CITYBOY
Member
- Nov 1, 2010
- 42
- 0
Ndugu zangu watanzania uchaguzi umekwisha tunachongoja ni matokeo ya jumla ya urais.Nifuraha yangu kuona upinzani umeongezeka bungeni,kwani hii itasaidia kupunguza makubaliano ya miswada ambayo haina maslahi kwa taifa letu.Basi ndugu zangu tupunguze ushabiki wa kidini,kikabila,rangi na kikanda.Kwani hakika utengano ni udhaifu na umoja ni nguvu,basi na tuwe wamoja tujenge taifa letu hili changa.Siasa za mwaka huu zina harufu ya udini,hivyo kuifanya amani ya taifa kua mashakani.Watakao taka kuandamana na kuleta machafuko ni hiyari yao,ila kumbuka unaweza pata kilema au kupoteza maisha,aliyekuhamasisha tawari amekwisha kuwakimbia akiacha nchi inawaka moto.Dr.Slaa anapinga matokeo ni vema kwenda mahakamani kuliko kuingia barabarani hii ni hatari!