Hatua kwa mafisadi

Zero One Two

JF-Expert Member
Sep 16, 2007
9,347
3,023
Wakuu heshima mbele.
Admin sijui hii utaiweka wapi,lakini ninapata maswali mengi kuzidi majibu kutokana na report ya kamati teule ya bunge ambayo pamoja na hoja na mapendekezo yake yaliyojiri ishirini na tatu,ililishauri bunge hatua za kuchukuliwa dhidi ya wote waliotajwa kuhusika na kashfa nzima ya Richmond.

Kama nilimuelewa vizuri waziri mkuu,ndugu Pinda,aliahidi kushughulikia mapendekezo yote ndani ya report ile baada ya uchunguzi wa pili wa serikali.
Tume ilikwishachunguza na kutoa mapendekezo ni kwa nini serikali nayo kwa upande wake ifanye uchunguzi?Na ni kwa hadidu rejea zipi?
Kwa maoni yangu sioni kama kuna haja ya kuendelea na mjadala wa richmond ifikapo kikao kijacho cha Bunge hapo april,badala yake watuhumiwa wote wafikishwe mahakamani kwa ushahidi ambao umetolewa na kamati teule ya bunge.
Ikumbukwe pia wote waliohusika hawakuwa na hoja ya kujitetea ndani ya bunge ili kujinasua na tuhuma za ufisadi.

Kumcheleweshea mtu hukumu dhidi dhidi ya TUHUMA ni kumnyima haki yake.
Kitendo chao kujiuzulu huku wakiwa wamelisababishia taifa hasara kubwa kiende sawa na kushitakiwa mahakamani ikiwa ni pamoja na kurejesha pesa zote za walipa kodi zilizopotea.

Haiingii akilini kuwa unalipa pesa kila siku iendayo kwa mungu kwa kampuni hewa halafu ukaendelea kuwa huru ukifurahia ujambazi ulioufanya.
Kitendo cha Richmond kuwa kampuni hewa ni sababu tosha kuwatia hatiani kwa kutumia jasho la walipa kodi kujinufaisha kwa mamilioni kila siku.

Safari hii tunataka tujue mwenendo wa kesi zao,tofauti na tulivyozoea kuona watuhumiwa wanafikishwa mahakamani halafu basi hakuna kinachoendelea,na mara nyingine unawakuta wakiwa huru wanaendesha miradi yao ya biashara ya ASALI!

Kwa kuanzia freeze accounts zao kuanzia Richmond na EPA then mahakama iwe suluhisho.
Kinyume na hapo,wabunge na sisi tuwe kitu kimoja ili sauti zetu zisikike.

Naomba kuwakilisha.
 
Wakuu heshima mbele.
Admin sijui hii utaiweka wapi,lakini ninapata maswali mengi kuzidi majibu kutokana na report ya kamati teule ya bunge ambayo pamoja na hoja na mapendekezo yake yaliyojiri ishirini na tatu,ililishauri bunge hatua za kuchukuliwa dhidi ya wote waliotajwa kuhusika na kashfa nzima ya Richmond.

Kama nilimuelewa vizuri waziri mkuu,ndugu Pinda,aliahidi kushughulikia mapendekezo yote ndani ya report ile baada ya uchunguzi wa pili wa serikali.
Tume ilikwishachunguza na kutoa mapendekezo ni kwa nini serikali nayo kwa upande wake ifanye uchunguzi?Na ni kwa hadidu rejea zipi?
Kwa maoni yangu sioni kama kuna haja ya kuendelea na mjadala wa richmond ifikapo kikao kijacho cha Bunge hapo april,badala yake watuhumiwa wote wafikishwe mahakamani kwa ushahidi ambao umetolewa na kamati teule ya bunge.
Ikumbukwe pia wote waliohusika hawakuwa na hoja ya kujitetea ndani ya bunge ili kujinasua na tuhuma za ufisadi.

Kumcheleweshea mtu hukumu dhidi dhidi ya TUHUMA ni kumnyima haki yake.
Kitendo chao kujiuzulu huku wakiwa wamelisababishia taifa hasara kubwa kiende sawa na kushitakiwa mahakamani ikiwa ni pamoja na kurejesha pesa zote za walipa kodi zilizopotea.

Haiingii akilini kuwa unalipa pesa kila siku iendayo kwa mungu kwa kampuni hewa halafu ukaendelea kuwa huru ukifurahia ujambazi ulioufanya.
Kitendo cha Richmond kuwa kampuni hewa ni sababu tosha kuwatia hatiani kwa kutumia jasho la walipa kodi kujinufaisha kwa mamilioni kila siku.

Safari hii tunataka tujue mwenendo wa kesi zao,tofauti na tulivyozoea kuona watuhumiwa wanafikishwa mahakamani halafu basi hakuna kinachoendelea,na mara nyingine unawakuta wakiwa huru wanaendesha miradi yao ya biashara ya ASALI!

Kwa kuanzia freeze accounts zao kuanzia Richmond na EPA then mahakama iwe suluhisho.
Kinyume na hapo,wabunge na sisi tuwe kitu kimoja ili sauti zetu zisikike.

Naomba kuwakilisha.

Kamati ya pinda si ya kuchunguza ni ya kupitia hatuwa za kuchukuliwa kutokana na mapendekezo ya kamati ya mwakyembe. Action Task Force.
 
Ok.
Ikishapitia,what is next? Na kama ikipitia na kubatilisha itakuwaje.
Huoni kama itapitia maelezo ya upande mmoja,kwa kuwa hakuna maelezo ya watuhumiwa?

Ni vipi wasipelekwe moja kwa moja kwenye vyombo vyenye mamlaka ambako ndiko haki itapatikana?
 
Jamani msiwe na wasiwasi kwani hiyo Action Task Force ya PM, Pinda itaandaa kazi za kufikishwa hao mafisadi huko Mahakamani. Kwa vile rais J.Kikwete aliahidi kwamba fedha zote ambazo serikali iliporwa zirudishwe hapa itachukuwa muda mrefu. Kwani kazi hii itahitaji pengine ushirikiano na serikali nyingine na mabenki kadhaa.
Kama watafikishwa mahakani kwa Karandinga basi watarudishwa Ukonga kila baada ya kesi yao kusomwa kwa vile upande wa mashitaka utasema bado unakusanya ripoti kamili za upelelezi.
Yule aliyedhaminiwa na kufukuzwa u-RC baada ya kuuwa sasa anauza ASALI. Basi kama hawa mafisadi wa Richmond nao watapata mdamani huenda wakauza UMEME kwa siri siri. Kwani makaa ya mawe ya Kiwira bado wanayo mikononi mwao!
 
Serikali ipewe mda tuone itachukua hatua gani maadamu imeahidi kuchukua hatua. Tusijikite kwenye kulaumu..Pinda kuunda hiyo timu ni pia kuweza kuifanya serikali ijiridhishe na mapendekezo ya tume ya bunge. Let's wait and see.
 
Nawashukuru wachangia hoja, mimi naomba kama mtaridhia, ili la mafisadi tusililinganishe na lile kosa la aliyekuwa RC- bro Ditto. Yeye aliua mmoja wazi wazi, wananchi wakaanza kumkwida mara moja pale pale Kawe, akaona amekosa na kujipeleka yeye mwenyewe kwa hiari yake penye vyombo vya usalama, yeye alitimiza wajibu wake kama raia tena akomba asiitwe Mheshimiwa, akakubali kosa maana naamini aliandika statement, na kujishusha hadi kuswekwa lupango. Angeweza kutunga hadithi km. aliyeua alikimbia, sikuwa mimi nk. na akafanikiwa, yeye hakufanya hivyo. Yaliyoendelea tunaweza kuvilaumu vyombo au mamlaka za kisheria na wala si ditto. Hawa mafisadi wameua na wataendelea kuua mamilioni indirectly kwa ugumu wa maisha waliotusababishia tayari na baadaye unless Rais aamue kutoa kipaumbele kwa taifa na si kikundi cha viongozi wabadhilifu. Hivyo basi tusidhoofishe madhara ya ufisadi kwa kulinganisha na kesi ya Ditto.
 
Ok.
Ikishapitia,what is next? Na kama ikipitia na kubatilisha itakuwaje.
Huoni kama itapitia maelezo ya upande mmoja,kwa kuwa hakuna maelezo ya watuhumiwa?

Ni vipi wasipelekwe moja kwa moja kwenye vyombo vyenye mamlaka ambako ndiko haki itapatikana?

Watakao onekana kweli wanatuhuma za kujibu watachukuliwa hatuwa zote za kisheria, unaweza kuwachukulia hatuwa watu wasio na makosa, kwani kuna watu walikuwa wanapewa orders na wakubwa na kwa uwoga wakukosa kazi walifuata tu amri ingawa hawakupendezwa nazo. Huo ndio ufisadi wa wenye ulevi wa madaraka, wao hutuma tu na kama hukufatisha unakiona cha mtema kuni. Hujawahi kusikia ile kauli ya kichaka 'You are either with us or against us' - by Bush November 6, 2001. Ulevi wa madaraka ni namna hiyo, hata kama hutaki unaogopa usiwe against na wakuu.
 
Haya wezentu na Dua la kuku, hamna cha hatua wala step ndio imetoka hiyo. Tunasubiri Ma X PM wawili wanyang'anye Uraisi 2015. Aluta.........
 
Back
Top Bottom