Hatua zinaendelea kuchukuliwa kuhusu tuhuma na shutuma zilizotolewa

Hivi Mhe. John Mnyika mimi nina swali hili,
Hivi kipindi kile watu tunashuhudia matusi makubwa tena mengine ya ndani kabisa yakivurumushwa fcbk na vijana wenu kama Mtela Mwampamba, Juliana Shonza co kwenda kwa viongozi wakuu wa chama, Mlikuwa wapi kukemea tabia ile? Au mlisubiri kwanza Ben Saanane aje kulianzisha na nyie ndo mfate? Pia kwanini zitto kwenye nyaraka mbalimbali ambapo sehemu ya kujaza chama yeye huwa anajaza" KIGOMA KASKAZIN" inamana mnataka tuamin CHADEMA kila mtu anajivua eneo analotoka na sio chama.?

Shardcole,

Nashukuru. Naomba urudie tena kusoma katikati ya mstari mchango wangu wa kwanza utabaini kuwa kabla hata ya tuhuma na shutuma za sasa kutolewa JF tayari chama kilishaanza kuchukua hatua kuhusu baadhi ya wanachama kuchafua viongozi kwenye mitandao ya kijamii na njia nyingine za mawasiliano.

JJ
 
Avanti, asante kwa maoni yako hata hivyo zingatia kuwa 'press' yangu ipi? Ikiwa wewe kweli ni mwanachama wa CHADEMA na una malalamiko dhidi ya kadi ya Dr Slaa andika rasmi kwa chama. Kabla ya kuandika malalamiko hayo usome kwanza katiba ya CHADEMA, katiba ya CCM na sheria ya vyama vya siasa. Dr Slaa ameshasema wazi kwamba yeye si mwanachama wa CCM, ni mwanachama wa CHADEMA toka alipohama CCM. Mwanachama akihama chama kimoja tayari anapoteza uanachama wake wa chama cha awali, hii ni kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa, katiba za vyama vya siasa na pia hukumu ya mahakama ambayo imewahi kutolewa kuhusu suala la kadi. Ukishazingatia hayo na bado ukaendeleza suala hilo na ikiwa kwenye ni mwanachama utakuwa umeingia kwenye mtego wa kipuuzi wa CCM.

JJ
Jibu zuri. uanacham uko moyoni na unaongowazwa na matendo ya mtu.utamtambua mtu kwa matendo na si kadi pekee. kadi ni nini? kwanza kama haitumiki ni karatasi tu!
 
Angalia usimponze tusibakishe hata panya huko nyumbani kwake!.

Hakiharibiki kitu, Mhe. JJ Mnyika ni mmoja ya wabunge wa jamhuri kwani anatetea maslahi mapana ya nchi. Ana sala ya watanzania walio wengi wapenda maendeleo. Mimi binafsi ninamuombea pamoja na kwamba si mwana CHADEMA.
 
Now I'm starting to believe that 'Operation chaos' is kind of working.

But what doesn't kill you can only make you stronger.

So hopefully CHADEMA will be able to ride out the storm.

Ila kilichonishangaza na kunisikitisha (na sijui hata kwa nini nimeshangaa na kusikitika) ni hayo mambo ya ushirikina.

Yaani "vijana" tena ambao tunaambiwa ni "vichwa" (whatever the hell that means) na "wasomi" wanatuhumiana mambo ya kula viapo mbele ya waganga wa kienyeji?

Nachoka kabisa!
NN unashangaa hayo??
subiri utaona zadi ya hayo?? wajua kwann??

tu wavivu wa kufikiri na wepesi wa kukata tamaa. hatuna subira hata babeli haikujengwa kwa siku moja. sasa mtu anataka leo hii akitoka na kuskiwa kesho apeweorganization a run tukasahau kwamba tunahitaj muda wa kujitathmini na kujipima na pia kupata experience juu ya kukabiliana na mambo.

yote haya yanapokosekana basi watu hukimbilia kwenye ushirikina wakiamni ndipo dawa ilipo kumbe dawa ni kujipoteza tu.

fikiri hivi tuliambiwa albino wanatumiwa kwa waganga na ndio maana watu wanawaua sasa je hawa vijana kama wanadiriki kwenda kwa waganga na waganga wanatumia albino je hawa vijana sio washiriki wa mauaji ya albino kwa kutumia laogic??
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Vumbi tu! Mlikuwa wapi muda wote? Matatizo lukuki, nazidi kusisitiza uongozi ni tatizo, kaka angalia nawe usije ukawa mojawapo ya tatizo kwa sababu tayari press yako iko biased kwamba "viongozi wamekashifiwa". Hao wanatakiwa kujibu tuhuma na kila mmoja ana haki kidemokrasia kutaja maonevu, mfano Dr Slaa kuwa na kadi ya CCM ambako mimi siafiki ni kashfa?

Sana sana, kama hamna kitachotamkwa kuhusu kadi mi najitoa CDM na wewe mwenyewe utakosa kura yangu.

wewe kuwa mwelewa bwana,kuna mambo makubwa na magumu yakuzungumzia sio kadi ya slaa,kadi ya mwanachama ni mali ya mwanachama mwenyewe ana hiari ya kuchoma ,kutupa ama kuwa nayo,ajenda ya kumiliki kadi haina mashiko kwa sie wanamabadiliko.hzo ni propaganda za nape alietaka kuhamia na kuanzisha ccj.tulipofika ni pazuri sasa mana ccm wanatapatapa wamekosa pakushka.peoplezzzz....chezea nguvu ya umma wewe?
 
Kama mnataka haki basi Dk.Slaa, Juliana Shonza na Zitto Kabwe waondoke madarakani kwa muda hadi uchunguzi ukamilike, vyenginevyo itakuwa ni kukiuka misingi ya haki na usawa katika sakata hili

Huwezi kamwe kutegemea Juliana Shonza awasilishe ushahidi wake dhidi ya Slaa katika kikao kinachoongozwa na Slaa, na haki itendeke.
Pole sana mtumwa wa Lumumba (Gaijan)naona jina la Dk.Slaa linawatesa sana.Kama mapepo wakisikia jina la YESU lazima yalipuke.
 
Freshthinking,

Naelewa kinachoendelea...Majaribio yote juu yangu yatashindwa.I promise you all,I'll defeat you

Ukiwa Mahakamani mnaambiwa mzime simu.Kuna kitu kinaitwa contempt of the court.Kisheria ukikutwa na kosa hilo hukumu
ni kifungo cha siku 14-Miezi 6.

-Umesahau kwamba simu zinatakiwa kuzimwa kwa kuepuka usumbufu.Vipi nikiweka silent?

-Je nikiweka Silent nikiwa nje ya chumba cha Mahakama inakuaje?


Look Mr.President,Majaribio yote mtashindwa
Mimi nilijua kwanza utashuuru nimekupa taarifa za 'ki-intelligensia'! Lakini ukiachilia mbali hilo ambalo mtajuana wenyewe. Wewe kama kiongozi in the making, kwanini hujengi usikivu na utii wa sheria halali za Tanzania? Unawafundisha nini wafuasi wako?
 
................Nilishatoa maoni kwamba ...maneno matupu bila vitendo ............. ni hatari... gharama ya kukifikisha chama kilipo ni kubwa mno.... kuliko gharama ya kukisambaratisha... unaweza kutafuta 10m kwa miaka .. lakini ukazifuja ndani ya siku chache.... take care
 
Shardcole,

Nashukuru. Naomba urudie tena kusoma katikati ya mstari mchango wangu wa kwanza utabaini kuwa kabla hata ya tuhuma na shutuma za sasa kutolewa JF tayari chama kilishaanza kuchukua hatua kuhusu baadhi ya wanachama kuchafua viongozi kwenye mitandao ya kijamii na njia nyingine za mawasiliano.

JJ

Point noted hon John Mnyika.
 
Last edited by a moderator:
Jorojik,

Asante, sio kila kitu lazima wasemaji wa chama tuingie kutoa ufafanuzi. Zingine ni propaganda za kijivu ambazo hata nyinyi mnaweza kuzitolea majibu.

Ikiwa kila uzushi na upuuzi unaoandikwa mtatulazimisha viongozi tuingie na kuutolea majibu mtakuwa mmefanikisha malengo yao ya kututoa nje ya mstari wa kuiwajibisha Serikali na viongozi wake kwa manufaa ya watanzania wakati huu na pia kuhamasisha umma kuunga mkono vuguvugu la mabadiliko kwa lengo la kuindoa CCM katika uongozi wa nchi.

Suala la Karatu na KAVIWASU tayari lilishafanyiwa maamuzi na Kamati Kuu ya chama, rejea: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-kutangaza-nguvu-ya-umma-rasmi-endapo-4.html

Dr Slaa hatuhumiwi na ufisadi wowote katika mradi huo, kuutambua uzushi katika maandiko yaliyowekwa hapa JF ni rahisi sana. Madai yanayotolewa ni kuwa CAG alifanya ukaguzi, ukweli ni kuwa CAG hajawahi kufanya ukaguzi wowote na mahesabu ya KAVIWASU hayakaguliwi naye. Kungekuwa na ripoti ya namna hiyo ya CAG inayomgusa Dr Slaa sio ndio ingekuwa wimbo wa taifa wa CCM iliyoshindwa kujivua magamba ya ufisadi?

JJ
Mkuu asante sana kwa ufafanuzi huu kwakweli hili jambo lilianza kuchafua hali ya hewa humu ndani na naomba muwe mnatolea ufafanuzi haya mambo mapema kabla hayajaanza kuleta sintofahamu.
 
Saa8 jiandae, huenda 2013 usiwe mwaka mzuri sana kwako maana huenda ukaandamwa na kesi nyingi. Kuna watu nasikia wanajipanga kukufungulia kesi wewe na Yericko Nyerere kwa kufanya Live broadcasting kwenye mahakama ya rufaa wakati wa kesi ya Mh Lema.

Ushahidi ni zile live posting kutoka mahakama ya rufaa. Wakikukosa CDM, jiandae hapa.

Kosa: Mlikiuka amri halali za mahakama ya rufaa ya kuzima simu wakati mkiwa mahakamani na kufanya live coverage kwenye court room.
Mna huzuni kubwa sana toka Ben Saanane awasaliti tena kwa style ya kuua kabisa kundi lenu.
Now is too late to fight against him.

Huko mahakamani hamtamuweza kabisa, it looks like Ben is very smart.
 
Mimi nilijua kwanza utashuuru nimekupa taarifa za 'ki-intelligensia'! Lakini ukiachilia mbali hilo ambalo mtajuana wenyewe. Wewe kama kiongozi in the making, kwanini hujengi usikivu na utii wa sheria halali za Tanzania? Unawafundisha nini wafuasi wako?

Nadhani lengo lako kubwa ni kututoa nje ya mada.kumbe na iyo ni habari ya kiintelijensia??!!!!
 
Nadhani lengo lako kubwa ni kututoa nje ya mada.kumbe na iyo ni habari ya kiintelijensia??!!!!

JJ kimtindo alikuwa anataka kusema watu wasiendelee kujadili hizi shutuma za pande mbili kwa vile chama kinafuatilia.Hizi mada zinashabihiana bana, utamwachaje mwanamapinduzi afe peke yake?
 
Mna huzuni kubwa sana toka Ben Saanane awasaliti tena kwa style ya kuua kabisa kundi lenu.
Now is too late to fight against him.

Huko mahakamani hamtamuweza kabisa, it looks like Ben is very smart.

Sasa wewe CCM umeingiaje CDM tena? Tatizo ni kukariri kuwa kila anayechangia tofauti ni pro-Zitto. Aaa, acheni hizo banaa.
 
Kwa taarifa ni kwamba PM -7 walikuwa wana print screen kadri updates zilivyokuwa zinaingia JF. Si unajua kuna time uliyopostia comment?
Ndugu usitishe watu hapa.
Hicho kitu hakiwezekani na wala hakitawezekana kabisa hapa Bongo, sio kwa raia wala kwa dola, hata mahakamani kuthibitisha tu ni ndoto.

Ben Saanane kawashika pabaya sana, tafuteni another issue lakini sio kitu kama hicho.
 
kafungue katiba ya Chadema ukaangalie "who is Juliana"



Kumuita kwa majina ya kejeli na matusi hakuondoi nafasi yake aliyoipata kihalali kwa mujibu wa taratibu za chama. Aidha kutokumjua kwako wewe hakumaanishi chochote kwenye muktadha wa suali hili

Kama Chadema inataka kuonyesha kuwa inafuata misingi ya haki, Dk.Slaa, Zitto Kabwe na Juliana Shonza wavuliwe vyeo vyao kwa muda hadi uchunguzi utakapomalizika.

