Hatimaye mwenge umeanza kutumika kubomoa upinzani nchini na kueneza chuki

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
Heshima kwenu wakuu,

Nimesikitika kusikia Mwenge umeanza kutumiwa katika kubomoa upinzani Tanzania, Je ndo malengo ya huu Mwenge?

Sisi zamani tulikaririshwa wimbo wa Mwenge ukakaa vichwani mwetu kama sara ya Baba yetu uliye mbinguni. “Sisi tunataka kuwasha Mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro. Umulike nje ya mipaka yetu. Ulete matumaini pale ambapo hakuna matumaini. Ulete upendo mahali ambapo pana chuki na ulete heshima mahali ambapo pamejaa dharau”.

Lakini leo hii mambo ni tofauti kabisa. Unatumika kutugawa, kueneza chuki na kuondoa matumaini. Je ni kweli Mwenge ni Tool ya CCM?

Leo nmeona John Heche akilalamika kwamba wanasiasa wametumia Mwenge kuwaambia wananchi wasimchague tena. Hapa ni ujumbe katumiwa.

21105966_1345272652238037_3514642346876662300_n (1).jpg


"Mh Mbunge Mwenge uko hapa Borega hawana sera, sera yao ni kukutukana wewe wanasema maendeleo haya sio wewe uliyeyafanya ni pesa ya serikali, wanasema usichaguliwe tena maana wewe unakamatwa kila siku, wanasema wewe ni kama jambazi wanakusema wewe tuu mpaka wananchi wachache waliopo wamepigia kelele bahati nzuri wengi ni wanafunzi wametolewa darasani, anaewaongoza kukutukana ni DC"

Nimepokea ujumbe huo kutoka kwa mwananchi.

Hii si sawa.
 
Leo nmeona John Heche akilalamika kwamba wanasiasa wametumia Mwenge kuwaambia wananchi wasimchague tena. Hapa ni ujumbe katumiwa.
Ila hao wanasiasa wakisema mwenge haufai hauna maana ni sawa
 
yule kijana muongoza mwenge amesikika akisema DC kamata weka ndani mbunge anayehamasisha wananchi kulima bangi jee huyo ni mwongoza mwenge wa kuleta matumaini siku zote nitamlaani Kikwete na Mkapa kwa kutulete magufuli mvunja umoja wa wa wananchi mbaguzi mkabila mkanda yaani sasa kinachotumika ni lugha za kufitinisha IGP unashangaa anaongea kupasuwa wa nanchi Raisi Mkuu wa mkoa hii nchi hatuko salama tusipo amka leo huko mbele giza
 
yule kijana muongoza mwenge amesikika akisema DC kamata weka ndani mbunge anayehamasisha wananchi kulima bangi jee huyo ni mwongoza mwenge wa kuleta matumaini siku zote nitamlaani Kikwete na Mkapa kwa kutulete magufuli mvunja umoja wa wa wananchi mbaguzi mkabila mkanda yaani sasa kinachotumika ni lugha za kufitinisha IGP unashangaa anaongea kupasuwa wa nanchi Raisi Mkuu wa mkoa hii nchi hatuko salama tusipo amka leo huko mbele giza
Ww ni mjinga totally unataka mhamasishaji wa kilimo cha bangi aendelee kudunda? Mpumbavu wewe!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Heshima kwenu wakuu,

Nimesikitika kusikia Mwenge umeanza kutumiwa katika kubomoa upinzani Tanzania, Je ndo malengo ya huu Mwenge?

Sisi zamani tulikaririshwa wimbo wa Mwenge ukakaa vichwani mwetu kama sara ya Baba yetu uliye mbinguni. “Sisi tunataka kuwasha Mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro. Umulike nje ya mipaka yetu. Ulete matumaini pale ambapo hakuna matumaini. Ulete upendo mahali ambapo pana chuki na ulete heshima mahali ambapo pamejaa dharau”.

Lakini leo hii mambo ni tofauti kabisa. Unatumika kutugawa, kueneza chuki na kuondoa matumaini. Je ni kweli Mwenge ni Tool ya CCM?

Leo nmeona John Heche akilalamika kwamba wanasiasa wametumia Mwenge kuwaambia wananchi wasimchague tena. Hapa ni ujumbe katumiwa.

View attachment 578375

"Mh Mbunge Mwenge uko hapa Borega hawana sera, sera yao ni kukutukana wewe wanasema maendeleo haya sio wewe uliyeyafanya ni pesa ya serikali, wanasema usichaguliwe tena maana wewe unakamatwa kila siku, wanasema wewe ni kama jambazi wanakusema wewe tuu mpaka wananchi wachache waliopo wamepigia kelele bahati nzuri wengi ni wanafunzi wametolewa darasani, anaewaongoza kukutukana ni DC"

Nimepokea ujumbe huo kutoka kwa mwananchi.

Hii si sawa.
Kumbe humu JF "Dubu " ndiye John Heche!!!
 
Nilibahatika kuushudia Mwenge mwaka huu, mkimbiza mwenge mkuu, moja kati ya ujumbe wake ni mshikamano, umoja wa kitaifa na uzalendo ktk nchi. Alisema, "mwenge si wa Ccm bali ni nembo ya taifa" vyama vyote vilishiriki huku. Kama si taarifa ya uongo basi imepokelewa vibaya ama kimakusudi kama ilivyo jadi imepotoshwa kimkakati. Kwanza mbunge alipaswa kuwepo uwanjani kwenye mkesha, hadi sasa mwenge bado nembo na ni tukio la kitaifa, ndo haya tuyapokeayo pasi na fikra chanya.

Ukija mwenge wa Olympic, hata South Africa wanapanda ndege kwenda kuushika, kombe la dunia, wanalipia wapige picha nalo, ni umasikini tu wa kufikiri uliotujaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza hicho kikorokoro cha nini mpaka leo?hakina faida zaidi ya kukuza ngono tu.
Miradi si huwa inazinduliwa na hao makada wanaowaita ma-CD.

Habeeb Marhan
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom