Hatimaye lile ludude la Iran laenda Syria kweli licha ya maneno ya khanga ya Washington

S V Surovikin

JF-Expert Member
Aug 8, 2015
13,563
32,529
Meli ya mafuta ya Iran iliyo katika mgogoro wa kimataifa imeonekana karibu na pwani ya Syria , kulingana na picha za Setlaiti.
Meli hiyo ya MV Adrian Darya 1/Grace 1ilikamatwa na Gibraltar mwezi Julai kupitia usaidizi wa vikosi vya Uingereza kutokana na hofu kwamba ilikuwa ikielekea Syria , hatua inayokiuka vikwazo vya Muungano wa Ulaya.
Iliachiliwa huru baada ya hakikisho kutolewa kwamba haitaelekea katika taifa hilo lenye vita vya wenyewe kwa wenyewe. Lakini picha zilizotolewa siku ya Jumamosi ziliionyesha meli hiyo ikiwa maili mbili kando ya pwani ya Syria.
Picha hizo kutoka kwa kampuni ya Marekani ya Marx Technology , ziliionyesha meli hiyo ikiwa karibu na bandari ya Syria ya Tartus mnamo tarehe sita Septemba.
Mshauri wa maswala ya usalama nchini Marekani John Bolton alituma ujumbe wa Twitter akisema kwamba mtu yeyote aliyekana kwamba meli hiyo ilikuwa ikielekea Syria alikuwa hataki kukubali tu.
''Tehran inafikiria ni muhimu kuufadhili utawala wa mauaji wa Assad badala ya kuwasaidia watu wake'' , alisema. Mbali na picha nyengine . Tunaweza kuzungumza , lakini Iran haitaondolewa vikwazo vyake hadi pale itakapowacha uongo na kusambaza ugaidi!
Hatahivyo hakuna thibitisho kwamba meli hiyo inapakua mzigo wake wa mapipa milioni 2.1 ya mafuta. Kufikia sasa Iran na Syria hazijatoa tamko lolote.

Jinsi ilivyozua mgogoro wa kimataifa

Meli hiyo iliokuwa ikiitwa Grace 1 wakati ilipozuiliwa na utawala wa Gibraltar mwezi Julai imesababisha mgogoro mkubwa wa kidiplomasia kati ya Washington na Tehran.
Wanamaji wa Uingereza walikuwa wameisaidia utawala wa Gibraltar kuikamata meli hiyo , swala lililoiingiza Uingereza katika mgogoro huo.
Marekani nayo iliwasilisha ombi rasmi la kuizuia meli hiyo mnamo mwezi Agosti lakini mahakama za Gibraltar zilipinga ombi hilo.
Marekani mwaka uliopita ilijiondoa katika mpango wa kinyuklia wa Iran ulioafikiwa mwaka 2015 na kuiwekea vikwazo nchi hiyo .
Marekani ilijaribu kumhonga nahodha wa meli ya mafuta ya Iran
Ikijibu , Iran ilianza kukiuka baadhi ya masharti iliowekewa katika makubaliano hayo.
Muungano wa Ulaya ulitaka kuokoa makubaliano hayo lakini meli hiyo ya mafuta ilikamatwa kwa kuwa ilikuwa ikituhumiwa kuelekea Syria, hatua ambayo ingekiuka mashari ya Muungano wa Ulaya.
Utawala wa Gibraltar uliiwachilia meli hiyo tarehe 15 Agosti baada ya kupokea hakikisho kutoka kwa Iran kwamba haitapeleka mzigo wake Syria.
Kwa nini Marekani inataka kuikamata?
Marekani imekuwa ikitaka kuikamata meli hiyo tangu ilipoachiliwa na Gibraltar, Ilitoa kibali cha kuikamata na kuipiga marufuku meli hiyo , huku ikitishia kuiwekea vikwazo nchi yoyote itakayoisaidia meli hiyo katika bahari ya mediterean.
Mapema wiki hii ilibainika kwamba afisa mmoja wa Marekani alimtumia ombi la kumpatia nahodha wa chombo hicho mamilioni ya madola ili kubadili njia na kuipeleka meli hiyo mahala ambapo Marekani inaweza kuikamata.
Meli ya Uingereza ilikamatwa na Iran mwezi Julai katika kile kilichoonekana kama kulipiza kisasi katika jukumu la Uingereza kusaidia kukamatwa kwa meli hiyo swala ambalo Tehran imekana.
Meli hiyo ya Stena Impero ilikuwa ikipita katika mkondo wa Hormuz wakati ilipokamatwa .
Bado imesalia katika bandari ya Iran ya Bandar Abbas.
Screenshot_2019-09-07-18-27-40.jpeg
 
