KadaMpinzani
JF-Expert Member
- Jan 31, 2007
- 3,715
- 86
Wafadhili wagoma kuipa serikali mabilioni
Na Hassan Mghenyi
BAADHI ya wafadhili walioahidi kutunisha bajeti ya serikali mwaka uliopita, wameshindwa kutimiza ahadi zao na hivyo kukwamisha miradi mingi ya maendeleo.
Taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliyotolewa Juni mwaka huu, inaonyesha kuwa misaada ya wahisani na mikopo nafuu ambayo haijalipwa katika kipindi cha bajeti ya 2006/07 inafikia asilimia 35.
Katika kipindi hicho, bajeti hiyo ya serkali ilitegemea wafadhili kwa asilimia 39. Jumla ya fedha kutoka nje iliyolipwa ni Sh939.7 bilioni kati ya Sh1.439 trilioni zilizoahidiwa.
Katika kipindi hicho, kiasi cha mikopo yenye thamani ya Sh673.8 bilioni kiliidhishwa na wafadhili, na sehemu ya fedha hizo zilitumika kupunguza pengo la bajeti na sehemu iliyobakia ilitumika kulipa deni la ndani.
Wakati hali ikiwa hivyo, serikali katika mwaka huu wa fedha imeongeza utegemezi wa fedha za wafadhili katika bajeti yake kutoka asilimia 39 hadi asilimia 42.
Vile vile serikali imeongeza utegemezi wa fedha za nje katika miradi ya maendeleo kutoka Sh1.092 trilioni mwaka jana hadi Sh1.462 trilioni mwaka 2007/08, sawa na ongezeko la asilimia 33.9.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, deni la taifa limeongezeka hadi dola za Marekani 6,112.4 milioni kufika Mei mwaka huu kutoka dola 6,041.6 milioni Aprili mwaka huu na sababu zinazoelezwa ni kutokana na shughuli za serikali na kupungua kwa thamani ya shilingi.
Kati ya deni hilo, asilimia 75.9 ni la nje na silimia 24.1 ni deni la ndani. Hadi kufika Mei mwaka huu deni la nje liliongezeka hadi kufikia dola za Marekani 4,636.3 milioni kutoka dola 4,597.2 milioni mwezi uliotangulia, ambalo ni ongezeko la asilimia 39.1.
Ripoti hiyo inaeleza kuwa watumiaji wakubwa wa fedha kutoka nje ni serikali kuu ambayo imetumia dola za Marekani 2,684.3 milioni sawa na asilimia 78.1, sekta binafsi dola 583.2 milioini (asilimia17) na mashirika ya umma dola 167.6 milioni (asilimia 4.9)
Mchanganuo wa ripoti hiyo unaonyesha kuwa deni la ndani nalo limeongezeka hadi kufikia Sh1.857 trilioni mwishoni mwa Mei mwaka huu kutoka Sh1.846 trilioni Aprili 2007 na sababu inayoelelzwa hapo ni amana za serikali ambazo ni asilimia 99.1.
Wadai wakubwa wa deni la ndani ni benki za biashara asilimia 43.2, mifuko ya pensheni asilimia 28 na Benki Kuu asilimia 19.2.
Kuhusu matumizi ya serikali ambayo yamekuwa yakiisumbua serikali kwa muda mrefu, yalifikia Sh3.796 trilioni kwa mwaka wa fedha 2006/07, wakati makusanyo ya kodi za ndani na fedha kutoka nje zilifikia Sh3.377 trilioni hadi Mei 2007, na kusababisha upungufu wa Sh419.7 bilioni.
Katika bajeti yake ya 2006/07, serikali ilikuwa imepanga kutumia jumla ya Sh4.85 trilioni ambapo makusanyo ya kodi za ndani yakiwa Sh2.46 trilioni na fedha kutoka nje Sh2.226 trilioni.
Serikali katika mwaka wake wa fedha mpya (2007/08) inategemea kutumia jumla ya Sh6.067 trilioni, kati yake makusanyo ya kodi za ndani ni Sh3.502 trilioni na fedha za nje ni Sh2.549 trilioni.
Serikali imetenga kutumia Sh3.866 trilioni kwa matumizi ya kawaida na matumizi ya miradi ya maendeleo ni Sh2.201 ambapo kati ya hizo fedha ya nje ni Sh1.462 trilioni.
source: http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=361
maoni yangu binafsi ni kwamba mie naona afadhali sana tena sana kabisa serikali yetu kunyimwa pesa kama mambo yenyewe yataendelea kuwa hivi, wee fikiria mtu kila mwaka anafikiria kukarabati ofisi yake, nyumba yake na mapati kila leo, mambo haya wapi na wapi jamani ? sasa kilichobaki nadhani ni serikali kuanza kupata hasira na inachotakiwa kufanya ni kuisafisha serikali nzima ikiwa pamoja na viongozi wake.
Na Hassan Mghenyi
BAADHI ya wafadhili walioahidi kutunisha bajeti ya serikali mwaka uliopita, wameshindwa kutimiza ahadi zao na hivyo kukwamisha miradi mingi ya maendeleo.
Taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliyotolewa Juni mwaka huu, inaonyesha kuwa misaada ya wahisani na mikopo nafuu ambayo haijalipwa katika kipindi cha bajeti ya 2006/07 inafikia asilimia 35.
Katika kipindi hicho, bajeti hiyo ya serkali ilitegemea wafadhili kwa asilimia 39. Jumla ya fedha kutoka nje iliyolipwa ni Sh939.7 bilioni kati ya Sh1.439 trilioni zilizoahidiwa.
Katika kipindi hicho, kiasi cha mikopo yenye thamani ya Sh673.8 bilioni kiliidhishwa na wafadhili, na sehemu ya fedha hizo zilitumika kupunguza pengo la bajeti na sehemu iliyobakia ilitumika kulipa deni la ndani.
Wakati hali ikiwa hivyo, serikali katika mwaka huu wa fedha imeongeza utegemezi wa fedha za wafadhili katika bajeti yake kutoka asilimia 39 hadi asilimia 42.
Vile vile serikali imeongeza utegemezi wa fedha za nje katika miradi ya maendeleo kutoka Sh1.092 trilioni mwaka jana hadi Sh1.462 trilioni mwaka 2007/08, sawa na ongezeko la asilimia 33.9.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, deni la taifa limeongezeka hadi dola za Marekani 6,112.4 milioni kufika Mei mwaka huu kutoka dola 6,041.6 milioni Aprili mwaka huu na sababu zinazoelezwa ni kutokana na shughuli za serikali na kupungua kwa thamani ya shilingi.
Kati ya deni hilo, asilimia 75.9 ni la nje na silimia 24.1 ni deni la ndani. Hadi kufika Mei mwaka huu deni la nje liliongezeka hadi kufikia dola za Marekani 4,636.3 milioni kutoka dola 4,597.2 milioni mwezi uliotangulia, ambalo ni ongezeko la asilimia 39.1.
Ripoti hiyo inaeleza kuwa watumiaji wakubwa wa fedha kutoka nje ni serikali kuu ambayo imetumia dola za Marekani 2,684.3 milioni sawa na asilimia 78.1, sekta binafsi dola 583.2 milioini (asilimia17) na mashirika ya umma dola 167.6 milioni (asilimia 4.9)
Mchanganuo wa ripoti hiyo unaonyesha kuwa deni la ndani nalo limeongezeka hadi kufikia Sh1.857 trilioni mwishoni mwa Mei mwaka huu kutoka Sh1.846 trilioni Aprili 2007 na sababu inayoelelzwa hapo ni amana za serikali ambazo ni asilimia 99.1.
Wadai wakubwa wa deni la ndani ni benki za biashara asilimia 43.2, mifuko ya pensheni asilimia 28 na Benki Kuu asilimia 19.2.
Kuhusu matumizi ya serikali ambayo yamekuwa yakiisumbua serikali kwa muda mrefu, yalifikia Sh3.796 trilioni kwa mwaka wa fedha 2006/07, wakati makusanyo ya kodi za ndani na fedha kutoka nje zilifikia Sh3.377 trilioni hadi Mei 2007, na kusababisha upungufu wa Sh419.7 bilioni.
Katika bajeti yake ya 2006/07, serikali ilikuwa imepanga kutumia jumla ya Sh4.85 trilioni ambapo makusanyo ya kodi za ndani yakiwa Sh2.46 trilioni na fedha kutoka nje Sh2.226 trilioni.
Serikali katika mwaka wake wa fedha mpya (2007/08) inategemea kutumia jumla ya Sh6.067 trilioni, kati yake makusanyo ya kodi za ndani ni Sh3.502 trilioni na fedha za nje ni Sh2.549 trilioni.
Serikali imetenga kutumia Sh3.866 trilioni kwa matumizi ya kawaida na matumizi ya miradi ya maendeleo ni Sh2.201 ambapo kati ya hizo fedha ya nje ni Sh1.462 trilioni.
source: http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=361
maoni yangu binafsi ni kwamba mie naona afadhali sana tena sana kabisa serikali yetu kunyimwa pesa kama mambo yenyewe yataendelea kuwa hivi, wee fikiria mtu kila mwaka anafikiria kukarabati ofisi yake, nyumba yake na mapati kila leo, mambo haya wapi na wapi jamani ? sasa kilichobaki nadhani ni serikali kuanza kupata hasira na inachotakiwa kufanya ni kuisafisha serikali nzima ikiwa pamoja na viongozi wake.