Hatimaye bondia kutoka Ufilipino avalishwa gloves zenye rangi ya bendera ya Tanzania ya jiwe Tanzania ya viwanda

Tutabishana tu, ila kifupi mwakinyo amepigwa hili ni dhahiri shahiri! Mtz mwenzetu ana mapungufu mengi, ana mikono mizito mnoo, kuna baadhi ya ngumi mtu akijaa haipigwi moja, yeye anadokoa na kukimbia, nadhani nyumbani kumembeba.

Hiki kitu nilisema siku alipopigana na yule muargentina, mwakinyo anatakiwa ajirekebishe.
 
Kuanzia Leo sishabikii tena ngumi, ni mchezo wa kiboya sana. Yaan Mfilipino kashinda live ila wanampora ushindi wake watu wanaona. Ushindi kama wa CCM
 
Bongo bado sana tunatia aibu kabisa yani refa anakata kamba za glov kwa meno huu ni upuuz mkubwa sana
Kabla ya game ya main card yaani gloves hazikuandaliwa mpaka wametumia za wale wa mapambano ya itangulizi, najiuliza kulikuwa hakuna prematch meeting?
 
Ameshinda kiana aina.......muda wote anakimbia kimbia tu

Majaji wote watatu wamependelea? kukimbiakimbia ni mbinu mojawapo ya kushinda ndio maana hapo juu kuna jamaa amekumbushia pambano la Myweather na Pacquiaqo ambapo Pacquiao alishindwa kwa mtindo huo huo wa kudokolewa dokolewa na kukimbiwa
 
Majaji wote watatu wamependelea? kukimbiakimbia ni mbinu mojawapo ya kushinda ndio maana hapo juu kuna jamaa amekumbushia pambano la Myweather na Pacquiaqo ambapo Pacquiao alishindwa kwa mtindo huo huo wa kudokolewa dokolewa na kukimbiwa
Huu mchezo umechezwa hadharani siyo chumbani, kila mtu ameona, Mwakinyo mwenyewe hana furaha na ushindi wake utakuwa wewe?
 
Back
Top Bottom