Hatimaye CCM yatimiza ahadi; Bajaji za Wagonjwa zapokelewa rasmi

Hivi hii pikipiki itamkingaje mgonjwa katika hali ya mvua,vumbi,tope na baridi?.

Mimi nadhani hizo pikipiki ni kwa ajili ya kubeba
maiti na si wamama wajawazito vijijini.
 
Hii kitu imenidisturb sana kusema ukweli.

Hii gari ni $3,400, $2,000 chini ya hizo mochuari on wheels!! Huu ni upuuzi wa hali ya juu!!

--a6908eac39.jpg


Hii ambulance ni $6,500 just $600 more.

19705a7n2f.jpg

19705a7n2e.jpg

19705a7n2c.jpg


Mitsubishi DELICA SPACE GEAR CHAMONIX 4WD - Japan Partner

1990 NISSAN CARAVAN AMBULANCE Japanese used cars on sale , Import from Japan at Autorec Enterprise,LTD

Ila watz kwa kulalamika Mungu atusaidie....Juzi hapa tuko tunapiga kelele ooh tunanunuaje vitu second hand sheria ya manunuzi haijafuatwa, leo Srikali imejitahidi angalau kutimiza promise iliyotoa ooooh kwanini hawakununua second hand Ambulance Japan......Kesho watanunua hizo second hands tutalia tena ooh kwanini wao Vx sisi second hand and the list goes.....

Jamani saa nyingine tutoe angalau kapongezi hata ka unafiki ili tuondoe bias ya kulia lia...

Hongera Mheshimwa Rais Jakaya Kikwete kwa kutimiza ahadi hii moja tunaomba utukumbuke na sisi kule BK meli yetu Victoria inaweza kufanya kama MV BK so tukumbuke na sisi huku kanda ya ziwa na ahadi yetu ya meli mpya...Mungu akubariki.
 
Subili tu muone. Utasikia wabunge wa CCM wakisema wapizani ni kupinga kila kitu. Hata piki piki hizi nzuri hivi wanapinga tu! Watazipamba kupitia vyombo vyote vya habari na zitauzika mawazoni mwa watu. Hivyo ndivyo tulivyo Wa=TZN. Nasema hivyo kwa sababu kama watu-hakina mama vijijini wanashukuru mwaka mzima kupewa kanga na t-shirt za CCM itakuwaje pikipiki!

Ukweli tuna kazi ya kuwaelimisha watanzania wajue kuwa wanadanganywa. Piki piki hizi zitadumu muda gani. Mgojwa aliye maututi anawezaje kupelekwa hivyo na kupitia barabara gani/zipi. Je mvua na jua!
 
Hii thread nimeiona toka jana nilasema nisipoteze muda nikaamua nisiisome kwani nilijua ni jokes, tena nililaumu sana aliyeipost, sasa leo naisoma sitaki kuamini nachokisoma my God!
Mimi nafikiri kunampambo umesukwa strategical kumuharibia.
Kuna thread moja ya mbunge mmoja Deo Filkunjombe wa Ludewa ikiwa yeye ameweza kununua ambulance mpya moja kwa jimbo lake serikali inashindwa nini kununua ha 50 kwa awamu kama siyo ulimbukeni
 
Ahadi za Kikwete (CCM)
1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora
2. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini
3. Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria-Igunga
4. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga
5. Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma
6. Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini
7. Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma
8. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera
9. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi-Kagera
10. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba-Bukoba Mjini
11. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
12. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera
13. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera
14. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu-Kagera
15. Hukumu kwa waliopatikana na hatia ya kuua albino- Mbeya
16. Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba-Kagera
17. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
18. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika-Mwanza
19. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza
20. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita
21. Kulinda Muungano kwa nguvu zote-Pemba
22. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro
23. Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa-Mbeya mjini
24. Kujenga bandari Kasanga –Rukwa
25. Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
26. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya
27. Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga
28. Kununua "bajaji" 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa
29. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani –Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi -Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro
30. Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini
31. Kuboresha barabara za Igunga -Tabora
32. Kusambaza walimu 16,000 katika shule za Sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu
33. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini
34. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)-Hydom Manyara
35. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa- Musoma
36. Kulinda haki za walemavu- Makete
37. Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini
38. Kujenga barabara Musoma–Mto wa Mbu Arusha-Arusha
39. Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
40. Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma– Kaliua,Tabora
41. Kukarabati barabara ya Arusha Moshi-Arusha Mjini
42. Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa mpaka Singida-Dodoma
43. Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido 45.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
44. Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha –Arusha mjini
45. Kukopesha wavuvi zana za kilimo-Busekera, Wilaya ya Musoma, .
46. Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido
47. Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
48. Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara
49. Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini
50. Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa
51. Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa
52. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania-Iringa
53. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda
54. Kutokomeza malaria 2015-Bunda, Mkoa wa Mara
55. Kuwapa wanawake nafasi zaidi-Kilolo, Iringa
56. ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar
57. Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa-Kabandamaiti mjini Zanzibar
58. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti
59. Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay-Ruvuma
60. Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbamba-bay Ruvuma
61. kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) –Ruvuma
62. Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania –Ruvuma
63. Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
64. Mtwara kuwa mji wa Viwanda –Mtwara
65. Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu-Kibaha
66. Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa-Kibaha
67. Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda -Kibaha

Ahadi namba 28 aliyoitoa iringa imeenza kutekelezwa, hebu tutizame na hizo nyingine utekelezaji wake ukoje?
 
Hizi pikipiki kwa kiingereza wanaziita motorcycle ambulances, nyingi zinatengenezwa na kampuni ya South Africa inayoitwa eRanger (eRanger: Home). Zimekuwa zikitumika kwenye nchi mbali mbali Afrika zikiwemo Sudan, Uganda, Ethipoia na Malawi.

VIDEO YA PIKIPIKI HII IKIFANYA KAZI (LOCATION: ETHIOPIA)



Ushauri wangu:
Pamoja na kuwa hizi pikipiki zitasaidia baadhi ya wagonjwa ambao, UMUHIMU WA AMBULANCE unabaki pale pale. Hizi pikipiki zisifanywe kuwa replcement ya Ambulance.
 
Last edited by a moderator:
Ahadi za Kikwete (CCM)
1.Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora
2.Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini
3.Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria-Igunga
4.Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga
5.Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma
6.Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini
7.Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma
8.Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera
9.Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi-Kagera
10.Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba-Bukoba Mjini
11.Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
12.Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera
13.Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera
14.Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu-Kagera
15.Hukumu kwa waliopatikana na hatia ya kuua albino- Mbeya
16.Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba-Kagera
17.Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
18.Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika-Mwanza
19.Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza
20.Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita
21.Kulinda Muungano kwa nguvu zote-Pemba
22.Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro
23.Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa-Mbeya mjini
24.Kujenga bandari Kasanga –Rukwa
25.Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
26.Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya
27.Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga
28.Kununua "bajaji" 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa
29.Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani –Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi -Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro
30.Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini
31.Kuboresha barabara za Igunga -Tabora
32.Kusambaza walimu 16,000 katika shule za Sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu
33.Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini
34.Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)-Hydom Manyara
35.Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa- Musoma
36.Kulinda haki za walemavu- Makete
37.Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini
38.Kujenga barabara Musoma–Mto wa Mbu Arusha-Arusha
39.Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
40.Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma– Kaliua,Tabora
41.Kukarabati barabara ya Arusha Moshi-Arusha Mjini
42.Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa mpaka Singida-Dodoma
43.Kuwafidia wanakijiji ng'ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido 45.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
44.Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha –Arusha mjini
45.Kukopesha wavuvi zana za kilimo-Busekera, Wilaya ya Musoma, .
46.Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido
47.Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
48.Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara
49.Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini
50.Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa
51.Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa
52.Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania-Iringa
53.Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda
54.Kutokomeza malaria 2015-Bunda, Mkoa wa Mara
55.Kuwapa wanawake nafasi zaidi-Kilolo, Iringa
56.ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar
57.Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa-Kabandamaiti mjini Zanzibar
58.Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti
59.Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay-Ruvuma
60.Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbamba-bay Ruvuma
61.kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) –Ruvuma
62.Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania –Ruvuma
63.Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
64.Mtwara kuwa mji wa Viwanda –Mtwara
65.Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu-Kibaha
66.Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa-Kibaha
67.Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda -Kibaha

Ahadi namba 28 aliyoitoa iringa imeenza kutekelezwa, hebu tutizame na hizo nyingine utekelezaji wake ukoje?

Mbona umezipunguza au macho yangu

AHADI - ALIITOA AKIWA WAPI...


  1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa - Nzega, Tabora
  2. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini
  3. Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria - Igunga
  4. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) - Shinyanga
  5. Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini - Dodoma
  6. Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini
  7. Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma
  8. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi - Kagera
  9. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi - Kagera
  10. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini
  11. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
  12. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda - Kagera
  13. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme - Kagera
  14. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu - Kagera
  15. Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino - Mbeya
  16. Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba - Kagera
  17. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
  18. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika - Mwanza
  19. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu - Mwanza
  20. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani - Geita
  21. Kulinda muungano kwa nguvu zote - Pemba
  22. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa - Morogoro
  23. Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini
  24. Kujenga bandari Kasanga – Rukwa
  25. Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
  26. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira - Mbeya
  27. Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama - Tanga
  28. Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini - Iringa
  29. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani – Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam - Same mkoani Kilimanjaro
  30. Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same - Same Mjini
  31. Kuboresha barabara za Igunga - Tabora
  32. Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu - Kisesa Magu
  33. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya Mjini
  34. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) - Hydom Manyara
  35. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa - Musoma
  36. Kulinda haki za walemavu - Makete
  37. Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini
  38. Kujenga barabara Musoma – Mto wa Mbu Arusha - Arusha
  39. Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
  40. Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma – Kaliua,Tabora
  41. Kukarabati barabara ya Arusha Moshi - Arusha Mjini
  42. Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa, mpaka Singida - Dodoma
  43. Kuwafidia wanakijiji ng'ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 - Longido
  44. Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
  45. Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini
  46. Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma
  47. Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido - Longido
  48. Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
  49. Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara
  50. Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini
  51. Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015 - Babati vijijini
  52. Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha - Iringa
  53. Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika - Iringa
  54. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania - Iringa
  55. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi -Ifunda
  56. Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, mkoa wa Mara
  57. Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa
  58. Ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii - Kibandamaiti Mjini Zanzibar
  59. Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa - Kibandamaiti mjini Zanzibar
  60. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada - Kibandamaiti
  61. Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay - Ruvuma
  62. Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbambabay Ruvuma
  63. kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma
  64. Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania – Ruvuma
  65. Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
  66. Mtwara kuwa mji wa Viwanda – Mtwara
  67. Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu - Kibaha
  68. Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa - Kibaha
  69. Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda - Kibaha



---2005 Alikuja na Maisha bora kwa kila Mtanzania,hili halina ubishi lilikuwa ni changa la macho kwa Watanzania,Kama haitoshi akasema anawajua kwa majina wala rushwa,lakini hatuoni hata mmoja aliyemchukulia hatua===hii ni kutaka sifa na popularity.

---Juzi amekuja na mpya ya kumpatia kila mwanafunzi Computer ambayo iko connected kwa internet, it's high time now kwa watanzania kuhoji uwezo wa RAIS wetu,ni kwamba anafanya Wa Tanzania ni wapumbavu sana kiasi kwamba hawawezi ku reason kuwa hilo sual haliwezekani???

Hata kwa wanafunzi tu wa vyuo vikuu hilo suala halitekelezeki leo anatuambia ataanza na shule za msingi,umeme ni tatizo..hivi jk anajua kuwa its only 10% ya wa Tanzania wana access na umeme na 0.05% ya watanzania ndo wanaweza kutuima computer na wana access na internet,hata kwa nchi ambazo zimeendelea kuzidi sisi hilo suala halipo,,yeye anataka kuhadaa Wa Tanzania aili aendelee kubaki madarakani!!!!!me nadhani pia JK na uwezo mdogo sana wa ku reason ndo maana hata hafikirii kuwa suala kama hilo watu wenye akili timamu hawawezi kusadiki,inahitaji mtu mwenye akili za mwenda wazimu kuamini ahadi kama hizo.
 
Kwa mara ya kwanza nilidhani ni utani kabsaaaa!! wakati Mh. Pindua Mizengwe alipo kuwa anatetea hoja yake bungeni kama kiranja mkuu. Alisisitiza kwamba serikari ina nia thabiti ya kufikia malengo ya milenia. MDGs hususani MDGs 4 & 5 (Infant & Martenal health). Na mbinu moja wapo ya kupunguza vifo vya wakina mama wakati wa kujifungua ni serikari kutatua tatizo la magari ya kubeba wagonjwa (Ambulance).
Serikari ilishadidia kuingiza bajaji kama njia muafaka.... haraka haraka nilijiuliza Bajaji hizi ni za namna gani? ni hizi tunazo ziona hapa mjini? ni hizi ambazo kiukweli zina pata taabu sana kupanda vijilima vya hapa mjini kama kimara na kwingineko?? In actual sense was looking the feasibility of this strategy and the kind of infrastructure we have in the country. Hakika nilipata shida ya kupata picha ya hii bajaji.

Namshukuru mdau aliye weka picha za hiii ambulance pikipiki ya aina yake!!! Nimeiona na nimefarijika na kuuzunika?? Kweli bajaji hizi zitaweza kufanya kazi maeneo magumu ambako zinahitajika? mfano nimebahatika kufika Simanjiro vijiji kama Emborate, Terrat, Kambi ya chokaaa!!! na kwingineko? Lets look Mbulu kama kule Endagchan, sirop, mewadan, Ngorati jamani kwa kuangalia miundombinu na aina ya piki piki sidhani kama zita kidhi aja... kweli Wadanganyika twadanganyika.
Najaribu kupiga picha mvua inanyesha,barabara ina matope?? mama yupo kwenye labor pain kweli huyu mama atakuwa confortable kwenye piki piki hii. Dereva ananyeshewa na sidhani kama zina sehemu ya kuweza kutundika hata drip au sehemu ya msindikizaji kumsaidia mgonjwa? Nimeshuudia wagonjwa wakipakizwa kwenye torori na wakati mwingine kwenye vitanda vya kamba miaka 50 baada ya uhuru !!! kama kweli serikari ina nia angalau wange wekeza kidogo kidogo kwa kununua ambulance za ukweli na sio kununua magari yenye 4 wheel drive ambayo watawala wanatembelea kutoka masaki hadi posta!!! inashangaza sana sana.
Ukiangalia kwa makini hapo kwenye picha utamwona Chief Medical officer... Dr Deo Mtasiwa anafurahi na mafanikio hayo. Hivi kweli hizi ambulance zitaweza kweli kutatua tatizo au ndo litazidi kuongeza idadi ya vifo kwa akina mama. Jamani nafikiri wakati wa siasa kwenye mambo nyeti hauna nafasi. Hii ni hatari. Swali hizi piki piki zina specification gani? na zina kipi special..tafadhali kama kuna mdau mwenye data aziweke hadharani. What is its engine capacity? Zina 4 wheel drive? jamani tuelezeni au la tuzipinge kwa nguvu zote. Naomba kuwakilisha.
 
4799484_1_small.jpg 5376153_1.jpg

7,270USD 4,858USD


Kwa nini serikali yetu ni kilaza hivi, haya ni magari maarufu kama mikate yanatumika sana China na yanatumia mafuta kidogo mmno. Hapa serikali imefanya blunder
 
Li inchi hili linatia aibu sana. Kwanini vigogo mapapa wasitumie wenyewe hizi bajaji kwendea ofisini na kutafutia nyasi za ng'ombe.

Patients deserve to be well treated and looked after.
 
siku ya mvua utampeleka wapi mgonywaaa,,,,,,,,,,,,,,,mbona watanganyika munadanganywa sana,hivi wake zao hawa mawaziri watawapakia katika hizo pikipiki ? Labda dcm kuwe hakuna tena kama hawatotiwa china ya mvungu wa dcm.

sikilizeni wazalendo haya sio maendeleo tunayotaka,tunataka kuona ambulace sio piki piki,kama kuna foleni barabarabi basi zitanueni bara bara,pesa za watoa jasho,na kodi,na mrima,na mgodi na gesi zinaenda wapi ?

Wakati barabara zote hizo na zimejengwa na wafadhili kutoka njee kwa misaada,wizara ya afya pia misaada,elimu misaada,sasa pesa zetu zninaenda wati jamani ?

wazalendo amkeni,hizi pikipiki wakatumie wao mawaziri na yale mashangingi wauze naamini kila changingi moja likiuzzwa tutapata ambulace mbili za uhakika au vipi ????????????
 
Tunasubiri ongezeko la vifo na ongezeko la takwimu za wanawake wanaojifungulia njiani kabla ya kufika hospital...haya ni masihara na mimba...pengine mgombea urais angekuwa mwanamke asingefikiria huu ujinga....
 
Mnajiropokea tu, nendeni Vijijini Mkaone Hali halisi Wajawazito wanavyotembea kwa Miguu na Wengine wanajifungulia njiani, chini ya miti nk Wakielekea Vituo vya Afya kilomita kadhaa kutoka Zahanati za Vijiji. Wenye Uwezo huko Vijijini hukodi Magari, wasio na Uwezo wanabeba wajawazito kwa Machela za kienyeji na Baiskeli za Kawaida hadi Wengine wanafia njiani. Waliobuni na Kuzitengeneza Pikipiki hizi wana Akili na Huruma zaidi ya hawa waliojiingiza kwenye Msafara wa "Great Thinkers" wakati kazi Yao ni Kuponda kila Jitihada zinazofanywa na Serikali za kuAlleviate matatizo ya Vijijini. Basi waambieni ndugu zenu Walioko vijijini kwenu wasio na Usafiri Wasizipande waendelee kutembea kwa Miguu! sie Wanyonge zitatufaa sana, KWENDENIZENUNI!!
 
Moja ibaki Dar kwa ajili ya Msafara wa Mkuu wa Dola, ili turudishe ile ya kukodi.
 
Mnajiropokea tu, nendeni Vijijini Mkaone Hali halisi Wajawazito wanavyotembea kwa Miguu na Wengine wanajifungulia njiani, chini ya miti nk Wakielekea Vituo vya Afya kilomita kadhaa kutoka Zahanati za Vijiji. Wenye Uwezo huko Vijijini hukodi Magari, wasio na Uwezo wanabeba wajawazito kwa Machela za kienyeji na Baiskeli za Kawaida hadi Wengine wanafia njiani. Waliobuni na Kuzitengeneza Pikipiki hizi wana Akili na Huruma zaidi ya hawa waliojiingiza kwenye Msafara wa "Great Thinkers" wakati kazi Yao ni Kuponda kila Jitihada zinazofanywa na Serikali za kuAlleviate matatizo ya Vijijini. Basi waambieni ndugu zenu Walioko vijijini kwenu wasio na Usafiri Wasizipande waendelee kutembea kwa Miguu! sie Wanyonge zitatufaa sana, KWENDENIZENUNI!!

una hasira sana eeh!
Serikali yako inajitahidi ila jitahada zake zinatuacha palepale na haitusogezi japo hatua moja mbele.
Sasa mama mjamzito atakayepanda hiyo piki piki arushwe rushwe hadi afike na yule atakayetembea mwenyewe akwepe mashimo ikibidi hata short cut apite bora yupi?
Huoni kama serikali yako imetuacha palepale kwenye shida?
 
Hebu Imagine upo kwenye conference inayohusu mambi ya afya na watu wa mataifa mchanganyiko, then mtu anauliza mpango wa Tanzania katika kupunguza vifo vya kinamama, unaweza kutamani kujificha....
 
Huu ndio ukomo wa uwezo wa kufikiri na ubunifu wa wanao tuongoza kuleta pikipiki ambulace, a terrible decision, yale yale ya shule kila kata, ubora ziro ukiwauliza wanakupa majibu rahisi kama fikira zao, ooh hizo changamoto za kimaendeleo, upuuzi mtupu. Kwanini usinunue ambulace za magari lets say 50 ambazo zina huduma ya kweli kuliko huu usanii zikawa zimeongeza idadi ya zilizopo. Kwa nini usijenge shule kila tarafa ambazo zinajitosheleza kwahuduma muhimu zote, kuliko shule kila kata ambazo ni matoyi ya shule. Kama wana amini katika hii ambulace pikipiki na tuione ikitumiwa kwenye msafara wa rais. Halafu mtu anashanga kwa nini tunalaumu kila kinachofanywa na serikali watu wana kitilia qn mark, anaacha kushangaa uwezo wa kimaamuzi wa hao wanaotiliwa qn mark. Hawa viongozi kama hawana washauri waombe msaada wako wengi wenye uwezo watawasaidi. Wanafanya mambo ambayo mwisho wa siku wanabakia kuwa kichekesho mbele ya uso wa jamii.
 
Back
Top Bottom