizara yake itaendelea kutatua migogoro ya ardhi, urasimishaji wa makazi holela, mikopo ya nyumba, ujenzi wa nyumba unaofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na ujenzi wa nyumba za biashara na makazi.


 
Kigamboni, kama alivyozungumza mbunge wao jana, kimenuka. Yalitengenezwa na wenye madaraka ili bei ya maeneo ipae. Kwa kiasi fulani walifanikiwa, lakini wananchi wa kuburuza Kigamboni hakuna.
 
Nusu ya Bajeti ya Ardhi kujenga Kigamboni mpya
Wednesday, 11 July 2012 20:36
Florence Majani, Dodoma
Mwananchi

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imetenga zaidi ya nusu ya bajeti yake kwa mwaka wa fedha, 2012/2013 kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni, Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam.Fedha zilizotengwa kwa ajili ya kuendeleza mji huo ni Sh60 bilioni ambazo ni sawa na asilimia 59 ya makadirio ya matumizi ya wizara hiyo, ambayo ni Sh101.731 bilioni.

Hata hivyo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alisema Bungeni jana kuwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi huo ni sawa na asilimia 10 tu ya mahitaji ya kiasi cha Sh605.
"Kwa hiyo tutatumia mbinu za kisasa (kupitisha bakuli letu la omba omba)kutafuta pesa nyingine Sh605 bilioni nje ya Bajeti kutekeleza mradi huu bila kuchelewa zaidi. Mradi huu unahitaji kiasi hicho cha fedha kwa miaka mitatu ya kwanza," alisema Profesa Tibaijuka alipokuwa akiwasilisha makadirio ya matumizi ya wizara yake jana na kuongeza:

"Nitasimamia mradi huu kwa kasi, ari na nguvu mpya. Ingawa pia sitakuwa nimetenda haki iwapo sitawashukuru wananchi wa Kigamboni kwa uvumilivu na ushirikiano wanaotuonyesha."

Katika Bajeti ya wizara hiyo ya Sh101.7 bilioni, matumizi ya kawaida ni Sh30.7 bilioni na Sh71 bilioni ni za maendeleo. Katika fedha hizo za maendeleo, Sh61 bilioni ni fedha za ndani na Sh10 bilioni ni fedha za nje.

Kuhusu wananchi wanaoishi katika eneo hilo, Profesa Tibaijuka alisema hakuna mkazi yeyote wa Kigamboni atakayehamishwa kwani idadi ya wananchi waliopo ni ndogo ikilinganishwa na idadi ya makazi mapya yanayotakiwa kujengwa katika eneo hilo.
Alisema ni ushauri wake kwamba wakazi wote wa Kigamboni wachague kubaki katika mji huo kwani wawekezaji wa ndani na nje watapewa maeneo kwa ajili ya kujenga makazi ambayo yatatumika kuwahamishia wananchi watakaoamua kubaki.

"Tunashauri wote wabaki kwa kuwa sasa hivi kuna wananchi takribani 82,000 wakati tunajenga mji mpya wenye uwezo wa wakazi 400,000. Hakuna sababu ya wananchi kuhama eneo hili ila makazi yao yatapangwa upya na kuboreshwa," alisema.

Gharama za mradi
Profesa Tibaijuka alisema ujenzi wa Mji wa Kigamboni utafanywa kwa awamu tatu, ambazo zitatekelezwa kati ya mwaka huu na 2032 na gharama zinazotarajiwa kutumika hadi utakapokamilika ni Sh11.6 trilioni.

Alisema awamu ya kwanza itakuwa kati ya mwaka 2012 na 2022, awamu ya pili kati ya 2022 na 2027 na awamu ya tatu ni kati ya 2027 na 2032.
Profesa Tibaijuka alisema miongoni mwa kazi zitakazofanywa katika mwaka huu wa fedha ni kuundwa kwa wakala mpya wa kusimamia mradi huo anayejulikana kama Kigamboni Development Agency (KDA).

Kazi nyingine ni kuidhinisha mpango na kuanza utekelezaji, kufanya uthamini wa mali zilizomo katika maeneo ya miundombinu, huduma za maji na eneo mbadala na kulipa fidia kwa mali zilizomo katika maeneo yaliyofanyiwa uthamini.
Kuhusu fidia, Waziri Tibaijuka alisema wananchi ambao hawajakiuka maagizo ya mradi kwa kufanya maendelezo haramu, wasiwe na wasiwasi kuhusu fidia kwa sababu mradi utazingatia haki na ni endelevu... "Fidia itatolewa kwa mujibu wa sheria kwa tathmini ya kiujumla ambayo itakokotolewa kutokana na viwango vya soko na kuhusishwa ili iwe sahihi."

Alisema atafanya ziara ya mafunzo kwa wawakilishi kutoka Kigamboni kutembelea mji mpya ili uwepo uelewa wa pamoja juu ya jinsi mji huo utakavyokuwa.

Hazina ya Ardhi
Katika hatua nyingine, Profesa Tibaijuka alisema wizara yake inakamilisha uanzishaji wa Hazina ya Ardhi pamoja na Mfuko wa Fidia ya Ardhi.
Alisema vyombo hivyo vitasimamia utoaji wa ardhi kwa wawekezaji wa ndani na nje kwa misingi ya kuingia ubia wa kumiliki pamoja hisa zitakazotolewa kwa uwiano kati ya wananchi na wawekezaji husika.

Kuhusu kuweka na kutunza alama za mipaka ya Tanzania na nchi jirani, Profesa Tibaijuka alisema majadiliano ya kupima maeneo hayo yalishakamilika.
Alisema majadiliano yalishafanyika baina ya Tanzania na nchi za Comoro na Msumbiji na mkataba wa kwanza kati ya Tanzania, Msumbiji na Comoro kwenye alama za utatu baharini inayotenganisha nchi hizo ulikamilika na kutiwa saini Desemba 5, mwaka jana.

"Mkataba wa pili kati ya Tanzania, Shelisheli na Comoro ulitiwa saini Februari 17, mwaka huu. Hivyo basi, Tanzania imekamilisha upimaji wa mipaka katika Bahari ya Hindi na itatangaza eneo lake la ukanda wa kiuchumi baharini bila kipingamizi kwa nchi jirani," alisema.

Alisema wizara yake imewasilisha andiko la kudai nyongeza ya eneo ya ukanda wa kiuchumi baharini Januari, mwaka huu na Tume ya Mipaka ya Baharini ya Umoja wa Mataifa, inapitia andiko hilo.

Profesa Tibaijuka alisema kupatikana kwa eneo hilo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 61,000 kutaiwezesha Tanzania kuvuna rasilimali za chini ya bahari kwa manufaa ya sasa na kwa vizazi vijavyo.

Kurasini kulipwa fidia
Kuhusu mradi wa uendelezaji wa eneo la Kurasini ulioanza 2006 kwa ajili ya upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Profesa Tibaijuka alisema wizara imetenga fedha chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara kulipa fidia kwa wananchi watakaopisha mradi huo katika eneo la Kurasini na Shimo la Udongo.

"Wizara itaendelea na malipo hayo kwani hata mwaka jana tulilipa kiasi cha Sh550 milioni kwa wakazi wa Mtaa wa Kurasini waliopo jirani na Mabwawa ya Majitaka," alisema.

Alisema wizara yake itaendelea kutatua migogoro ya ardhi, urasimishaji wa makazi holela, mikopo ya nyumba, ujenzi wa nyumba unaofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na ujenzi wa nyumba za biashara na makazi.


Another CDA (Capital City Development) in progress. Hivi CDA imefikia wapi vile? Au tule tumiradi twetu?
 
Goooo goo go go Prof. Tibaijuka hakuna wakuzuia maendeleo ya Watanzania...wakazi wakigamboni wanapaswa kujua Mjimpya sio kwaajili yao tuu, ni kwa ajili ya watanzania wote..tunataka maendeleo sio sumu za kisiasa toka kwa DR.Ndugulile, ya kwake tunayajua hivyo apishe maendeleo yaje...
 
Goooo goo go go Prof. Tibaijuka hakuna wakuzuia maendeleo ya Watanzania...wakazi wakigamboni wanapaswa kujua Mjimpya sio kwaajili yao tuu, ni kwa ajili ya watanzania wote..tunataka maendeleo sio sumu za kisiasa toka kwa DR.Ndugulile, ya kwake tunayajua hivyo apishe maendeleo yaje...

Hapo kwenye red,

Maendeleo ya Watanzania yamezuiwa kwa miaka mingi sasa, labda kama wewe hujui.

Maendeleo hayo yamezuiwa kwa namna zifuatazo:-
  • Mali na raslimali zote za Tanzania zinaliwa na wawekezaji ( Angalia migodi ya dhahabu, tanzanite, almasi, n.k)
  • Fedha zote za Tanzania zinaliwa na viongozi mafisadi (Angalia ulaji wa EPA, majengo ya BoT, Richmond, Dowans, n.k)
  • Mapato yote ya kodi za Tanzania zinaliwa na wetendaji serikalini (Angalia bajeti ya mwaka huu - chai na maadazi ya wafanyakazi serikalini zitagharimu Sh. 15 Billioni !!!, n.k)
  • Selikali haina pesa za kununulia CT scan kwa ajili ya hospitali zetu, ila ina pesa kwa ajili ya kujenga 'mji' wa Kigamboni !! ( Linganisha CT scan moja ni Sh. 200 million tu , ila mji wa Kigamboni Sh. 11,000 millioni !!!)

Upo hapo ??? Hapo kuna maendeleo ???

Kweli, mji wa kigamboni utajengwa, ila wewe na watanzania wengine mnaweza msiuone maana mtakuwa mmeshakufa kwa kukosa matibabu hospitali, maana hakuna vifaa vya kuwatibia kama vile CT scan na vifaa vinginevyo !!!
 
Jamani mimi naomba nifahamishwe, labda kuna kitu sielewi! Hivi Professor Anna Tibaijuka ni waziri wa Ardhi wa Tanzania? au ni Waziri wa Ardhi wa Dar es Salaam? Kutenga 59% ya budget yote ya Wizara ya Ardhi kwaajili ya Kigamboni tu THIS IS A BIG JOKE AND AN INSULT kwa Watanzania tusio wana Dar es Salaam.

Hata ukisoma budget yako mipango yake yote aliyoongelea ni ya Dar es Salaam. Sijaona ukizungumzia watanzania tusio wana Dar es Salaam. Tangu ateuliwe ukifuatilia utendaji wake utaona yeye anashughulika na mamabo ya Dar es Salaam, kubomoa nyumba, viwanja vya wazi DSM tu?

Sasa nimeanza kuelewa kwanini CDM wana advocate SERIKALI ZA MAJIMBO. Huyu Professor sisi watu wa mikoa hatufai kabisa. Mbona Magufuri tunamuona kila kona ya nchi hii. Yaani mimi huyu Mama ameni bore stiff, Yeye anafikiri Tanzania ni DSM tu.

CDM tuleteeni serikali za majimbo tuachane na hawa WARASIMU wa DSM
 
Tatizo kubwa la serikali ya CCM siku zote haina priority list ya projects zake. Sijui kwanini inapenda kukurupuka kila mara. Si lazima projects zote zianze kwa pamoja. tatizo kubwa hapa ni kuwa Kigamboni ina masilahi binafsi especially kwa viongozi wetu. Nani hajui kuwa wengi wao wameshakamata maeneo huko!
Kinachofuata ni daraja la kigamboni kujengwa kwa haraka iwezekanavyo ili wasipate adha wanayoipata wakazi wake walalahoi sasa hivi.
kujengwa Kigamboni ni maendeleo makubwa pia ila ndiyo kipaumbele kwa kipindi hiki kigumu cha uchumi?
 
waacheni wajenge kigamboni jamani, viwanja vyenyewe wanachukua wao vyote.....

Wanajiandalia mji wao.....
 
waacheni wajenge kigamboni jamani, viwanja vyenyewe wanachukua wao vyote.....

Wanajiandalia mji wao.....

Oysterbay walishaiharibu kwa kujaza mabaa kila sehemu sasa wanaona wajitafutie makazi mapya ya hadhi yao na kuwaondoa watu wote wa kawaida.
 
Wakuu nashangazwa sana na kasi ya hii serikali kushikilia kujenga mradi wa majumba ya kifahari Kigamboni kana kwamba ndio suruhisho la umaskini wetu. Nchi yetu haina maji safi sehemu nyingi na umeme wa mashaka kila siku lakini tunaona Mabilioni yakawekezwe kwenye majumba ambayo hatujui nani atapanga huku tukiwatimua watu toka makazi yao.Mimi kwa haraka naona kuna kitu kimejificha kwenye huu mradi mpaka unapelekwa puta hivi. Waziri wa ardhi katangaza bajeti ya mwaka huu kwenye huu mradi tena ni 10% ambayo ni Mabilioni na akasema hizo 90% zilizobaki 'watajua namna ya kuzipata'!! Hapa lazima kuna jambo.. Utaanzishaje mradi wakati hata fedha hujui utatoa wapi? Wenye kujua kidogo kuhusu huu mradi watujuze labda wengine tunashindwa kuelewa kwa akili ya kawaida.

safi sana umeongea kitu kizur ila Ngoja watu tulipwe ela zetu au hutaki maendeleo!? Kutokana na Thread yako nakupa 44%. Nakutania tu Mjomba
 
Hatujui kuchagua vipaumbele. Ujenzi wa mji si kipaumbele hata kidogo kwa nchi yetu maskini. Vipaumbele vinatakiwi viwe nishati, elimu, maji, mawasiliano, barabara na afya.
 
Goooo goo go go Prof. Tibaijuka hakuna wakuzuia maendeleo ya Watanzania...wakazi wakigamboni wanapaswa kujua Mjimpya sio kwaajili yao tuu, ni kwa ajili ya watanzania wote..tunataka maendeleo sio sumu za kisiasa toka kwa DR.Ndugulile, ya kwake tunayajua hivyo apishe maendeleo yaje...

Wananchi wa Kigamboni hawajaukataa mji mpya, tatizo ni taratibu hazifuatwi na watendaji wa wizara ya ardhi katika kushughulikia mradi huu.

Wamekuwa wakiwalazimisha wananchi kukubali pasipo kuwekwa wazi na hatima ya mali zao. Huwezi kuambiwa usaini kitu usichokielewa, na ndio yaliyofanyika Kigamboni.

Lakini ni imani yangu kutokana na maelezo ya Waziri wa ardhi, wananchi wa kigamboni watakuwa wamemuelewa na endapo kama waziri hajaongea kisiasa, basi suluhisho litapatikana.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Tatizo kubwa la serikali ya CCM siku zote haina priority list ya projects zake. Sijui kwanini inapenda kukurupuka kila mara. Si lazima projects zote zianze kwa pamoja. tatizo kubwa hapa ni kuwa Kigamboni ina masilahi binafsi especially kwa viongozi wetu. Nani hajui kuwa wengi wao wameshakamata maeneo huko!
Kinachofuata ni daraja la kigamboni kujengwa kwa haraka iwezekanavyo ili wasipate adha wanayoipata wakazi wake walalahoi sasa hivi.
kujengwa Kigamboni ni maendeleo makubwa pia ila ndiyo kipaumbele kwa kipindi hiki kigumu cha uchumi?


Tanzania jambo likifanyika kwa kuwekewa mkazo zaidi ujue lazima kuna 10% ya viongozi.


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Mbunge wao sasaa naye anawekewa zengwe kwa kuwatetea raia wake! Kuna jambo sio siri.
 
Kigambini ndio sehemu watakayoishi wamarekani watakaokuja kutwaa uranium yetu, ninyi wajinga si mnajengewa miundo mbinu kuelekea sehemu kutakakochimbwa uranium kama vile barabara za lami na umeme kupitia Millenium Challenge Account
 
Back
Top Bottom