Hatuna Intelijensia katika Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa?

TAI MWEKUNDU

Member
Jun 17, 2013
5
0
Kutokana na matukio ya ugaidi na uhalifu mwingine kuongezeka hapa nchini; je hatuna Intelijensia katika Jeshi la Polisi
na katika Idara ya Usalama wa Taifa? Maana vyombo hivi vya dola vinaowajibu wa kukusanya taarifa mbalimbali za kiusalama kwa lengo la kuzuia matukio mabaya kufanyika. Kitendo cha Polisi na Usalama wa Taifa kushughulikia matokeo ya vitendo vya uhalifu (criminal Aftermath), si uthibitisho kwamba vyombo hivi vya dola vimeshindwa kuwalinda raia na mali zao?
 
Kutokana na matukio ya ugaidi na uhalifu mwingine kuongezeka hapa nchini; je hatuna Intelijensia katika Jeshi la Polisi
na katika Idara ya Usalama wa Taifa? Maana vyombo hivi vya dola vinaowajibu wa kukusanya taarifa mbalimbali za kiusalama kwa lengo la kuzuia matukio mabaya kufanyika. Kitendo cha Polisi na Usalama wa Taifa kushughulikia matokeo ya vitendo vya uhalifu (criminal Aftermath), si uthibitisho kwamba vyombo hivi vya dola vimeshindwa kuwalinda raia na mali zao?
Matukio kama haya yametokea marekani,congo,japani,rwanda,pakstani,china na meneo mengine mengi duniani hapo napo utasemaje.

mkuu siyo kila tukio vyombo vya dola vitaweza kulijua mfano hapo ulipo wewe ukiamua kwenda kuchoma moto pale hospitali ya simiyu nani atajua kuwa unawazo kama ila baada ya tukio ndipo vyombo vitadili na wewe.

Kwa hiyo inategemea aina ya tukio kunamengine watakubaini na mengine hawatakubaini.
 
Nchi hii anailinda Mungu mwenyewe tu sikuakichoka hatuna ulinzi hapa. Kama wasomali wanaweza kuingiza malori makubwa na wkawajaza watu na wengine wakafia njiani na wakawateremsha maiti bila kukmtwa utasema tuna usalama hapo?
 
Matukio kama haya yametokea marekani,congo,japani,rwanda,pakstani,china na meneo mengine mengi duniani hapo napo utasemaje.

mkuu siyo kila tukio vyombo vya dola vitaweza kulijua mfano hapo ulipo wewe ukiamua kwenda kuchoma moto pale hospitali ya simiyu nani atajua kuwa unawazo kama ila baada ya tukio ndipo vyombo vitadili na wewe.

Kwa hiyo inategemea aina ya tukio kunamengine watakubaini na mengine hawatakubaini.

Thanks for your justification true great thinker ! mjinga msifu tu
 
Mkuu nakubaliana na majibu yako. Katika baadhi ya nchi ulizotaja mfano Marekani; baadhi ya matukio kama vile ya ugaidi yanatokana na uzembe au kujiamini kupita kiasi. Mfano; tukio la Septemba 11, 2001 na lile la kulipuliwa kwa ubalozi wake Dar es Salaam na Nairobi mwaka 1998. Kama unafuatilia utakubaliana nami kwamba; CIA walikuwa na taarifa juu ya kuwepo kwa mashambulizi hayo ya kigaidi. Huo ndio ubora wa Intelijensia japo hawa kua act kuzuia mapema. Nipe mfano hai wa hapa kwetu; ni tukio lipi ambalo baada ya kutokea ilionekana TISS au Polisi walikuwa na taarifa zake?
 
Mimi naona hao hao walioaminiwa ndio hao hao wanaoendesha hayo matukio,wanataka tusahau mambo mabovu ya serikali na kutupeleka kuwaza mauaji huko uchumi ukidorora kila siku iendayo kwa Mungu,haiji akilini ati ni kwenye mikutano ya CDM tu ambayo haishi salama,wanataka tuamini CDM ni watu wa vurugu na tuogope kwenda kwenye mikutano ya CDM,kwa hilo intelejensia imekula wa nhuuna ndio tutazidi kwenda kwenye mikutano hiyo ya CDM kwani mbaya wa hayo yote anajulikana
 
Mkuu nakubaliana na majibu yako. Katika baadhi ya nchi ulizotaja mfano Marekani; baadhi ya matukio kama vile ya ugaidi yanatokana na uzembe au kujiamini kupita kiasi. Mfano; tukio la Septemba 11, 2001 na lile la kulipuliwa kwa ubalozi wake Dar es Salaam na Nairobi mwaka 1998. Kama unafuatilia utakubaliana nami kwamba; CIA walikuwa na taarifa juu ya kuwepo kwa mashambulizi hayo ya kigaidi. Huo ndio ubora wa Intelijensia japo hawa kua act kuzuia mapema. Nipe mfano hai wa hapa kwetu; ni tukio lipi ambalo baada ya kutokea ilionekana TISS au Polisi walikuwa na taarifa zake?

Wanajamii, matukio haya ya watu wasio na hatia kuuawa yanaumiza kila mtu, lakini tunapoyajadili na kuhitimisha kuwa vyombo vya usalama ndio cha tatizo na kutoa "comparisons" tusizozifahamu vyema hatujitendei haki ktk jukwaa hili na hatuwatendei haki hao tunaojaribu kuwalaumu. Huwezi kusema CIA walijua tukio la Sept.11 halafu wasichukue hatua yeyote just because walijiamini kupita kiasi, kwa vyovyote kama walijua maana yake walikusanya taarifa za kutosha za kiusalama zilizo justfy kutokea kwa tukio hilo na wangeweza kuzuia, so kwanini hawakufanya hivyo. Tusikubali kulishwa propaganda za kisiasa bila hata kutafuna. Vipi kuhusu tukio la hivi karibuni ktk jiji la Boston? Je, Boston Police Department/FBI/CIA/NSA...you name it, hawana intelligence ktk vyombo vyao ili wazuie matukio hayo kutokea? Tukio tata la ajali ya Princess Diana kipindi hicho, au kupigwa visu hadi kuuawa kwa mwanajeshi mmoja huko UK, je MI5 or MI6 hawana intelligence ktk vyombo vyao?. Kuna baadhi ya matukio kutokana na asili yake huwezi kuyazuia mara moja yanapokuwa tayari organized, ni lazima uwe na taarifa toshelevu ili u-act haraka kwa kujua ni nani,ni saa ngapi,na wapi tukio limepangwa kufanyika. Sasa kama vyombo vyetu vimeshindwa ku-act haraka katika matukio ya mabomu yaliyotokea hapa kwetu it's very unfortunate, labda kutokana na asili ya matukio yenyewe, lakini hatuwezi kuvilaumu vyombo hivyo kwamba havifanyi kazi na ndio chanzo cha kutokea matukio hayo, wakati tuhafahamu uendeshwaji wa siasa zetu ni wa kibinafsi, hakuna anayejali maslahi ya taifa ya muda mrefu ila kinachotafutwa mwisho wa siku ni huruma ya wananchi ili chama cha siasa kiishi.
 
matukio kama haya yametokea marekani,congo,japani,rwanda,pakstani,china na meneo mengine mengi duniani hapo napo utasemaje.

Mkuu siyo kila tukio vyombo vya dola vitaweza kulijua mfano hapo ulipo wewe ukiamua kwenda kuchoma moto pale hospitali ya simiyu nani atajua kuwa unawazo kama ila baada ya tukio ndipo vyombo vitadili na wewe.

Kwa hiyo inategemea aina ya tukio kunamengine watakubaini na mengine hawatakubaini.

mkuu tatizo lingekuwa ni moja ningekubaliana nawewe lakini matukio zaidi ya kumi yoote ayana majibu ukweli ni kuwa hawafanyi kazi yao vyema!
 
Kama kweli chadema wana ushahidi wa hili la ar kwann wanapiga danadana? Hapo maana yake wamehusika wanaogopa kuaibika
 
Tunayo inteligensia katika chadema tu maana wameupata ushahidi baada tu ya mabomu kulipuka na hawampi mtu
 
kuuliza sio ujinga inteligensia inaundwaje na inafanya kazi gani? nikijulishwa takua na haki ya kuchangia mada. asanteni
 
Kutokana na matukio ya ugaidi na uhalifu mwingine kuongezeka hapa nchini; je hatuna Intelijensia katika Jeshi la Polisi
na katika Idara ya Usalama wa Taifa? Maana vyombo hivi vya dola vinaowajibu wa kukusanya taarifa mbalimbali za kiusalama kwa lengo la kuzuia matukio mabaya kufanyika. Kitendo cha Polisi na Usalama wa Taifa kushughulikia matokeo ya vitendo vya uhalifu (criminal Aftermath), si uthibitisho kwamba vyombo hivi vya dola vimeshindwa kuwalinda raia na mali zao?

