Hatimaye BAVICHA yapata Katibu Mkuu, ni Deo Munishi

Wakuu habari!

Baraza la Vijana CHADEMA(BAVICHA) hatimaye limepata Sekretariet iliyokamilika na hivyo kuwa na Uongozi uliokamilika.Kikao Cha Kamati Tendaji Cha BAVICHA kilifanyika Siku ya Jumamosi tarehe 12 Nov Mjini Dodoma.Wajumbe wa Kikao hicho ambao ni Wenyeviti wa BAVICHA wa Mikoa,Viongozi Vijana wa Chama Taifa,Wawakilishi Watano wa Wabunge Vijana na Wawakilishi Watano wa Madiwani Vijana.

Katika Uchaguzi huo uliokuwa na mchuano mkali,wafuatao walichaguliwa;
1. Katibu Mkuu wa Baraza hilo Bwana Deogratius Munishi
2. Naibu Katibu Mkuu Bara wa Baraza hilo Bi Esther Daffa
3. Naibu Katibu Mkuu Zanzibar bwana Suleiman Maabad
4. Mratibu wa Uhamasishaji au Katibu Mwenenzi wa Baraza hilo Bwana Rafiki Rufunga
5. Mwekahazina wa Baraza Bwana Mrisho Ramadhani

Mbali na Uchaguzi huo Kikao hicho pia kilijadili Hali ya Siasa nchini na mambo mengineyo.

Aluta Continua.

Hongera sana Munishi.

Hongera kanda ya kaskazini.
Hongera mkoa wa Kilimanjaro kutoa kiongozi.

Uzi ule ule
 
Nimjuavyo Munishi Katibu mkuu mpya wa BAVICHA.

Mosi, ni mpambanaji wa ukweli asiyetetereka. Wanafunzi wa UDSM tunamkumbuka kwa hili na evidence ni katika kupigania maslai ya wanafunzi wa elimu ya juu mwaka 2008. Akiwa kama mbunge wa DARUSO, aliongoza kikosi cha kuplani mikakati bora ya kufanikisha mapambano yale hata baada ya wanafunzi kutimuliwa vyuoni na hivi leo wanafunzi wanaosoma science wanafaidi mkopo wa 100%. Munishi anamkono wake hapo.

Pili, hapendi unafiki. Hata kama ni rafiki yake wa karibu kama ni manafiki hutaiva na Munishi. Tuliokuwepo UDSM tulishuhudia uchaguzi wa DARUSO wa mwaka 2009 wa CAS. Hakusita kuwataja hadharani wale wenye ubinafsi na waliokuwa wakitafuta madaraka kwa kwa maslahbinafsi. Obama na Masalu ni baadhi ya wahanga wa Munishi.

Tatu, mwaka 2008 baada ya kubaini TAHLISO imevamiwa na usalama wa taifa kwa kupachikiwa mamluki kwenye uchaguzi uliofanyika pale Dodoma yeye pamoja na Silinde David walivamia mkutano huo na kuhakikisha unavunjika na uchaguzi haufanyiki. Huyu ndiye aliyekua mmojawapo wa waliohakikisha TAHLISO inavunjwa ili usalama wa taifa wakiongozwa na Ngubiagai wanabaki wenyewe na vyuo vya umma wakaunda umoja wao ujulikanao kama UVEJUTA.

Nne, ni mtu anayechanganya mbinu za kimapambano yaani diplomasia na violence akiweka kipengele cha muda. Tulioongoza mapambano ya mgomo wa vyuo vya umma mwaka 2008 tunamfahamu kwa hili.

Tano, ni mtu flexible anayemudu kufanya vitu vingi kwa mpigo. Wakati akiwa DARUSO pia alikua anaongoza harakati za vijana nje ya mfumo wa elimu kupitia asasi ya Tanzania Youth Vision Association kama katibu mkuu na kute kukionekana ufanisi.

Munishi nimesoma nae Uru Seminary na kote uko alikua kiongozi mwenye msimamo mkali asiyetaka ubabaishaji katika kazi.
Naamini BAVICHA na Chadema kwa ujumla wamepata jembe, tena jembe kali kweli kweli
 
Munishi ni kijana ambaye ana uchu wa madaraka na vyeo sijapata ona.Amemaliza UDSM mwaka jana SOCIOLOGY kwa waliosoma naye watakwambia,HAKUNA KITU.Anamikogo na majivuno ya ajabu.Sio mtendaji na kwa sababu hiyo sitegemei akawa na impact positive kwa chandimu.Nikimlinganisha na SHEGELA ni sawa na kulinganisha kichuguu na mlima k'njaro,kwa maana shegela ni k'njaro.Niwapongeze CDM kuchagua katibu bapa asiye na makali.

Inaonesha hata Shigella mwenyewe humfahamu!
 
Nimjuavyo Munishi Katibu mkuu mpya wa BAVICHA.

Mosi, ni mpambanaji wa ukweli asiyetetereka. Wanafunzi wa UDSM tunamkumbuka kwa hili na evidence ni katika kupigania maslai ya wanafunzi wa elimu ya juu mwaka 2008. Akiwa kama mbunge wa DARUSO, aliongoza kikosi cha kuplani mikakati bora ya kufanikisha mapambano yale hata baada ya wanafunzi kutimuliwa vyuoni na hivi leo wanafunzi wanaosoma science wanafaidi mkopo wa 100%. Munishi anamkono wake hapo.

Pili, hapendi unafiki. Hata kama ni rafiki yake wa karibu kama ni manafiki hutaiva na Munishi. Tuliokuwepo UDSM tulishuhudia uchaguzi wa DARUSO wa mwaka 2009 wa CAS. Hakusita kuwataja hadharani wale wenye ubinafsi na waliokuwa wakitafuta madaraka kwa kwa maslahbinafsi. Obama na Masalu ni baadhi ya wahanga wa Munishi.

Tatu, mwaka 2008 baada ya kubaini TAHLISO imevamiwa na usalama wa taifa kwa kupachikiwa mamluki kwenye uchaguzi uliofanyika pale Dodoma yeye pamoja na Silinde David walivamia mkutano huo na kuhakikisha unavunjika na uchaguzi haufanyiki. Huyu ndiye aliyekua mmojawapo wa waliohakikisha TAHLISO inavunjwa ili usalama wa taifa wakiongozwa na Ngubiagai wanabaki wenyewe na vyuo vya umma wakaunda umoja wao ujulikanao kama UVEJUTA.

Nne, ni mtu anayechanganya mbinu za kimapambano yaani diplomasia na violence akiweka kipengele cha muda. Tulioongoza mapambano ya mgomo wa vyuo vya umma mwaka 2008 tunamfahamu kwa hili.

Tano, ni mtu flexible anayemudu kufanya vitu vingi kwa mpigo. Wakati akiwa DARUSO pia alikua anaongoza harakati za vijana nje ya mfumo wa elimu kupitia asasi ya Tanzania Youth Vision Association kama katibu mkuu na kute kukionekana ufanisi.

Munishi nimesoma nae Uru Seminary na kote uko alikua kiongozi mwenye msimamo mkali asiyetaka ubabaishaji katika kazi.
Naamini BAVICHA na Chadema kwa ujumla wamepata jembe, tena jembe kali kweli kweli


Hongera aisee..kina munisi, kavishe, lema na mbowe...

Sifa ya pili muhimu lazima umetoka seminary..very good indeed..
 
Hongera aisee..kina munisi, kavishe, lema na mbowe...

Sifa ya pili muhimu lazima umetoka seminary..very good indeed..[/QUOTE

Mbona wakina Rwebangira, Rweyemamu, Rutashobia, Shija, Machibya, nk nao wengi wamepita Seminary. Nayo ni sifa yao kubwa tu na siyo yakina lema na kavishe na lema peke yao bana.
 
Hongera aisee..kina munisi, kavishe, lema na mbowe...

Sifa ya pili muhimu lazima umetoka seminary..very good indeed..
Dah.... unajua uongo ukizungumzwa sana mwisho wake hua kweli vile - Makosa yale yale yanarudiwa na Chadema kila siku. Nasema siku zote WATU na MAZINGIRA kuwa kigezo cha maazimio yoyote..Chadema leo ilipo haitakiwi kabisa kufanya makosa kama haya pamoja na kwamba mimi naamini kabila, dini, Utaifa (Zanzibar - Tanganyika) wala jinsia siii sababu hata kidogo lakini nilisomeshwa na Mwalimu Kitila ya kwamba ktk siasa za Tanzania (ktk kujenga Utaifa), kabila na dini vinahitajika kutazamwa sambamba na CV ya mhusika...Sasa ikiwa hivyo ndivyo na Chadema wanaelewa fika kwamba wanashukiwa Udini na Ukabila kwa nini wanaendeleza kufanya makosa yale yale..
 
nilipita imagi hill pale j2 wakati wanaendelea na mchakato.... makamanda walikuwa wamependeza sana kwa kombati zao za ukweli.... hata mimi sasa natamani kwenda kushona mpya......

kweli hii sio chama ya musimu!
 
pongezi sana chadema mmefanya jambo la kheri naona mmebalance hakuna udini wala ukabila Nadhani hapa wanga wamefungwa midomo.....
 
Safi sana makamanda, Harakati ya ukombozi ndiyo inaanza.
Mapinduzi yote yaliyofanyika duniani yalifanywa na vijana, hata libya maandamano yalifanywa na vijana.
 
Deogratius Munishi, my udsm mate na mbunge wangu pindi tupo 1st & 2nd year CASS namwamini sana, atafanya makubwa Bavicha!
 
wewe Regia pole sana mama...hicho ni kiini macho hao wachaga wachache akina mbowe wamemuweka huyo Mushi kw malengo yao hao wengne hakuna kitu pale...wachaga kweli noma ndio mana mwl aliwakataa. yule Heche aliye wekwa pale ni ziro kabisa, kwanza hana elimu anapelekeshwa tu...toa upupu wako hapa...

Kana nke oleye moghati oghete!
 
Dah.... unajua uongo ukizungumzwa sana mwisho wake hua kweli vile - Makosa yale yale yanarudiwa na Chadema kila siku. Nasema siku zote WATU na MAZINGIRA kuwa kigezo cha maazimio yoyote..Chadema leo ilipo haitakiwi kabisa kufanya makosa kama haya pamoja na kwamba mimi naamini kabila, dini, Utaifa (Zanzibar - Tanganyika) wala jinsia siii sababu hata kidogo lakini nilisomeshwa na Mwalimu Kitila ya kwamba ktk siasa za Tanzania (ktk kujenga Utaifa), kabila na dini vinahitajika kutazamwa sambamba na CV ya mhusika...Sasa ikiwa hivyo ndivyo na Chadema wanaelewa fika kwamba wanashukiwa Udini na Ukabila kwa nini wanaendeleza kufanya makosa yale yale..
Nilikuwa nakuona umeelimika lakini kwa sentensi hiyo nimekupuuza sana.
 
Kaka munisha hongera sana sana niko na masawe hapa ngowi muro kimambo mallya olomi na wote wanakuinywa mbege kwa furaha yako.[/QUOTE]

mawazo.maono.ndoto.njozi za mtu MKABILA.
 
Back
Top Bottom