Hatimaye CCM yatimiza ahadi; Bajaji za Wagonjwa zapokelewa rasmi

hizibajaji za wajawazito zitajengewa barabara au zita pita kwenye hizi barabara za Somalia
attachment.php
 
Piki piki za kubebea wagonjwa zimeanza kuwasili toka SA. Hili wakati JK akisema wakati wa kampeni nilidhani :blah: za siasa tu, kumbe amepania...hii ni hatari kwa wagonjwa:confused3:

At least ametimiza mmoja ya ahadi zake za kampeni!! Bado naisubiri kwa hamu ya kuifanya Rock City yetu Califonia ya Tanzania!!
 
Hiyo pikipiki ianze kumbeba Salma Kikwete kwanza akipata mimba na akiwa na uchungu, impitishe kwenye barabara ya vumbi na mashimo (ndio barabara zetu vijijini), akifika hospitali salama basi zitakuwa na uwezo, vinginevyo naona hii ni strategy ya kuongeza vifo vya akina mama na vitoto vyao tumboni, lazima abruptio ziwapate hawa wamama kwa mtikisiko, masikini wakina mama wa Tanzania nani atawaokoa?
 
God forbid it.

How mjamzito wa miezi tisa ajikunje kwenye hicho kijichemba cha bajaji?? na wanawake wengi ni wanene??? si ndio kuzidisha maafa?

kwa nini wasingeleta sample mbili za hii mikweche kuona kama inafanikiwa kabla ya kuagiza hizo mia nne?? This is ridiculous.

Itakuwa kampuni ya JK huko South Africa hamna lingine.
 
Naona Aibu kuitwa mtanzania... wenzertu wanaplan za kutembea kwenye sayari ya Mars.. sisi bado tunashangilia bajaji.. hii serikali haioni hata aibu!
 
400*5900*1520= 3,587,200,000 / 60,000,000 = 59.7 Hesabu hiyo inaonyesha kuwa kama serikali ingeachana na hu mpango mbovu wa kununua hizo pikipiki 400 kwa dola 5900 ambazo ni sawa na 3.58 Billion ingeweza kuagiza magari ya ambulance 60 kwa gharama ya million sitini kwa kila gari,jambo ambalo lingefanyika kwa awamu kadhaa basi magari ya wangonjwa yangekuwa ymepatikana kukidhi haja za watanzania,hizo pikipiki,zitakuwa zinachagua njia,hali ya hewa,na muda wa kufuata wagonjwa kwa kuwa si salama kwa anyeendesha na abiria wake.Serikali hii ina washauri kweli ? Du JK acha kukurupuka !!!
 



Naona kama vile uzito utaelemea upande mmoja wakushoto manake wajawazito ni wazito kweli kweli. Hivyo kupelekea chombo hiki kupindukia mbali na mjamzito ndani.

Au ni macho yangu mwenyewe?
 
Hizi pikipiki zinaletwa kuja kuharibu Mimba za wake zetu kwa kama unampenda mke wako ni bora ukakodi gari impeleke Hosptali kuliko kupanda hizo pikpiki zitaharibu mimba za wake zetu. Zifanyiwe Test huko Ikulu kwa kuwapakiza wake za Mafisadi Mawaziri na FIsadi Kikwete.

Hii ina maanisha ni jinsi gani Mafisadi wanavyozidi kutudharau badala ya kutuletea Ambulance na kutujazia madawa na kutupunguzia kero huko Hospitalini wao wanatuongezea Matatizo ya kuja kutopotezea watoto wetu. wakati wao wanapeana Ma-VX Bungeni

Mafruku mke wangu au ndugu yangu kupanda hizo Stupid Pikipiki, wampelekee Mkwe wa Fisadi Kikwete akapande. Pumbavu yao

 


We are not serious hizi machela huwa zinatumiwa kwenye mpira wa miguu au cricket kubebea majeruhi kutoa uwanjani na si safari ya mwendo mrefu. Natamani kumwona mama Fasta Lady ndani ya hiyo machela.
 
Hiki sasa kichekesho, hicho kitanda kwanza kwa bara bara zetu za vijijini kinaweza kukatika, gharama ya kununua hizo pikipiki ni bora wangenunua haice...hivi mama mjamzito uanze kumvalisha helment kwanza?
Mpango wa Serikali iliyouanzisha wa ununuzi wa Pikipiki za kubebea wagonjwa ili kuzuia vifo vya wakinamama na watoto katika maeneo ya vijijini. Serikali inakusdia kununua Pikipiki 400 ambazo zitasambazwa maeneo mbalimbali hapa nchini.

Pikipiki maalum iliyotengezwa na Kampuni ya E Ranger ya Afrika Kusini kwa ajili ya shughuli za kubebea wagonjwa ili kudhibiti vifo vya mama na watoto. Pikipiki hizo kila moja imegharimu Dola za Kimarekani 5,900.





 
Duh! Moja ipelekwe ukumbi wa bunge. Waziri au mbunge akipata dharura ya kimatibabu apakizwe kwenye hicho kitanda cha bajaj, tena naomba Mungu kiwe kipindi cha masika au vumbi kali.
Kweli kabisa waone matokeo ya kupigia makofi vitu visivyo na maana tena nashauri moja iwe kwenye misafara ya Spika na Kikwete.
 
Alichokifanya Kikwete ni zaidi ya kawazalilisha wanawake....hivi ile ndege ya rais ina msada gani kwa watanzania kwanini isiuzwi akanunua ambulance za kutosha hala bei ya hizi bajaji imenitisha....
 


We are not serious hizi machela huwa zinatumiwa kwenye mpira wa miguu au cricket kubebea majeruhi kutoa uwanjani na si safari ya mwendo mrefu. Natamani kumwona mama Fasta Lady ndani ya hiyo machela.
uko sawa kabisa mkuu...Nakumbuka wakati wa kombe la mataifa Afica lilipofanyika naijeria kama sikosei hivi vibajaji vilitumika.
 
Mpango wa Serikali iliyouanzisha wa ununuzi wa Pikipiki za kubebea wagonjwa ili kuzuia vifo vya wakinamama na watoto katika maeneo ya vijijini. Serikali inakusdia kununua Pikipiki 400 ambazo zitasambazwa maeneo mbalimbali hapa nchini.

Pikipiki maalum iliyotengezwa na Kampuni ya E Ranger ya Afrika Kusini kwa ajili ya shughuli za kubebea wagonjwa ili kudhibiti vifo vya mama na watoto. Pikipiki hizo kila moja imegharimu Dola za Kimarekani 5,900.






Hivi hawa jamaa wametufanya watz ni wajinga sana au? Hizi zimejaribiwa wapi?
 
Jamani,

Utadhani utani bwana, kumbe watu ndo washamaliza hivyo. Hii ndiyo TZ aliyotuachia baba wa taifa.
 
Hivi kama mvua inanyesha au jua kali kweli huyu mgonjwa atafika salama hospitali? Hivi kweli TZ tumefika mahali pa kutumia pikipiki kama ambulace? kama tunauwezo wa kununulia wabunge zaidi ya magari 300, mawaziri na watumishi wengine wa serikali kweli tunashindwa kununua ambulance? kweli taifa badala ya kwenda mbele tunarudi nyuma. Hii dhuluma kwa watu masikini ipo siku itatutokea puani.
 
Hizo pikipiki zimefanyiwa test watu hawajakurupuka tu wakasema ziwe za wagonjwa ndo maana muundo wake nitofauti na pikipiki za kawaida, japokuwa hazina ufanisi kama gari la wagonjwa bt ni suluhisho kwa kiasi flani hasa kwa watu wa vijijini wanaotumia vichanja na baiskeli kufikisha wajawazito mahospitalini..... ....tusiponde tu tuangalie na positive side.......
 
sisi hatusimami,tunarudi kinyumenyume!
Kwenye reli, wenzetu waliendeleza kwa treni za umeme, sisi tukaua tukaazisha barabara,
sasa wenzetu wako kwenye ambulance sisi ndo tunaongeza vibajaja

Gari la wagonjwa linakuwa na vifaa vya utabibu pamoja na paramedic ambaye anaanza kutoa huduma ya kwanza kabla mgonjwa hajafika hospitali. Atafanyaje katika hiyon pikipiki? Ujinga kweli huo. watu wanaongea karne ya 20 sis bado tunajivunia kuingia karne ya 17. Nyeye alifundisha kuwa We Must run while they walk. Sisi badala yake tunasimama kabisa wakati wenzetu wanakimbia.
 
Au labda ni mbinu mpya ya kupunguza uzazi usio na mpango, wkifa akinamama wawili kwenye hinyo vibajaji wengine watakoma kabisa!
 
Back
Top Bottom