Elections 2010 Hatimaye Yule Mtoto wa Mkulima Kashaapishwa Kuwa Waziri Mkuu!

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Haya tena kile watanzania walichokua wanakisubiri kwa yule Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda AKA Mtoto wa Kilimo kwanza kashaapa kulitumikia taifa la watanzania kua waziri Mkuu kwa awamu ya pili ndani ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kule Ikulu ndogo ya Chamwino mjini Dodoma! Tumuachie tuone atawaletea nini watanzania wanaosubiri ile ahadi ya kuiona ile nnchi ya ASALI NA MAZIWA hususani kwa wale wenzetu wa kule vijijini! Nafuu yetu sisi tunaoishi mijini angalau tunajiita Misheni Town tunapata japo milo mitatu kwa siku! Nakutakia kazi njema muheshimiwa Mtoto wa Kilimo kwanza subiria hao wanaokuja nyuma yako ambao muheshimiwa Baba Riziwani atakuchagulia wakuchapie kazi nahisi watafuata unachotaka kuwafanyia watanzania!:thinking:
 
Back
Top Bottom