Hatua gani stahiki za kuwakabili Panya Road?

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
May 13, 2018
439
742
Kwa siku za hivi karibuni kumeibuka kundi la vijana wadogo maarufu kama Panya Road wakijihusisha na uhalifu wa kuvunja nyumba za watu na kuiba vitu vya ndani kama radio, tv, pesa na vinginevyo. Aidha limekuwa likiwadhuru na kuwajeruhi watu kwa vitu vyenye ncha kali. Wakike kwa wakiume wamekumbana na kadhia hii.

Kundi limezua hofu na mashaka makubwa kwa raia wema hususani wanaorejea majumbani nyakati za usiku wakitoka makazini mwao pamoja na wale wanaokwenda makazini nyakati za mchana huku nyumba zikiwa hazina uzio wala walinzi.

Dar es Salaam kama mji wa kibiashara ni lazima suala la uhakika wa ulinzi na usalama likawa kipaumbele cha kwanza. Hili linawezekana kwa sisi raia au jamii kutoa ushirikiano wa kutosha kwa vyombo vya dola hususani jeshi la polisi kupitia kwa viongozi wa mitaa katika maeneo yetu, wajumbe/mabalozi na vikundi vya ulinzi shirikishi.

Ukitazama wahusika katika kundi hili la Panya Road ni vijana/watoto jambo linalotoa ujumbe mpana kuwa wazazi/walezi/viongozi wa dini/jamii hatukutimiza wajibu wetu wa malezi kwao kikamilifu. Vile vile ni kiashiria kuwa serikali inapaswa kujenga mazingira rafiki na wezeshi kwa makundi mbalimbali katika jamii yaweze kujitafutia kipato kwa njia halali kwa maana ya kurahisisha mazingira ya ufanyaji shughuli za kiuchumi.

Swali ni kuwa kundi hili lipo na linaendelea kufanya uhalifu kwenye jamii toka eneo moja kwenda jingine. Ikiashiria kusambaa kwake, Je jamii na jeshi la polisi tunashindwa kulidhibiti na kurejesha hali kuwa shwari?? Unashauri nini mwana jukwaa kama njia ya kusaidia mawazo ya kukabiliana na kundi hili baya kwa mustakabali wa usalama hapa Dar es Salaam!

Karibu sana.

#DarUsalamaKwanza #PanyaRoadSasaBasi
 
Kwanza kabisa ijulikane panya road hawajaanza leo, walikuwepo, wanakuja na kupoa, japo sijui kama ni walewale au huwa wanaibuka wapya.

Nini Kifanyike: Jeshi la Polisi lina kila dhana na uwezo wa kupambana na yeyote, litumie dhana hizo kuwasaka, kuwakamata na kuwapoteza, namaanisha kuwapoteza mazima, hawa madogo hawana ujuzi wowote ule wa kijasusi zaidi ya kuvuta bangi, so sioni kwanini iwe shida kwa vijana wa Sirro kuwapata hawa pabya road kirahisi mpaka wawe gumzo mitaani.
 
Huu ujinga unatoa wapi.

Mbona kipindi cha Magufuli tuliweza tokomeza sasa kwanini kipindi hiki cha udhaifu kama wa awamu ya nne warudi tena. Uzembe au ni planned tu. Watoto wanakuwa wahalifu chapa viboko, kill kama hawaeleweki
 
Panya road ni washirika wa polisi... ni kama machangudoa tu.
Haiwezekani polisi washindwe kuweka doria kuwazuia panya road... tena kundi la vibaka wanaotumia silaha za jadi.
Mbona hao hao polisi mchana barabarani wanahakikisha wanasimamisha magari mengi kadri wawezavyo?
Kwanini usiku wanalala na wakipewa taarifa za mtonyo hawatokei kwa wakati? Why?