Tai; vyombo vya usalama havipo kwa ajili ya kuondoa (to eliminate) crime isipokuwa kupunguza (minimize) crime kwa kuzuia pale panapokuwa na uwezekano. Maximum crime rate kwa mwaka yaweza kuwa inafikia matukio tuseme hata 360 ya kigaidi kama hayo uliyoyaona yametokea, ila wakazuia 358 na hayo mawili yakawaponyoka. Kwa vile huwa hawatangazi kwamba wamezuia mangapi, kwa raia wa kawaida kama mimi nitajikita kwenye hayo matukio mawili tu niliyoyaona na kufanya analysis yangu kuonyesha kuwa hawafanyi kazi, kwa sababu yale ambayo wamezuia sikuweza kuyafamu kwa hiyo na-assume kuwa hayakuwepo kumbe yalikuwepo. Ninachohisi ni kwamba wakiamua kuachia hata lisaa limoja tu wakaacha kufanya kazi, pengine hata wewe mwenyewe huwezi tena kuendelea kuwepo kwa sababu hautabaki salama. Sisi siyo professionals ndiyo lakini wakati mwingine tuwe tunatoa hoja kwa kuangalia tusije kuwakosesha moyo watu wengine kwenye kazi zao. Mimi naamini tuko salama, na tutaendelea kuwa salama Mungu yupo na watu wanaofanya kazi kuhakikisha tunaendelea kubaki salama wapo.
 
Wanajamii, matukio haya ya watu wasio na hatia kuuawa yanaumiza kila mtu, lakini tunapoyajadili na kuhitimisha kuwa vyombo vya usalama ndio cha tatizo na kutoa "comparisons" tusizozifahamu vyema hatujitendei haki ktk jukwaa hili na hatuwatendei haki hao tunaojaribu kuwalaumu. Huwezi kusema CIA walijua tukio la Sept.11 halafu wasichukue hatua yeyote just because walijiamini kupita kiasi, kwa vyovyote kama walijua maana yake walikusanya taarifa za kutosha za kiusalama zilizo justfy kutokea kwa tukio hilo na wangeweza kuzuia, so kwanini hawakufanya hivyo. Tusikubali kulishwa propaganda za kisiasa bila hata kutafuna. Vipi kuhusu tukio la hivi karibuni ktk jiji la Boston? Je, Boston Police Department/FBI/CIA/NSA...you name it, hawana intelligence ktk vyombo vyao ili wazuie matukio hayo kutokea? Tukio tata la ajali ya Princess Diana kipindi hicho, au kupigwa visu hadi kuuawa kwa mwanajeshi mmoja huko UK, je MI5 or MI6 hawana intelligence ktk vyombo vyao?. Kuna baadhi ya matukio kutokana na asili yake huwezi kuyazuia mara moja yanapokuwa tayari organized, ni lazima uwe na taarifa toshelevu ili u-act haraka kwa kujua ni nani,ni saa ngapi,na wapi tukio limepangwa kufanyika. Sasa kama vyombo vyetu vimeshindwa ku-act haraka katika matukio ya mabomu yaliyotokea hapa kwetu it's very unfortunate, labda kutokana na asili ya matukio yenyewe, lakini hatuwezi kuvilaumu vyombo hivyo kwamba havifanyi kazi na ndio chanzo cha kutokea matukio hayo, wakati tuhafahamu uendeshwaji wa siasa zetu ni wa kibinafsi, hakuna anayejali maslahi ya taifa ya muda mrefu ila kinachotafutwa mwisho wa siku ni huruma ya wananchi ili chama cha siasa kiishi.
Ndugu yangu kabisa mimi kabisa nakubaliana na wewe. Unajua kawaida yetu sisi raia, huwa yanakuja matukio ya hatari, yanakwepeshwa na vyombo husika pasipo sisi wenyewe kujua, halafu tunaendelea na maisha kwa kujua kuwa tuko salama tu kwa guarantee sijui ya nani, kumbe kuna watu nyuma wanafanya kazi usiku na mchana kukwepesha matukio ya ajabu yasitupate, pasipo sisi wenyewe kujua.Tuseme ikitokea kwa mfano, mtu siku akajikuta yuko kwenye janga ambalo ni la hatari limekuwa likimunyemelea kisirisiri tena siku nyingi ila alikuwa hajui kama lipo, halafu kwa bahati nzrui akaja akajua kuwa lipo (which is a very rare chance) na akajua pia kuwa pamekuwa na watu nyuma yake siku nyingi wakiliangalia kwa jicho la uchungu ili kumunusuru mtu huyo kwa sababu ni innocent, na pasipo wao kumwambia yeye, siku hiyo ndiyo atakuja kujua kuwa kuna vyombo vinafanya kazi hapa!
 
Back
Top Bottom