Guus
JF-Expert Member
- Jul 16, 2013
- 1,131
- 823
Baada ya siku kadhaa za maandamano ya kutaka kuvunjwa kwa kilichokuwa Kikosi Maalumu cha Kuzuia Wizi (Special Anti-Robbery Squad maarufu kama SARS) nchini Nigeria, IGP wa Polisi jana Jumapili ametangaza rasmi kuvunjwa kwa kikosi hiko.
SARS, ambacho kilikuwa kitengo maalumu chini ya jeshi la polisi toka 1992, kwa muda mrefu kimekuwa kikilaumiwa kwa unyanyasaji, ukamataji pasipo kufuata sheria, utesaji na hata mauaji.
Maandamano ya sasa yakichagizwa na wasanii wakubwa wa muziki (kama anavyoonekana wizkid katika video), yalizuka baada ya video moja kusambaa ikiwaonesha askari wa SARS wakimpiga risasi hadi kumuua mwanamume mmoja katika jimbo la Delta ya Kusini.
SARS, ambacho kilikuwa kitengo maalumu chini ya jeshi la polisi toka 1992, kwa muda mrefu kimekuwa kikilaumiwa kwa unyanyasaji, ukamataji pasipo kufuata sheria, utesaji na hata mauaji.
Maandamano ya sasa yakichagizwa na wasanii wakubwa wa muziki (kama anavyoonekana wizkid katika video), yalizuka baada ya video moja kusambaa ikiwaonesha askari wa SARS wakimpiga risasi hadi kumuua mwanamume mmoja katika jimbo la Delta ya Kusini.