Kwanini taarifa za maandamano ya CDM wanajizatiti kwa silaha, mavazi na magari ya kutisha??
Why washindwe kwa panya road? Kama si washirika wao na wamewashindwa waseme wananchi waanze kuwashughulikia hao panya road!!
 
Kwanza kabisa ijulikane panya road hawajaanza leo, walikuwepo, wanakuja na kupoa, japo sijui kama ni walewale au huwa wanaibuka wapya.
Nini Kifanyike: Jeshi la Polisi lina kila dhana na uwezo wa kupambana na yeyote, litumie dhana hizo kuwasaka, kuwakamata na kuwapoteza, namaanisha kuwapoteza mazima, hawa madogo hawana ujuzi wowote ule wa kijasusi zaidi ya kuvuta bangi, so sioni kwanini iwe shida kwa vijana wa Sirro kuwapata hawa pabya road kirahisi mpaka wawe gumzo mitaani.
Police hawako serious. Unashindws kumkamata mtu ambae amepora smart phone Karne hii ya 22. Kazi ambayo hata voda ukiwapa wana track simu na kukwambia mtu alipo.
 
..
SHOOT TO KILL ndiyo jawabu,na wala wasiuawe in the long range,kamata kwanza,peleka nyumbani kwao,funga kamba barazani kwao,ita wananchi washuhudie jinsi unavyouwa kwa risasi.
Kule NBO yule Reserve Police akiitwa Shaw aliwa kill hao panyaroad saana.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kwa siku za hivi karibuni kumeibuka kundi la vijana wadogo maarufu kama Panya Road wakijihusisha na uhalifu wa kuvunja nyumba za watu na kuiba vitu vya ndani kama radio, tv, pesa na vinginevyo. Aidha limekuwa likiwadhuru na kuwajeruhi watu kwa vitu vyenye ncha kali. Wakike kwa wakiume wamekumbana na kadhia hii.


Kundi limezua hofu na mashaka makubwa kwa raia wema hususani wanaorejea majumbani nyakati za usiku wakitoka makazini mwao pamoja na wale wanaokwenda makazini nyakati za mchana huku nyumba zikiwa hazina uzio wala walinzi.


Dar es Salaam kama mji wa kibiashara ni lazima suala la uhakika wa ulinzi na usalama likawa kipaumbele cha kwanza. Hili linawezekana kwa sisi raia au jamii kutoa ushirikiano wa kutosha kwa vyombo vya dola hususani jeshi la polisi kupitia kwa viongozi wa mitaa katika maeneo yetu, wajumbe/mabalozi na vikundi vya ulinzi shirikishi.


Ukitazama wahusika katika kundi hili la Panya Road ni vijana/watoto jambo linalotoa ujumbe mpana kuwa wazazi/walezi/viongozi wa dini/jamii hatukutimiza wajibu wetu wa malezi kwao kikamilifu. Vile vile ni kiashiria kuwa serikali inapaswa kujenga mazingira rafiki na wezeshi kwa makundi mbalimbali katika jamii yaweze kujitafutia kipato kwa njia halali kwa maana ya kurahisisha mazingira ya ufanyaji shughuli za kiuchumi.

Swali ni kuwa kundi hili lipo na linaendelea kufanya uhalifu kwenye jamii toka eneo moja kwenda jingine. Ikiashiria kusambaa kwake, Je jamii na jeshi la polisi tunashindwa kulidhibiti na kurejesha hali kuwa shwari?? Unashauri nini mwana jukwaa kama njia ya kusaidia mawazo ya kukabiliana na kundi hili baya kwa mustakabali wa usalama hapa Dar es Salaam!

Karibu sana.

#DarUsalamaKwanza #PanyaRoadSasaBasi
Wahukumiwe kabisa, askari wanaopelekwa ni kwenda kuwasaka na kutimiza hukumu tu, siyo kuwakamata.

Napedekeza hukumu yao hao na viongozi wao kuwa ni risasi tu.
 
Imarisha ulinzi shirikishi, kuwasaka wazazi wao na kuwapa onyo, kukamata viongozi wa panya na kuwapa mfano
 
Wakianza kuuliwa tu wazazi wao huwa wanawatoroshea mikoani ndivyo huwa wanafanya
 
Wahukumiwe kabisa, askari wanaopelekwa ni kwenda kuwasaka na kutimiza hukumu tu, siyo kuwakamata.

Napedekeza hukumu yao hao na viongozi wao kuwa ni risasi tu.
Lakini dada yetu... huoni endapo watakamatwa wakafinywaaaa watasaidia kutoa taarifa zaidi. Ikibidi hata kesi zao ziendeshwe kwenye mahakama za wazi ili kuruhusu watu kuhudhuria.
Nina interest ya kuwafahamu zaidi, wao ni nani, mtandao wao ukoje, mafundisho yao, maficho yao, n.k.
Usikute ni jeshi kamili lisilo rasmi
Wahukumiwe kabisa, askari wanaopelekwa ni kwenda kuwasaka na kutimiza hukumu tu, siyo kuwakamata.

Napedekeza hukumu yao hao na viongozi wao kuwa ni risasi tu.
 
Kwa siku za hivi karibuni kumeibuka kundi la vijana wadogo maarufu kama Panya Road wakijihusisha na uhalifu wa kuvunja nyumba za watu na kuiba vitu vya ndani kama radio, tv, pesa na vinginevyo. Aidha limekuwa likiwadhuru na kuwajeruhi watu kwa vitu vyenye ncha kali. Wakike kwa wakiume wamekumbana na kadhia hii.


Kundi limezua hofu na mashaka makubwa kwa raia wema hususani wanaorejea majumbani nyakati za usiku wakitoka makazini mwao pamoja na wale wanaokwenda makazini nyakati za mchana huku nyumba zikiwa hazina uzio wala walinzi.


Dar es Salaam kama mji wa kibiashara ni lazima suala la uhakika wa ulinzi na usalama likawa kipaumbele cha kwanza. Hili linawezekana kwa sisi raia au jamii kutoa ushirikiano wa kutosha kwa vyombo vya dola hususani jeshi la polisi kupitia kwa viongozi wa mitaa katika maeneo yetu, wajumbe/mabalozi na vikundi vya ulinzi shirikishi.


Ukitazama wahusika katika kundi hili la Panya Road ni vijana/watoto jambo linalotoa ujumbe mpana kuwa wazazi/walezi/viongozi wa dini/jamii hatukutimiza wajibu wetu wa malezi kwao kikamilifu. Vile vile ni kiashiria kuwa serikali inapaswa kujenga mazingira rafiki na wezeshi kwa makundi mbalimbali katika jamii yaweze kujitafutia kipato kwa njia halali kwa maana ya kurahisisha mazingira ya ufanyaji shughuli za kiuchumi.

Swali ni kuwa kundi hili lipo na linaendelea kufanya uhalifu kwenye jamii toka eneo moja kwenda jingine. Ikiashiria kusambaa kwake, Je jamii na jeshi la polisi tunashindwa kulidhibiti na kurejesha hali kuwa shwari?? Unashauri nini mwana jukwaa kama njia ya kusaidia mawazo ya kukabiliana na kundi hili baya kwa mustakabali wa usalama hapa Dar es Salaam!

Karibu sana.

#DarUsalamaKwanza #PanyaRoadSasaBasi
Kuwavizia na kuwaua tu, hakuna kuwaonea huruma hata kidogo
 
Huko nchi flani huu ujinga uliisha kitambo,huko naskia ukileta ujinga kama hao panya what ..wanakuwahisha mapema,hawacheki na kima.

Kuna kipindi nilikaa kidogo huko huwezi skia hata kelele ya mwizi.
Vijana wanajua,wakishikwa no case Wala nini ni moja kwa moja inabaki historia.
 
Back
Top Bottom