EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Hivi Uingereza ikisema itasimamisha misaada mpaka Tanzania itakapowafikisha watuhumiwa mahakamani, bado tutaleta nyodo kama zile kuukataa ushoga? Kwamba misaada yenu huko huko, lakini hafikishwi mtu mahakamani? Kwamba Uingereza kutulazimisha kuwafikishwa watuhumiwa mahakamani ni kinyume na utamaduni wetu?
Hoseah anasema "Kama Bunge la Uingereza linasema wafikishwe mahakamani na hukumu ilitolewa huko huko Uingereza, hapa kuna mkanganyiko." Lakini wakifikishwa mahakamani hapa na hukumu kutolewa hapa hapa kuna mkanganyiko? Kama Uingereza ikiamua kuwashtaki hao watuhumiwa kwenye mahakama zao, Tanzania iko radhi kuwa-extradite?
Hoseah anasema "Kama Bunge la Uingereza linasema wafikishwe mahakamani na hukumu ilitolewa huko huko Uingereza, hapa kuna mkanganyiko." Lakini wakifikishwa mahakamani hapa na hukumu kutolewa hapa hapa kuna mkanganyiko? Kama Uingereza ikiamua kuwashtaki hao watuhumiwa kwenye mahakama zao, Tanzania iko radhi kuwa-extradite?