Sio kesi ya kima kupelekewa huyo huyo kima walau hata ingekuwa ngedere
utatoa povu sana lakini wewe na genge lako hamtafanikiwa.CHADEMA kina watu makini wenye lengo na nia ya dhati ya kuwaongoza watz kwenye ukombozi wa nchi hii!to hell with your childish plans!viva Mnyika,viva CHADEMA.
 
Copy: Nnauye Jr
Mag,

Shukrani. Kwa maana rahisi mgogoro ni mchakato ambao kila upande una matakwa yake na unaona upande mwingine unakwenda kinyume na matakwa hayo na kufanya vitendo vya kuhujumiana; mgogoro ni kipeo cha kutokuelewana na kutokubaliana kwa kiwango cha kukabiliana. Migogoro mara nyingi huwa na athari na taathira hasi lakini wakati mwingine huleta matokeo chanya.

Baadhi ya wanazuoni wa nadharia ya taasisi (organizational theory) wanagawa migogoro kuwa ya aina kuu tatu: mahusiano, michakato/mifumo na majukumu. Haya masuala na matukio ya wanachama wachache kutuhumiana na kushutumiana yanahusu migogoro yao wenyewe, huwezi kuyaita kwamba CHADEMA kama taasisi ina mgogoro au mpasuko mkubwa.

Migogoro ya yenye athari kubwa kubwa kwa taasisi kama chama ni ile iliyojikita katika michakato/mifumo hata kama imetokana na mahusiano.Ni vyema pia kutenganisha kati ya matukio yenye athari na taathira kwa wanachama wachache au ngazi Fulani ya uongozi wa chama na CHADEMA kama taasisi badala ya kutoa tu hitimisho la ujumla.

Hii itawezesha kutofautisha katika ya tuhuma au shutuma na matokeo ya kuchukua hatua dhidi ya utovu wa nidhamu kwa lengo la kusimamia maadili kwa upande mmoja na migogoro au mipasuko kwa upande mwingine.

JJ
 
Unauliza swali kisha kumbe huelewi hata umeuliza nini?!

Umeambiwa kafungue katiba utaona "who is Juliana" na sio "Juliana", elewa tofauti

Kila aliyeshinda uchaguzi alistahili ndio maana alishinda, au lengo la uchaguzi siku hizi limebadilika?

Amefanya ushirikina kwa kuwa Ben Saanane kasema?!

Iko wapi haki mnaipigania Watanzania wakati tayari mshahukumu kwa yale mnayoyataka kuyasikia tu?

Dk.Slaa, Zitto na Shonza wa-step down kwa muda kupisha uchunguzi
pole mzee!!
 
Ndugu usitishe watu hapa.
Hicho kitu hakiwezekani na wala hakitawezekana kabisa hapa Bongo, sio kwa raia wala kwa dola, hata mahakamani kuthibitisha tu ni ndoto.

Ben Saanane kawashika pabaya sana, tafuteni another issue lakini sio kitu kama hicho.

ushahidi kutoka online post hautambuliki kisheria kwa mahakama za tanzania. Tofauti na nchi kama Uingereza comments kwenye mitandao kama fb na twitter zinatambulika kisheria mahakamani. Kwa sheria zetu hata picha za video lazima uwe umezirekodi mwenyewe siyo tu umeokoteza sijui youtube sijui wapi...kitu cha kwanza ni lazima wawe na uthibitisho pasipo shaka kuwa ben na yeriko walikuwepo mahakamani, pili simu zao hazikuzimwa, tatu simu zao zilikuwa na mtandao (yaani internet) ya kuweza kufanya hizo updates, nne wakiwa ndani ya mahakama walikamatwa wakiwa na simu zao hazijazimwa na wakiwa wamefungua www.jamiiforums.com wakiripoti hiyo kesi kinyume na maagizo ya mahakama.....kisheria wao hawana haki ya kuwafungulia madai yoyote yale ben na yeriko.
 
Back
Top Bottom