Hatuna haja ya kuleta wataalamu kutoka Misri kujifunza umwagiliaji

MTENDAHAKI

JF-Expert Member
Mar 3, 2011
4,013
1,443
Hakuna shaka kwamba Misri ndio babu wa umwagiliaji duniani. Hata hivyo tumeshajifunza kitambo toka kwao, na hata sehemu nyingine duniani kwamba umwagiliaji ni uhandisi unaotaka uwekezaji wa kutosha!

Siasa tamu za kusema wataalamu watanzania wanaweza kunufaika na ziara ya Rais wa Misri kwa kwenda kujifunza wenzetu wao walivyofanikiwa kwenye umwagiliaji ni upuuzi!

Inajulikana tatizo letu ni fedha, sio wataalamu!Tunao wabobezi wa umwagiliaji kila kona, kuanzia wizarani mpk ngazi ya kata!Wapo magwiji wa umwagiliaji vyuo vikuu wakiongozwa na SUA!

Wataalamu hawana cha kujifunza kutoka Misri, serikali inatakiwa ijifunze kutoa hela za umwagiliaji na isirushe mpira wa kitoto! Serikali haijawahi kutoa pesa za umwagiliaji kulingana na usanifu, nimefanya utafiti wa miradi kadhaa na kugundua serikali hutoa wastani wa chini ya 30% ya fedha ya usanifu wa mradi wa umwagiliaji, ndio maana hakuna mradi wa umwagiliaji uliojengwa ukakamilika toka Nyerere astaafu.

Kwa mito tuliyonayo, maziwa na mabwawa hakika Tanzania inatakiwa iwe mzalishaji mkuu wa mazao ya biashara na chakula duniani!Tanzania ni kati ya nchi zenye maji mengi zaidi yanoyofaa kwa kilimo cha umwagiliaji lakini ndio kati ya nchi zinazotumia umwagiliaji kwa kiwango cha chini kabisa!

Mpaka njaa itukomeshe, au mpaka apatikane kiongozi anayejua chakula ni kipaumbele cha kwanza ndipo tutakapopiga hatua! Hizi za kunufaika kutoka Misri ni siasa tamu za mgongo wa chupa!

Mtendahaki
 
Umeandika andiko la mwaka huu. Yaani uliyo ongea yako wazi 100% mimi ni mmoja wa waathirika wa sera za kilimo cha Tanzania. Professional yangu ni drip irrigation. Lakini ukiingiza vifaa vya umwagiliaji wa matone TRA hawajui kipi ni kipi watakuambia lazima hiki ulipie yaani siasa kila mahali. Ina kera. Inaudhi sasa nimeamua kukaa kimya ili roho yangu iwe na amani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Misri kiteknolojia wako mbele zaidi kuliko sisi ndio maana pamoja na kua na chanzo kimoja cha maji lakini wameweza kulima kilimo cha umwagiliaji na kupata chakula cha kutosheleza nchi yao na kuuza nje. Pamoja na mafanikio hayo yote wewe unasema hatuna cha kujifunza basi anzisha mradi wako wa kilimo cha umwagiliaji ili tujifunze kwako badala ya kwenda musri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inajulikana tatizo letu ni fedha, sio wataalamu!Tunao wabobezi wa umwagiliaji kila kona, kuanzia wizarani mpk ngazi ya kata!Wapo magwiji wa umwagiliaji vyuo vikuu wakiongozwa na SUA!
Mkuu, well said!! hata kwenye ile thread ya jana ya Rais wa Misri kuna mtu nilimpinga kwa hii hoja ya kujifunza. Hii lugha ya kila kitu eti tujifunze kwa wenzetu naona inatudharirisha sana.

Anyway, hapo nilipokuquote, nafikiri tatizo letu siyo kuwa hatuna pesa bali ni priorities!! Imagine kama pesa za Boeing Dreamliner zingepelekwa kwenye kilimo ingekuwaje!!? Kilimo chetu kinazidi kuzorota badala ya kuimalika!! Binafsi huwa nalinganisha na enzi zile za late 70s na early 80s nilipokuwa mdogo tukiwenda likizo kuwasalimia Bibi na babu kijijini, kwa kweli ukilinganisha na sasa utaona ni kiasi gani uzalishaji ulivyoshuka. AT LEAST KIJIJINI KWETU!!

Awamu hii wanadai VIWANDA ............. tatizo kama hakuna mali gafi, viwanda ni ndoto za mchana!!
 
Umeandika andiko la mwaka huu. Yaani uliyo ongea yako wazi 100% mimi ni mmoja wa waathirika wa sera za kilimo cha Tanzania. Professional yangu ni drip irrigation. Lakini ukiingiza vifaa vya umwagiliaji wa matone TRA hawajui kipi ni kipi watakuambia lazima hiki ulipie yaani siasa kila mahali. Ina kera. Inaudhi sasa nimeamua kukaa kimya ili roho yangu iwe na amani

Sent using Jamii Forums mobile app
inasikitisha sana unapoona kila sekta wataalamu husika wamekata tamaaa kama wewe hii ni sababu ya sera mbovu. pole sana mtaalamu wa drip irrigation.
 
Misri yenyewe anapewa hela na marekani kila mwaka, wao ni matonya kama sisi tu ila umatonya wao kidoogo una nafuu kuliko sisi.
Hawana cha maana cha kutusaidia!
Ni kweli lakini kutoa ni moyo ndio maana hata marekani mwenyewe kwenye bajeti yake kila mwaka anakopa karibu 500trn lakini ndo taaifa linaloongoza kwa kutoa misaada mikubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Misri kiteknolojia wako mbele zaidi kuliko sisi ndio maana pamoja na kua na chanzo kimoja cha maji lakini wameweza kulima kilimo cha umwagiliaji na kupata chakula cha kutosheleza nchi yao na kuuza nje. Pamoja na mafanikio hayo yote wewe unasema hatuna cha kujifunza basi anzisha mradi wako wa kilimo cha umwagiliaji ili tujifunze kwako badala ya kwenda musri.

Sent using Jamii Forums mobile app
mkuu soma vizuri. tatizo ni kwamba siyo wataalamu hawapo?. tatizo ni pesa ya kujenga miladi hiyo?. sasa sijui hujamuelewa. mimi kunaclassmate wangu pia mwaka jana alikuwa misri kujifunza mambo ya maji but sasa kaludi anakaaa tu na utaaramu huo.
 
tunachohitaji kutoka kwa wa misri ni uzoefu ktk utendaji na ushauri wa kitaalaam ktk utekelezaji wa mikakati ktk kilimo...

kuhusu ujuzi(elimu) naamin wapo wataalam wengi wenye ujuzi wa kilimo hasa cha umwagiliaji kutoka ktk vyuo vya hapahapa tz... sua, chuo cha maji nk.
 
Umeandika andiko la mwaka huu. Yaani uliyo ongea yako wazi 100% mimi ni mmoja wa waathirika wa sera za kilimo cha Tanzania. Professional yangu ni drip irrigation. Lakini ukiingiza vifaa vya umwagiliaji wa matone TRA hawajui kipi ni kipi watakuambia lazima hiki ulipie yaani siasa kila mahali. Ina kera. Inaudhi sasa nimeamua kukaa kimya ili roho yangu iwe na amani

