Hatimaye vyombo vya habari vya Magharibi vimeanza kuzungumia maabara ya virusi ya Fort Detrick ya Marekani

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,000
1,019
VCG111336684807 (1).jpg

Katika muda wa miezi michache iliyopita, ukitafuta maneno “Fort Detrick” kwa kutumia Google, hakuna chochote cha maana kilichoonekana, na hata baadhi ya watu katika nchi za magharibi, hasa Marekani kwenyewe wengi walikuwa hawajui kama Marekani ilikuwa na maabara ya virusi inayoitwa Fort Detrick, na kwamba maabara hiyo imeleta madhara makubwa kwa watu wengi, wanyama na hata mazingira.

Watu wenye akili wanajua kuwa kwenye dunia ya sasa ya uhuru wa habari kitu chochote kile, iwe ni kibaya au kizuri, kinaweza kupatikana kwenye mtandao wa internet. Kuna mambo mengi tu mabaya ya kutisha na haya kustahili kuwepo kwenye internet, lakini mambo hayo yapo. Kwa hiyo hali ya kutopatikana kwa habari yoyote kwenye internet kuhusu maabara ya Fort Detrick, ilifanya watu wenye akili watambue kuwa kuna jambo linafichwa kiasi kwamba hata mambo yanayohusu maabara hiyo yamefutwa au kuzuiwa kwenye internet.

Mwanzoni msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Zhao Lijian, mara kwa mara alionekana kuitaja maabara hiyo kila alipozungumzia suala la virusi vya Corona. Baadhi ya watu waliona kama ni mzushi, lakini sasa kile ambacho amekuwa akikisema kimeonekana kuwa na mantiki na kimeanza kuonekana kwenye vyombo vikubwa vya habari.

Wiki hii tovuti ya shirika la habari la Uingereza BBC, imeandika makala kuhusu maabara hiyo. Japo kuwa makala hiyo imejaa propaganda, lakini kuandikwa kwa habari hiyo ni hatua nzuri ya kufungua mjadala kuhusu hatari iliyoletwa na maabara hiyo kwa usalama wa afya ya binadamu. Mwandishi wa makala hiyo anaonekana kujua mambo mengi kuhusu makala hiyo, lakini ametumia maneno “historia yenye utata kuhusu maabara hiyo” bila kusema ni utata gani. Lakini kama nilivyosema mwanzo, wenye akili wakisoma hilo neno “utata” wanajua maana yake ni nini.

Ajabu ni kuwa makala hiyo pia imesema maabara hiyo ilikuwa inafanya utafiti kuhusu virusi vya Ebola na virusi vya ndui. Inashangaza kidogo kuona kuwa maabara iliyokuwepo tangu miaka ya 50, inatajwa kuwa ni maabara ya kutafiti virusi vilivyoibuka muda mrefu baada ya hapo na watu wengi mwaka 2014-2016 kwenye eneo la Afrika Magharibi. Na ugonjwa wa ndui uliotajwa kwenye makala hiyo pia ni ugonjwa ambao mwaka 1977 Shirika la Afya Duniani lilitangaza kuwa umetokomezwa.

Jambo linalotia moyo ni kuwa jambo hilo ambalo lilikuwa siri, sasa linaanza kujadiliwa na vyombo vikubwa vya habari ambayo vinaheshimika katika nchi za magharibi. Makala nyingine iliyoandikiwa na tovuti ya Politico ya Marekani, imeonekana kuvutia ufuatiliaji zaidi baada ya kueleza mambo ya kutisha yaliyofanywa kwenye maabara hiyo. Makala hiyo imesema kemikali za ajabu zilikuwa zikitengenezwa na kufanyiwa majaribio kwa wafungwa katika magereza ya Marekani, na nyingine hata kutumiwa na jeshi la Marekani kwenye uwanja wa vita, na kusababisha madhara makubwa ambayo hadi leo yanaendelea kutesa watu.

Makala hiyo imesema tafiti za ajabu kwenye maabara hiyo zilionekana kufanyiwa majaribio zaidi kwa wazungu maskini na wafungwa wenye asili ya Afrika, na barani Ulaya wafungwa walikuwa wakifanyiwa majaribio.

Kama makala ya tovuti ya politico ingetolewa kwenye tovuti ya China, basi habari hiyo ingepuuzwa au kutajwa kuwa ina malengo ya kisiasa. Jambo la kutia moyo kwa sasa ni kuwa mjadala umeanza kufuatiliwa polepole, na anachokitaja mara kwa mara msemaji wa wizara ya mambo ya nje kuwa kinatakiwa kupatiwa majibu, inaonekana kuwa ni kweli kinahitaji majibu.
 
Ni dhambi kuwa na maabara ya kutengeneza virusi? ni dhambi kuwa na maabara ya kutafiti virusi..?...
Ni dhambi kuwa na maabara za siri kwa ajili ya matumizi ya kijeshi na tafiti kwa ajili usalama binafsi wa Taifa husika..

Hivi USA asingekuwa na Atomic bomb na kumuadhibu Japan leo hii lingekuwepo Taifa la USA? Dunia mbaya sana hii, lazima uwe na plans za kutosha kujilinda na kulinda watu wako..Dunia imetoka mbali kihistoria ikiwa na kila aina ya marais vichaa na binadamu vichaa..
 
Si dhambi kuwa na maabara za kutengeneza virusi hatari ulimwenguni. Dhambi ni pale virusi hivyo vinapotumiwa kwa makusudi au kwa bahati mbaya na kuweza kuleta majanga yasiyomithilika, kama vile COVID-19 ambayo inaitesa Dunia kwa sasa.
 
Pengine watu wataamka na kuelewa kwamba most viruses ni 'man made' kwa malengo ya kibiashara na other poli-economic agendas, kuanzia HIV/AIDS, Ebola na Corona.

Bad enough ni kwamba, hata scientists wanatumika kwa kiasi kikubwa kutetea kwa hoja na false experiences za maabara kulinda the status quo.

Baadhi ya magonjwa hayo (related to virus) yanaweza tibika ama kukingwa kabisa (vaccinated) lakini itakuwa na faida gani sasa? .. biashara kubwa ipo kwenye kumdumisha mteja kwa madawa yasiyoisha mpaka kifo chake kuliko tiba ya moja kwa moja.

Kwa mantiki hiyo, panapoibuka njia mbadala ambayo inaweza kusaidia kukabiliana na magonjwa hayo, hupigwa vita na kukemewa maramoja! Hupondwa na kutokomezwa kabisa. Why? Simply, because you touch high table's meals.

Rejelea sakata la AMA (American Medical Association) mwaka 1959. Taasisi credible ya Afya ilivyopotosha watu juu ya madhara ya uvutaji wa sigara kwa kusema haina mahusiano na ugonjwa saratani! Kisa nini? Tobacco Industry waliwa-finance $ 18,000,000 USD.

Mungu si Athumani, Dr. MacDonald na Dr. Garland (ambao walikuwa mbele kuunga mkono uongo huo) wanakuja kufa kwa sigara! MacDonald anaunguza nyumba kwa sigara na Garland anakufa kwa saratani ya mapafu.

Watu wanabaini ukweli sasa. Lakini swali la kujiuliza, how much harm had already been done? Na je, ni mangapi yasiyo ya ukweli tumelishwa na the so-called 'Credible Organs' bado hatujayafahamu?

Rejelea visa vya Doctor Ernst T. Krebs, Dr. Burkitt na Dr. McCarrison kule India.

Shida hawa orthodox doctors ally much with these systems to generate income, knowingly or unknowingly.
 
Na haya yote yanatokea kwasababu mzungu anataka kua the dominant race. Ukisoma historia ya jinsi watu weusi walivyokua wanafanyiwa experiments na mzungu enzi za ukoloni utagundua kua this is nothing new. Mi naona utengenezaji wa virusi sio issue hapa ila the bigger picture is the urge of the white man to dominate the world. New world order is real.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom