Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Hatimaye Mkapa aikana Kiwira
RAIS Mstaafu Benjamin Mkapa amevunja ukimya na kutoa kauli kuhusu tuhuma zinazomkabili za kununua mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, akisema: "Hayo ni maneno ya watu; wameyazusha kwa manufaa yao wenyewe.
Mkapa, ambaye amekuwa hajibu tuhuma za kashfa zinazomuandama na hasa ya umiliki wa mgodi huo, alitoa kauli hiyo jana mbele ya waandishi wa habari huku akisisitiza kauli aliyowahi kuitoa kuwa hana hisa katika mgodi huo na wala hajawahi kumiliki hisa kwenye mgodi huo ambao sasa upo mikononi mwa serikali.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa mada kuhusu uongozi bora kwa rika zote Afrika ambayo alishiriki kama mchangiaji, Mkapa alisema hajui kwa nini wala sababu za kuzushiwa hayo.
Mkapa alisema anashangaa na hajui sababu za yeye kuundiwa kashfa hiyo ambayo imekuwa gumzo miongoni mwa jamii hata ndani ya vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanania.
"Sijui kwa sababu gani... na mimi nashangaa. Hata nyinyi wana habari mmeandika sana hayo, lakini nasema sina share (hisa) katika mgodi wa Kiwira, alisema Mkapa.
Kama hiyo haitoshi rais huyo mstaafu aliyeongoza Tanzania kwa miaka 10, Mkapa aliwataka waandishi wa habari kujiridhisha zaidi kwa kwenda kusoma nyaraka za umiliki wa mgodi huo ingawa hakuweka wazi.
Mmeandika sana hayo, nasema sina share Kiwira, ninyi nendeni mkasome vizuri, alisema rais mstaafu Mkapa.
Hata hivyo Mkapa alihoji kuwa ikiwa kwenye mgodi huo kulikuwa na mradi wa kuzalisha umeme, uliishia wapi na kuwataka waandishi wa habari kuhoji hilo huku akisisitiza kuwa hana hisa katika mgodi huo
"Kama ule ulikuwa mradi wa kuzalisha umeme, cha kuuliza hapa uliishia wapi; ulizeni; mimi sina share yoyote Kiwira," alisema Mkapa
Kwa muda Mkapa amekuwa katika kashfa ya kuhusishwa na umiliki wa mgodi huo akishutumiwa kwa kujiuzia kwa bei ya kutupa chini ya thamani yake halisi akishirikiana na mkewe Mama Anna pamoja na aliyekuwa waziri katika serikali yake, Daniel Yona.
Sakata hilo la umiliki wa mgodi wa Kiwira lilisababisha baadhi ya wabunge, hasa wa kambi ya upinzani na baadhi wakiwa wa CCM, kudai mabadiliko ili kuwezesha Mkapa afikishwe mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro alilifikisha sakata hilo bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 2008, akidai kuwa kwa kushirikiana na mkewe, pamoja na Daniel Yona aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini mwaka 2004, walianzisha kampuni ya TanPower Resources Ltd na mwaka mmoja baadaye wakauziwa mgodi huo kwa kificho.
Kimaro alidai kuwa ingawa thamani ya mradi huo ilikuwa ni zaidi ya Sh4 bilioni, ilikubaliwa mgodi huo uuzwe kwa Tanpower Resources kwa Sh700 milioni, lakini hata ikalipwa Sh70 milioni tu.
Hata hivyo aliongeza akidai kuwa mwaka 2006 Mkapa, Anna na Yona, waliingia mkataba wa kufua umeme na Tanesco kwa makubaliano ya kulipwa Sh46milioni katika kila siku , pasipo kujali kama umeme umefuliwa ama la.
Chanzo: Mwananchi
RAIS Mstaafu Benjamin Mkapa amevunja ukimya na kutoa kauli kuhusu tuhuma zinazomkabili za kununua mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, akisema: "Hayo ni maneno ya watu; wameyazusha kwa manufaa yao wenyewe.
Mkapa, ambaye amekuwa hajibu tuhuma za kashfa zinazomuandama na hasa ya umiliki wa mgodi huo, alitoa kauli hiyo jana mbele ya waandishi wa habari huku akisisitiza kauli aliyowahi kuitoa kuwa hana hisa katika mgodi huo na wala hajawahi kumiliki hisa kwenye mgodi huo ambao sasa upo mikononi mwa serikali.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa mada kuhusu uongozi bora kwa rika zote Afrika ambayo alishiriki kama mchangiaji, Mkapa alisema hajui kwa nini wala sababu za kuzushiwa hayo.
Mkapa alisema anashangaa na hajui sababu za yeye kuundiwa kashfa hiyo ambayo imekuwa gumzo miongoni mwa jamii hata ndani ya vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanania.
"Sijui kwa sababu gani... na mimi nashangaa. Hata nyinyi wana habari mmeandika sana hayo, lakini nasema sina share (hisa) katika mgodi wa Kiwira, alisema Mkapa.
Kama hiyo haitoshi rais huyo mstaafu aliyeongoza Tanzania kwa miaka 10, Mkapa aliwataka waandishi wa habari kujiridhisha zaidi kwa kwenda kusoma nyaraka za umiliki wa mgodi huo ingawa hakuweka wazi.
Mmeandika sana hayo, nasema sina share Kiwira, ninyi nendeni mkasome vizuri, alisema rais mstaafu Mkapa.
Hata hivyo Mkapa alihoji kuwa ikiwa kwenye mgodi huo kulikuwa na mradi wa kuzalisha umeme, uliishia wapi na kuwataka waandishi wa habari kuhoji hilo huku akisisitiza kuwa hana hisa katika mgodi huo
"Kama ule ulikuwa mradi wa kuzalisha umeme, cha kuuliza hapa uliishia wapi; ulizeni; mimi sina share yoyote Kiwira," alisema Mkapa
Kwa muda Mkapa amekuwa katika kashfa ya kuhusishwa na umiliki wa mgodi huo akishutumiwa kwa kujiuzia kwa bei ya kutupa chini ya thamani yake halisi akishirikiana na mkewe Mama Anna pamoja na aliyekuwa waziri katika serikali yake, Daniel Yona.
Sakata hilo la umiliki wa mgodi wa Kiwira lilisababisha baadhi ya wabunge, hasa wa kambi ya upinzani na baadhi wakiwa wa CCM, kudai mabadiliko ili kuwezesha Mkapa afikishwe mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro alilifikisha sakata hilo bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 2008, akidai kuwa kwa kushirikiana na mkewe, pamoja na Daniel Yona aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini mwaka 2004, walianzisha kampuni ya TanPower Resources Ltd na mwaka mmoja baadaye wakauziwa mgodi huo kwa kificho.
Kimaro alidai kuwa ingawa thamani ya mradi huo ilikuwa ni zaidi ya Sh4 bilioni, ilikubaliwa mgodi huo uuzwe kwa Tanpower Resources kwa Sh700 milioni, lakini hata ikalipwa Sh70 milioni tu.
Hata hivyo aliongeza akidai kuwa mwaka 2006 Mkapa, Anna na Yona, waliingia mkataba wa kufua umeme na Tanesco kwa makubaliano ya kulipwa Sh46milioni katika kila siku , pasipo kujali kama umeme umefuliwa ama la.
Chanzo: Mwananchi