Jamaa wabishi kweli
Meli ya mafuta ya Iran iliyo katika mgogoro wa kimataifa imeonekana karibu na pwani ya Syria , kulingana na picha za Setlaiti.
Meli hiyo ya MV Adrian Darya 1/Grace 1ilikamatwa na Gibraltar mwezi Julai kupitia usaidizi wa vikosi vya Uingereza kutokana na hofu kwamba ilikuwa ikielekea Syria , hatua inayokiuka vikwazo vya Muungano wa Ulaya.
Iliachiliwa huru baada ya hakikisho kutolewa kwamba haitaelekea katika taifa hilo lenye vita vya wenyewe kwa wenyewe. Lakini picha zilizotolewa siku ya Jumamosi ziliionyesha meli hiyo ikiwa maili mbili kando ya pwani ya Syria.
Picha hizo kutoka kwa kampuni ya Marekani ya Marx Technology , ziliionyesha meli hiyo ikiwa karibu na bandari ya Syria ya Tartus mnamo tarehe sita Septemba.
Mshauri wa maswala ya usalama nchini Marekani John Bolton alituma ujumbe wa Twitter akisema kwamba mtu yeyote aliyekana kwamba meli hiyo ilikuwa ikielekea Syria alikuwa hataki kukubali tu.
''Tehran inafikiria ni muhimu kuufadhili utawala wa mauaji wa Assad badala ya kuwasaidia watu wake'' , alisema. Mbali na picha nyengine . Tunaweza kuzungumza , lakini Iran haitaondolewa vikwazo vyake hadi pale itakapowacha uongo na kusambaza ugaidi!
Hatahivyo hakuna thibitisho kwamba meli hiyo inapakua mzigo wake wa mapipa milioni 2.1 ya mafuta. Kufikia sasa Iran na Syria hazijatoa tamko lolote.

