Hatima ya nafasi ya watanzania maskini katika ajira

marshal

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
353
157
Habari za Kuaminika za kichunguzi zinaonesha kuwa kuna mtoto wa aliekuwa waziri wa maliasili na utalii kupewa nafasi kama administrator katika ofisi za bodi ya utalii Tanzania bila kufuata taratibu za ajira.Aidha nafasi hiyo ilikuwa na mtu ambae alifukuzwa kazi(terminated) bila kupewa sababu za kufukuzwa kazi kama sheria na taratibu za utumishi zinavyohitaji.Na kabla ya mtu huyo(aliefukuzwa) hajamaliza muda wake wa notisi aliyopewa tayari mwanadada(mtoto wa waziri) alikuwa kisha take over.Maisha ya watanzania yako rehani kwa vigigo wachache wenye uchu wa kuifanya nchi hii kuwa ya kwao. I was sympathetic kwa huyu dada aliefukuzwa kazi maana ni yatima na analea wadogo zake kwa kazi hiyo aliyokuwa akifanya!Sasa watoto wa vigogo wanchukua nafasi za yatima na kuyafanya maisha yao yawe ya dhiki ya kutupwa! kwenu wana JF,leo wamechukua ajira ya yatima huyu kesho ni yangu na keshokutwa ni wewe!!
 
Nilishasema hiki kitu kuwa ajira ya Watanzania zinachukuliwa na mafisadi na wageni. Ni muda wa kusimama kidete na kupigania haki zetu
 
Haya yanatukuta siyo tu serikalini hata katika sector binafsi ambako sasa soko linaendelea kujaa wakenya, wanatoa nafasi kwa walionacho au walio serikalini ili kupata uhalali wa kukaa hapa kuendelea kunyonya maziwa si kwa mirija ila mabomba....kwa nini tusiwe mashujaa tukazuiya haya mambo?
 
Sijui tuorganise yale ya Egypt? Pita ofisi za uhasibu za wilaya na mikoa ujionee!kuna wahasibu std8 na form4 wakati mwaka jana udsm,ifm,tia, iaa,saut zooote zimetoa wahasibu ila mpaka leo wako dsm na bahasha wanazungukia maofisi kama wakaguzi wa kujitegemea! Sasa mkisema tunaanza kuibiana ajira,hapa vita yaanza! Mi nkiona mgeni ofsini ntampokea mi ili nimuulize 'tukusaidie nini'? Akijib namtaka Hr namwambia hayupo,nipo mi!
 
Habari za Kuaminika za kichunguzi zinaonesha kuwa kuna mtoto wa aliekuwa waziri wa maliasili na utalii kupewa nafasi kama administrator katika ofisi za bodi ya utalii Tanzania bila kufuata taratibu za ajira.Aidha nafasi hiyo ilikuwa na mtu ambae alifukuzwa kazi(terminated) bila kupewa sababu za kufukuzwa kazi kama sheria na taratibu za utumishi zinavyohitaji.Na kabla ya mtu huyo(aliefukuzwa) hajamaliza muda wake wa notisi aliyopewa tayari mwanadada(mtoto wa waziri) alikuwa kisha take over.Maisha ya watanzania yako rehani kwa vigigo wachache wenye uchu wa kuifanya nchi hii kuwa ya kwao. I was sympathetic kwa huyu dada aliefukuzwa kazi maana ni yatima na analea wadogo zake kwa kazi hiyo aliyokuwa akifanya!Sasa watoto wa vigogo wanchukua nafasi za yatima na kuyafanya maisha yao yawe ya dhiki ya kutupwa! kwenu wana JF,leo wamechukua ajira ya yatima huyu kesho ni yangu na keshokutwa ni wewe!!
Kama kweli hali ndo hiyo basi tumefika pabaya. Inawezekana kweli kufukuzwa bila sababu hata ya kusingiziwa? Hapo napata mashaka kama kweli hata yeye aliyefukuzwa kama kweli aliajiriwa kwa utaratibu.
 
Dah! Wengine sijui tutatokaje kwa mpango huo.
Ulimwengu kweli hauna usawa.
Wapi sheria za kazi? Wapi watetezi?
 
Haya yanatukuta siyo tu serikalini hata katika sector binafsi ambako sasa soko linaendelea kujaa wakenya
Kwa elimu ya shule za Kata unategemea kuna Mtanzania atashindana na Mkenya/Mganda kwenye soko la ajira miaka 20 ijayo?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom