kufuatia matokeo ya uchaguzi 2010, ambapo inaelekea kuchachuliwa kwa namna mbali mbali hivyo kupotosha utashi na matumaini wa watanzania, hofu ya watu /yangu ni hatima ya vyama vya upinzani, pamoja na hatima ya tanzania kama nchi, kwani walioshinda ni "si watanzania bali mafisadi" ambao wana nguvu ya kipesa na pia wana tumia vyombo vya dola kugandamiza demokrasia, na tatizo hili linajionyesha kuwa kubwa zaidi, toka zama zile za kuwachoma vibaka/kibaka/jambazi nk. Sasa zama hizi ni za mafisadi na serikali iliyo kuwepo/zilizo pita zimeshindwa kuwachukulia hatua stahili mafisadi iwe kwa kuwa na nasaba nao au kutokana na uzembe wa serikali zetu au kutokuwepo na nia ya kupambana na huo ufisadi,, njia iliyo baki kwa wananchi ilikuwa ni kwa kufanya kampeni na uchaguzi katika hali iliyo sawa na serikali iliyopo madarakani, lakini bahati mbaya imeonekana njia hiyo nayo ni ngumu, kwa watu kuitumia kuonyesha kupinga kwao ufisadi, sasa tatizo linalo kuja hapo baadae , nalo linaweza kuwa ni watu kujichukulia sheria mkononi, ndipo hapo ninapo kuwa na mashaka ya baadae ya tanzania ya leo yenye "amani", la pili ni kuwepo kwa vyama mbadala kwani kwa mafisadi kuwa wame neemeka na utawala/tawala zilizo pita wanazidi kujikita zaidi na zaidi katika siasa na uchumi wa nchi hii, hivyo kuwanyima nafasi watu wengine au vyama mbadala, matokeo hali hii haimpi mtu yoyote yule matumaini kwa tanzania ijayo, kwani wahenga walisema kama huwezi kupigana nao basi jiunge nao, wapo walio amua kijiunga nao kama hatua za kupunguza makali ya maisha na wapo ambao hawata jiunga nao. je watachukua hatua gani ili kujikomboa?