Jinsi ilivyozua mgogoro wa kimataifa

Meli hiyo iliokuwa ikiitwa Grace 1 wakati ilipozuiliwa na utawala wa Gibraltar mwezi Julai imesababisha mgogoro mkubwa wa kidiplomasia kati ya Washington na Tehran.
Wanamaji wa Uingereza walikuwa wameisaidia utawala wa Gibraltar kuikamata meli hiyo , swala lililoiingiza Uingereza katika mgogoro huo.
Marekani nayo iliwasilisha ombi rasmi la kuizuia meli hiyo mnamo mwezi Agosti lakini mahakama za Gibraltar zilipinga ombi hilo.
Marekani mwaka uliopita ilijiondoa katika mpango wa kinyuklia wa Iran ulioafikiwa mwaka 2015 na kuiwekea vikwazo nchi hiyo .
Marekani ilijaribu kumhonga nahodha wa meli ya mafuta ya Iran
Ikijibu , Iran ilianza kukiuka baadhi ya masharti iliowekewa katika makubaliano hayo.
Muungano wa Ulaya ulitaka kuokoa makubaliano hayo lakini meli hiyo ya mafuta ilikamatwa kwa kuwa ilikuwa ikituhumiwa kuelekea Syria, hatua ambayo ingekiuka mashari ya Muungano wa Ulaya.
Utawala wa Gibraltar uliiwachilia meli hiyo tarehe 15 Agosti baada ya kupokea hakikisho kutoka kwa Iran kwamba haitapeleka mzigo wake Syria.
Kwa nini Marekani inataka kuikamata?
Marekani imekuwa ikitaka kuikamata meli hiyo tangu ilipoachiliwa na Gibraltar, Ilitoa kibali cha kuikamata na kuipiga marufuku meli hiyo , huku ikitishia kuiwekea vikwazo nchi yoyote itakayoisaidia meli hiyo katika bahari ya mediterean.
Mapema wiki hii ilibainika kwamba afisa mmoja wa Marekani alimtumia ombi la kumpatia nahodha wa chombo hicho mamilioni ya madola ili kubadili njia na kuipeleka meli hiyo mahala ambapo Marekani inaweza kuikamata.
Meli ya Uingereza ilikamatwa na Iran mwezi Julai katika kile kilichoonekana kama kulipiza kisasi katika jukumu la Uingereza kusaidia kukamatwa kwa meli hiyo swala ambalo Tehran imekana.
Meli hiyo ya Stena Impero ilikuwa ikipita katika mkondo wa Hormuz wakati ilipokamatwa .
Bado imesalia katika bandari ya Iran ya Bandar Abbas.View attachment 1200883
 
Meli ya mafuta ya Iran iliyo katika mgogoro wa kimataifa imeonekana karibu na pwani ya Syria , kulingana na picha za Setlaiti.
Meli hiyo ya MV Adrian Darya 1/Grace 1ilikamatwa na Gibraltar mwezi Julai kupitia usaidizi wa vikosi vya Uingereza kutokana na hofu kwamba ilikuwa ikielekea Syria , hatua inayokiuka vikwazo vya Muungano wa Ulaya.
Iliachiliwa huru baada ya hakikisho kutolewa kwamba haitaelekea katika taifa hilo lenye vita vya wenyewe kwa wenyewe. Lakini picha zilizotolewa siku ya Jumamosi ziliionyesha meli hiyo ikiwa maili mbili kando ya pwani ya Syria.
Picha hizo kutoka kwa kampuni ya Marekani ya Marx Technology , ziliionyesha meli hiyo ikiwa karibu na bandari ya Syria ya Tartus mnamo tarehe sita Septemba.
Mshauri wa maswala ya usalama nchini Marekani John Bolton alituma ujumbe wa Twitter akisema kwamba mtu yeyote aliyekana kwamba meli hiyo ilikuwa ikielekea Syria alikuwa hataki kukubali tu.
''Tehran inafikiria ni muhimu kuufadhili utawala wa mauaji wa Assad badala ya kuwasaidia watu wake'' , alisema. Mbali na picha nyengine . Tunaweza kuzungumza , lakini Iran haitaondolewa vikwazo vyake hadi pale itakapowacha uongo na kusambaza ugaidi!
Hatahivyo hakuna thibitisho kwamba meli hiyo inapakua mzigo wake wa mapipa milioni 2.1 ya mafuta. Kufikia sasa Iran na Syria hazijatoa tamko lolote.

