Hatimaye mfumo wa Iron Dome kuwekwa katika eneo la Ghuba. Mzizi wa fitina kukatwa?

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
May 27, 2016
5,416
7,828
Habari!

Marekani iko mbioni kuutumia mfumo wa ulinzi wa anga wa "Iron Dome" kwenye vituo vya kijeshi katika nchi kadhaa za Ghuba kwa mara ya kwanza. Marekani ilinunua mfumo wa Iron Dome kutoka Israel baada ya makubaliano kati ya nchi hizo mnamo mwaka 2019.

Kulingana na ripoti na vyanzo ndani ya Israel, Israel imethibitisha kuiruhusu Marekani kuweka mfumo wa Iron Dome kwenye vituo vyake vya kijeshi katika nchi kadhaa za Ghuba, maeneo mengine ya bara la Asia pamoja na barani Ulaya.

Hili linafuatia baada ya Israel kutia saini makubaliano ya uhusiano na Falme za Kiarabu na Bahrain mnamo Septemba 2020. Hata hivyo, kambi gani haswa zitakazowekwa mfumo wa Iron Dome katika nchi za Ghuba bado hazijawekwa wazi. Kuhusiana na hili, tuendelee kuvuta subira, tutapata kufahamu panapo muda muafaka.

Itafahamika kuwa, Iron Dome ni mfumo wa ulinzi wa anga ulioundwa na kampuni ya Israel ya Rafael (Rafael Advanced Defense Systems) na kujumuishwa kwenye jeshi la Israel tangu mwaka 2011. Mfumo huu umekuwa ukitumika kwa ajili ya ulinzi dhidi ya roketi na makombora ya masafa mafupi.

Kama tuna kumbukumbu, basi tutakumbuka matukio kadhaa ya mashambulizi ya makombora ambayo yamekuwa yakiathiri eneo la Ghuba hususani nchi ya Saudi Arabia, hali iliyopelekea kuanzishwa kwa mpango mahususi wa kukabiliana ama kuyathibiti mashambulizi haya.

Pia, haya yanajiri baada ya uwepo wa ripoti mbalimbali za kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi kwa mifumo ya ulinzi wa anga ambayo imekuwa ikitumika hususani ule wa Patriot hasa pale unapojaribu kukabiliana ama kuzilenga shabaha zenye kusafiri katika kimo cha chini ama kwa lugha nyingine, low-flying targets.

Mfumo wa Iron Dome unatajwa kuonesha uwezo mkubwa dhidi ya hatari hizi, mfumo unaotazamiwa kuukata huu "mzizi wa fitina" ambao umekuwa ukiiathiri Saudi Arabia na maeneo mengine ya Ghuba kwa ujumla.

Mchakato umeanza. Lakini, tutarajie kitu gani baada ya kusambazwa kwa mfumo huu wa Iron Dome katika eneo hilo?

Huu ni muendelezo wa yale ambayo tumekuwa tukiyajadili. Pia, waweza pitia hapa:
 
Unaweza kuweka zulia dunia nzima ili mguu wako usikanyage ardhi, au unaweza kuvaa viatu tu ukafikia lengo lile lile.

Hiyo Iron Dome ya Israel yenyewe wanasema efficiency yake ni 85% -90%.

Kwa hiyo bado shughuli ipo tu.

Ukizingatia maadui kila siku wanakuja na mbinu mpya, mara wametumia ndege kuangusha majengo, mara wameweka sumu kwenye maji, mara wamelipua mabomu mjini.

Ni teknolojia nzuri, ila sijui kama inaweza kuwa cost effective.
 
Unaweza kuweka zulia dunia nzima ili mguu wako usikanyage ardhi, au unaweza kuvaa viatu tu ukafikia lengo lile lile.

Hiyo Iron Dome ya Israel yenyewe wanasema efficiency yake ni 85% -90%.

Kwa hiyo bado shughuli ipo tu.

Ukizingatia maadui kila siku wanakuja na mbinu mpya, mara wametumia ndege kuangusha majengo, mara wameweka sumu kwenye maji, mara wamelipua mabomu mjini.

Ni teknolojia nzuri, ila sijui kama inaweza kuwa cost effective.
Mashambulizi ni timing tu, hasa kwa vita vya dunia ya sasa.. atae muwahi mwenzake ya jicho na kuchapa lapa ndio mshindi
 
Watahangaika sana na hiyo mifumo ya ulinzi lakini wenzao washahama huko siku nyingi. Wachina kwa sasa wamejikita kwenye Bioweapons zinazoweza kushambulia kundi au aina fulani tu ya watu.

So, ipo siku hizo iron dome wataziona ni makopo tu.
 
Watahangaika sana na hiyo mifumo ya ulinzi lakini wenzao washahama huko siku nyingi. Wachina kwa sasa wamejikita kwenye Bioweapons zinazoweza kushambulia kundi au aina fulani tu ya watu.

So, ipo siku hizo iron dome wataziona ni makopo tu.
Ur speculations will never prove right.Kamwe haitakaa itokee
 
Unamaanisha nini kamwe haitakaa itokee?

Kwamba the use of biological weapons is an impossibility?
I mean ugunduzi wa biological weapons hautaondoa ulazima wa kuwepo mifumo ya ulinzi wa anga like iron dome na mingine mingi.Bado itahitajika sana tofauti na jamaa alivyodai
 
Habari yako haipo clear sana.

Hio dome italinda kambi ya USA au italinda Nchi za waarabu?
 
I mean ugunduzi wa biological weapons hautaondoa ulazima wa kuwepo mifumo ya ulinzi wa anga like iron dome na mingine mingi.Bado itahitajika sana tofauti na jamaa alivyodai
Sawa, but the Iron Dome should not be touted as some kind of armor of invincibility. It is not.

Mike Tyson famously said "Everybody has a plan, until they get punched in the face". Attacks mostly come from unexpected sources. Like 9/11. The so called "Fifth Risk" that you can't even think of today.

The best of these systems have an efficiency rate of 85 to 90%, what about the rest? That last 10% to 15%?

Most of the actors that can be stopped by these systems can be engaged diplomatically and stopped at a fractionnof the cost of keeping these systems.

What about terrorism and biological weapons?

The best and most cost effective defence is diplomacy and engagement.

If you prioritize technology, you will be surprised how vulnerable you can get.

A healthy dose of humility goes a long way.
 
Sawa, but the Iron Dome should not be touted as some kind of armor of invincibility. It is not.

Mike Tyson famously said "Everybody has a plan, until they get punched in the face". Attacks mostly come from unexpected sources. Like 9/11. The so called "Fifth Risk" that you can't even think of today.

The best of these systems have an efficiency rate of 85 to 90%, what about the rest? That last 10% to 15%?

Most of the actors that can be stopped by these systems can be engaged diplomatically and stopped at a fractionnof the cost of keeping these systems.

What about terrorism and biological weapons?

The best and most cost effective defence is diplomacy and engagement.

If you prioritize technology, you will be surprised how vulnerable you can get.

A healthy dose of humility goes a long way.
Ni kwel chief nakuunga mkono kwenye mengi uloyasema .Hasa kwenye ishu ya diplomacy na engagement.U r absolutelly right.
But let us come back to iron dome perfomance specs.Do u really understands when we talk about efficiency of 90%. i assume u r aware that there is no machine of 100% efficiency/perfect machine.
So about this 10% inefficiency,do u think it is soo obvious to be taken advantage by attackers? It is unknown.. so it is not practical kwa maadui to sit and design the offensive weapons basing on the 10% inefficiency of their target.And yet even the rockets are not 100% efficient.

Ku critisize efficiency ya 80-90% ni ku dependon chances kitu ambacho si sawa
 
Tunaelewa iron dome uwezo wake ni kuzuia viberiti vya wanamgambo wa hamas tu... Tena haiwezi kuvizuia kwa 100%
 
Unaweza kuweka zulia dunia nzima ili mguu wako usikanyage ardhi, au unaweza kuvaa viatu tu ukafikia lengo lile lile.

Hiyo Iron Dome ya Israel yenyewe wanasema efficiency yake ni 85% -90%.

Kwa hiyo bado shughuli ipo tu.

Ukizingatia maadui kila siku wanakuja na mbinu mpya, mara wametumia ndege kuangusha majengo, mara wameweka sumu kwenye maji, mara wamelipua mabomu mjini.

Ni teknolojia nzuri, ila sijui kama inaweza kuwa cost effective.
Ni kweli, adui hutafuta mbinu mpya za kufanya mashambulizi kwa ufanisi. Ndio maana pia hata katika upande wa kujilinda napo mbinu mpya zinaibuliwa mara kwa mara ili kukidhi mahitaji.

Leo hii makombora ya adui yanashambuliwa kwa makombora lakini tayari kuna majaribio ya mbinu mpya ikiwemo kutumia mifumo ya laser kuzuia makombora na hatari nyinginezo. Changamoto ni nyingi lakini mambo yanakwenda sambamba pande zote.
 
Watahangaika sana na hiyo mifumo ya ulinzi lakini wenzao washahama huko siku nyingi. Wachina kwa sasa wamejikita kwenye Bioweapons zinazoweza kushambulia kundi au aina fulani tu ya watu.

So, ipo siku hizo iron dome wataziona ni makopo tu.
Ndugu, una habari kuwa bioweapons zimekuwepo even before common era? Watu waliuana kwa makundi kwa kuwekeana sumu tangu enzi ya Roman Empire.

Hizi missile defense systems unazoziona na kuzisikia leo zimekuja juzi juzi tu, karne ya 20. Bado ni teknolojia mpya sana!
 
Habari yako haipo clear sana.

Hio dome italinda kambi ya USA au italinda Nchi za waarabu?
Mfumo ulionunuliwa na Marekani utalinda kambi za Marekani zilizopo katika nchi za Ghuba (nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi).

Mifumo itakayolinda nchi za Ghuba chini ya udhibiti wa nchi hizo itatokana na mikataba kati ya Israel na nchi hizo ambapo mpaka sasa tayari kuna taarifa za uwepo wa mataifa kadhaa ya Ghuba yaliyokwisha kuonesha nia ya kuununua mfumo huo.
 
Back
Top Bottom