Ni miaka 12 sasa tangu tulipokutana kwa mara ya kwanza,baada ya urafiki wa miaka 3 nikaamua kumueleza hisia zangu,,akasema mambo ya mapenzi mpaka tumalize shule kwa sasa tuendelee kuwa marafiki tu, kwa sababu alikuwa kila kitu kwangu nilikubali alichokisema na urafiki ukaendelea,kwetu pakawa kwao na kwao pakawa kwetu kila aliyetujua hakuuamini urafiki wetu kuwa ni wa kawaida tu.Miaka ikapita hatimaye tukamaliza kidato cha 6 na hapo tukaanza rasmi mahusiano yetu.Nilikiwa mwanaume wa kwanza kwake,na hapo ndipo aliponikamata kabisa kwani ata pale nilipokuwa najipoza wakati naendelea kumsubiri huyu nikaachana napo,amebaki peke yake.Msichana wa kwanza kumpenda na natamani awe wa mwisho.
Baada ya miaka yote hiyo lile tatizo ambalo mwanzoni tuliliona la kawaida limekuwa kubwa.Dini inaenda kututenganisha,niliona ni rahisi kwangu kubadili dini sababu nimekuwa kwenye misingi ya dini yake kwa muda mrefu,(shule pia ilichangia kwani nimesoma boarding katika shule za dini tangu primary adi advance) lakini kila nikikumbuka mzee alivyotengwa na familia yake baada ya kubadili dini kisa bi mkubwa na huu ugomvi uliotokea siku ya kifo chake akili yangu inagoma kabisa.Sijui natokaje hapa..
Baada ya miaka yote hiyo lile tatizo ambalo mwanzoni tuliliona la kawaida limekuwa kubwa.Dini inaenda kututenganisha,niliona ni rahisi kwangu kubadili dini sababu nimekuwa kwenye misingi ya dini yake kwa muda mrefu,(shule pia ilichangia kwani nimesoma boarding katika shule za dini tangu primary adi advance) lakini kila nikikumbuka mzee alivyotengwa na familia yake baada ya kubadili dini kisa bi mkubwa na huu ugomvi uliotokea siku ya kifo chake akili yangu inagoma kabisa.Sijui natokaje hapa..