Jinsi ilivyozua mgogoro wa kimataifa

Meli hiyo iliokuwa ikiitwa Grace 1 wakati ilipozuiliwa na utawala wa Gibraltar mwezi Julai imesababisha mgogoro mkubwa wa kidiplomasia kati ya Washington na Tehran.
Wanamaji wa Uingereza walikuwa wameisaidia utawala wa Gibraltar kuikamata meli hiyo , swala lililoiingiza Uingereza katika mgogoro huo.
Marekani nayo iliwasilisha ombi rasmi la kuizuia meli hiyo mnamo mwezi Agosti lakini mahakama za Gibraltar zilipinga ombi hilo.
Marekani mwaka uliopita ilijiondoa katika mpango wa kinyuklia wa Iran ulioafikiwa mwaka 2015 na kuiwekea vikwazo nchi hiyo .
Marekani ilijaribu kumhonga nahodha wa meli ya mafuta ya Iran
Ikijibu , Iran ilianza kukiuka baadhi ya masharti iliowekewa katika makubaliano hayo.
Muungano wa Ulaya ulitaka kuokoa makubaliano hayo lakini meli hiyo ya mafuta ilikamatwa kwa kuwa ilikuwa ikituhumiwa kuelekea Syria, hatua ambayo ingekiuka mashari ya Muungano wa Ulaya.
Utawala wa Gibraltar uliiwachilia meli hiyo tarehe 15 Agosti baada ya kupokea hakikisho kutoka kwa Iran kwamba haitapeleka mzigo wake Syria.
Kwa nini Marekani inataka kuikamata?
Marekani imekuwa ikitaka kuikamata meli hiyo tangu ilipoachiliwa na Gibraltar, Ilitoa kibali cha kuikamata na kuipiga marufuku meli hiyo , huku ikitishia kuiwekea vikwazo nchi yoyote itakayoisaidia meli hiyo katika bahari ya mediterean.
Mapema wiki hii ilibainika kwamba afisa mmoja wa Marekani alimtumia ombi la kumpatia nahodha wa chombo hicho mamilioni ya madola ili kubadili njia na kuipeleka meli hiyo mahala ambapo Marekani inaweza kuikamata.
Meli ya Uingereza ilikamatwa na Iran mwezi Julai katika kile kilichoonekana kama kulipiza kisasi katika jukumu la Uingereza kusaidia kukamatwa kwa meli hiyo swala ambalo Tehran imekana.
Meli hiyo ya Stena Impero ilikuwa ikipita katika mkondo wa Hormuz wakati ilipokamatwa .
Bado imesalia katika bandari ya Iran ya Bandar Abbas.View attachment 1200883
Nikipata uhakika wa ilipo ntatoa neno
 
Hii meli ina majina mawili itakuwa ina usajili pacha.

Mmiliki wa awali aliisajili baadae ilipokodiwa yote (Bare boat charter) ikasajiliwa tena na mtu aliyekodisha kwa usajili wa Uingereza.
 
Kama inaenda kuua watu kwa nini hawatumi tomahawk moja tu kuisambaratisha wakiwapa crew dakika 20 tu za kujiokoa.
 
Kama inaenda kuua watu kwa nini hawatumi tomahawk moja tu kuisambaratisha wakiwapa crew dakika 20 tu za kujiokoa.
Hii meli si ya serikali ila imesajiliwa na inapeperusha bendera ya Iran. Katika usajili wa meli hii kitu ambayo Iran anatete na kuilinda meli hii ni kama sehemu ya nchi yake.

Hii ni closed registry ambapo nchi iliyokusajilia meli lazima iwe na genuine link na hiyo meli au uhusiano wa karibu.

Hivyo hakuna mtu atayethubutu kulipua hii meli (Merchant ship) labda ingekuwa meli ya kijeshi (Navy ship).
 
Nimekuwa naifuatilia sana tu,marekani walifika kutoa dau dola milioni 15 kwa kapteni wa hiyo meli ili aipeleke sehemu ambayo marekani wataikamata,
baada ya juhudi kushindikana wakaanza kumtisha huyo kapteni kuwa watamwekea vikwazo,
kapteni akaomba kuacha kazi hiyo majuzi,alikuwa mhindi kwasasa meli ina kapten mpya wa iran ,ambae ndo atairudisha meli homeport,

kwasasa tanker lipo mile 2 toka bandari ya Tartus,syria,

vyanzo vya iran vinadai imeshashusha mzigo,

vyanzo vingine vinadai bado haijashusha mzigo kwa hiyo naangalia hizi siku mbili tatu kitaeleweka tu,ila kwa ufupi meli kwasasa iko eneo salama
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom