Mbonea
JF-Expert Member
- Jul 14, 2009
- 640
- 20
Friday October 09, 2009 10:56 AM BT
Hatimaye zawadi za mshindi wa shindano la Bongo Star Search siku ya jana ziliwekwa wazi na Chief Judge wakati akiongea na waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Habari Maelezo.
Hatimaye zawadi za mshindi wa shindano la Bongo Star Search siku ya jana ziliwekwa wazi na Chief Judge wakati akiongea na waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Habari Maelezo.
Akizitaja zawadi pamoja na tarehe na ukumbi zitakapofanyika fainali za mwaka huu, Chief Judge Madame Rita alisema mshindi wa Mwaka huu atajinyakulia jumla ya shilingi Milioni 25 (Tsh 25,000,000/-) wakati mshindi wa Pili ataondoka na Tsh 5,000,000/- na yule watatu ataondoka kibindoni na Tsh 3,000,000/- na Tsh 500, 000/- toka Shear Illusion na wa Nne ataondoka na Tsh 1,500,000/-, Wakati yule wa tano ataondoka na Tsh 1,000,000/-.
Madame Rita aliongeza zaidi ya kuwa kutakuwa na burudani pia toka kwa wasanii wakubwa hapa Bongo kama AY, Shaa, Baby Madaha, Feisal na Abubakary Mzuri.
"Kama nilivyowaambia tumeboresha zaidi zawadi za washindi na kila mwaka ndio zinazidi kukuwa, Asante kwa Sponsor's wetu wote kwa kuiwezesha Bongo Star Search mwaka huu" alisema Chief Judge.
Washiriki watakaopanda jukwaani kugombea kitita hicho ni Jackson George (Tanga), Peter Msechu (Kigoma), Pascal Cassian (Mwanza), Kelvin Mbati (Dar) na Beatrice William (Mwanza).
Chief Judge alitumia Fursa hiyo kuwashukuru Sponsor's wa BSS 2009 ambao ni Vodacom Tanzania, Kilimanjaro Premium Lager, Family Health na Kilimanjaro Drinking Water.
Zaidi ya Kuonekana Live kwenye Tv kwa mara ya kwanza kabisa katika historia ya shindano hilo litaonyeshwa LIVE kupitia kwenye tovuti yao hapa hapa Dar411.com
Kwa kujipatia tiketi yako mapema unatakiwa ufike kwenye vituo vifuatavyo, Maduka ya Shear Illusion, Steers (Samora), Zizzou Fashion, Manywele (Kinondoni) na Best Bite Namanga.
Hatimaye zawadi za mshindi wa shindano la Bongo Star Search siku ya jana ziliwekwa wazi na Chief Judge wakati akiongea na waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Habari Maelezo.
Hatimaye zawadi za mshindi wa shindano la Bongo Star Search siku ya jana ziliwekwa wazi na Chief Judge wakati akiongea na waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Habari Maelezo.
Akizitaja zawadi pamoja na tarehe na ukumbi zitakapofanyika fainali za mwaka huu, Chief Judge Madame Rita alisema mshindi wa Mwaka huu atajinyakulia jumla ya shilingi Milioni 25 (Tsh 25,000,000/-) wakati mshindi wa Pili ataondoka na Tsh 5,000,000/- na yule watatu ataondoka kibindoni na Tsh 3,000,000/- na Tsh 500, 000/- toka Shear Illusion na wa Nne ataondoka na Tsh 1,500,000/-, Wakati yule wa tano ataondoka na Tsh 1,000,000/-.
Madame Rita aliongeza zaidi ya kuwa kutakuwa na burudani pia toka kwa wasanii wakubwa hapa Bongo kama AY, Shaa, Baby Madaha, Feisal na Abubakary Mzuri.
"Kama nilivyowaambia tumeboresha zaidi zawadi za washindi na kila mwaka ndio zinazidi kukuwa, Asante kwa Sponsor's wetu wote kwa kuiwezesha Bongo Star Search mwaka huu" alisema Chief Judge.
Washiriki watakaopanda jukwaani kugombea kitita hicho ni Jackson George (Tanga), Peter Msechu (Kigoma), Pascal Cassian (Mwanza), Kelvin Mbati (Dar) na Beatrice William (Mwanza).
Chief Judge alitumia Fursa hiyo kuwashukuru Sponsor's wa BSS 2009 ambao ni Vodacom Tanzania, Kilimanjaro Premium Lager, Family Health na Kilimanjaro Drinking Water.
Zaidi ya Kuonekana Live kwenye Tv kwa mara ya kwanza kabisa katika historia ya shindano hilo litaonyeshwa LIVE kupitia kwenye tovuti yao hapa hapa Dar411.com
Kwa kujipatia tiketi yako mapema unatakiwa ufike kwenye vituo vifuatavyo, Maduka ya Shear Illusion, Steers (Samora), Zizzou Fashion, Manywele (Kinondoni) na Best Bite Namanga.