Sent using Jamii Forums mobile app
Wote mnalalamika na kulia pale tu mnapoona maslahi yenu yanaingiliwa.
Watu wa IT walitokwa na mapovu waliposikia wanaletwa wataalam toka Rwanda.
Ukweli ni kuwa wataalam wetu hamjiongezi zaidi ya kukaa ofisini tu na kusubiri kufanyiwa kila kitu na serikali
Wewe umeagiza vifaa vya drip irrigation kwa mradi upi?uliusajili mradi wako TIC ili upate msamaha wa kodi au ulikurupuka tu kuagiza mabomba na motor?
Mbona wanapoletwa madaktari huwa hatusikii wakilalama kuwa hakuna haja ya kuleta madaktari,serikali iongeze tu fungu?
Elimu ni sawa na bahari,wewe ukijua hivi wenzako wanajua vile,pengine kwa bajeti hii ndogo ya serikali hao wamisri wanaweza kutufundisha mbinu za hali ya juu kabisa.
Sio kila kitu cha kupingwa
 
Mkuu, well said!! hata kwenye ile thread ya jana ya Rais wa Misri kuna mtu nilimpinga kwa hii hoja ya kujifunza. Hii lugha ya kila kitu eti tujifunze kwa wenzetu naona inatudharirisha sana.

Anyway, hapo nilipokuquote, nafikiri tatizo letu siyo kuwa hatuna pesa bali ni priorities!! Imagine kama pesa za Boeing Dreamliner zingepelekwa kwenye kilimo ingekuwaje!!? Kilimo chetu kinazidi kuzorota badala ya kuimalika!! Binafsi huwa nalinganisha na enzi zile za late 70s na early 80s nilipokuwa mdogo tukiwenda likizo kuwasalimia Bibi na babu kijijini, kwa kweli ukilinganisha na sasa utaona ni kiasi gani uzalishaji ulivyoshuka. AT LEAST KIJIJINI KWETU!!

Awamu hii wanadai VIWANDA ............. tatizo kama hakuna mali gafi, viwanda ni ndoto za mchana!!
pesa huwa siyo tatizo ila mipango tufanye nini na pesa ndiyo huwa tatizo
 
unauhakika na hiki ulichogandamizia RED?

Vipi lower moshi irrigation scheme?
Vipi dakawa irrigation scheme?

Kapunga?
Kilosa?
name them.........................
Scheme zote hizo zinasuasua , productivity ni very low.
 
Tangu enzi na enzi mababu zetu walikuwa wanamwagilia kwa kutumia mifereji ya asili, leo tunashindwa? Huu ni zaidi ya ujinga.
Wakati mwingine elimu ya darasani hupumbaza.
Eti wataalam wetu wanasema hawapewi pesa.Kukusanya vijana 100 wakachimba mtaro,wakafanya kazi kwenye shamba husika la mpunga wakalipwa kutokana na mavuno nako kunahitaji pesa gani?halafu mtu anajiita msomi
 
Wote mnalalamika na kulia pale tu mnapoona maslahi yenu yanaingiliwa.
Watu wa IT walitokwa na mapovu waliposikia wanaletwa wataalam toka Rwanda.
Ukweli ni kuwa wataalam wetu hamjiongezi zaidi ya kukaa ofisini tu na kusubiri kufanyiwa kila kitu na serikali
Wewe umeagiza vifaa vya drip irrigation kwa mradi upi?uliusajili mradi wako TIC ili upate msamaha wa kodi au ulikurupuka tu kuagiza mabomba na motor?
Mbona wanapoletwa madaktari huwa hatusikii wakilalama kuwa hakuna haja ya kuleta madaktari,serikali iongeze tu fungu?
Elimu ni sawa na bahari,wewe ukijua hivi wenzako wanajua vile,pengine kwa bajeti hii ndogo ya serikali hao wamisri wanaweza kutufundisha mbinu za hali ya juu kabisa.
Sio kila kitu cha kupingwa
Mkuu, tatizo letu kuwa ni kuwa hakuna government initiatives na lack of vision!!

Hivi kweli kati ya viwanda na kilimo kipi kilitakiwa kiwe kipaumbele chetu kwanza!!? Nchi ya 70 % wakulima, over 80 % elimu ya msingi ........... Seriously!!?
 
Back
Top Bottom