Hatimaye Babaj Yawa Zimamoto

na nnadhani hicho kimetengenezwa kwa ajili ya kuuza tanzania tuu, coz watu makini na nchi zao na wananchi wao hawawezi leta upuuzi kama huo khaaa, halafu eti Pinda na yeye anashangaaaa na baadaye atakisifia bungeni. Mambo yanayotokea kila siku ktk serikali hii ya ****** ni ya ajabu saana, kabisa mnaenda nunua bajaj eti ndo zima moto, mara eti ndo ambulance, mbona hawa wabunge wanajinunulia ma VX ya mwaka 2009 ya mamilioni ya fedha, kwa nini na wao wasipewe bajaj wakazungukia majimbo yao? kweli hii only in TZ. Wa tanganyika tumelala mno tutachezewa kama mwendawazimu na hawa watu wasio na machungu na nchi hii, tuamke sasa!
 
Ni mradi wa mojawapo watoto wa Sir George Kahama ambaye anayo ofisi ya kifahari sana pembeni tu mwake nyumba ya Mhe Kikwete maeneo ya pale Morocco Dar es Salaam.

Sasa anza kuunganisha hiyo midoti mwenyewe kwamba hiyo mionyesho ya kuhudhuriwa na Waziri Mkuu bado kutakwepo tena na tender ya kiukweli wafanyabiashara wote kupata fursa sawa?

Huu ni mbadala wa gari la zimamoto hasa uswazi ambako hakuna njia. Swali ni je hii bajaji inabeba maji kiasi gani?

Serikali ya Kikwete kiboko, haya sio masihara kweli??.

208308_1918882580898_1507034707_32048858_6018225_n.jpg
 
Mmmmmh! We must do something, to stop these jokes, HAPA TUNADHARAULIKA MNO WAKUU, HADI KICHEFUCHEFU.........
 
Jamani msiwe negative ( - hasi ) kiasi hicho – si kitu kizuri. Hapa wengi wenu mnakosoa tu na wengine mnaleta chuki za kibaguzi. Sikuona hata mtu mmoja amekuja na fikra tofauti ya kuboresha hiyo bajaj.

Mimi naona hii ni fikra nzuri ya kuanzia na baada ya matumizi utapatikana uzoefu wa kuboresha. Wote tunajua kuwa kitu muhimu sana katika uzimishaji wa moto ni kuwahi kufika na kuushambuliya. Hii bajaj itaweza kupita kwenya barabara finyu , Kufatana na bei yake nafuu zinaweza kutapakazwa sehemu mbali mbali vitongojini na kuweza kufika kwa haraka sehemu yenye moto.

Huu ndio uwezo wetu wa sasa na hii technologia ndio jawabu kwa hali yetu ya kipesa na kimakazi . tusiangaliwe wale wenye mabarabara mapana na magari makubwa ya zimamoto.

Kuwa negative sana ni kinyume na spirit of great thinkers.
 
Inabidi na viongozi wa nchi maadamu wamekubali bajaj yaweza okoa watu na mali zao waanze kuzitumia Kama usafiri waachane na mashangingi yanayotutia umaskini kila siku
 
hata nyumba yangu ya chumba kimoja ikiungua sijui kama maji ya hilo tank yatatosha kuuzima moto wake......duh
 
Serikali ya Tanzania ina masihara sana na maisha ya wananchi wake,hizo bajaji zina uwezo gani.? wa kuhifadhi maji ya kuzimia na speed kiasi gani..? kuwahi eneo la tukio,
 
nchi ya vibajaji hii,

kuanzia taxi, ambulence mpaka zimamoto ni bajaji!!! mtanzania wa leo atakuwa anazaliwa kwa mama yake kujifungulia kwenye kibajaji, akikua, usafiri wake ni kibajaji, sasa ikitokea janga pia ataokolewa na kibajaji!!!

kumbe hata dubai ya kigoma iliyoahidiwa itakuwa "dubai ya kibajaji"!!!??? na katiba naona nayo wanataka kutupa katiba ya kibajaji!!!

kwa kweli, tutajibeba awamu hii!!!
 
tunapinga bila kufikiri...... HONGERA KAMPUNI MLIYOLETA BAJAJI KUZIMIA MOTO....! wanaopinga wanaishi masaki na oysterbay ambako kuna barabara za mpangilio, sisi kwetu MANZESE na watani zetu MWANYANYAMALA na TANDALE zitatufaa na kutusaidia.......! tena niliwashukurru nadhani DAWASCO walipoleta vibajaji vya kubeba maji kupunguza adha ya maji...! tena nawapa ushauri kwa kutoa ombi....!
ikiwezekana mtengeneze yenye uwezo wa kunyonya maji-taka kwani vyoo vyetu vinajaa na only option tuliyonayo ni kuvitapisha wakati wa mvua kwani magari ya kisasa yatakiwayo na wana-JF hayafiki huku kwetu kutikana na sisi wenyewe kujenga !
 
Mnaponda sana wakati munajua itakuwa effective kule uswazi kwetu ambako fire hawafiki ila kikombe cha babu mnakipa support.tukubali sisi na viongozi wetu wote wendawazimu
 
Jamani msiwe negative ( - hasi ) kiasi hicho – si kitu kizuri. Hapa wengi wenu mnakosoa tu na wengine mnaleta chuki za kibaguzi. Sikuona hata mtu mmoja amekuja na fikra tofauti ya kuboresha hiyo bajaj.

Mimi naona hii ni fikra nzuri ya kuanzia na baada ya matumizi utapatikana uzoefu wa kuboresha. Wote tunajua kuwa kitu muhimu sana katika uzimishaji wa moto ni kuwahi kufika na kuushambuliya. Hii bajaj itaweza kupita kwenya barabara finyu , Kufatana na bei yake nafuu zinaweza kutapakazwa sehemu mbali mbali vitongojini na kuweza kufika kwa haraka sehemu yenye moto.

Huu ndio uwezo wetu wa sasa na hii technologia ndio jawabu kwa hali yetu ya kipesa na kimakazi . tusiangaliwe wale wenye mabarabara mapana na magari makubwa ya zimamoto.

Kuwa negative sana ni kinyume na spirit of great thinkers.


Kuwa great thinker sio kukubaliana na upumbafu, kama unaona kinaboresheka kakinunue, ukiweke mtaani kwako watu wawe wanakikodi wakitaka kuzimia mishumaa wakati wa kulala.
 
kaka kweli kuna moto wa ukweli unadhani ni bajaji ngapi litahitajika kuzima moto kama magari makubwa yanashindwa kila siku, lakini pia hiyo bajaji haiwezi kufika eneo la tukio kwa wakati maana wakikipiga full tank speed yake lazima iwe ndogo na kumbuka heshima ya bajaji ni ndogo sana kama utaenda na speed kubwa lazima ikuweke mtaloni
tunapinga bila kufikiri...... HONGERA KAMPUNI MLIYOLETA BAJAJI KUZIMIA MOTO....! wanaopinga wanaishi masaki na oysterbay ambako kuna barabara za mpangilio, sisi kwetu MANZESE na watani zetu MWANYANYAMALA na TANDALE zitatufaa na kutusaidia.......! tena niliwashukurru nadhani DAWASCO walipoleta vibajaji vya kubeba maji kupunguza adha ya maji...! tena nawapa ushauri kwa kutoa ombi....!
ikiwezekana mtengeneze yenye uwezo wa kunyonya maji-taka kwani vyoo vyetu vinajaa na only option tuliyonayo ni kuvitapisha wakati wa mvua kwani magari ya kisasa yatakiwayo na wana-JF hayafiki huku kwetu kutikana na sisi wenyewe kujenga !
 
Viongozi wetu bwana, haiingii akilini kabisa, yaani kweli tunawapa wabunge milioni 90 kwaajili ya kununua SUV za kutembelea lakini kwenye mambo ya maana kama kusafirisha mama wajawazito kwenda hospitali haraka au kuokoa majanga ya moto tunafanya mzaha. Ole wenu nyinyi mnao walaghai Watanzania wasio na hatia maana siku yenu inakuja.
 
Back
Top Bottom