Hatua kwa hatua-Jinsi ya Kutengeneza website ya Biashara

tzhosts

JF-Expert Member
Nov 5, 2016
375
465
logo.gif


Habari za wakati huu;

Leo nataka nilete darasa fupi la jinsi ya kutengeneza website (Tovuti ) kwa ajili ya biashara yako kwa gharama nafuu kabisa.Nitaanza kwa kuelezea kidgo tovuti ni nini na kazi yake ni nini?

Tovuti ni nini?
Tovuti ni anuani ya mtandaoni.Ni sehemu katika mtandao ambamo unaweza kuweka taarifa zako ili ziwafikie watu wengi kwa urahisi.Tovuti ni zana ya kufanyia masoko na inaweza pia kuwa zana ya mauzo na zana ya kusimamia biashara yako.Katika zama hizi kumiliki tovuti ni muhimu sana katika kuendesha biashara .

Hatua zifuatazo zinahusika katika kuanzisha na kuendesha tovuti

1. Hatua ya kwanza ni kuchagua jina la tovuti(Domain name)


Katika hatu hii unachagua jina ambalo ni rahisi kukumbuka,linaakisii biashara yako.linavutia.Unaweza kuchagua jina linalokufaa kupitia link hii:
Domain Registration - Search and Buy Domain

2. Kuandaa maudhui ya tovuti(Content/Profile)

Maudhui yako yahusisha taarifa zote muhimu kuhusu biashara yako ili kumwezesha msomaji kuelewa kwa kina malengo,shughuli na uwezo wako kibiashara.Hapa unaweza kutafuta mtaalamu wa kuandika maudhui/copywriter ili akuandalie muadhui ya kuvutia wateja.

3. Kuandaa mpangilio wa maudhui(Layout/structure)

Mpangilio wa maudhui yako uwe rahisi kufikiwa na kusomwa na watu pamoja na robots za mtandaoni.Mpangilio uoneshe kwamba wewe ni serious business na unalenga kutoa huduma bora kwa wateja wako wote.Hapa unaweza kutafuta mtaalamu wa kutengeneza mwonekano wa tovuti yako au unaweza kutafuta mionekano(templates ) ambazo zinaweza kufanyiwa marekebisho.WordPress inakuwa na uwezo zaidi kwa sababu ya idadi kubwa ya watumiaji.

4. Kuweka maudhui yako mtandaoni(Hosting)

Tafuta hosting agent ambaye ana uzoefu,na anakupa thamani halisi ya pesa yako bila kuathiri ubora.Unaweza kupata packages za kuhost ambazo zinaendana na budget yako kupitia link hii.



5. Kusambaza maudhui yako mtandaoni

Hakikisha unatumia mbinu mbalimbali za kusambaza maudhui yako ikiwamo mitandao ya kijamii na search engines ili kuwafikia watu wengi Zaidi

6. Kufuatilia utendaji wa tovuti yako

Fuatilia utendaji wa tovuti yako kwa kuhakikisha kwamba unaangalia idadi ya watembeleaji,wanakotekea na matokeo unayopta ili kuhakikisha kwamba unakuwa na takwimu sahihi kuhusu tovuti yako.

Iwapo ungependa kufahamu zaidi kuhusu uanzishaji na uendeshaji wa tovuti tafadhali wasiliana nasi kwa email:info@tzhosts.com
 
Nilitegemea wewe ungekuwa na website ambayo ingekuwa kama ni portfolio yako
 
Karibuni Wateja mjipatie website ambazo ni fully optimized for SEO kwa gharama nafuu ya shilingi 99000 kwa mwaka all inclusive.Hii ni ofa maalum ya mwisho wa mwaka.
 
Karibuni Wateja mjipatie website ambazo ni fully optimized for SEO kwa gharama nafuu ya shilingi 99000 kwa mwaka all inclusive.Hii ni ofa maalum ya mwisho wa mwaka.
Mkuu niko na maswali mawili.
1.Hiyo 99000 ikilipwa inajumuisha na kodi zote za serikali/TCRA.
2.Kwa mfano mtu yuko nje ya nchi let say China/Dubai je akianzisha website itakuwa na domain ya Tanzania au ya nchi aliyopo?na kama jibu ni domain ya Tanzania je anaweza kuoperate hiyo website yenye domain ya Tanzania akiwa nje ya nchi,na kama jibu ni ndio hawezi kusumbuliwa na serikali ya nchi aliyopo?
Sheria za kimataifa za kumiliki website zinasemaje?
 
Mkuu niko na maswali mawili.
1.Hiyo 99000 ikilipwa inajumuisha na kodi zote za serikali/TCRA.
2.Kwa mfano mtu yuko nje ya nchi let say China/Dubai je akianzisha website itakuwa na domain ya Tanzania au ya nchi aliyopo?na kama jibu ni domain ya Tanzania je anaweza kuoperate hiyo website yenye domain ya Tanzania akiwa nje ya nchi,na kama jibu ni ndio hawezi kusumbuliwa na serikali ya nchi aliyopo?
Sheria za kimataifa za kumiliki website zinasemaje?
Sheria za kumiiliki website za kimataifa ni rahisi,Uwe na domain iliyosajiliwa na taarifa zako ziwe sahihi na uweke maudhui ambayo ni halali kwa mujibu wa sheria za kimataifa na kwa mujibu wa sheria za nchi husika.Ila kuwa na domain ya nchi husika ni lazima uwe na anuani katika nchi husika.Mfano domain ya .tz inahitaji uwe na anuani ndani ya Tanzania.

Kuhusu ofa yetu ya 99000 hii ni gharama ambayo utakuwa unalipa kila mwaka ambapo utapata website pamoja na emails 3.Hii no ofa maalum ya mwisho wa mwaka na vigezo na masharti yatazingatiwa.

Karibu
 
logo.gif


Je unahitaji kumiliki tovuti kwa ajili ya biashara yako?Jipatie simple business card website kwa ajili ya biashara yako.Wasiliana nasi kwa email:inf@tzhosts.com
 
Karibuni kwa wale ambao wanahitaji website ya haraka.Unajipatia website pamoja na domain name kwa bei ndogo kabisa ya Punguzo.Tuwasiliane leo.
 
Karibuni kwa wale ambao wanahitaji website ya haraka.Unajipatia website pamoja na domain name kwa bei ndogo kabisa ya Punguzo.Tuwasiliane leo.
 
Sheria za kumiiliki website za kimataifa ni rahisi,Uwe na domain iliyosajiliwa na taarifa zako ziwe sahihi na uweke maudhui ambayo ni halali kwa mujibu wa sheria za kimataifa na kwa mujibu wa sheria za nchi husika.Ila kuwa na domain ya nchi husika ni lazima uwe na anuani katika nchi husika.Mfano domain ya .tz inahitaji uwe na anuani ndani ya Tanzania.

Kuhusu ofa yetu ya 99000 hii ni gharama ambayo utakuwa unalipa kila mwaka ambapo utapata website pamoja na emails 3.Hii no ofa maalum ya mwisho wa mwaka na vigezo na masharti yatazingatiwa.

Karibu
Sawa asante.
Lakini pia nataka kujua nikishakulipa hiyo 99000 na kodi ya serikalini nalipa kiasi gani kila mwaka?
Au nikikulipa hiyo 99000 inajumuisha na kodi zote za serikali?

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom