Zimeanza zimeanza kuota
Senior Member
- Oct 1, 2018
- 129
- 86
wakuu ile sehemu ya jina unaandika jina lako au?
Ndio unaandika jina lako kama lilivyo kwenye M-PESA.Iko vizuri nimeitumia kufanya malipo Ebay na AlliExpress.wakuu ile sehemu ya jina unaandika jina lako au?
Na uzuri hawa jamaa hawana MAKATO kama ukilipa kwa njia nyingine.Ndio unaandika jina lako kama lilivyo kwenye M-PESA.Iko vizuri nimeitumia kufanya malipo Ebay na AlliExpress.
Unamanisha makato ya nini.Na uzuri hawa jamaa hawana MAKATO kama ukilipa kwa njia nyingine.
Mkuu una kwama wapi?Wakubwa mi nimejaribu kutumia kwenye alliexpress inazingua tu daah, sjui niconnect tu na equity
Me nimetumia hiyo ya Voda so naandika majina nayo tumia M-Pesa?Card yako ina jina gani? maana yake weka jina ambalo likitumika kusajiri hiyo Card, kama unaitwa Masau bwire jaza kama umeazima kwa jirani weka jina lake
ndio mkuu majina yako ya MpesaMe nimetumia iyoo ya voda ko naandika majina nayo tumia mpesa?
Mkuu naomba nisaidie kidogo katika manunuzi pale unapotakiwa kuonyesha njia ya kupokelea mzigo mbona inalimit tu post adress badala hata ya dhlYap, na mm ninanunua huko huko ebay ingawa delivery inachelewa sometimes.
Wakubwa mi nimejaribu kutumia kwenye alliexpress inazingua tu daah, sjui niconnect tu na equity
Ndugu ongeza pesa kwenye MasterCard yako unapo ambiwa bidhaa ni TZS 10000 usiwe weke hiyo 10000, weka hata 12000.Me nimetumia iyoo ya voda ko naandika majina nayo tumia mpesa?
Card holder linatumiwa jina gani?Pale kwenye menu kuna sehemu imeandikwa KADI YANGU, unaweza endeleza card vile vile unaweza kuisitisha.
Jina lako uliosajili m-pesa.Card holder linatumiwa jina gani?
Tatizo ni makato
BancABC kwa kushirikiana na MasterCard, wamezindua huduma mpya iitwayo M-Pesa-Mastercard ni ya kwanza na ya kipekee Tanzania itakayomuwezesha mteja wa M-Pesa kuweza kulipia huduma na bidhaa mitandaoni katika tovuti mbali mbali Duniani zinazopekea malipo kwa MasterCard. Kupata huduma hii ya Virtual Card piga *150*00# chagua lipa kwa M-Pesa, chagua M-Pesa MasterCard, kutengeneza kadi yako. Utapata Card Number, Expiration date pamoja na CVV Number ndani ya sekunde chache tu!
===
Kwa mtu yeyote aliyewahi kufanya manunuzi ya kitu chochote bila kuinuka kitini ama kutoka nyumbani kwake anaweza kuelezea urahisi na wepesi wa kufanya manunuzi mtandaoni, lakini hii imekuwa ni ndoto kwa Watanzania walio wengi, mpaka sasa ambapo Mastercard wameungana na Vodacom na BancABC kutengeneza kadi ya kwanza itakayowezesha manunuzi mtandaoni – M-Pesa Virtual Card.
“Huduma ya M-Pesa kutoka Vodacom ina wateja Zaidi ya milioni 8.2 huku ikiwa na Zaidi ya wakala laki moja waliotapakaa nchi nzima, hii inawezsha upatikanaji wa uhakika wa huduma za kifedha, lakini imekuwa ni ngumu pale linapokuja suala la kulipia manunuzi mtandaoni haswa kupitia tovuti za kimataifa. Uzinduzi na ufanyaji kazi wa Virtual Card kupitia M-Pesa utaleta mapinduzi katika kuwezesha Watanzania kufanya manunuzi mtandaoni na kuondosha vikwazo ikiwamo kuwa na akaunti ya benki na pia hatari ya mteja kuweka taarifa zake za kibenki mtandaoni,” alisema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Plc Hisham Hendi.
Inategemewa kwamba uunganisho wa intaneti kwa bara la Afrika itaongezeka sana ikiwa ni matokeo ya upatikanaji wa simu janja (Smartphone) na pia ukuaji wa utoaji huduma yenye kasi zaidi ya intaneti kutoka kwa watoa huduma kama Vodacom. Ongezeko hili la upatikanaji wa huduma ya intaneti litaongeza uhitaji wa maudhui ya kidijitali, mitandao ya kijamii, M-Commerce, elimu ya mtandaoni na pia malipo mtandaoni kurahisishwa na kuongezewa usalama zaidi.
Kadi hii itawawezesha wateja wa M-Pesa kufanya malipo ya aina yeyote kwa tovuti za kimataifa au za hapa nyumbani, ama kwa kutumia zana (App) yeyote ambayo inatumia na Mastercard kwa malipo, bila kuhitajika kuwa na akaunti ya benki au kadi ya mkopo (Credit Card). Wateja wanaweza kutengeneza virtual card kupitia menyu ya M-Pesa ama kupitia App yetu ya M-Pesa (huduma hii tutaiongeza hivi karibuni) na kuijaza pesa kupitia mfumo wetu wa M-Pesa. Kadi hii inakuwa tayari kwa matumizi mara tu baada ya kujazwa pesa.
Kaimu Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi (Kati), Raisi wa Kusini mwa Sahara wa Mastercard, Raghay Prasad (kushoto) na Mkuu wa hazina na kitengo cha soko la kimataifa wa Banki ABC, Barton Mwasamengo (kulia) wakionesha ushirikiano kati ya M-Pesa na Mastercard uliozinduliwa jana jijini Dar es Salaam.
Chanzo: Michuzi
duhhMakato makubwa mnoooo. Ukifanya malipo ya 1M unakatwa karibu lak 2
Sent using Jamii Forums mobile app