Mbunge Tundu A.M.Lissu amesema kuwa dereva wake waliyekuwa wrote siku ya shambulio dhidi yake Septemba 7 mwaka 2017 huko nchini Ubelgiji.
Lissu ameyasema hayo jana alipokuwa akihojiwa na Mwandishi Mwamoyo Hamza wa Sauti ya Amerika almaarufu VoA. Studioni alikuwepo pia Balozi wa Tanzania nchini Marekani Ndugu Wilson Masilingi.
Kauli ya Lissu juu ya alipo dereva wake inamaliza fununu na ramli kuhusu alipo dereva huyo. Kwakuwa imeshajulikana alipo,ni muda muafaka kwa wahusika kusuka utaratibu wa kwenda kumhoji dereva Hugo na Lissu mwenyewe atakayekuwapo Ubelgiji tarehe 20 mwezi huu.
Hakujawahi HATA SIKU MOJA kuwepo utata kuhusu alipo dereva wa Lissu. Inafahamika siku zote kuwa yuko na Lissu. Kinachoshangaza ni kwa nini watu wazima na heshima zao na vyeo wanaamua kudanganya? Ikumbukwe alipokuwa Nairobi chama kupitia mwenyekiti aliuambia ulimwengu kuwa dereva alilazimika kupelekwa hospitalini Nairobi atibiwe kisaikologia baada ya tukio la shambulizi. Baada ya miezi yote pale Nairobi ikatangazwa kuwa Lissu amepata rufaa kwenda kutibiwa Ubeljiji. Wakati ule dereva hakutajwa. Baada ya wadadisi kuhoji alipo dereva Lissu akajitutumua na kudai dereva atasoma cheti, yaani certificate, halafu diploma na baadaye shahada yaani degree huko Ubeljiji. Yaani system ya elimu Ubeljiji ni sawa na Tanzania? Kwa nini wadanganye kuhusu sababu za dereva kuwa nje ya nchi??? Na ikumbukwe kuwa Lissu amewahi kutamka kuwa dereva wake hatahojiwa bila yeye kuwepo kama wakili wake!!!! Kama yote haya hayaibui maswali sijui ni kituko kipi kitakachoibua maswali. Lissu akiyatafakari haya anaogopa kurudi. Kubalini au kataeni. Lissu anaogopa kurudi kwa sababu mashtaka atakayofunguliwa dereva yatamjumlisha na yeye japo mwishoni aliumia sana mno.