GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,542
- 108,847
Huku akiongea kwa ' Kufoka ' kama kawaida yake na akitawaliwa na ' Hasira ' zake za Kimachame aliyewahi kuwa Msemaji wa Klabu ya Omba Omba Bakuli FC ( Yanga ) na sasa akiwa ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mheshimiwa akizungumza TBC Taifa kupitia Mtangazaji wake Jesse John ameamua Kuvunja ukimya na ' Kutapika ' nyongo dhidi ya Klabu yake hiyo, Viongozi wake, Kocha wake na Msemaji wake.
Akiwa pia amekubali mwenyewe kuvalia Jezi ya Mnyama Mnyamani ( Timu ya Mwenyezi Mungu na iliyobarikiwa nae ) ya Simba SC huku akiitama ikicheza Kandanda safi kabisa na Kuifunga Timu ya African Lyon katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta leo Mheshimiwa Jerry Muro aliamua kusema haya maneno yake ambayp nitayanukuu hapa moja kwa moja bila kuongeza wala kupunguza chochote kile.
Nukuu # 1. " Tusidanganyane Yanga hakuna Viongozi sasa bali kuna Wajanja Wajanja tupu na kamwe tusitegemee makubwa kutoka Kwao "
Nukuu # 2. " Yanga haina Kocha bali ina Mhamasishaji tu na Mtu ambaye amewashika akili Watu wachache kwa Kujifanya anachangia Pesa zake huku akiwa hakuna chochote anachokifundisha na amekuwa ni Msemaji zaidi zaidi ya Mwalimu "
Nukuu # 3. " Mimi Jerry Muro ndiye niliweza kuleta Hamasa kwa Mashabiki na Wapenzi wa Yanga hadi wakawa na mwamko na Timu yao lakini cha Kushangaza huyu Msemaji wa sasa niliyedhani kuwa ataweza kuvaa vizuri Viatu vyangu naona vimempwaya kabisa na anafanya Yanga inyanyasike mno na Msemaji wa Simba Kaka yangu Haji Manara "
Nukuu # 4. " Mimi ni Yanga tena lialia kama siyo kindakindaki kabisa ila sitaki kuwa Mnafiki na ukweli ni kwamba Simba wako vizuri, wamesajili Kiufundi kabisa na watafanya vyema kabisa kwani wanajua nina wanachokifanya kwakuwa wana Watu makini "
Nukuu # 5. " Yanga ina mengi sana ya Kuiga na Kujifunza kutoka kwa Simba na hili wala tusijifiche au tusijifanye hatuoni. Wenzetu wameshatutangulia na kupiga hatua za Kimaendeleo na Sisi tunabaki tu kutembeza Bakuli kila Siku hii ni aibu "
Nukuu # 6. " Kwa aina ya Kikosi kile cha Simba kilichosheheni Mafundi watupu ni Mjinga na Mpumbavu tu pekee ndiyo angejua kuwa mechi ya juzi Yanga tusingefungwa na kuna uwezekano Wachezaji wa Simba walituonea huruma kwani walikuwa na uwezo hata wa Kutupiga / Kutufunga Goli 5 na zaidi ila waliamua Kutusitiri tu Watani zao tusiumbuke "
Nukuu # 7. " Mashabiki wa Yanga nao hawaeleweki kwani wanaenda Uwanjani kwa ' Kubipu ' tofauti na wenzao wa Simba ambao kiukweli nawasifu mno kwakuwa wamekuwa bega kwa bega na Timu yao na wanaishangilia muda wote tofauti na Wetu ambao huwa kimya utadhani ni Wakiwa "
Hongera sana na mno Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro kwa kuamua ' Kunyoosha ' maelezo yako hivi. Wenye akili na wanaojua mpira wamekusikia. Binafsi huwa napenda sana Watu wawazi na wakweli kama hivi Wewe na wenye tabia hii kama yako ya ' Kunyoosha ' maelezo bila Kupepesa macho, Kutikisa masikio na Kumung'unya maneno tupo wachache hapa duniani.
Nawasilisha.
Akiwa pia amekubali mwenyewe kuvalia Jezi ya Mnyama Mnyamani ( Timu ya Mwenyezi Mungu na iliyobarikiwa nae ) ya Simba SC huku akiitama ikicheza Kandanda safi kabisa na Kuifunga Timu ya African Lyon katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta leo Mheshimiwa Jerry Muro aliamua kusema haya maneno yake ambayp nitayanukuu hapa moja kwa moja bila kuongeza wala kupunguza chochote kile.
Nukuu # 1. " Tusidanganyane Yanga hakuna Viongozi sasa bali kuna Wajanja Wajanja tupu na kamwe tusitegemee makubwa kutoka Kwao "
Nukuu # 2. " Yanga haina Kocha bali ina Mhamasishaji tu na Mtu ambaye amewashika akili Watu wachache kwa Kujifanya anachangia Pesa zake huku akiwa hakuna chochote anachokifundisha na amekuwa ni Msemaji zaidi zaidi ya Mwalimu "
Nukuu # 3. " Mimi Jerry Muro ndiye niliweza kuleta Hamasa kwa Mashabiki na Wapenzi wa Yanga hadi wakawa na mwamko na Timu yao lakini cha Kushangaza huyu Msemaji wa sasa niliyedhani kuwa ataweza kuvaa vizuri Viatu vyangu naona vimempwaya kabisa na anafanya Yanga inyanyasike mno na Msemaji wa Simba Kaka yangu Haji Manara "
Nukuu # 4. " Mimi ni Yanga tena lialia kama siyo kindakindaki kabisa ila sitaki kuwa Mnafiki na ukweli ni kwamba Simba wako vizuri, wamesajili Kiufundi kabisa na watafanya vyema kabisa kwani wanajua nina wanachokifanya kwakuwa wana Watu makini "
Nukuu # 5. " Yanga ina mengi sana ya Kuiga na Kujifunza kutoka kwa Simba na hili wala tusijifiche au tusijifanye hatuoni. Wenzetu wameshatutangulia na kupiga hatua za Kimaendeleo na Sisi tunabaki tu kutembeza Bakuli kila Siku hii ni aibu "
Nukuu # 6. " Kwa aina ya Kikosi kile cha Simba kilichosheheni Mafundi watupu ni Mjinga na Mpumbavu tu pekee ndiyo angejua kuwa mechi ya juzi Yanga tusingefungwa na kuna uwezekano Wachezaji wa Simba walituonea huruma kwani walikuwa na uwezo hata wa Kutupiga / Kutufunga Goli 5 na zaidi ila waliamua Kutusitiri tu Watani zao tusiumbuke "
Nukuu # 7. " Mashabiki wa Yanga nao hawaeleweki kwani wanaenda Uwanjani kwa ' Kubipu ' tofauti na wenzao wa Simba ambao kiukweli nawasifu mno kwakuwa wamekuwa bega kwa bega na Timu yao na wanaishangilia muda wote tofauti na Wetu ambao huwa kimya utadhani ni Wakiwa "
Hongera sana na mno Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro kwa kuamua ' Kunyoosha ' maelezo yako hivi. Wenye akili na wanaojua mpira wamekusikia. Binafsi huwa napenda sana Watu wawazi na wakweli kama hivi Wewe na wenye tabia hii kama yako ya ' Kunyoosha ' maelezo bila Kupepesa macho, Kutikisa masikio na Kumung'unya maneno tupo wachache hapa duniani.
Nawasilisha.